Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Jack Daniel

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2021
Posts
2,912
Reaction score
12,904
Kisa cha kusisimua, ni kisa kitamu chenye mafundisho na kuburudisha pia.

Nimesoma visa na stori kibao humu ziwe ni dhahania au za kweli lakini zimenipa nguvu na faraja kuwa kwenye record zilizowaweka watu kwenye wakati mgumu sipo peke yangu.

Hivyo basi na Mimi nakuja na kisa cha kweli kilichonitokea mwaka 2011. Ni kisa ambacho huwa sipendi kukumbuka na kujikumbusha Mara kwa Mara ila haina budi ni jambo lilitokea.

Lazima watu wajifunze japokuwa ajali haina kinga lolote litakutokea muda wowote na mahali popote.

Kisa kinaitwa,
MIMI NA BOSS WANGU

Kaa mkao wa kula.
 
TAHADHARI: zipo simulizi nyingi sana humu pia tumesha soma simulizi nyingi humu kuna watu wa kila aina wakosoaji , wasifiaji, jitahidi sana wende kwenye point.

Naamini utakutana na changamoto za kukosolewa tafadhali kama umeamua kutupa simulizi focus kwanye simulizi.

Sijajua muda wako ila pia jitahidi walau kwa siku usiache kutupa walau episode moja.

Mwisho kabisa kila simulizi lazima itakuwa na kasoro moja au zaidi tafadhali sana kosoa kistarabu kama utaona ni chai wacha sisi tunywe.

Maana tuna vitafunwa visivyo na chai au kama wew pia una chai lete wanywaji tupo ijapokuwa kukosolewa ni sehemu ya burudani nawasilisha.
 
Tarehe 17 mwezi wa kumi mwaka 2011, mimi, bosi na mke wake tulikuwa kwenye eneo fulani tukipata Chakula Cha mchana.

Si kawaida mimi kuandamana nao ila ni kwasababu, ilikuwa ni kwaajili ya mpango maalumu yaani Mimi kutumwa kufuata mzigo fulani mkoani.

Nirudi nyuma kidogo,

Mwaka 2011, nilikuwa na wakati mgumu sana kimaisha ni baada ya mwaajiri wetu kubadili kazi kutoka kazi uinjinia na tenda za kutengeneza barabara na kuhamishia nguvu kwenye biashara hoteli ikiwa ni hatua kubwa kwake

Huku wengine tukiachwa solemba maana ikabaki tu ile

Unajua nini Dani, Mimi nitakufanyia mpango palepale mi siwezi kukuacha tumetoka mbali bwana.

Huku nikiwaza, atanifanyiaje mpango Mimi kwenye biashara hiyo mpya ikiwa Sina utaalamu kwenye eneo lolote lile, anataka kunipa kazi gani?

Ulinzi? Au niwe naelekeza watu wapi pa kupaki magari au nikawe Gardner kwenye bustani zake, hahahaha siwezi kufanya hizo kazi na haya ni maneno ananipa ili kunifariji Hana kazi ya kunipa kwa Sasa.

Basi kadri maisha yanavyoenda ndivyo ugumu wa maisha ukawa unaongezeka, kila nikihangaika kutafuta kazi ikawa ni ngumu kupita maelezo, ikafikia wakati nikamnyang'anya pikipiki kijana fulani ambaye ni mtoto wa kaka yangu binamu.

Nikachukua pikipiki yangu kwakuwa haikuwa na mkataba ikawa rahisi tu, lengo siyo niendeshe Mimi ila ilikuwa iuzwe ili inisaidie kunyoosha mambo fulani ambayo pale nyumbani yalishaanza kukaa shaghala baghala.

Ikafikia hatua, nikiangalia baadhi ya vitu mule ndani naona kama vingi halafu vimebanana, basi friji la jokoni likawa muhanga, ni sawa na mchezaji ambaye kashindwa kuonesha kiwango bora kwenye timu,

Ni kipindi ambacho mke wangu alikuwa anahuzunika sana, kwanini kuuzauza vitu, akinisihi zaidi kupambana nipate kazi maana yake nilikokuwa naelekea si kuzuri.

Mambo yalienda hivyohivyo huku nikijitahidi kujikakamua kulipa ada ya mwanangu ambaye nilimpeleka nursery ya bei kubwa, ambapo nadhani ilikuwa ni kuiga ama kufuata mkumbo maana hata kazi yangu ya mwanzo sikuwa na mshahara wa kihivyo.

Basi huku tukiishi maisha fulani ya unga nusu na robo, siku moja tukiwa kwenye Chakula Cha usiku mke wangu alivunja ukimya.

Mume wangu, mume wangu, baba Jackiiiiiii, si nakuita wewe au?

Aliuliza,

Si kwamba nilikuwa simsikii hapana Bali macho yangu yalikuwa kwenye TV ambapo yeyote angedhani labda naangalia kwa makini kinachoonesha kile, kumbe Mimi naitathmini TV yangu ilivyo kubwa yaani naona hii nikiuza sikosi laki nane Hadi milioni.

Ni TV flani za mtumba hakika kama ni TV niliipata.

Naam mke wangu, teh teh nikijichekesha.

Mke wangu aliniangalia huku akionesha kukasirishwa ila hakusema chochote kibaya

Mume wangu Mimi hapa Nina mambo mawili nataka tuzungumze,

Nikamwashiria kwa kichwa kwamba aendelee,

Akasema, jambo la kwanza hapa ni kuhusu huyu dada wa kazi, ni mtu mzuri, ana tabia nzuri na ni mchapakazi lakini tuna miezi minne Sasa hatujampa haki yake, mbaya zaidi hatuna matarajio atapewa posho yake lini, alisisitiza mke wangu.

Nikawa nimekaa kimya.

Akaendelea jambo la pili, mimi ni mjamzito..

Enheeeeeeeeeeeeeeeeeeehh

Unasemaje?

Itaendelea.....
 
Unashangaa Nini?

Yaani kusema Nina ujauzito, unashangaa hivyo, au unahisi siyo ujauzito wako aliongeza.

Hapana, hapana mke wangu ni taarifa sikutarajia kuipokea, nafurahi kusikia hivyo imepita miaka mingi takribani sita tangu tupate mtoto wetu wa kwanza, nadhani ni muda muafaka kabisa wa wewe kubeba ujauzito.

Ahaaa, mimi nilifikiri umepokea kivingine, hayo tuachane nayo, hujanijibu kuhusu huyu dada wa kazi, alihoji mke wangu.

Hilo siyo tatizo sana kwakuwa umetambua hali halisi ya hapa nyumbani ni uamuzi sahihi

Tunaweza kumruhusu aende, mimi namtakia Kila la kheri.

Lakini vipi kuhusu stahiki zake maana Mimi Sina kitu kabisa msimu huu, tunamruhusu vipi bila kumlipa? Niliuliza.

Hilo usijali mume wangu, nina akiba yangu ambayo itatosha kumpa haki yake yote, kwahiyo kilichobaki ni sisi tumuite asubuhi tumwambie ajiandae na safari.

Sikuwa na neno zaidi ya kumuahidi ifikapo asubuhi tutamuaga ndugu yetu, tayari kuianza safari.

Usiku wa siku hiyo nilichelewa sana kupata usingizi, nikitafakari mambo mbali mbali hususani ugumu wa maisha, nawezaje kuishi bila kazi ya uhakika, halafu

Hivi wanawake ni watu wa aina gani?

Anyway siyo wote, lakini mke wangu mbona ananifanyia makusudi anabebaje mimba kwenye kipindi ambacho nahubiri na kuhubiri ni jinsi gani hii riziki ninayopata ni kwa mbinde, nikijihusisha na udalali ambao niligundua lazima uvae moyo wa dhuluma ili ufanikishe mambo yako.

Halafu, ananiambia habari za ujauzito huku anataka kumtoa dada wa kazi, yaani mke wangu hafikirii kuwa kipindi akiwa na ujauzito wa mtoto wa kwanza ndiyo tulianza kuwatafuta Hawa wadada wa kazi, nilifikiria sana.

Sawa pointi yake ya kumruhusu Ina mashiko Tena sana, ndiyo tutamlipa Nini? Habari za kupelekana serikali za mitaa sijui polisi, ndo kuaibishana huku. Acha aende tu, nilijisemea.

Asubuhi ilifika, dada wa kazi asiyejua nini kiliongelewa Jana, nikawa namuona akiwa kwenye majukumu yake ili watu wapate kifungua kinywa kwa siku ile.

Basi, baada ya kupata breakfast, dada wa kazi aliitwa, Mimi simuongeaji, kwakuwa sikumleta Wala sijasema aondoke Bali Kila kitu anaratibu mke wangu, mimi ni msimamizi wa familia nzima hili ndiyo jukumu langu.

Mke wangu akavunja ukimya kwa kumueleza yule dada, nini anatakiwa kufanya na taratibu zingine ziendelee.

Cha ajabu dada wa kazi alishauri hizo hela nusu zitumwe nyumbani kwake na nusu zibaki, siyo na yeye

Zibaki tuzitumie wote kama familia na yeye hayupo tayari kuondoka,

Mimi na mke wangu tuliangaliana huku Kila mmoja akitabasamu.

Itaendelea......
 
Shukurani

Ushauri
Andika iwe tayari kwenye mfano Word doc, ukija hapa ni copy and paste. Usifanye kuchelewa mwanzoni kuendelea kumbuka lengo ni unataka kusimulia yako na sio kusaka wasomaji na kupozi. Wasomaji watakuja tu, only hadithi ya Yoga ndio inavumilika kuisubiria iendelee.
 
Shukurani

Ushauri
Andika iwe tayari kwenye mfano Word doc,ukija hapa ni copy and paste. Usifanye kuchelewa mwanzoni kuendelea kumbuka lengo ni unataka kusumulia yako na sio kusaka wasomaji na kupozi. Wasomaji watakuja tu, only hadithi ya Yoga ndio inavumilika kuisubiria iendelee.
Hapana mkuu ni majukumu mengine yanakwamisha kitu isifike kwa wakati

Subira ni muhimu.
 
Nilicheka kivivu, huku nikijiona Kuna kitu nimepoteza, why mpaka housemaid naye anataka pesa zibaki ili zitusaidie, si dharau hii.

Halafu mbona mke wangu, hakumwambia kuwa hatuna hela ya kumlipa, bali alimwambia sababu zingine tu.

HAPANA nilimwambia dada wa kazi kwamba Kama anatuma atume hela zake zote huko kwao Kisha yeye abaki tutaishi na mke wangu akakubali kuwa abaki si kasema anaweza kukaa bila kupewa posho yake, sawa tutaishi kuwa na amani mdogo wangu hatukuwa na lengo la kukufukuza, alimalizia mke wangu.

Lakini Mimi niliwaza tofauti, maana si kwa kupigika kule nakosa hata hela ya kumlipa huyu dada, hapana lazima nifight nihakikishe huyu hakai hapa bure kama alivyodai hata kama kwao inaonesha kuna maisha magumu zaidi lakini hatofanya kazi bure hapa kwangu.

Hela yake ya miezi minne nikiwa na kazi, si nilikuwa nikipita kwenye baa ya mshikaji wangu Shedrack nilikuwa naikata masaa mawili tu.

Lazima nitamlipa, nilijisemea.

Kama kawaida Sina kazi ya maana, nilikotuma maombi siitwi hata kwenye usaili, nikaona kweli shetani akiamua anaweza.

Mbona nikiwa na kazi yangu ndiyo kwanza mabosi wakawa wananitafuta, Leo hii jiji Zima hili sionekani wakati nikijiwazia hayo simu yangu ikaita kucheki jina ni mshikaji wangu shedy,

Nikaipokea,

Oy babuu mbona unalala tena, we Jana tuliongea Nini?

Unajua wewe, lazima ukubali kuwa kwasasa ile kazi yako huna Tena na ukikubali hutopata taabu kuliko kukaa ukijiliza kwa mkeo.

Alibwata sana,

Hiyo ndiyo salamu mwanangu, niliuliza.

Salaam kitu gani kaka kama ukitaka kusalimiwa pita maeneo ya shule za kayumba utachoka wewe tu.

Wahi bwana, akakata simu.

Nilihisi kudharauliwa, Shedy ni mshikaji wangu hakusoma kabisa yeye ni form four failure lakini yupo vizuri kimaisha, shughuli zake kubwa ni udalali na anapata hela kiasi Cha kumiliki vimiradi vidogo vidogo vingi huko pembeni ya mji.

Lakini pia ana bonge la baa hapa mjini, ndiyo sehemu yangu kubwa kipindi hicho kabla sijajivika ulokole kwa muda.

Lakini pia, Mimi naheshimika pale kwake, hata akiongea na Mimi jambo huwa mstaarabu, Leo hii ananikoromea?

Kama ni pata pesa tujue tabia yako,

Kwangu ikawa,

Kosa pesa ujue tabia zao.

Nilichukua mkoba wangu, huku kichwani Nina bonge la kapelo ili kuzuia watu wasinijuejue.

Hatimaye nikatimba ile sehemu nikamkuta Shedy yupo na washikaji kibao ambao ndiyo wenye Mali, ilikuwa ni gari ya mizigo aina ya Scania pulling 113.

Almaarufu one one three.

Nikawa nipo nipo tu, sijui biashara zinaendaje, basi nikavuta kiti nikakaa nikisubiri nipewe maelekezo,

Maana gari si yangu, kwamba nauza. Mimi Sina hela kwamba nanunua, nikawa nafikiria kila siku tunafanya udalali, lakini ya Leo kali.

Oyaa bro, unawaza Nini hapo, njioy huku basi yule jamaa kashafika, changamka basi au unafikiri unagonga mihuri kuidhinisha wakandarasi hapa.

Yule dogo akanikejeli.

Basi Shedy akanifuata na kusema,

Unajua ndugu yangu wee huna kazi ila nimekuita ili na wewe uwe sehemu ya huu mgao lakini kifupi huna majukumu makubwa kwenye hii ishu.

Nikamshukuru tu maana hata hivyo bado alikuwa na utu

Nikaingia ndani, nikakuta kuna watu wanne sura ngeni, kumbe ndiyo mabosi wenyewe wakiwa na fundi wao wa kujiridhisha kama chombo kizima ili biashara ifanyike.

Nilichogundua kwenye zile biashara usimwamini mtu, wale jamaa wakamwambia Shedy kwa gari iwashwe ili wasikie muungurumo lakini aingie yule fundi wao aendeshe waangalie namna ya uingiaji wa gia
Kama zinaingia zote.

Basi mshikaji wangu Shedy akaniambia Sasa hiyo ndiyo kazi yako na wewe muongozane na huyo fundi wao ili uwe ni sehemu ya wataoleta mrejesho

Basi wanaume bila kuzubaa tukaingia kwenye gari kule mbele kukiwa kuchafu maana inaonekana waliipaki tu huko yard

Aisee yule fundi alichangamka kichizi huku akionekana muongeaji sana,

Sikia mwanangu hii gari ni majanga ni hamna kitu hamna mipira, anaongea huku anaendesha ujue,

Sikia, sikia hii clutch haimalizi ujue, yaani gia zinaingia kiugumu.

Lakini gia namba nne ndiyo haiingii kabisaa, lakini mwanangu lazima tutengeneze pesa, tukitoka hapa tukawaambie gari ni nzima haina tatizo, dili likitiki nitakupa laki mbili.

Nikaona mbona freshi Haina shida nikamkubalia lakini nikawaza isije ukasifia kitu usichokijua, halafu wakakwambia uwaoneshe kinafanyeje kazi si ishu hiyo.

Tukarudi kuleta mrejesho,

Bahati nzuri wale mabosi wanunuzi walimwamini sana fundi wao, ambaye Mimi niliye Kaa naye dakika kumi tu nilijua huyu ni jipu.

Tukaisifia gari biashara ikafanyika, Tena bila longolongo.

Mambo ya documents na taka taka zote zihusuyo hiyo gari wakapewa.

Macho yangu yapo kwa yule mchizi, maana Shedy hawezi kunidhulumu si aliniita mwenyewe lakini huyu fundi aliyekosa uaminifu.

Bahati nzuri akaniita pembeni hakuna watu akanipa laki mbili cash huku akionekana ana burungutu ...jamani maisha haya, nilimshukuru sana yaani ilikuwa Kama mchezo wa kuigiza.

Watu tukasambaratika huku hata mshikaji wangu shedy akiwa hajui kama Nini mia mbili pembeni,

Angejuaje, na kwa nini ajue.

Itaendelea.........
 
TAHADHARI: zipo simulizi nyingi sana humu pia tumesha soma simulizi nyingi humu kuna watu wa kila aina wakosoaji , wasifiaji, jitahidi sana wende kwenye point


Naamini utakutana na changamoto za kukosolewa tafadhali kama umeamua kutupa simulizi focus kwanye simulizi
Cjajua mda wako ila pia jitahidi walau kwa siku usiache kutupa walau episode moja

Mwisho kabisa kila simulizi lazma itakuwa na kasoro moja au zaidi tafdhali sana kosoa kistarabu kama utaona ni chai wacha sisi tunywe
Maana tuna vitafunwa visivyo na chai au kama wew pia una chai lete wanywaji tupo ijapokuwa kukosolewa ni sehemu ya burudani nawasilisha
Kwanza hii si chai, pili ondoa Shaka mkuu sibabaishwi na mitazamo ya watu wengine
 
Baada ya biashara kufanyika na mimi nishazisunda mfukoni zile mia mbili, Shedy akaniambia tuondoke mpaka kwenye baa yake, tukawakuta wahindi wawili ambao walionekana kusubiri sana, wakataka kumaindi lakini tabasamu la Shedy likawafanya washushe Presha zao.

Akaingia kwenye gari la wale jamaa, kama dakika kumi hivi alitoka huku wao wakitoa gari lao,haooo wakaishia, kimbembe Sasa, ikawa zamu yangu kusubiri.

Unajua bwana, hela ni hela tu, pesa ni pesa wakuu, jamaa yangu akawa kabadilika sana, muda ule mkali mkali hasa kwa wafanyakazi wake Kila kitu amri kwa kwenda mbele.

Ubabe ubabe mwingi, nikawaza kwanini asinitoe mimi niondoke yaani ni Bora hata hii laki mbili angekuwa kanipa yeye kwa maisha yangu inanitosha kabisa.

Nikavumilia nikaona basi, kama kukosa nikose tu ila lazima nikamuage.

Maana huko ndani inawezekana kashasahau kama Daniel nipo nje, kabla sijainuka nipige hatua nikamuona anaashiria niende upande alipo yeye, kufika pale zikaanza swaga, mara oh samahani kwa usumbufu, mara jamaa yangu ni Kama una mkosi umekuja siku mbaya.

Huwezi amini biashara imefanyika lakini sivyo nikivyotarajia yaani kile Cha juu kimeingia kiasi kidogo sana.

Sema Nini mwanangu we vumilia tu, litakuja dili lingine utapata pesa.

Wakati huo Mimi namwangalia tu, ningefanyaje, akanipigisha sound kibao na stori za hapa na pale huku Kila Mara akipiga na kupokea simu ambazo zilikatisha maongezi yetu Mara kwa Mara.

Sikumlaumu, wala sikushtuka binadamu ndivyo tulivyo hakuna, lazima nipambane na hali yangu siyo kulaumu wengine, baada ya kumaliza maongezi yake kwenye simu akachomoa pesa ambazo tayari alizihesabu huko huko akanipa.

Bila kuhesabu niliweka mfukoni
Nikamshukuru sana

WEMA hulipwa kwa WEMA

Tuliagana na safari ya kurudi nyumbani ikaanza huku nikitafuta mahali pazuri ili nihesabu zile pesa nijue ni shilingi ngapi,

Laki tano taslimu ndiyo nilizozipata kutoka kwa mshikaji wangu.

Ameniambia hiki ni kidogo au chochote kitu, mbona ni nyingi hizi kwani yeye kapata shilingi ngapi
Anyway sipaswi kujua.

Hapo nikawa na jumla na laki saba, nikapitia dukani kufunga vyakula na nafaka zote ili nisije tia aibu kama hapo awali.

Nikashika njia ya kurudi nyumbani nikiwa walau robo ya furaha,

Huku nilifikiria jinsi watu wanavyoendesha kazi zao ili maisha yaende yaani udalali unahitaji uwe muongo sana, ndiyo lile gari kama watu wangesema ukweli pengine lisingechukuliwa.

Lakini bado licha ya kupata hela bado hii ni kamari, yule aliyenunua chombo pindi kitakapomsumbua ni lazima lawama nyingi zitaelekezwa kwako wewe uliyewaaminisha, hali itakayopelekea kukosa uaminifu na wasikutumie tena.

Ni hatari sana, hii si Kazi, kazi gani hii nitawezaje kulipa mkopo mkubwa niliochukua kwaajili ya ujenzi wa nyumba, kazi gani watu mmemaliza fresh lakini unaanza kumsujudia binadamu mwenzio kisa tu ye ndiyo mwenye mpango mzima.

Lazima nitafute kazi ya uhakika nilijisemea,

Kitambo fulani nikawa nishafika nyumbani nikipokelewa kwa uchangamfu fulani na mke wangu ambao si wa kawaida, kabla sijafanya chochote nikapitiliza hadi bafuni nikajimwagia Kisha nikatulia.

Kabla hata sijapata Chakula mke wangu alinionesha barua,

Yes ni barua kutoka kampuni fulani hapa nchini, ni barua nimeiona Ina Nini ndani.

Tukutane sehemu ijayo........
.
 
Baada ya biashara kufanyika na Mimi nishazisunda mfukoni zile mia mbili, Shedy akaniambia tuondoke mpaka kwenye baa yake,tukawakuta wahindi wawili ambao walionekana kusubiri sana ,wakataka kumaindi lakini tabasamu la Shedy likawafanya washushe Presha zao,

Akaingia kwenye gari la wale jamaa, kama dakika kumi hivi alitoka huku wao wakitoa gari lao,haooo wakaishia,kimbembe Sasa,ikawa zamu yangu kusubiri,

Unajua bwana,hela ni hela tu,pesa ni pesa wakuu, jamaa yangu akawa kabadilika sana,muda ule mkali mkali hasa kwa wafanyakazi wake Kila kitu amri kwa kwenda mbele.

Ubabe ubabe mwingi, nikawaza kwanini asinitoe Mimi niondoke yaani ni Bora hata hii laki mbili angekuwa kanipa yeye kwa maisha yangu inanitosha kabisa,

Nikavumilia nikaona basi,kama kukosa nikose tu ila lazima nikamuage ,

Maana huko ndani inawezekana kashasahau kama Daniel nipo nje.kabla sijainuka nipige hatua nikamuona anaashiria niende upande alipo yeye, kufika pale zikaanza swaga,Mara oh samahani kwa usumbufu,Mara jamaa yangu ni Kama una mkosi umekuja siku mbaya

Huwezi amini biashara imefanyika lakini sivyo nikivyotarajia yaani kile Cha juu kimeingia kiasi kidogo sana .

Sema Nini mwanangu we vumilia tu .litakuja dili lingine utapata pesa

Wakati huo Mimi namwangalia tu,ningefanyaje ,akanipigisha sound kibao na stori za hapa na pale huku Kila Mara akipiga nakupokea simu ambazo zilikatisha maongezi yetu Mara kwa Mara .

Sikumlaumu ,Wala sikushtuka binadamu ndivyo tulivyo hakuna ,lazima nipambane na hali yangu siyo kulaumu wengine , baada ya kumaliza maongezi yake kwenye simu akachomoa pesa ambazo tayari alizihesabu huko huko akanipa.

Bila kuhesabu niliweka mfukoni
Nikamshukuru sana

WEMA hulipwa kwa WEMA

Tuliagana na safari ya kurudi nyumbani ikaanza huku nikitafuta mahali pazuri ili nihesabu zile pesa nijue ni shilingi ngapi,

Laki tano taslimu ndiyo nilizozipata kutoka kwa mshikaji wangu,

Ameniambia hiki ni kidogo,au chochote kitu,mbona ni nyingi hizi kwani yeye kapata shilingi ngapi
Anyway sipaswi kujua,

Hapo nikawa na jumla na laki saba,nikapitia dukani kufunga vyakula na nafaka zote ili nisije tia aibu kama hapo awali.
Nikashika njia ya kurudi nyumbani nikiwa walau robo ya furaha,

Huku nilifikiria jinsi watu wanavyoendesha kazi zao ili maisha yaende yaani udalali unahitaji uwe muongo sana,ndiyo lile gari kama watu wangesema ukweli pengine lisingechukuliwa,

Lakini bado licha ya kupata hela bado hii ni kamari ,yule aliyenunua chombo pindi kitakapomsumbua ni lazima lawama nyingi zitaelekezwa kwako wewe uliyewaaminisha .hali itakayopelekea kukosa uaminifu na wasikutumie tena,

Ni hatari sana,hii si Kazi, kazi gani hii nitawezaje kulipa mkopo mkubwa niliochukua kwaajili ya ujenzi wa nyumba, kazi gani watu mmemaliza fresh lakini unaanza kumsujudia binadamu mwenzio,kisa tu ye ndiyo mwenye mpango mzima.

Lazima nitafute kazi ya uhakika nilijisemea,

Kitambo fulani nikawa nishafika nyumbani nikipokelewa kwa uchangamfu fulani na mke wangu ambao si wakawaida, kabla sijafanya chochote nikapitiliza hadi bafuni nikajimwagia Kisha nikatulia,

Kabla hata sijapata Chakula mke wangu alinionesha barua,

Yes ni barua kutoka kampuni fulani hapa nchini.ni barua nimeiona Ina Nini ndani.

Tukutane sehemu ijayo........
.
Daah mwamba utanifanya niwe nakusumbua kila wakati
 
Nilitulia, nikapata chakula fresh huku nikiwa na shauku nini kipo kwenye ile barua

Nikaifungua nikaisoma nikawa nimeelewa, ni moja ya kampuni mpya ambazo nilituma maombi miezi miwili iliyopita, kwahiyo ni barua ya wito ikiwa inanitaka nifike kwenye kampuni zao ili taratibu zingine ziendelee.

Nikapumzika, Kisha nikamwita mke wangu,

Enhee habari za hapa,

Ni nzuri sisi tumeshinda salama kabisa mume wangu ila nina mazungumzo kidogo na wewe maana hapa nilipo hali yangu nishakueleza tangu jana, kwahiyo nafikiri ni muda muafaka wa Mimi kuanza kuhudhuria kliniki mapema.

Lakini mume wangu mbona hii taarifa tangu jana hata leo ,naona upo mbali sana, kwanini?

Nipo mbali kivipi, umeniambia upo hivyo ile Jana nimekubali, umeniambia kuhusu habari za kliniki, Mimi sijakupinga!!!!

Ulitaka nifanyeje labda, ulitaka niruke ruke kama wanandoa waliokaa miaka ishirini bila kupata mtoto.

Kwamba pindi nisikiapo hii kauli nishituke? Sisi siyo wagumba mke wangu tumshukuru MUNGU kwakuwa wazima kwahiyo taarifa hiyo haijanishtua, kifupi nimefurahi sana, mahari yangu naona inalipa haikupotea bure, nilitania wote tukacheka.

Basi sawa mume wangu, mimi nimekuambia ili ujue kuwa humu ñdani una mgonjwa tayari, huku akiinuka kuelekea nje.

Nilikaa kitambo pale ndani nikichezea chezea simu huku sijui hata nabonyeza button kwa malengo gani maana nilishachoka, huku nikijiwazia.

Dunia ya Sasa, inahangaika kutengeneza uzazi wa mpango wa kila namna ikiwa ni njia ya ku decrease population ya watu.

Maana tupo wengi mno lakini kumekuwa na milipuko kadha wa kadha ikiwemo Ebola inayowapukutisha watu huko Afrika magharibi, wajuaji wanasema pengine ni mpango wa wazungu katika kupunguza watu.

Lakini pia Nina marafiki wengi ambao wapo vizuri kimaisha lakini ndoa zao zinayumba sababu zikiwa kutopata watoto, na ni kweli, mbona hata rafiki yangu Shedy haelewani na mkewe japo yeye ndiye mtuhumiwa kwamba mimba zinaharibika, watoto wanakufa Mara tu baada ya kuzaliwa, huku lawama zikikaa kishirikina zaidi kwamba jamaa anaua watoto ili nyota ing'ae na kupush biashara zake.

Walimwengu bwana.

Pengine hata haiko hivyo, nilijisemea

Yote kwa yote acha mke wangu azae hata akizaa watoto kumi nipo tayari. Nikainuka nikatoka nje nikawakuta mke wangu na dada wa kazi wanacheka huku wakionesha wanafuraha sana.

Nikawapita, nikaona ngoja hata niende sehemu nikapige stori, huyoo mpaka kwa fundi TV mmoja hivi ambaye vitu vyangu vingi hurekebisha yeye pindi vikisumbua.

Aaaa karibu kaka, karibu sana, ilibaki kidogo nikupigie yaani ni kama MUNGU kasaidia wewe ufike hapa,

Aliongea yule fundi,

Yule jamaa aliyekuwa anataka TV kubwa ananisumbua bwana maana yule bwana ana Banda la kuonesha mipira, kwahiyo alikuwa anahitaji screen kubwa ili kuleta ushindani, maana wateja wamekuwa wakimtukana kwa kwamba TV zake ni ndogo kama side mirror, kwahiyo inamuwia vigumu sana.

Na hela kaka ipo ana mia tano Cash, halafu kaka ile TV yako kubwa mno, yaani kuuuuuuubwa kama nani za projector ni Bora uuze halafu utafute TV fulani ndogo ndogo na Kuna mama mmoja wa kipemba anayo TV anauza yaani ni nchi 21 ila kizuri balaa anauza laki tatu tu.

Kwahiyo ungeuza yako, bado ungebakiwa na hela nyingi tu ha hahaaa akajichekesha.

Baada ya kimya Cha muda mrefu nikamjibu siuzi.

Aaaaa kaka huuzi vipi wakati ulisema mwenyewe na Mimi tayari Kila kitu kipo sawa na hela kaniachia laki tano hizi hapa, sawaa hata Kama kakuachia hela Mimi siuzi TV, tubadilishe hizo stori.

Mara Kuna pikipiki kubwa likatia timu. Oyaaa fundi vipi bwana hadi saizi TV bado au hiyo laki nane umeenda kumuonesha kwanza mkeo ili ajue una hela teh teh yalicheka majamaa, huku nikiwaza kumbe angepata chajuu laki tatu nzima, siyo mbaya mjini hapa lazima ujiongeze.

Fundi akawa anajiumauma maana hata kuwatajia kwamba, ni huyu hapa mwenye TV asingesema, maana dili litabuma. Wanaweza kuongea na mimi yeye asipate chochote.

Nikamuaga fundi huyo nikaelekea sehemu nyingine bado akawa anapiga simu kunishawishi, isingekuwa hivyo niuze TV yangu mwenye nilivurugwa tu na maisha Hadi nikaropoka kuiuza lakini siyo siwezi kuuza.

TV toka Australia niliyopewa zawadi na wazungu sababu ya kuwasaidia wasipelekwe jela baada ya kujikanyaga kwenye serikali ya JK.

Wakakosa hela ya kunilipa ikabidi waniachie vitu vyao ikiwemo tv, ni kama tuzo, kwenye ushindi wa super star, nani auze tuzo?

Njaa tu hizi kuziendekeza,

Jioni nikarudi nyumbani huku nikiwa na hamu ile tarehe ya wito iwe hata kesho, wakati sijaingia hata ndani wale jamaa waliokuwa wanataka TV nilioonana nao pale kwa fundi japo sikufahamiana nao, wakatia timu wakiwa na yule fundi.

Itaendelea............
 
Baada ya wale jamaa kutia timu nyumbani kwangu,kijihasira kikaanza kuninyemelea,kwakuwa nilishajua lengo lao.

Hivi huyu fundi ni mtu wa aina gani,mtu gani asiyeelewa? Ndiyo,?! Lazima mtu akikataa Chake ujue kakataa kuendelea kubembeleza inakuwa kero itakayosababisha ukahisiwa vingine. niliwaza sana.

Kaka,kamkubwa samahani bwana kwa usumbufu,tumerudi tena.aliongea yule fundi huku akijichekesha chekesha.

Kwani wanataka nini hawa?
Kuna usalama kweli hapa mume wangu? Nikamjibu,

Hakuna shida ngoja tuwasikilize,

Oy, bro eeh unajua nini babu mwanaume ukiamua kunyoosha jambo lako fanya kweli, wee umemwambia mwanetu kuwa una chombo unataka kusukuma,mkakubaliana ile fresh yaani, Sasa tumesikia unarusha yaani ile sitaki nataka,

Mchizi hapa alikuambia anatembea kilomita miatano au vipi,wee ukaona ni karibu,ni vyema ukafu....ukafunguka unataka kilomita ngapi ziongezeke,usikae kinyonge tiririka mwamba.

Aliongea kijana mmoja ambaye, haya majani mabaya yanayokatazwa na serikali,ni kama yanalimwa nyumbani kwake.

Kwa kifupi nilishakasirika,

Sikia wewe fundi,kuzoeana na wewe isiwe sababu ya wewe kuja kila unapojisikia hapa nyumbani kwangu,halafu unaleta watu design tofauti tofauti Mimi siwajui, heshima na Imani ninakupa wewe ndiyo maana huwa unafika kwangu Kila unapohitajika,kwahiyo nakuomba uondoke hapa hakuna biashara Mimi na wewe,

Halafu hivi,mbona hujiheshimu huyooooo mpaka uwanjani kwa watu kwahiyo hi fence kutomalizika ndiyo kigezo Cha nyinyi kujikuta mnaweza kufika muda wowote ule .nilibwata.

Baada ya kuona hapa maelewano hakuna wakaondoka bila kuaga wale wengine huku huyu fundi,akiniomba msamaha ambapo kwa muda huu sikuwa nakamatika,Kila mtu akawa ananiogopa,ikabidi yule fundi naye aondoke maana hali ya hewa ilishakuwa mbaya.

Twende ndani mume wangu,aliongea mke wangu Huku akiwa akinitazama kwa woga,maana tangu anijue sijawahi kuwa wa moto hivyo mbele yake,akawa ananiangalia sana , nikamwita kwa ishara ya kufumba na kufumbua kiganja, taratibu akaja mpaka pale kwenye kiti nilipokaa.

Usiogope mke wangu ni lazima kuweka mipaka,kwa baadhi ya watu ili kulinda heshima na hadhi yetu ,si Kila mtu lazima kuzoeana naye,

Au nimekosea mke wangu,?

Siwezi sema umekosea, au umepatia kwakuwa sijui chanzo Cha ugomvi wenu mume wangu.ni vyema ukanieleza Nini kilitokea.....

Nikamueleza Kila kitu tangu mwanzo mpaka nawapiga mkwara siku hiyo.

Lakini mume wangu,wewe uliwatamanisha sana, kwamba unauza Mali yako wakawa na Imani kuwa muda si mrefu watapata bidhaa,kifupi umewachanganya ndiyo maana wakafika hapa,

Ila kiukweli sijapenda,stahili waliyokuja nayo Mimi nikajua unadaiwa ,maana maisha tunayoishi tunayajua wenyewe.

Alisisitiza.

Mke wanguuuuu,yaani hata Kama nadaiwaaaa,ndiyo nidaiwe na wale wavuta bangi ,

Haaaaaa Dani my husband usiseme hivyo,hapa unajiona una maisha magumu lakini unaweza kushuka zaidi ya hapa ukajikuta wale ndiyo kampani yako.

Ila ni kweli mke wangu, tuachane na hizo stori naona kama unanitisha.niliongeza.

Siyo tuachane na hii stori,kwanza kwanini ulitaka kuiuza hii TV bila kushauriana ma mimi,najua Mimi hapa kwako Sina nachomiliki.mwenzangu ulisoma kwa kiasi fulani Mimi sikusoma.

Uliuza pikipiki bila kunitaarifu au kushauriana na Mimi,nilisikitika moyoni lakini sikuwa na namna ni vitu vyako kwanini nihoji,

Umeuza vitu vidogo vidogo vingi tu,sikuulizi,siyo kwamba siwezi Bali naepusha maneno madogo madogo

Najivunia kuwa na wewe mume wangu,Kila unachokileta ama kukitafuta huwa nafurahi na kukuombea uzidi kupata zaidi huku nikiringa na kutamba kuwa na mume Bora,ulinioa miaka nane nikiwa kwenye uyatima wa kukosa wazazi wote wawili,lakini baada ya kuolewa na wewe nikajikuta, nimepata mfariji,mlezi,baba wa watoto wangu na la mwisho nimepata mume mwema,

Leo hii,unauza vitu vidogo sana bila kuniambia,unadhani utaniambia kwenye mambo makubwa!

Una Mashamba lakini una hii nyumba
Na siku zote najivunia kuwa na wewe ni mpambanaji,naamini Sina Cha kukulipa zaidi ya kukuzalia watoto.

Najua kuwa hata hiki kiumbe kingine kilichoko tumboni mume wangu hujapenda lakini nikwambie tu kuwa najua ni wajibu wangu,kukuzawadia watoto ili ukuze jina lako mume wangu.

Mmmmmmmh mume wangu ipo siku utauza hii nyumba,Tena baada ya kuwa ushaanza udalali baada yakuwa huna kazi,na sifa za madalali nazijua wakikosa vya kuuza, huuza hata vitu vyao,

Hamna mke wangu, kamwe siwezi kuuza nyumba,.niliropoka,

Na nikiuza,au ukisikia tu tetesi za kuuza nipeleke mahakamani.

Nani akupeleke mahakamani,Daniel Mimi Sina huo muda,wa kugombania Mali sizizo kuwa zangu,we ukiuza utakuwa umeuza Mali zako.aliongea huku akilengwa na machozi,nilimuhurumia nikamkumbatia,muda huo hata sikuwa na Cha kumwambia zaidi ya kuona aibu tu,tulikumbatiana kitambo mpaka tuliposhituliwa na sauti ya dada wa kazi,

Akiita DADAA,!!!!!!.....

Itaendelea.........

Usichoke huu ni utangulizi tu mambo mazuri yanakuja.
 
Back
Top Bottom