Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Simulizi: Mimi na Boss Wangu

SEHEMU INAYOFUATA.....

Aaaamh samahani dada vipi Kuna tatizo? aliuliza dada wa kazi,

Hakuna,alijibu mke wangu Huku akiinuka pale ili waende usawa wa jikoni akamsikilize zaidi.

Nilitulia pale sebuleni huku nikicheka peke yangu,,

Leo hii ni Kali sana aiseeh yaani mke wangu kaniita jina kabisa,ndiyo naitwa Daniel,lakini yeye hajazoea kuniita hivyo Leo kakasirika tena sana,ila afadhali katema nyongo maana inawezekana alikuwa nayo haya muda mrefu .

Ila ni kweli maana Kila alichoongea si kibaya,halafu..,

Kumbe kajua kuwa kubeba kwake ujauzito sikufurahi,,ni kweli lazima hili nitalikataa katakata.

Ni kweli nilifikiria hivyo lakini hapaswi kujua kama sijapenda.

Usiku wa siku hiyo,hakukuwa na stori kama tulivyozoea,ila ile saa kumi na moja alfajiri nikiwa Sina usingizi niligundua hata mke wangu naye Hana usingizi,

Nikavunja ukimya.

Mke wangu,akaitika

Hivi unanipenda?

Hivi mume wanguuu,samahani lakini tuna Kuna vitu vingi vya kuviongelea usianze na habari sijui nakupenda sijui nini,hizi habari ziache kwenye matamthilia huko .alijibu

Nikaona ohooo naianza siku vibaya hii,Bora hata ningepiga kimya,

Wewe ni mume wangu na Mimi ni mkeo hatuna haja ya kukumbushana vitu vilivyokaa kitoto kama hivyo,Mimi na wewe hatuko kwenye mahusiano.

Bali tuko kwenye NDOA ,tunaitumikia ndoa tuliyokula kiapo kanisani Mimi na wewe kwamba tutavumiliana kwenye shida na raha,Kuna vilima na mabonde,kama zilivyo nyakati za mvua na jua.

Nikaona nisharikoroga hapa,nikamjibu

Siyo hivyo mke wangu Mimi nakupenda ila Kuna jambo umenisingizia Jana,limeniumiza sana,

Jambo lipi Hilo? alidakia

Ni kuhusu ujauzito wako, unadai eti sijapenda jambo ambalo si kweli,mke wangu kwani uwaze tofauti,?

Alicheka kidogo Kisha akaendelea,

Sikia mume wangu,Mimi najua unanipenda sana,na kitendo Cha Mimi kushika ujauzito,si kwamba hujafurahia,ila ulishituka kwasababu ya nyakati unazopitia,

Laiti ungekuwa na kazi yako halafu nikahisi hivi pengine ingeniwia vigumu kutambua,lakini wewe umetishwa na vile ambavyo huna kazi ya uhakika,lakini nikwambie tu mi nakuombea Kila kitu kitakaa sawa kwa upande wako tena tutaishi kwa furaha kama mwanzo, na safari hii huyu mtoto atakuwa wa kidume,

We umejuaje, niliuliza

Hakukuwa na majibu zaidi ya vicheko kwa Kila mmoja.

Tuliamka huku maandalizi ya kwenda kanisani yakiwa yamepamba moto,

Mume wangu vipi,naona upo nyuma nyuma kulikoni,

Huendi kanisani,tena ujue huu ndiyo muda wa wewe kuwa karibu na kanisa,kule Kuna maombi mbalimbali unaweza kuungana na wengi wenye matatizo Tena Leo Kuna maombi
Maalumu kwa wenye uhitaji na wewe kwangu naona ni WA muhimu mno.

Nilicheka sana,

Hivi nahitaji kuwa karibu na kanisa au kuwa karibu na MUNGU.niliuliza

Ohooo ushaanza,si tunatangulia huwa siyawezi maswali yako.wakaondoka wakiniacha mwenyewe,akili ikiwaza ifike siku ya kesho jumatatu nikaitike wito wa barua yangu.

Nani aende kanisani, Mimi hahahaaa ngoja kwanza,Mimi nimebatizwa utotoni baba yangu alikuwa Katekista kabla hajaacha kutokana na uzee akaona apumzike,Mimi ni mbatizwa wa tangu utotoni,nikapata kitubio na kipaimara nikiwa shule ya msingi,

Kutokana na mzee kuwa maarufu nikawa kiongozi tangu nikiwa primary sekondari mpaka chuo nilikuwa na rundo la uongozi.

Nimezunguka mikoa mingapi Mimi kwenye matamasha,makongamano na semina mbalimbali huku safari nyingi zikijaa kujitolea zaidi ya hela za mfukoni ndiyo zaidi.
Mbaya zaidi ikaja kuibwa hela ya harambee na nikawa mtuhumiwa Mimi wakati siyo muhasibu Wala mweka hazina,

Walinionea sana halafu,licha ya kubadilisha kanisa japo ni like lile catholic bado Nako nilikula za uso nikituhumiwa na jamaa mmoja kuwa natembea na mke wake jambo ambalo si kweli

Mpaka alipogundua yeye mwenyewe kuwa si Mimi wakati mambo yashaharibika, anyway mke wangu ana haki ya kuniambia hivyo yuko sahihi kabisa.

Lingine ni michango,michango,michango naamini nikienda huko itakuwa kero tu maana hata jumuiya waliyoipa jina linalofanana na Mimi nimeitelekeza kulingana na kuwa bize na mambo yangu zaidi.

Ah wewe nitasimangwa huko tukashikana mashati bure maana vichwa vyenyewe vimepata moto halafu mtu akakuulize maswali huko si mnaweza kugombania bure?

Acha niweke mambo yangu vizuri huko nitaenda tu,

Mwenyezi MUNGU nisamehe mja wako nakiri Mimi ni mwenye dhambi.

Nikainuka baada ya kujikumbusha mengi yahusuyo kanisani ,yalitosha kabisa kuona Mimi sipaswi kwenda kanisani kana kwamba kanisa ni night club Tena V.I.P.

Itoshe kusema kwa siku hiyo,shetani alishinda,Tena tatu bila.

Nikaingia ndani nizisabahi suti zangu huku nikiwa makini kwamba lazima nitafute nguo itakayonipendeza lakini itabidi nisipendeze zaidi kuliko wao mabosi japo sijui watavaaje,lakini Nina uzoefu mkubwa kwenye hizi mambo unaweza kukosa kazi kwenye jambo dogo,halafu usijue Nini kilisababisha mpaka unaingia kaburini.

Kumbe labda ulikuwa more than smarter,ni hatari sana.

Nikaona pia ni muda wa kwenda saloon nikapunguze hizi ndevu ,khaaaa wewe nakua kama mwigizaji ambaye anataka uhalisia kwenye movie zake,nilizugazuga pale home nikiwa karibu na PC yangu ili kujikumbusha Documents fulani

Maana sipaswi kuwa mzembe ,wakati najiandaa kutoka nielekee saloon,ilisikika hodi .ni sauti ya mke wangu,najua akiwa na wageni huwa anabisha hodi akiwa mbali ili kama mtu upo vibaya,...
...hili linaeleweka kwa Kila mtu.

Nikawakaribisha ndani, mke wangu,dada wa Kazi na mgeni wa kike ambaye sura haikuwa ngeni,kama naliwahi kumwona sehemu,vijana wanaita pisi Kali yes, ni pisi yaani unaweza kuapa nakuweka nadhiri kwamba kwa Sasa sitaki ukaribu na wanawake na kuwa bize na mambo yangu,nakwambia usije kuapa hivyo utakufuru

Ukaja pata LAANA bure.

Kuna watu wameumbika jamani yaani,namlaumu mke wangu unamletaje mtu kama yule ndani kwako hata Kama ni kwa maongezi ya dakika tatu?

Itaendelea..........
 
SEHEMU INAYOFUATA.....

Aaaamh samahani dada vipi Kuna tatizo? aliuliza dada wa kazi,

Hakuna,alijibu mke wangu Huku akiinuka pale ili waende usawa wa jikoni akamsikilize zaidi.

Nilitulia pale sebuleni huku nikicheka peke yangu,,

Leo hii ni Kali sana aiseeh yaani mke wangu kaniita jina kabisa,ndiyo naitwa Daniel,lakini yeye hajazoea kuniita hivyo Leo kakasirika tena sana,ila afadhali katema nyongo maana inawezekana alikuwa nayo haya muda mrefu .

Ila ni kweli maana Kila alichoongea si kibaya,halafu..,

Kumbe kajua kuwa kubeba kwake ujauzito sikufurahi,,ni kweli lazima hili nitalikataa katakata.

Ni kweli nilifikiria hivyo lakini hapaswi kujua kama sijapenda.

Usiku wa siku hiyo,hakukuwa na stori kama tulivyozoea,ila ile saa kumi na moja alfajiri nikiwa Sina usingizi niligundua hata mke wangu naye Hana usingizi,

Nikavunja ukimya.

Mke wangu,akaitika

Hivi unanipenda?

Hivi mume wanguuu,samahani lakini tuna Kuna vitu vingi vya kuviongelea usianze na habari sijui nakupenda sijui nini,hizi habari ziache kwenye matamthilia huko .alijibu

Nikaona ohooo naianza siku vibaya hii,Bora hata ningepiga kimya,

Wewe ni mume wangu na Mimi ni mkeo hatuna haja ya kukumbushana vitu vilivyokaa kitoto kama hivyo,Mimi na wewe hatuko kwenye mahusiano.

Bali tuko kwenye NDOA ,tunaitumikia ndoa tuliyokula kiapo kanisani Mimi na wewe kwamba tutavumiliana kwenye shida na raha,Kuna vilima na mabonde,kama zilivyo nyakati za mvua na jua.

Nikaona nisharikoroga hapa,nikamjibu

Siyo hivyo mke wangu Mimi nakupenda ila Kuna jambo umenisingizia Jana,limeniumiza sana,

Jambo lipi Hilo? alidakia

Ni kuhusu ujauzito wako, unadai eti sijapenda jambo ambalo si kweli,mke wangu kwani uwaze tofauti,?

Alicheka kidogo Kisha akaendelea,

Sikia mume wangu,Mimi najua unanipenda sana,na kitendo Cha Mimi kushika ujauzito,si kwamba hujafurahia,ila ulishituka kwasababu ya nyakati unazopitia,

Laiti ungekuwa na kazi yako halafu nikahisi hivi pengine ingeniwia vigumu kutambua,lakini wewe umetishwa na vile ambavyo huna kazi ya uhakika,lakini nikwambie tu mi nakuombea Kila kitu kitakaa sawa kwa upande wako tena tutaishi kwa furaha kama mwanzo, na safari hii huyu mtoto atakuwa wa kidume,

We umejuaje, niliuliza

Hakukuwa na majibu zaidi ya vicheko kwa Kila mmoja.

Tuliamka huku maandalizi ya kwenda kanisani yakiwa yamepamba moto,

Mume wangu vipi,naona upo nyuma nyuma kulikoni,

Huendi kanisani,tena ujue huu ndiyo muda wa wewe kuwa karibu na kanisa,kule Kuna maombi mbalimbali unaweza kuungana na wengi wenye matatizo Tena Leo Kuna maombi
Maalumu kwa wenye uhitaji na wewe kwangu naona ni WA muhimu mno.

Nilicheka sana,

Hivi nahitaji kuwa karibu na kanisa au kuwa karibu na MUNGU.niliuliza

Ohooo ushaanza,si tunatangulia huwa siyawezi maswali yako.wakaondoka wakiniacha mwenyewe,akili ikiwaza ifike siku ya kesho jumatatu nikaitike wito wa barua yangu.

Nani aende kanisani, Mimi hahahaaa ngoja kwanza,Mimi nimebatizwa utotoni baba yangu alikuwa Katekista kabla hajaacha kutokana na uzee akaona apumzike,Mimi ni mbatizwa wa tangu utotoni,nikapata kitubio na kipaimara nikiwa shule ya msingi,

Kutokana na mzee kuwa maarufu nikawa kiongozi tangu nikiwa primary sekondari mpaka chuo nilikuwa na rundo la uongozi.

Nimezunguka mikoa mingapi Mimi kwenye matamasha,makongamano na semina mbalimbali huku safari nyingi zikijaa kujitolea zaidi ya hela za mfukoni ndiyo zaidi.
Mbaya zaidi ikaja kuibwa hela ya harambee na nikawa mtuhumiwa Mimi wakati siyo muhasibu Wala mweka hazina,

Walinionea sana halafu,licha ya kubadilisha kanisa japo ni like lile catholic bado Nako nilikula za uso nikituhumiwa na jamaa mmoja kuwa natembea na mke wake jambo ambalo si kweli

Mpaka alipogundua yeye mwenyewe kuwa si Mimi wakati mambo yashaharibika, anyway mke wangu ana haki ya kuniambia hivyo yuko sahihi kabisa.

Lingine ni michango,michango,michango naamini nikienda huko itakuwa kero tu maana hata jumuiya waliyoipa jina linalofanana na Mimi nimeitelekeza kulingana na kuwa bize na mambo yangu zaidi.

Ah wewe nitasimangwa huko tukashikana mashati bure maana vichwa vyenyewe vimepata moto halafu mtu akakuulize maswali huko si mnaweza kugombania bure?

Acha niweke mambo yangu vizuri huko nitaenda tu,

Mwenyezi MUNGU nisamehe mja wako nakiri Mimi ni mwenye dhambi.

Nikainuka baada ya kujikumbusha mengi yahusuyo kanisani ,yalitosha kabisa kuona Mimi sipaswi kwenda kanisani kana kwamba kanisa ni night club Tena V.I.P.

Itoshe kusema kwa siku hiyo,shetani alishinda,Tena tatu bila.

Nikaingia ndani nizisabahi suti zangu huku nikiwa makini kwamba lazima nitafute nguo itakayonipendeza lakini itabidi nisipendeze zaidi kuliko wao mabosi japo sijui watavaaje,lakini Nina uzoefu mkubwa kwenye hizi mambo unaweza kukosa kazi kwenye jambo dogo,halafu usijue Nini kilisababisha mpaka unaingia kaburini.

Kumbe labda ulikuwa more than smarter,ni hatari sana.

Nikaona pia ni muda wa kwenda saloon nikapunguze hizi ndevu ,khaaaa wewe nakua kama mwigizaji ambaye anataka uhalisia kwenye movie zake,nilizugazuga pale home nikiwa karibu na PC yangu ili kujikumbusha Documents fulani

Maana sipaswi kuwa mzembe ,wakati najiandaa kutoka nielekee saloon,ilisikika hodi .ni sauti ya mke wangu,najua akiwa na wageni huwa anabisha hodi akiwa mbali ili kama mtu upo vibaya,...
...hili linaeleweka kwa Kila mtu.

Nikawakaribisha ndani, mke wangu,dada wa Kazi na mgeni wa kike ambaye sura haikuwa ngeni,kama naliwahi kumwona sehemu,vijana wanaita pisi Kali yes, ni pisi yaani unaweza kuapa nakuweka nadhiri kwamba kwa Sasa sitaki ukaribu na wanawake na kuwa bize na mambo yangu,nakwambia usije kuapa hivyo utakufuru

Ukaja pata LAANA bure.

Kuna watu wameumbika jamani yaani,namlaumu mke wangu unamletaje mtu kama yule ndani kwako hata Kama ni kwa maongezi ya dakika tatu?

Itaendelea..........
Arostoooo
 
SEHEMU INAYOFUATA....

Niliwakaribisha wageni huku nikikimbilia chumbani nibadilishe nguo maana nilizovaa wala hazikuwa rafiki kwa wakati ule,

Nikarudi sebuleni huku mke wangu akiwa anaelekea jikoni nadhani kutoa maagizo fulani kwa dada wa kazi ili tu Kila kitu kiwe sawa.

Karibu mdogo wangu,alikaribisha Tena mke wangu,

Ahsante dada,ahsante sana, hakika MUNGU ni WA ajabu,ametukutanisha Tena wasaa na muda kama huu,itoshe kusema ahsante yesu kwa kutupa kibali Cha kuungana na familia hii ahsante Yesu kwa kutupa nguvu na uvumilivu wa kufika mahali nasema roho mtakatifu akakae Kila pembe ya hii nyumba,

MUNGU wewe ni mwema,alipotea Yusuf kijana mtanashati na kipenzi Cha baba yake,lakini kwa ukuu wako ulimuinua na kuwa mkuu katika taifa la misri,nasema MUNGU turudidhie Kila anayekata tamaa na kuhisi ametengwa na Dunia mfanye ajione mpya na mwenye nafasi na umuhimu kwenye Dunia hii.

Nimalize kwa kusema Yesu wa Nazareth fungua milango ya BARAKA na neema mahali hapa,

Akaendelea kuongea lugha ambayo sikuijua,wanaita kunena kwa lugha sijui,huku mke wangu akiwa na tabasamu muda wote,

Hatimaye akajitambulisha,japokuwa tangu anaingia nilishamkumbuka vizuri sana tu

Naitwa ESTA ni mkristo ambaye tangu utotoni nilikuwa Roman Catholic lakini kwasasa nimehamia sehemu mpya,ambako anapatikana Yesu aliye hai.

Ni kweli namfahamu,ni mwanamke namfahamu miaka mingi,alikuwa ni muimbaji namba moja kwenye kwaya ya Mt.Don Bosco ni mwanamke ambaye aliwafanya wenye pesa zao na wakware kusali kanisani kwetu huku wakiwa na lengo moja kumpata ESTA lakini wengi waliishia kugombana wao kwa wao,huku mwanamke akiwa bize na Yesu,labda pengine kwa kuwa hakuwa mwenye maisha magumu

Mimi mwenyewe nilimsarandia sana,tumia mbinu nyingi bado sikufanikiwa,hata alipokuja kuomba kazi ofisini kwetu nilitumia nguvu na pesa nyingi ili apate kazi hata pale ambapo hakuwa na sifa ni clear Kila kitu,lakini msimamo wake,ukawa ni thabiti,licha ya kuwa nilihangaika lakini ndani ya miezi mitatu akawa kashatafutiwa kazi ya maana hapa mjini,huku akiwa anatembelea gari ya kisasa kabisa wakati huo ,

Hali iliyofanya nikate tamaa na kuhamishia nguvu kwa mtu mwingine ambaye tunaitana mume na mke Hadi leo.

Ni ESTA huyu ambaye taratibu alipunguza ile Ari ya kuja kanisani,huku baadhi ya vyeo alivyokuwa nao wakipewa watu wengine,kubwa zaidi ni pale ambapo Kuna jamaa alikuwa anafunga NDOA kipindi hicho tukiwa kwenye kamati tukaona list ya magari yatakayo tumika hayatoshi tukaenda kuomba msaada wa kumuazima gari ndugu yetu, muumini mwenzetu,

Matusi tuliyopata sitosahau,na ndiyo ukawa mwisho wa yeye kukanyaga kanisani pale.

Ndiyo,ni ESTA ambaye alikula Bata sana na bwana wake ,nchi gani hakufika,alibadilika akawa mlevi wa kutupwa,kutoka kuimba sauti ya kwanza kanisani huku kanisa Zima likizizima mpaka kuwa muimbaji club akiwa anawaimbia watu nyimbo za akina Madonna huku sauti ikiwa imejenga urafiki na pombe kwa kiasi kikubwa mno.

Ni ESTA aliyezalishwa watoto mapacha bila ndoa,huku wale watoto baada ya mwezi mmoja wote wakipotea katika mazingira ya kutatanisha.

Baada ya furaha ikageuka huzuni inayoishi,huku huyo bwana wake akihusishwa na upotevu wa wale watoto, masikini ESTA hakuwa na sehemu ya kushitaki ,angethubutu vipi , jamaa alikuwa mtu mzito huku ESTA akitimuliwa na kunyang'anywa Kila alichopewa,alilia akalia na kulia.

Halafu imsaidie nini,ikabidi aukimbie huu mji ambao Kila kitu kizuri ,kinapatika,ukijichanganya tu,utaona Kila kitu kibaya kinapatikana hapa na si kwingine.

ESTA akaukimbia huu mji ikawa ndiyo mwisho wa kumuona tena.

Lakini Leo anakuja kwangu,akiwa Mpole na ni mtumishi wa MUNGU,

Dah ama kweli yaani sikuizi Dini zimekuwa biashara yaani kahama kanisa lake,kahamia kwenye ulokole, eti Kuna Yesu aliye hai,huyu atanifundisha nini mimi,

Masikini mke wangu,yeye hamjui huyu halafu anamwita mdogo wake,huyu ESTA mkubwa sana tu sema tu vile ni baby face,

Mume wangu, naam,

Mbona umejiinamia hivyo una mawazo gani,? yaani nakuona unasinzia kabisa .

Labda mr.ana uchovu,niliisikia sauti ya ESTA ikiongeza,

Aaaa h samahani jamani,ni mawazo ya hapa na pale,

Usijali Mr,yaani shemeji huyu dada (mke wangu) kanieleza mambo mengi kuhusu wewe hata hivyo kilichonisikitisha ni wewe kutokuwa mshirika kanisani,lakini niseme tu bado hujapotea,hata mwana mpotevu mwenyewe alirudi kwa baba yake na akasamehewa,

Niseme tu bado una nafasi shemu,alizungumza huku akijifanya hanijui,hatujuani huku mke wangu akiwa na furaha, jinsi mwenzie anavyotema madini,

Kiufupi Kila nikimwangalia ESTA alizidi kunivutia nikijiapiza kuwa nikipata nafasi moja tu, safari hii hachomoki lazima niambulie,

Tena anaonekana kapungua ule mwili yaani kazidi kuwa mzuri,halafu eti anakuja kunihubiria nyumbani kwangu,anihubirie nini huyu Mimi

Nilijisemea moyoni,

Huku nikiwaza namna ya kuwapiga chenga ili niende kwenye mambo yangu kwa ajili ya kujiandaa na usaili wa kesho,ila sijui niombe namba kabisa , nilijisemea

Chakula kililetwa tukajumuika mchana ule tukala huku furaha ikitawala ñdani yetu,

Masikini Mimi,nilimuwaza sana ESTA

Nikasahau kuhusu magonjwa ya zinaa na ukimwi.

Itaendelea.......
 
Hii ni simulizi ya kweli ya maisha yangu,ila majina yanayotumika humu ni ya kufikirika,ndiyo maana sitaji hata location mbali mbalimbali ili watu wasiunganishe matukio

Simulizi haiko kwaajili ya mtu kujitambulisha Bali ni kufundisha,kuelimisha na kuburudisha

Mambo mazuri yanakuja Kila siku usikose kufuatilia
 
Usiseme kitu kwanza subili amalize
IMG_20220604_102556.jpg
 
SEHEMU INAYOFUATA..... ..

Tulimaliza kula Chakula muda ule Kisha nikamuita mke wangu chumbani ili tuongee jambo na nimuage kuwa natoka.

Hapana mume wangu, unataka kwenda wapi,huyu mgeni Leo yupo na sisi ili tu tutafakari neno kwa pamoja, kwahiyo sioni sababu ya wewe kutoka, alisisitiza mke wangu

Nyamaza wewe,tena unyamaze unajua fika kuwa kesho Nina enda kufanya usaili sehemu,halafu na wewe unaniletea ratiba zako nisizo jua,halafu huyo mgeni wako nimemsikia anasema umemueleza Kila kitu kuhusu matatizo yangu,

Kwanini mambo yangu yawe mabango Kila mtu ajue,nani kasema umwambie? Nilifokaa

Hapana mume wangu,alianza yeye kutaja matatizo yako Hadi nikashangaa anapajua mpaka ulipokuwa unafanyia kazi mwanzo,hivi mume wangu kwa mfano ukakutana na mtu anayeonesha anaifahamu zaidi familia yetu,na ni mtumishi we ungefanyaje? Tumsikilize mume wangu pengine ni mtu aliyetumwa kuiokoa familia hii,

Nilicheka sana, nikamwambia
Pole sana ,kama ni kwasababu kakwambia hayo mambo ndiyo umlete hapa, Hawa ni matapeli tu kama wale wanaotafuta viewers na followers kinguvu,Hana maajabu huyo kifupi Mimi sikai hapa,Nina mambo yangu,

Sawa mume wangu,alijibu kinyonge.

Nikarudi sebuleni,nikamkuta ESTA yupo bize na vifungu kwenye biblia,

Shemu, Mimi nawaacha kidogo Kuna dharula imejitokeza.

Haaaaaaaa shemu wangu,unajua ujio huu ni wako?

Najua, najua shemeji
lakini niendako ni muhimu zaidi,hata hivyo nashukuru kwa ujio wako naona nyumba na familia nzima tumebarikiwa kwa kweli,na wewe MUNGU akubariki na akutie nguvu,kwa huduma nzuri unayoitoa

Huku nikijichekesha kinafiki,

Amina shemeji ubarikiwe,alijibu

Nikaingia mtaani nikaweka setup ya mambo yangu,nikarudi nikiwa tayari na kamili,

Siku ya kesho ilifika,nikapokelewa vizuri mno,tofauti na nilivyofikiri , hakukuwa na longolongo nikawa bado Mimi kuanza kufanya, japo kwa hapa ilikuwa ishu ni mshahara ikiwa umeachana Mara mbili zaidi,yaani ulikuwa mdogo mno ni kama asilimia 47 nzima ya mshahara ilipungua,

Lakini bado nilikuwa na furaha kubwa kwakuwa maisha ninayoishi ni ya kuunga unga mno,Leo unapata milioni nzima unafurahi halafu unakaa miezi minne Bila kuingiza kitu chochote ndiyo umefanya nini,

Nikaona ni Bora ajira Ina heshima yake na ipo kwenye mifumo rasmi inayotambulika,na hata hivyo mbona huu mshahara bado mkubwa sana tu naweza kuendesha vizuri kabisa maisha yangu, mambo mengine yatakuja tu,

Lakini Ukiwa na kazi ni rahisi kuonekana sehemu nyingi, kwahiyo hii ni nafasi nzuri sana tu,nikarudi home nikampa feedback mke wangu tukafurahi wote.

Nilipinga kazi pale huku waajiri wangu wakitambua kuwa navijua vitu vingi ikabidi, nipelekwe saiti nikafanye fanye research namna kazi inavyoenda kule,

Kweli nilifanya kazi kwa umakini na uaminifu huku nijitahidi kuepuka mitego ya kuja kumfukuzisha mtu kazi kwahiyo nikawa timamu zaidi,nilirudisha majibu ofisini yakapokelewa vizuri huku wakinipongeza kwa mengi niliyoyabaini ambayo hata wao hawakuyapata kabla.

Kutokana na uaminifu wangu yule boss mkuu akawa yupo karibu na Mimi kiasi Cha kunipeleka Hadi nyumbani kwake kunitambulisha kwenye familia yake,wakafurahi sana lakini pia boss ni mtu wa kusafiri sana kwahiyo kazi zake zingine asipokuwepo yeye alikuwa ana ratibu mke wake.basi maisha yakaendelea kama kawaida kama mjuavyo wakati wa JK mambo ya dili yalikuwa mengi sana kwahiyo sehemu niliyokuwepo ikawa na majaribu ya kutosha tu huku nikijitahidi kukwepa

But siku moja nilipigiwa simu na HR mmoja ambaye yupo upande wa saiti akanieleza kuhusu mpango fulani ambao ni dili ya maana na tutapata pesa ya maana kama tungefanikisha.

Nilimkatalia katakata.

Unajua Nini msomaji,kwenye tenda za barabara huwa Kuna utekelekezaji wa vifaa vingi yaani (equipment) kwahiyo Kuna kimoja hicho kilikaa muda Hadi majani yakawa yamefunika kabisa,

Yeye akaona kiuzwe,lakini nilimkatalia,huku nikimkumbusha kuwa siyo tabia nzuri, lakini ajue Kila kitu kipo kwenye record kiwe kimeharibika au vipi ajue tu kuwa hivyo vyote vinatambulika,

Alinimaindi sana,nikawa nishapata mgomvi wa kwanza kwenye kampuni hiyo mpya kwangu.

Maisha yaliendelea huku changa moto ndogo ndogo zikiwa ni sehemu ya kazi,lakini siku moja tulibaini upungufu fulani kwenye vifaa vyetu ikiwa ni spares muhimu ambayo tuliitafuta hapa mjini tukaikosa,

Akafikiria kuiagiza nje ni gharama zaidi,lakini pia itachukua muda kufika hapa, akaona wazo zuri ni kwenda kuichukua huko mkoani ambako Kuna vifaa havina kazi kwahiyo ni vyema ikafunguliwe ije huku.

Akatafutwa fundi akapewa maelekezo, na bosi akaona mtu wa kuongozana na fundi ni mimi,

Nilifurahi sana,tena sana, unajua kwanini,

Ni kwamba naenda mkoani sehemu nilipozaliwa,tena ni kijijini kwangu kabisa walipo wazazi wangu,ambao baada ya Mimi kuwa Sina kazi ni kipindi kirefu Sasa sijaenda nikaona hii ni nafasi muhimu sana kwangu,

Kitu pekee nilichokuwa nimekigundua ni yule fundi kuwa kivyake vyake sana,hata boss alilijua Hilo ,akaniambia ,

Najua huyu hapendi kuongozana na wewe, lakini ni lazima iwe hivyo kwasababu tabia za mafundi zinajulikana anaweza kwenda kufungua hata vitu ambavyo hajatumwa kwa masilahi yake binafsi.ni rahisi kuwarubuni walinzi kwa visenti kidogo ili tu,afanikishe mipango yake

Nikaona huu si mtihani huu, anyway Kila mtu na habari zake Mimi nitahakikisha nakuwa naye bega kwa bega kisipungue hata kimoja tofauti na kifaa kilichoagizwa.

Unajua Nini msomaji,ukiniuliza

Uchawi ni Nini sitakujibu,kwakuwa sijui Wala sijui unafanyaje kazi na unatengenezwaje,

Lakini uchawi upo,tena kuna watu ni wachawi sana,

Itaendelea....
 
SEHEMU INAYOFUATA.......

Tarehe 17 mwezi wa kumi mwaka 2011 Mimi,boss na mke wa boss tulikaa kwenye hoteli fulani huku tukipata Chakula Cha pamoja ikiwa ni kuonesha upendo tu kwangu lakini kuagana tayari Mimi kwenda mkoani ,

Tulimaliza nikapewa pesa nyingi tu za kuacha nyumbani, dharula yaani nilikuwa full,hata ingekuwa kusafiri kwa flight nauli ingetosha ya kwenda na kurudi lakini nilichagua usafiri wa bus,huku nikipata taarifa kuwa yule fundi yeye kaenda Leo,

Nikajua yote hayo hataki kuongozana na mimi,

Nilikuja ubungo,nikakata ticket, Kisha nikampigia simu mke wangu,nimpe maelekezo kuwa sitarudi naunganisha tu maana nikisema nirudi, nyumbani ni mbali yaani pembeni kabisa ya mji kwahiyo nikachukua chumba lodge nikalala.

Kutokana na hizi kampuni za mabasi kuwa na ushindani mkubwa kwenye mwendo saa kumi na nusu tayari nilikuwa mkoani,nikapokelewa vizuri nikajitambulisha kwa watu wa ile yard wakaniambia taarifa zangu wanazo,lakini wakaomba vitambulisho wajiridhishe,nikafanya hivyo huku nikiwaambia kuwa Mimi ni mwenyeji wa mkoa ule na pale ndiyo maeneo ya nyumbani kwahiyo wasinione mgeni,

Mmoja akadakia kwa kusema siyo kweli mbona naonekana haiba yangu haifanani na watu wa mkoa ule,

Huyo ni muongo bwana,aseme ukweli mbona Mimi kabila langu ni ******** akataja kabila lake,maneno haya anayasema yule fundi aliyenitangulia jana.

Nikaona ni kawaida kwa mtu ambaye hakupendi ,atakukosoa na kukupinga kwa Kila jambo ili uonekane we hufai,lakini huyu ni mshamba nadhani pia umri wake ni tatizo ni kijana bado lakini pia hajafanya kazi sehemu nyingi ,pili hata hilo kabila alilolitaja kama si lake,maana ana mchanganyiko wa uarabu huyu si msomali huyu,any way pengine ni kabila lake,

Ikabidi baadhi waniongeleshe lugha ya pale ,hatimaye wakajiridhisha,nikawaambia hata hivyo Mimi ndiyo mwenyeji wenu maana wengi wenu siyo wa hapa tukataniana tukacheka,

Yule fundi kusikia vile akawa Hana la kufanya akawa Sasa yupo karibu na Mimi ananiongelesha na vijistori vya hapa na pale huku akiwa anainanga ile kampuni,

Yaani bro hili Chaka uliloingia siyo kabisa,hii siyo kampuni kaka,hebu fikiria we spea inawezekanaje ikosekane mjini ifatwe huku mkoani, ndiyo ujue jinsi yule boss alivyombahili yaani yule dawa yake ni moja,kumpiga tu (kumuibia)

Nikacheka kwakuwa nilishapewa taarifa kuwa yule HR na huyu fundi ni watu wa kuwaangalia sana,hata hivyo boss huwa hawafukuzi kazi sijui kwanini,

Nikamjibu,kwani wewe na mafundi wenzio si mmezunguka jiji Zima kutafuta spare mkadai hamjaiona,

Hamna bro,spea zipo ila bosi wako mkuda kinoma, aliona eti zinauzwa bei ya juu mno.

Nikamuona ni mpuuzi tu,nikamuaga kuwa Mimi nitalala nyumbani kwa wazazi wangu ili kesho nije tuendelee na kazi,Cha ajabu tulitumia karibu wiki nzima Kila akija anagusa gusa tu kwa madai ni ngumu kufunguka lakini pia ni inatakiwa itolewe kiutaalamu tusije haribu nikaona mbona Kama ananifanyia mchezo,

Hatimaye boss wa kike akaanza kupiga simu maana mume wake alishasafiri,alikuwa akilaumu mbona siku zinazidi kwenda na kazi zinakwama Mimi nikawa Kila lawama naielekeza kwa fundi Hadi alipotishiwa kuwa ataletewa fundi mwingine ,ndipo akaitoa.

Huku kwa ndugu zangu tuliongea mengi huku nikipewa baraka na kufanyiwa mambo ya kimila,japo si muumini sana wa mambo yale lakini lazima uheshimu taratibu ambazo unaelekezwa na wazazi

Unajua mwanangu Daniel una dharau sana wewe ndiyo maana mitihani haiishi kwako, Dunia hadaa ulimwengu shujaa mwanangu,alisema mama huku nikimpata kwa umakini mkubwa sana.

Kwakuwa pesa nilikuwa nayo nikawaachia kiasi fulani,huku nikipanga safari hii naenda kulala na ESTA mwanamke ambaye ningemuoa pengine na licha ya kuwa ni kama kachuja lakini bado ni mzuri sana tu,kwakuwa namba zake ninazo baada ya kuziiba kwenye simu ya wife ngoja nimpigie kabisa ili nikifika tu mjini nijue pa kuonana naye.

Nikampigia ,nikampiga sound nyingi sana japo kulikuwa na ugumu kutokana na misimamo ya kilokole lakini hakuwa ESTA wa zamani,ESTA huyu alikuwa na njaa,Tena alipigika hivyo asingechomoka kwa kile nilichomuahidi,

Kwakuwa bosi alisema yule fundi kazi yake ni kufungua tu,kuhusu kuisafirisha lilikuwa ni jukumu langu kwakuwa wale mafundi hawakuwa waaminifu,

Nikaipakia kwenye gari,nikihakikisha ipo salama kwenye ile buti,nikaagana na baadhi ya ndugu zangu huku wakiniombea Kila la kheri,huku njiani simu za ESTA zikawa nyingi kuliko za mtu yoyote yule,nikaona kumbe je,

Pesa ni sabuni ya roho vingi tunashindwa kuvipata shida ni umasikini.

Hatimaye tukawa Ubungo stand kuu,
Hapa Kuna kitu vitu wale wabeba mizigo kwenye toroli walinichanganya wakati mizigo inashushwa toka kwenye buti Mimi Niko bize na simu, ESTA kanichanganya.

Mzigo ukapakiliwa kwenye kitoroli Cha mtu mwingine,Mimi nikaomba mzigo wangu uwekwe stoo ili baadaye nitapiga simu ili gari ndogo ije kufuata yule dogo mbeba mizigo akaniambia si huu ndiyo unaenda stoo nikamjibu ndiyo,yaani chuma hiki nakiona kabisa,lakini alijichanganya akapewa mtu mwingine bila Mimi kujua.

Nilikuwa naweza kuufikisha mzigo vizuri tu,lakini tamaa za ngono ziliniambia nenda huku kwanza Kisha mzigo utapeleka tu,

Weeeeeee ningejua.....

Itaendelea.......
 
SEHEMU INAYOFUATA.......

Tarehe 17 mwezi wa kumi mwaka 2011 Mimi,boss na mke wa boss tulikaa kwenye hoteli fulani huku tukipata Chakula Cha pamoja ikiwa ni kuonesha upendo tu kwangu lakini kuagana tayari Mimi kwenda mkoani ,

Tulimaliza nikapewa pesa nyingi tu za kuacha nyumbani, dharula yaani nilikuwa full,hata ingekuwa kusafiri kwa flight nauli ingetosha ya kwenda na kurudi lakini nilichagua usafiri wa bus,huku nikipata taarifa kuwa yule fundi yeye kaenda Leo,

Nikajua yote hayo hataki kuongozana na mimi,

Nilikuja ubungo,nikakata ticket, Kisha nikampigia simu mke wangu,nimpe maelekezo kuwa sitarudi naunganisha tu maana nikisema nirudi, nyumbani ni mbali yaani pembeni kabisa ya mji kwahiyo nikachukua chumba lodge nikalala.

Kutokana na hizi kampuni za mabasi kuwa na ushindani mkubwa kwenye mwendo saa kumi na nusu tayari nilikuwa mkoani,nikapokelewa vizuri nikajitambulisha kwa watu wa ile yard wakaniambia taarifa zangu wanazo,lakini wakaomba vitambulisho wajiridhishe,nikafanya hivyo huku nikiwaambia kuwa Mimi ni mwenyeji wa mkoa ule na pale ndiyo maeneo ya nyumbani kwahiyo wasinione mgeni,

Mmoja akadakia kwa kusema siyo kweli mbona naonekana haiba yangu haifanani na watu wa mkoa ule,

Huyo ni muongo bwana,aseme ukweli mbona Mimi kabila langu ni ******** akataja kabila lake,maneno haya anayasema yule fundi aliyenitangulia jana.

Nikaona ni kawaida kwa mtu ambaye hakupendi ,atakukosoa na kukupinga kwa Kila jambo ili uonekane we hufai,lakini huyu ni mshamba nadhani pia umri wake ni tatizo ni kijana bado lakini pia hajafanya kazi sehemu nyingi ,pili hata hilo kabila alilolitaja kama si lake,maana ana mchanganyiko wa uarabu huyu si msomali huyu,any way pengine ni kabila lake,

Ikabidi baadhi waniongeleshe lugha ya pale ,hatimaye wakajiridhisha,nikawaambia hata hivyo Mimi ndiyo mwenyeji wenu maana wengi wenu siyo wa hapa tukataniana tukacheka,

Yule fundi kusikia vile akawa Hana la kufanya akawa Sasa yupo karibu na Mimi ananiongelesha na vijistori vya hapa na pale huku akiwa anainanga ile kampuni,

Yaani bro hili Chaka uliloingia siyo kabisa,hii siyo kampuni kaka,hebu fikiria we spea inawezekanaje ikosekane mjini ifatwe huku mkoani, ndiyo ujue jinsi yule boss alivyombahili yaani yule dawa yake ni moja,kumpiga tu (kumuibia)

Nikacheka kwakuwa nilishapewa taarifa kuwa yule HR na huyu fundi ni watu wa kuwaangalia sana,hata hivyo boss huwa hawafukuzi kazi sijui kwanini,

Nikamjibu,kwani wewe na mafundi wenzio si mmezunguka jiji Zima kutafuta spare mkadai hamjaiona,

Hamna bro,spea zipo ila bosi wako mkuda kinoma, aliona eti zinauzwa bei ya juu mno.

Nikamuona ni mpuuzi tu,nikamuaga kuwa Mimi nitalala nyumbani kwa wazazi wangu ili kesho nije tuendelee na kazi,Cha ajabu tulitumia karibu wiki nzima Kila akija anagusa gusa tu kwa madai ni ngumu kufunguka lakini pia ni inatakiwa itolewe kiutaalamu tusije haribu nikaona mbona Kama ananifanyia mchezo,

Hatimaye boss wa kike akaanza kupiga simu maana mume wake alishasafiri,alikuwa akilaumu mbona siku zinazidi kwenda na kazi zinakwama Mimi nikawa Kila lawama naielekeza kwa fundi Hadi alipotishiwa kuwa ataletewa fundi mwingine ,ndipo akaitoa.

Huku kwa ndugu zangu tuliongea mengi huku nikipewa baraka na kufanyiwa mambo ya kimila,japo si muumini sana wa mambo yale lakini lazima uheshimu taratibu ambazo unaelekezwa na wazazi

Unajua mwanangu Daniel una dharau sana wewe ndiyo maana mitihani haiishi kwako, Dunia hadaa ulimwengu shujaa mwanangu,alisema mama huku nikimpata kwa umakini mkubwa sana.

Kwakuwa pesa nilikuwa nayo nikawaachia kiasi fulani,huku nikipanga safari hii naenda kulala na ESTA mwanamke ambaye ningemuoa pengine na licha ya kuwa ni kama kachuja lakini bado ni mzuri sana tu,kwakuwa namba zake ninazo baada ya kuziiba kwenye simu ya wife ngoja nimpigie kabisa ili nikifika tu mjini nijue pa kuonana naye.

Nikampigia ,nikampiga sound nyingi sana japo kulikuwa na ugumu kutokana na misimamo ya kilokole lakini hakuwa ESTA wa zamani,ESTA huyu alikuwa na njaa,Tena alipigika hivyo asingechomoka kwa kile nilichomuahidi,

Kwakuwa bosi alisema yule fundi kazi yake ni kufungua tu,kuhusu kuisafirisha lilikuwa ni jukumu langu kwakuwa wale mafundi hawakuwa waaminifu,

Nikaipakia kwenye gari,nikihakikisha ipo salama kwenye ile buti,nikaagana na baadhi ya ndugu zangu huku wakiniombea Kila la kheri,huku njiani simu za ESTA zikawa nyingi kuliko za mtu yoyote yule,nikaona kumbe je,

Pesa ni sabuni ya roho vingi tunashindwa kuvipata shida ni umasikini.

Hatimaye tukawa Ubungo stand kuu,
Hapa Kuna kitu vitu wale wabeba mizigo kwenye toroli walinichanganya wakati mizigo inashushwa toka kwenye buti Mimi Niko bize na simu, ESTA kanichanganya.

Mzigo ukapakiliwa kwenye kitoroli Cha mtu mwingine,Mimi nikaomba mzigo wangu uwekwe stoo ili baadaye nitapiga simu ili gari ndogo ije kufuata yule dogo mbeba mizigo akaniambia si huu ndiyo unaenda stoo nikamjibu ndiyo,yaani chuma hiki nakiona kabisa,lakini alijichanganya akapewa mtu mwingine bila Mimi kujua.

Nilikuwa naweza kuufikisha mzigo vizuri tu,lakini tamaa za ngono ziliniambia nenda huku kwanza Kisha mzigo utapeleka tu,

Weeeeeee ningejua.....

Itaendelea.......
mambo ya ngoswe haya
 
Hii ni simulizi ya kweli ya maisha yangu,ila majina yanayotumika humu ni ya kufikirika,ndiyo maana sitaji hata location mbali mbalimbali ili watu wasiunganishe matukio

Simulizi haiko kwaajili ya mtu kujitambulisha Bali ni kufundisha,kuelimisha na kuburudisha

Mambo mazuri yanakuja Kila siku usikose kufuatilia
Weee kumbee basi usipotee sana jack
 
SEHEMU INAYOFUATA...........

Nilizubaa zubaa pale stand ya ubungo,huku simu ikiwa inaita kwa fujo, lakini bado akili yangu ilitaka nionane ESTA kwanza,nikamalize haja zangu maana ,kutokana na ratiba zangu kubana.

Sioni muda mwingine nitakaopata,

Jamani Dani,umeniambia umeshafika,mbona muda unazidi kwenda ,fanya haraka bwana nataka niwahi kurudi,alisema ESTA upande wapili

Uwahi kurudi? kurudi wapi, Mimi nilitegemea nachukua logde tunalala,mpaka asubuhi,hayo mambo ya short time hayo bwana mi siwezi,sisi ni watu wazima mamaa,
Niliongea kwa sauti ya kukata tamaa,

Hapana Dani,natambua hilo lakini jua kuwa hata Mimi ni ratiba zangu ambazo sitakiwi kuzivunja,hata hivyo kumbuka nilikukatalia muda mrefu sana kuwa kwa Leo ratiba zimebana ukaniambia unahitaji masaa mawili tu ya kuwa na Mimi, iweje unanibadilikia unataka tulale,aliongeza ESTA

Nikaona dah,ni kweli nikiwa nambembeleza alikataa hata hivyo nikamuomba masaa mawili, yaani ni Kama maneno ya kutongozea , kumbe kashikilia hapo hapo, siyo mbaya hata Kama nusu saa lazima nikamvue nguo yule,

Simu ya mke wa boss iliingia,

Naam boss,nilisema hivyo baada ya kupokea

,niambie Dani umefikia wapi,hujaingia Dar es salaam bado?

Ah samahani boss gari nililopanda nilitegemea niingie saa kumi,hata hivyo liliharibika njiani lakini pia Kuna jamu tuliipata njiani foleni imechukua muda kifupi ndiyo naingia muda huu,

Jamani Dani my friend,tumetumia muda mwingi sana kusubiri hicho kifaa,na imani yetu wote,ipo kwako lakini mbona ni kama unatoka nje ya mstari,kiufupi fanya mpango hiyo spare ifike,kesho ipelekwe site

,alisema mke wa boss safari hii akiwa anaamrisha,

Nikaona dah mbona ishu ishakuwa ngumu nirudi kule store nifate spare Mara kuipelekaaaaaa,

Ah sinitafika nyumbani saa usiku wa manane Mimi,wakati nikiwaza hayo nikapokea simu yenye code number ya South Africa, nilitetemeka kidogo kwakuwa nilishajua,

Halooo,sauti ya bosi wa kiume ilisikika Mara tu baada ya kupokea simu,

Daniel, Daniel, Daniel nimekuita Mara tatu,sihitaji maelezo mengi,kifupi mbona unatupa wasi wasi? Alisema yule boss wa kiume.

Nilijitetea sana ,Tena sana kwamba spare ninayo na kesho asubuhi amtume dereva aifuate,hakujibu kitu lakini baada ya dakika tano nikapokea sms toka kwa boss boss mwanamke ikiwa inasomeka

"HATUKUELEWI"

Nikaona ni wasiwasi wao tu mbona Kila kitu kipo ok.

Nikampigia ESTA nimfahamishe kuwa tayari nakuja,

Naomba uwahi yaani sitalala maana nahitaji nirudi kikajiandae maana kesho Nina safari Tena ni ya lazima kwahiyo nakwambia kabisa ili usije kunibadilikia maana wanaume ndivyo mlivyo nyinyi.

Nikaishika barabara ya Sam nujoma kuelekea alipo yule ESTA.

Lakini wakati huo nikaona nimpigie wife maana tangu nipo kwenye gari ya mkoa niliongea naye saa nne asubuhi,nimeshuka kwenye gari naongea na watu wengine tu,

Ngoja niongee naye nimwambie gari imeharibika njiani kwahiyo sitafika Leo,

Mke wangu akapokea simu tuliongea mengi ya hapa na pale huku akinitaka niwe makini,

Lakini mume wangu,naomba ruhusa kesho nataka nimsindikize rafiki yangu mahali fulani,

Ni wapi unaenda,niliuliza

Akataja ni maeneo ya njia ya kilwa road kuelekea Mkuranga huko,

Nikauliza ni nani unampeleka,huko

Akajibu,

Ni yule rafiki yangu aliyekuja siku ile akajitambulisha kwa jina la ESTA,
Unajua Nini mume wangu yule ile siku anakuja pale nyumbani alikuwa na mambo mengi ya kuongea hata hivyo,we ulikuwa una haraka tu,ni kwamba yule ni muathirika anaishi na virusi vya ukimwi mwaka wa tatu Sasa hata hivyo yeye dozi yake huwa anachukulia hospitali ya..........(akaitaja hiyo hospital)

Kwahiyo Kuna ulazima gani wa wewe kwenda huko,niliuliza huku nilitetemeka baada ya kusikia habari inayomuhusu ESTA,kumbe nimwathirika huyu,nikaanza kumchukua ghafla kana kwamba yeye ndiye aliyenitongoza.

Mke wangu akaendelea,,

Hapana mume wangu,siyo kwamba lengo ni yeye tu hapana nahitaji kwenda kuangalia/kukagua Mashamba yetu ambayo Kila siku unanilaumu kuwa umenunua rasilimali za wote lakini nashindwa kuzifuatilia,nilimpongeza sana,huku nikishuka kituo Cha karibu kabisa nikighairi safari ya kwenda kwa ESTA baada tu ya kusikia habari hiyo mpya kwangu, kwahiyo alitaka kuniua huyu malaya nilitukana kimoyo moyo,

Nikampigia simu kuwa nimepata dharula kwahiyo hakuna uwezekano wa kuja Tena,akalaumu kiasi japo alinielewa.

Nikatafuta logde nyingine nikalala,

Asubuhi nilishitushwa na simu ya dereva wa kampuni akiwa anataka tukutane ubungo tuchukue kifaa chetu,

Muda wa saa mbili nikafika pale ubungo terminal nikimkuta dereva fulani mwenye lafudhi ya kimakonde akiwa kachangamka huku nikicheka chinichini alivyojipigilia suti yake iliyopauka na tai paana,haoooooo

Tupo store na wahudumu wa pale waliangalia vyumba vyote hatukuiona store pekua pekua na wewe hakuna kipindi hicho shati langu lote limeloa kwa jasho,ikabidi niwashirikishe maaskari waliokuwa kituo kidogo Cha mule ndani ,licha ya wale vijana kuhojiwa bado walidai ilikuwa ndani mulemule,

Nikaona mtihani huu, lakini yule dereva aliwaambia maaskari kuwa niwekwe chini ya ulinzi ikiwa ni maelekezo toka kwa boss wake,

Maaskari wakataka simu ipigwe kwa boss wajiridhishe,wakidai wananiwekaje chini ya ulinzi,wakati Mimi niliwakabidhi watu hiyo spare na waliokabidhiwa wanakiri waliipokea,lakini

Upande wa pili bosi alisema kuwa Hana uhakika kama kweli hao niliwakabidhi maana usumbufu niliuonesha tangu jana,huenda hao vijana wa matoroli wanajichanganya tu lakini spare hawakuipokea,

Watu wakapata pointi kuanzia maaskari Hadi wale vijana wasukuma matoroli wakanigeuka nikawa chini ya ulinzi rasmi.

Inaendeleaa usichoke..............
.,,,,
 
Back
Top Bottom