Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nashukuru sana mkuu !!!Shukran sana mkuu.
Tuko pamoja mkuu.
Tuko pamoja mkuuShukrani sana mkuu
amina mkuu, pamoja sanaaShukrani Sana mkuu....ubarikiwe [emoji120]
HONGERA KWA UTUNZI MAHIRI SANASEHEMU YA 55
Mida ya safari yatu ilipofika tulienda mpaka maeneo yale ambayo kuna mlango wa Muifufu, kwa kutumi mikono yake Mnaro akafanya kama anatanua kitu, na kweli kukaonekana uwazi ambapo alinitaka kupita, kisha na yeye akafuata kabla hapajajifunga tena. "mpaka sasa Magugi ameshajua kama nimeingia Muifufu, hivyo kuwa tayari kwa mapambano" alisema Mnaro nami nikalishika vizuri panga langu, tukaanza safari katikati ya pori tukiutafuta mji wa Muifufu. Tofauti na mara ya kwanza safari hii tulikuwa na nguo zetu, tofauti na ambavyo nilikuwa nikijua kuwa mtu akiingia Muifufu lazima nguo na vyote alivyokuwanavyo kabla vibaki nje. "mbona leo tumebaki na nguo zetu?" nilimuuliza Mnaro. "hata mimi sijui, labda ndo manufaa ya safari ya ujinini" alijibu Mnaro, tukaendelea na safari. Tulipokuwa tumetoka eneo la pori na kuanza kuingia eneo la mji ilisikika suti kubwa, sauti ile ilikuwa haitofautiani sana na na sauti ya honi ya meli ambayo inalia karibu na masikio ya msikilizaji. "hao wanaitana kwaaajili yetu, jiandae" alisema Mnaro. Baada ya dakika kama kumi lilionekna kundi kubwa la watu mbele yetu, wakikimbia kuja upande wetu, Mnaro akawakusanya kwa mkono wake na kuwatupa mbali, huku tukiendelea kwenda. Mbele kidogo tukaona mawe mkubwa sana yakitupwa kuja upande wetu, Mnaro akayazuia yakabaki yakielea hewani, tukamuona mrushaji wa mawe yale akiendelea kuyarusha, lilikuwa ni limtu kubwa sana ambalo lilionekana kuwa na nguvu nyingi mno, kwa kutumia upanga wangu nikakata mkono wake wa kushoto ambao alikuwa anautumia kurushia mawe, lakini likaanza kurusha na mkono wa kulia, kanibidi kuukata na huo. Jitu lile ambalo lilionekana kuwa na hasira likatimua mbio kutufuata, Mnaro akalitandika na yale mawe ambayo lilikuwa linarusha na kulibwaga chini baada ya sehemu kubwa ya mawe yale makubwa kulipata kichwani. Basi mwendo wetu ukawa wa kukutana na vikwazo njiani lakini tulivimudu. Tulipambana na wachawi wazee vijana, mpaka watoto wengine walisikitisha sana kuwaua kwani niliona kama hawakuwa na hatia maana walichokuwa wanakifanya ni kutokana na maamrisho ya Magugi, wengine hata akili zao hazikuwa sawa, lakini ilikuwa ni lazima kuwazuia kama sisi ulitaka kutimiza lengo letu na njia ya kuwazuia ilikuwa ni kuwauwa tu kwani maneno yetu yasingeweza kusikilizwa.
Tukaenda mwendo huo wa kupambana na vikwazo mbalimbali mpaka kwa Magugi, leo tena nyumba haikuwepo. "tayari ameificha nyumba, utafanyaje sasa" niliuliza kwa kukata tamaa. "fumba macho yako" alisema Mnaro ambaye nilipomtazama niligundua kuwa yakweke yalikuwa yamefumbwa tayari, nimi nikafanya hivyo na kushangaa naiona nyumba ya Magugi vizuri tu. Tukaenda moja kwa moja na kuingia mpaka ndani ambapo tulimkuta Magugi akiwa amekaa kwenye kiti chake na pembeni yake alikuwepo yule jini ambaye husimama pembeni yake siku zote, sikujua namna gani yeye aliacha kuonekna msaliti maana Magugi alidai kuujua mpango wetu wote wa kutoroka Muifufu, sasa kwanini huyu bado anamuamini ikiwa pia alinisaidia, nilijiuliza. "washughulikie wapumbavu hawa" aliamuru Magugi, jini yule akatembea kuelekea upande wetu, Mnaro akaandaa mikono yake kupambana naye lakini nikamzuia, jini yule akatuvuka na kutoka akituacha tumfanye Magugi chochote ambacho tungependa kumfanya. "mbio za sakafuni huishia ukingoni, leo ndo mwisho wa ufalme wako" alisema Mnaro, akaunyoosha mkono wake na kumkaba Magugi kamnyanyua miguu yake ikabaki ikining'ia kisha akamtembea naye akimtoa nje katika hali hiyo. Huko nje kulikuwa na watu wengi ambao walionekana kama walikuja kwaajili ya kupambana ila muonekano wa Magugi ukawafanya wakashikwa na bumbuwazi, wakabaki kuwa watazamaji tu. Mnaro akambwaga Magugi chini pale uwanjani, akasimama na kutaka kukimbia, alikuwa anachekesha maana alikuwa ni mzee na hakuwa na uwezo huo wa kukimbia. Manaro akamnyanyua na kumsogeza mpaka kwake,kisha akamkaba shingo kwa mikono yake kabisa, mara Magugi akatoa kisu kidogo na kumchomanacho Mnaro shingoni, Mnaro akayumba na kumuachia Magugi ambaye alijiandaa kumjeruhi tena kwa kisu chake, nikawahi na kukata mkono wa Magugi, japo nilikuwa mbali hilo liliwezekana kwa msaada wa panga lile la ajabu sumu iliyopo kwenye hiki kisu ni kali sana, huwezi kupona tunakufa wote, alisema Magugi kumwambia Mnaro amabye alikuwa ameshika shingo yake kuzuia damu iliyokuwa inachuruzika, nikajisikia hasira sana na kukata shingo ya Magugi, kichwa chake kikadondoka chini. Nikenda kumtizama Mnaro ambaye nguvu zake zilionekana kumpunga kila muda ulivyozidi kwenda. "yule mmoja wetu ambaye anakufa leo ni mimi" alisema Mnaro, nikakosa hata cha kujibu. Twende haraka nikakufungulie mlango, usije ukabaki huku.
Mwendo wetu wa polepole ukatufikisha mahali ambapo Mnaro hakuweza kutembea tena, akasimama na kuniangalia kisha akatabasamu na kusema "nakuonea wivu sana, wewe unapata kila ambacho unakitaka na hata usichokitaka, umemtaka mkeo umempata, umetaka maisha yako umeyapata, mwisho umepata na kumuua Magugi, jambo ambalo hukuwa hukulitaka ila mimi niliyeliaka sana nimelikosa pia". Nilikuwa namuonea huruma sana Mnaro, mwisho wake haukuwa wa kupendeza ila sikuwa na chakufanya, hata cha kusema tu nilikikosa pia, machozi yaliyokuwa yakinichuruzika yalitosha kuelezea hisia zangu. "siwezi kuendelea, hii sumu ni kali kweli, kimbia haraka nikufungulie mlango kabla sijakata roho" alisema Mnaro nami nikaamua kukimbia kuelekea ulipo mlango, ambapo hapakuwa mbali na pale alipokwamia Mnaro, akajikaza na kuutanua mlango, lakini nguvu zikawa zinamuishia na mlangu unaanza kujibana polepole, nikakaza mwendo na kufnikiwa kupita na baada ya hapo ukajibana kwa kasi, nadhani ndipo Mnaro alipoaga dunia.
Maisha yangu yalirudi kuwa kawaid, nina furaha nikiwa na mke wangu na mtoto wetu wa kiume ambaye tumemuita Mnaro, sasahivi ana mimba ya mtoto wa kike nadhani huyu tutamiita Sauda. Famila yetu imejikita kwenye uchamungu, kwani nimegundua kuwa chamungu ni silaha kubwa dhidi ya nguvu za giza.
Mwisho
Pseudepigraphas Simulizi
SEHEMU YA 55
Mida ya safari yatu ilipofika tulienda mpaka maeneo yale ambayo kuna mlango wa Muifufu, kwa kutumi mikono yake Mnaro akafanya kama anatanua kitu, na kweli kukaonekana uwazi ambapo alinitaka kupita, kisha na yeye akafuata kabla hapajajifunga tena. "mpaka sasa Magugi ameshajua kama nimeingia Muifufu, hivyo kuwa tayari kwa mapambano" alisema Mnaro nami nikalishika vizuri panga langu, tukaanza safari katikati ya pori tukiutafuta mji wa Muifufu. Tofauti na mara ya kwanza safari hii tulikuwa na nguo zetu, tofauti na ambavyo nilikuwa nikijua kuwa mtu akiingia Muifufu lazima nguo na vyote alivyokuwanavyo kabla vibaki nje. "mbona leo tumebaki na nguo zetu?" nilimuuliza Mnaro. "hata mimi sijui, labda ndo manufaa ya safari ya ujinini" alijibu Mnaro, tukaendelea na safari. Tulipokuwa tumetoka eneo la pori na kuanza kuingia eneo la mji ilisikika suti kubwa, sauti ile ilikuwa haitofautiani sana na na sauti ya honi ya meli ambayo inalia karibu na masikio ya msikilizaji. "hao wanaitana kwaaajili yetu, jiandae" alisema Mnaro. Baada ya dakika kama kumi lilionekna kundi kubwa la watu mbele yetu, wakikimbia kuja upande wetu, Mnaro akawakusanya kwa mkono wake na kuwatupa mbali, huku tukiendelea kwenda. Mbele kidogo tukaona mawe mkubwa sana yakitupwa kuja upande wetu, Mnaro akayazuia yakabaki yakielea hewani, tukamuona mrushaji wa mawe yale akiendelea kuyarusha, lilikuwa ni limtu kubwa sana ambalo lilionekana kuwa na nguvu nyingi mno, kwa kutumia upanga wangu nikakata mkono wake wa kushoto ambao alikuwa anautumia kurushia mawe, lakini likaanza kurusha na mkono wa kulia, kanibidi kuukata na huo. Jitu lile ambalo lilionekana kuwa na hasira likatimua mbio kutufuata, Mnaro akalitandika na yale mawe ambayo lilikuwa linarusha na kulibwaga chini baada ya sehemu kubwa ya mawe yale makubwa kulipata kichwani. Basi mwendo wetu ukawa wa kukutana na vikwazo njiani lakini tulivimudu. Tulipambana na wachawi wazee vijana, mpaka watoto wengine walisikitisha sana kuwaua kwani niliona kama hawakuwa na hatia maana walichokuwa wanakifanya ni kutokana na maamrisho ya Magugi, wengine hata akili zao hazikuwa sawa, lakini ilikuwa ni lazima kuwazuia kama sisi ulitaka kutimiza lengo letu na njia ya kuwazuia ilikuwa ni kuwauwa tu kwani maneno yetu yasingeweza kusikilizwa.
Tukaenda mwendo huo wa kupambana na vikwazo mbalimbali mpaka kwa Magugi, leo tena nyumba haikuwepo. "tayari ameificha nyumba, utafanyaje sasa" niliuliza kwa kukata tamaa. "fumba macho yako" alisema Mnaro ambaye nilipomtazama niligundua kuwa yakweke yalikuwa yamefumbwa tayari, nimi nikafanya hivyo na kushangaa naiona nyumba ya Magugi vizuri tu. Tukaenda moja kwa moja na kuingia mpaka ndani ambapo tulimkuta Magugi akiwa amekaa kwenye kiti chake na pembeni yake alikuwepo yule jini ambaye husimama pembeni yake siku zote, sikujua namna gani yeye aliacha kuonekna msaliti maana Magugi alidai kuujua mpango wetu wote wa kutoroka Muifufu, sasa kwanini huyu bado anamuamini ikiwa pia alinisaidia, nilijiuliza. "washughulikie wapumbavu hawa" aliamuru Magugi, jini yule akatembea kuelekea upande wetu, Mnaro akaandaa mikono yake kupambana naye lakini nikamzuia, jini yule akatuvuka na kutoka akituacha tumfanye Magugi chochote ambacho tungependa kumfanya. "mbio za sakafuni huishia ukingoni, leo ndo mwisho wa ufalme wako" alisema Mnaro, akaunyoosha mkono wake na kumkaba Magugi kamnyanyua miguu yake ikabaki ikining'ia kisha akamtembea naye akimtoa nje katika hali hiyo. Huko nje kulikuwa na watu wengi ambao walionekana kama walikuja kwaajili ya kupambana ila muonekano wa Magugi ukawafanya wakashikwa na bumbuwazi, wakabaki kuwa watazamaji tu. Mnaro akambwaga Magugi chini pale uwanjani, akasimama na kutaka kukimbia, alikuwa anachekesha maana alikuwa ni mzee na hakuwa na uwezo huo wa kukimbia. Manaro akamnyanyua na kumsogeza mpaka kwake,kisha akamkaba shingo kwa mikono yake kabisa, mara Magugi akatoa kisu kidogo na kumchomanacho Mnaro shingoni, Mnaro akayumba na kumuachia Magugi ambaye alijiandaa kumjeruhi tena kwa kisu chake, nikawahi na kukata mkono wa Magugi, japo nilikuwa mbali hilo liliwezekana kwa msaada wa panga lile la ajabu sumu iliyopo kwenye hiki kisu ni kali sana, huwezi kupona tunakufa wote, alisema Magugi kumwambia Mnaro amabye alikuwa ameshika shingo yake kuzuia damu iliyokuwa inachuruzika, nikajisikia hasira sana na kukata shingo ya Magugi, kichwa chake kikadondoka chini. Nikenda kumtizama Mnaro ambaye nguvu zake zilionekana kumpunga kila muda ulivyozidi kwenda. "yule mmoja wetu ambaye anakufa leo ni mimi" alisema Mnaro, nikakosa hata cha kujibu. Twende haraka nikakufungulie mlango, usije ukabaki huku.
Mwendo wetu wa polepole ukatufikisha mahali ambapo Mnaro hakuweza kutembea tena, akasimama na kuniangalia kisha akatabasamu na kusema "nakuonea wivu sana, wewe unapata kila ambacho unakitaka na hata usichokitaka, umemtaka mkeo umempata, umetaka maisha yako umeyapata, mwisho umepata na kumuua Magugi, jambo ambalo hukuwa hukulitaka ila mimi niliyeliaka sana nimelikosa pia". Nilikuwa namuonea huruma sana Mnaro, mwisho wake haukuwa wa kupendeza ila sikuwa na chakufanya, hata cha kusema tu nilikikosa pia, machozi yaliyokuwa yakinichuruzika yalitosha kuelezea hisia zangu. "siwezi kuendelea, hii sumu ni kali kweli, kimbia haraka nikufungulie mlango kabla sijakata roho" alisema Mnaro nami nikaamua kukimbia kuelekea ulipo mlango, ambapo hapakuwa mbali na pale alipokwamia Mnaro, akajikaza na kuutanua mlango, lakini nguvu zikawa zinamuishia na mlangu unaanza kujibana polepole, nikakaza mwendo na kufnikiwa kupita na baada ya hapo ukajibana kwa kasi, nadhani ndipo Mnaro alipoaga dunia.
Maisha yangu yalirudi kuwa kawaid, nina furaha nikiwa na mke wangu na mtoto wetu wa kiume ambaye tumemuita Mnaro, sasahivi ana mimba ya mtoto wa kike nadhani huyu tutamiita Sauda. Famila yetu imejikita kwenye uchamungu, kwani nimegundua kuwa chamungu ni silaha kubwa dhidi ya nguvu za giza.
Mwisho
Pseudepigraphas Simulizi