Pomoja sana mwamba JB59....usisite kutupia ukipata wasaaa. mambo yanazidi kunoga.Pole, mazingira yananinyima muda wa kuandika, muda mwingi nipo mbio mbio barabarani. Imagine juzi nilikuwa Mbeya, leo nipo kwingine kabisa!
Kwo brazee unatushaurije?...Kwa watakao soma baada ya simulizi kuisha watafaidi sana mtiririko!
Kwa sasa inaweza isioneshe vizuri, simulizi haijaandikwa, hivyo nikitupia humu ni 'advance copy' moja kwa moja kutoka kichwani kupitia android.
Shukrani JBTupio la XXXVII – The Party
Endelea…
Nilivyorudi nyumbani Manzese wakati natafuta usingizi, whatsapp msg kutoka kwa Mourine iliingia…
“Hi Handsome, nimekumiss ujue, halafu nisamehe kwa kukukatalia kuangalia msg kwenye simu yangu, lakini ipo siku utajuwa kwanini, muda bado, naisubiri kwa hamu hiyo party ya kesho. Umesema umewaalika na marafiki zako?!”
Mimi: “Okay, ndiyo nimewaalika washkaji wa chuo, sio wengi lakini nataka tufurahi pamoja.”
Tulisogoa mawili matatu kisha tukaagana, mimi nikaendelea kuutafuta usingizi.
Kule Masaki nyumba yetu (yangu) na nyumba ya akina Emilia ni mjengo wa aina moja, yani kila kitu kilijengwa sawa, Wazazi wa Emmy wote wawili walikuwa wanafanyia Mamlaka ya Bandari pia.
Kwa upande wa Zai tangia siku ile tuamke wote nyumbani pale Manzese, ni kama alikuwa ananionea aibu hivi, muda mwingi alikuwa ananikwepa kukutanisha macho ingawaje msg zake zilikuwa hazikatiki kwenye simu yangu.
“Ahsante, umeufungua moyo wangu upya…”
“Ulinikamua vizuri siku ile, upwiru wote umeisha, niliinjoi sana…”
“Nimesha-msahau sasa Hemedi, apotelee huko huko…”
Yani kwa siku nilipokea msg zake za namna hiyo zaidi ya 17.
---
Usingizi ulinichukua, nilizinduka alfajiri kwa ajili ya kwenda haja ndogo, baada ya hapo nikaanza maandalizi madogo kwa ajili ya chuo na kuweka utaratibu vizuri kwenye karatasi kwa ajili ya party ya jioni.
Kabla sijaenda chuo nilipitia kwanza kule Masaki kuangalia maandalizi, nilikuta Mlinzi na house maid wapo vizuri kama nilivyo waelekeza, nyumba kwa nje ilipambwa vizuri eneo ambalo ndilo nilitarajia tungeanzia kufanya party yetu na kisha kungekuwa na kipande cha kuizindua nyumba ambapo tungeingia ndani.
Waliandaa alama ya tambala la tangazo lililoandikwa kuashiria part iko nyumba ile. Nilifurahia sana ubunifu ambao baadaye nilijuwa kuwa ulitoka kwa vijana walinzi wa SumaJkt.
Tulimtumia mwanachuo mwenzetu mmoja kuchukuwa kazi ya kutuandalia chakula, maana dada yake huwa ana shughulika na kazi hizo za catering, kwa uzoefu wake tulijuwa kuwa hakuto haribika kitu na tenda hii ilikuwa tofauti kabisa na alivyozoea kwenye maharusi nk.
Ilihitajika uchomaji wa nyama za mbuzi, ng’ombe na kuku wa kienyeji kwenye viwanja ya nyumba (ndani ya uzio. Nyumba ilikuwa na uzio mkubwa sana wa ukuta wa matofali. Kulihitajika viazi mbatata vya kuchoma na pia chips zake na vikorombwezo vingine.
Baada ya muda wa chuo, kukawa na msafara usio rasmi kwa baadhi ya waalikwa wakinifuata kuelekea Masaki, wengine walipitia sehemu wajuazo kwanza kisha wakaungana nasi kwa kutumia gps location, kwenye hili la kukaribisha wageni, Emmy alinisaidia sana.
Saa kumi na mbili jioni tayari magari ya walikwa yalikuwa yamejaa sehemu za kuegeshea ndani ya uzio nan je ya uzio, wote niliowaalika walikuja pamoja na wazamiaji wachache (partners), watu walianza kunywa, kula nyama na kuburudika na miziki mbali mbali kabla hata shughuli yenyewe haijafunguliwa rasmi.
Mourine naye akafika kwa kuchelewa lakini aliwahi kabla ya tamko la kufunguliwa kwa party, Emmy alikuwepo tangia mwanzo na alijipa kitengo cha ukaribishaji, ajabu siku hiyo sikumwona yule msanii wake.
Niliifungua party rasmi kwa kutangaza kwamba imefunguliwa, baada ya kuwashukuru waalikwa wote walifika, na kwamba madhumuni ya party ile ilikuwa kuizindua nyumba ambayo tuliitelekeza kwa miaka kadhaa na sasa tumerudi tena. Nilitumia wingi ili kuonesha siko peke yangu mle ndani.
“Kwa wazazi wake hapa, nyumba za Bandari hizi…” alisikika jamaa mmoja akimwambia mwenzake
“Nyumba zimeshauzwa hizi, itakuwa wameinunua…” alimjibu mwingine kurekebisha
“Pazuri sana, hewa safi, upepo mzuri kutoka baharini, na bustani umeandaliwa vizuri…” mdada mwingine alichangia
Ilikuwa furaha sana, huku Emmy akijisogeza sogeza kuonesha tupo jirani…
Baadaye kidogo nilimuashiria Dj Bony asitishe mziki ili nitoe utambulisho, maana kuna watu kadhaa mule ndani walikuwa hawajuani…
“Eeee napenda kuwatambulisha kwenu dada yangu mpenzi Mourine, (nikamshika bega), yeye ni mjasiri-amali yupo hapa hapa Dar na anaishi maeneo haya haya ya Masaki…”
Waalikwa tayari walikuwa na vinywaji kichwani, walipiga makofi…
“Pia yule pale ni house keeper wetu anaitwa Alice, yule kule mzee wetu anaitwa Nchumari bila kuwasahau walinzi wetu kama mnavyo waona na timu ile kule ya catering ni ya dada Neema…”
“Tuendelee kuburudika na baada ya muda mfupi tutaizindua nyumba kwa kuitembelea angalau sehemu chache…, Dj!”
Mziki ukaweka na watu wakaendelea kufurahia. Hapakuwa na ratiba ya kula lakini kila mtu akihitaji chochote yeye mwenyewe alikuwa anaenda kule upande wachomapo nyama na kuchukuwa sehemu anayoridhika kwa aina ya nyma aitakayo na kuendelea kuparty .
Ingawaje kulikuwa na viti vya kukaa, lakini muda mwingi watu walikuwa wamesimama huku wakinywa vinywaji vyao pendwa.
Baada ya muda ikafika wakati wa kuitembelea nyumba kwa sehemu nilizochaguwa watu wafike, tukaanza kuingia ndani na kufika sebuleni ambapo tulisimama, palikuwa pamependeza sana, yani sana hadi Emmy alishindwa kujizuia…
“Hongera Alex, umebadilisha kabisa muonekano wa ndani, sio kama kule kwetu…” alisema hivyo huku ‘akinipalatia’, Mourine alikuwa mtulivu sana, Zai wala hakuonesha lolote ila uso wake ulikuwa na furaha.
Tulivyomaliza ziara ya mle ndani tukashuka chini na kurudi kuendelea na kuburudika kwa nyama na vyakula vingine na vinywaji vilikuwa havikauki. Wengine walianza kuchukuliwa na ulevi ikanibidi nimuombe Dj Bony asitishe mziki ili nitoe tangazo…
“…Pamoja na kuwashukuru kwa kuitikia wito wa kujumuika nasi hapa, kuzindua nyumba, kula na kunywa na kufurahi lakini pia nina tangazo rasmi leo…”
Pakawa na ukimya kila mmoja akijiuliza ni tangazo gani…
Dj Bony kama nilivyompanga aliweka wimbo wa kuchombeza taratibu wakati naanza kuongea…
“…Tangazo lenyewe ni kwamba leo rasmi nawatangazia mpenzi wangu ….”
Utulivu ukazidi
“Tangia nimeanza uhusiano naye, moyo wangu umetulia, yeye ni mpole, mnyenyeku na ana sifa zote za kuwa mke bora…”
Watu wakawa wanaangaliana kisha macho yote yakawa yanamuelekea Mourine ambaye ndiye wanachuo walikuwa hawamjui lakini hapo alionesha ukaribu sana nami ingawaje nilimtambulisha kuwa ni dada.
“…Kwa sababu hiyo basi, napenda wote humu na dunia yote ifahamu kuwa….”
Wafukunyuku wakawa wanarikodi lile tukio kwa simu zao, kumbe wengine walikuwa wapo live tiktok na youtube wakirusha baadhi ya matukio…
“….napenda mfahamu kuwa kuanzia sasa Zaituni Nassoro Ahmed ndiye mpenzi wangu mpya!....”
Watu wengine walishangaaa, wengine walifurahia na nderemo na vifijo vikasikika…
Nikamsogelea Zaituni ambaye muda wote wala hakutaka kuonesha kama yupo karibu nami kimahusiano isipokuwa Emmy tu ndio ambaye angeweza kuhisi kutokana na siku ile tulivyokutana kule Rombo Green view Hotel…
Emmy alikuwa ameduaa kama ameloweshwa maji, akiwa amesimama huku mikono yake yote miwili akishika mdomo wake kwa kufanya kama anauziba…
Nikazidi kumsogelea Zai ambaye sasa alikuwa anaona aibu huku akitabasamu, kichwa ameinamisha chini huku akinema nema!
Nikapiga goti moja…
Watu wote mle ndani walilipuka kwa shangwe hata kabla sijasema neno…
“Zai…” nilisema na watuwakitikia weweeeeeeee!
“Zai, will you marry me!?”
Nikatoa kasha ya pete uchumba kisha nikaifunua lile kasha na ile pete kuonekana… nikishikilia kusubira response ya Zai.
Badala ya kujibu akawa anaruka ruka kwa furaha huku akiwa anafunika macho kwa aibu na furaha…
Waalikwa wakawa wanasema..
“Say yes, say yes!”
Bado nikiwa katika hali ile ya kupiga goti, Zai alinisogelea huku akirusharusha miguu kwa furaha kama anapiga maktaim na kunyoosha mkono wake huku akisemaa…
“Yes Alex, I will” Nikamvalisha pete maridadi kabisa ya uchumba
DJ naye hakuwa mbanizi wa kufuata maelekezo, ilipigwa bonge la blues ambapo nilisimama na kumkumbatia Zai huku tukishangiliwa na waalikwa…
“Jamani, Emmy ameanguka!” tulikatishwa ghafla na sauti ya Laula, rafiki yake Emmy
Mourine fasta akamsogelea Emmy na kuanza kumkagua…
Mziki ukazimwa na wote tukawa tunamwangalia Emmy
“Anapumua, mlazeni ubavu wa kulia…” Mourine aliamrisha
Mara Emmy akainuka mwenyewe akawa amekaa na akaanza kulia….
Akainuka na kuchukuwa mkoba wake kisha akatoka nje ya geti na kutokomea…
“Mfuateni, asije akaenda kujigongesha barabarani…” Mourine alisema kuwaambia wenzake ambapo Laura na Rachel walimfuata, Mlinzi mmoja akaongozana nao, Emmy alionekana akitembea harakaharaka akielekea numbani kwao huku akilia.
“We Alex, ungeua mtoto wa watu!” Mourine alisema huku akiwa amekasirika…
“Dada, hujui tu huyo alichonifanyiaga, leo hii ni zamu yake. Hata hivyo yeye alishaniacha siku nyingi na ameshabadilisha mabwana wawili sasa hivi yupo na msanii (nikamtaja), hivyo hana sababu ya kuumia wala kuhuzunika, Emmy siyo mpenzi wangu…” Nilimjibu Mourine
“Kama siyo mpenzi wako mbona kazimia!, nyie mna yenu!” Mourine alikazia
“Hakuna lolote dada, muulize Zai, ni yeye Emmy alitutambulisha pia kwa mpenzi wake mpya huyo msanii na Zai ni shahidi…” Nilimjibu
Tuliobaki mule ndani tukapata wasaa wa kukaa kwenye viti na stori zikawa za Emmy na tabia zake na jinsi nilivyolipiza kisasi kimtindo.
Zai kuanzia hapo muda wote alikuwa hakai mbali nami, alikuwa mwenye furaha sana na uso ulikunjuka kisawasawa!
Tuliendelea kunywa na kula huku waalikwa wakitupongeza…
“Halafu nyie watu mna siri, kumbe mna date halafu wadau hatujui…!” Margareth alisema kiushabiki
Itaendelea…
Ngoja nisubiri iishe sasa, manake hii ya vipande baada ya siku inapoteza ladha 😄 😄 😄 😄 😄Kwa watakao soma baada ya simulizi kuisha watafaidi sana mtiririko!
Kwa sasa inaweza isioneshe vizuri, simulizi haijaandikwa, hivyo nikitupia humu ni 'advance copy' moja kwa moja kutoka kichwani kupitia android.
Itafahamika tu!Kwa watakao soma baada ya simulizi kuisha watafaidi sana mtiririko!
Kwa sasa inaweza isioneshe vizuri, simulizi haijaandikwa, hivyo nikitupia humu ni 'advance copy' moja kwa moja kutoka kichwani kupitia android.
Msegemnege😁Title ya story, ilinileta wima wima, nusu nijikwaee, content enyewe sasa tofauti, nkarudi kusoma title vizuri, kumbe nlikua Opie kabisaaaa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] woiiiiiiiih
9JF huwa ni moja ya sehemu zangu za kujiburudisha hususani kwa ‘ID’ hii. Kwa kuwa nimepata muda kidogo wa kuandika na tarehe ya leo ni kumbukumbu yangu ya siku ya kuzaliwa, nimeona nianze kuwaletea simulizi iitwayo “Msegemnege”.
MSEGEMNEGE
Ni simulizi ya kubuni.
Haina uhalisia wowote.
---
Msegemnege
Tupio la I – Alex.
Alex alikuwa akiishi na wazazi wake nyumba za mamlaka ya bandari eneo la Masaki, Tour Drive, mita kadhaa kabla ya kufika Sea-Cliff Hotel. Lakini baada ya wazazi wake kufariki alifukuzwa kwenye nyumba hiyo ya Masaki, yeye na dada yake wakahamia uswahilini Manzese kwa ‘mfuga mbwa’ sehemu ambayo iliendana na hali yao wakati huo na palikuwa jirani na chuo alichokuwa akisoma Alex.
Alex ni kijana asiye na majivuno wala maringo hata wakati wa uhai wa wazazi wake ambao walikuwa wana ukwasi wa kutosha kibongobongo, hakuwa mtu mwenye kujikweza. Mama yake alikuwa mfanyakazi wa mamlaka ya bandari na baba yake alikuwa mfanyabiashara. Baba yake na mama yake waliuwawa katika tukio la ujambazi. Ujambazi ambao uliacha maswali mengi kwa kitengo cha upelelezi cha Polisi kwani kwenye gari waliokuwa wakitokea mjini kurudi nyumbani walishambuliwa eneo la makutano ya ‘tour drive’ na ‘Tumbawe road’ na katika upekuzi kwenye gari walilokuwa wakitumia marehemu, kulikutwa kiasi fulani cha hela kwenye droo ya gari pamoja na vitu vingine vya thamani kwenye kiti cha nyuma ikiwemo tarakirishi mpakato Hp moja na vishikwambi viwili aina ya ‘Surface’. Hii iliashiria kuwa halikuwa tukio la ujambazi wa kawaida bali kuna jambo lipo nyuma ya tukio hilo. Hii ilikuwa ni takribani miaka mitano iliyopita na upelelezi ulikuwa bado haujakamilika.
Alex alikuwa ni mtoto wa kiume pekee wa mzee Jonathan na Miriam ambao katika maisha yao ya ndoa walibahatika kupata watoto wawili, wa kwanza akiwa wa kike aitwaye Queen ambaye habari zake tutaziona huko mbele, lakini kwa upande wa Alex yeye alikuwa anapenda mambo ya urubani na kufanya wazazi wake wampeleke kuanza mafunzo ya urubani katika chuo cha Taifa cha usafirishaji (NIT) ambapo akiwa mwaka wa pili ndipo wazazi wake wakafariki na kukatisha masomo yake miezi kadhaa baadaye kwa kukosekana kwa ada na hela za kulipia mafunzo kwa vitendo.
Alex hakuwa na jinsi bali kujiingiza katika biashara ndogo ndogo za kimachinga. Aliuza vocha, akauza karanga, akauza viatu vya ‘kulenga’, aliuza matunda ya msimu ili mradi kila alichoona kinafaa yeye alifanya ili aweze kujikimu. Kwa kuwa alikuwa anapenda kusoma, alikusanya fedha na kudahiliwa tena chuo cha IFM kwa masomo ya usimamidhi wa fedha na kwa bahati nzuri alipata mkopo kwa asilimia mia moja. Pamoja na kusoma lakini pia hakuacha kufanya biashara ndogo ndogo akiwa Chuoni IFM.
Kama ilivyo kawaida ya vijana wa vyuo, Alex naye alikuwa na rafiki wa kike ambaye wanafahamiana kwa muda mrefu tangia Alex alipokuwa akiishi Masaki ingawaje alimuacha madarasa matatu nyuma wakati huo. Walipo kutana IFM wakaanzisha uhusiano wa kimapenzi na walikuwa wanapendana ingawaje sasa Alex hakuwa kama vile alivyokuwa wakati wazazi wake wakiwa hai. Alikuwa anavaa kawaida tu siyo kama zamani, hakuwa na chombo cha usafiri, kwa ujumla maisha yalikuwa ya kuunga-unga.
Miezi michache baada ya uhusiano wao, Emilia aliona bora atafute mwanafunzi mwingine ili aachane na Alex maana Emmy alikuwa na marafiki zake ambao mabwana zao walikuwa vizuri kiasi cha kumfanya Emmy kuanza kumdharau Alex licha ya kujua historia yake.
Siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa Emilia ndiyo ilikuwa chaguo zuri kwake kumuacha Alex mbele ya marafiki zake kwenye sherehe fupi iliyofanyika kwenye bustani ya moja ya Hotel Kubwa maarufu iliyopo jirani na hapo chuo.
Neema, Rachel, Margareth, Lidya, Zaituni na Laura ndio walikuwa marafiki wa Emilia ambapo tayari walikuwa viwanja vya Hyatt Regency pamoja na mabwana zao ambapo Emmy sasa alikuwa na bwana mpya aitwaye John.
SMS
“Alex, uko wapi?” – Aliandika Emmy
“Nipo Library” – Alijibu Alex.
“Chukuwa boda fasta njoo hapa Hyatt Regency Hotel” - aliandika tena Emmy.
“Dakika sifuri” – alijibu Alex asijue hili wala lile, kumbe maskini ndio anaenda ‘kupigwa kibuti mubashara’ mbele za watu.
Baada ya dakika chache Alex akawa Mapokezi pale hotelini, akamtumia text msg Emmy, “Upo room ipi mie nipo hapa receiption”
“Hapana sipo room, zunguka huku uwanjani kuna party fupi, umesahau leo ni birthday yangu?!”
Kutokana na mchanganyiko wa mambo tangia Alex apoteze wazazi wala hakuwa tena anakumbuka tarehe ya kuzaliwa ya Emmy. Hivyo ni kama alishtukizwa tu.
Alex akaenda moja kwa moja hadi huko uwanjani ambako alikuwa watu wakifurahi na kunywa huku kila mmoja akiwa amekaa na mpenzi wake ‘including’ Emmy.
Ghafla Emmy akamuacha John na kwenda kumpokea Alex na kumbusu kiaina na kumkaribisha kwenye party.
Hakuna katika rafiki zake Emmy aliyekuwa anajuwa kuwa Alex ameitwa ili apigwe kibuti mbele zao.
Watu walikuwa wanendelea kuburudika na vinywaji na mziki kwa mbali kisha sauti ikasikika…
“Jamani nina tangazo…” Emmy alisema.
“Nina furaha kutimiza miaka kadhaa leo (aliitaja) na kwamba leo ninatengana rasmi na Alex na kuanza rasmi uhusiano na John…”
Alex alipigwa na butwaa, akaachama mdomo wazi, na kupata ububu wa ghafla…
Rafiki zake Emmy wote nao wakashangaa na mmoja akasema…
“Emmy, unafanya nini !!??” – Zai alisema kwa kumshangaa Emmy.
Emmy naye akajibu kuwa ndiyo hivyo kama mlivyosikia, kisha akamfuata John na kumkumbatia na kumbusu.
Wakati huo Alex bado alikuwa ameduwaa asijue la kufanya huku mikono yake akiwa amejishika kichwa.
“We Emmy, kwa nini unamfanyia hivi Alex?, Alex anakupenda sana, na unajuwa jinsi anavyo kupambania, unajua fika kuwa pato lake sasa hivi ni dogo lakini amepambana na kukufanyia mengi makubwa na hivi karibuni amekununulia simu nzuri latest…” Alisema Laura.
“Simu ndio nini, kwa nini ning’ang’anie Samsung wakati nimepata Iphone, chukuwa lisimu lako hili…” Emmy alijibu na kumtupia simu Alex ambapo kwa kuzubaa ilimpiga kifuani na kuanguka chini.
Alex hakuiokota. Akageuka na kuanza kuondoka huku akiwa na mawazo tele.
---
Alex alitarajia kumuoa Emmy, ilikuwa ni faraja yake maana wanafahamiana kwa muda mrefu na kwamba Emmy alikuwa anajuwa historia ya Alex na hali aliyokuwa nayo mwanzo, hivyo Alex alidhani amepata wa kumfariji.
Aliondoka huku machozi yaki mlenga-lenga na alikuwa amejiinamia huku anatembea alitoka mle hotelini ili achukue bodaboda kuelekea IFM.
Huku nyuma Zai aliiokota ile simu na kuanza kuikagua…
“Mmmmh, lakini wewe Emmy wewe,…” alisema Zai.
“Wewe nini!, kama unamtaka wewe mfuate…” alimaliza Emmy.
Zai akaangaliana na bwana ‘ake kisha akamtupia tena maneno Emmy…
“Kumbe ulishaifuta kila kitu, lakini ona sasa umeipasua kioo…”
Emmy alionekana kuto kujali na kuendelea kugigida kinywaji na ‘party’ iliendelea japo si kwa muda mrefu tena baada ya pale.
Ilikuwa siku ya Ijumaa mida ya alasiri, Alex akiwa Hostel za IFM kwa rafiki yake Boniface, akiwa amejilaza kwenye kitanda akitafakali kilichotokea, mara ghafla meseji ikaingia kwenye simu yake. Hakutaka hata kuifungua…
Alimshirikisha Bony suala hilo na Bony alimtia moyo na kumshauri amfute moyoni mwake na ndio itakuwa tiba ya kuvunjika kwa moyo alikokupata baada ya tukio lile.
Bony ndiye aliyekuwa rafiki yake mkubwa Alex pale chuoni, na ‘alimbeba’ kwa malazi (hostel) siku amabazo Alex alikuwa hawezi kurudi nyumbani kwake Manzese.
Sasa kabla ya kumuaga Bon ili arudi home Manzese, aliamua kusoma ile sms na kukuta imeandikwa hivi…
Ndugu Alex Jonathan na bi Queen Jonathan, shauri lenu la mirathi limefikia hitimisho, hivyo mnatakiwa mfike bila kukosa Mhakama ya Mwanzo Sinza siku ya Jumatatu saa mbili asubuhi bila kukosa kwa ajili ya kukamilisha taratibu zingine. – Hakimu Mkazi, Mahakama ya Mwanzo Sinza.
Ghafla sura ya Alex ikakunjuka na furaha moyoni ikarudi, maana ni zaidi ya miaka minne shauri lao linazungushwa na Mahakama na hawakuwa na ‘connection’ wala fedha za kuhonga kitu kilichofanya shauri lao kupigwa kalenda kila siku wakienda na kisha ‘kupotezewa’.
Inaendelea…
usitusahau sana mkuu tuna arostoHata nusu ya simulizi bado.
Nikisha kaa sawa nitaendelea kuandika, dunia inanishughulisha kwanza.