SIMULIZI: Sababu ni Kifo chako baba (Season one)

SIMULIZI: Sababu ni Kifo chako baba (Season one)

SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA! (Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA TISA (09)
MTUNZI: Man Middo Tz
WHATSAPP: +255 655 969 973

Damu zikawa zinatoka nyingi harafu ziwezi hata kuusukuma ule mzigo kwa pembeni, nikaa kama dakika 5 bila kupata msaada ndipo baadhi ya wanafunzi waliokua wamepanga karibu wakanikuta.

“HE! Jaman pole Hesha, hujaumia?”

Nikajibu kwa kutikisa kichwa, sikuweza hata kuongea, mwingine akasema

“Lakini huu mzigo mbona mzito sana harafu kuni zenyewe mbichi na usiku unaingia kwani hakuna watu wengine wakupeleka mpaka wewe au kwasababu wewe ni bonge”

Waliendea kuongea pale huku wakinionea huruma, basi baadhi yao wakachukua zile kuni na kuzipeleka bustanini na mimi wakanirudisha nyumbani.

Sasa kufika nyumbani mama Frida kuniona tu akasema

“Khee! Kumetokea nini tena na kuni zangu zimefika?” Wale vijana wakamjibu

“Tumemkuta kadondoka chini na kuni zimemlalia anaonekana anaumwa ila kuni tumezipeleka ila..”

“Haya hongereni”

Kabla hajamaliza yule mama akamkata kauli, alikua ni mmoja kati ya wale vijana walionisaidia, wakashangaa kisha wakaondoka.

Basi nikafikiria huenda nitapelekwa hospitali kwa hali yangu lakini wapi. Sasa maumivu yakawa makubwa mnoo, nikajiuliza

“Inamaana huyu mama haoni kuwa hali yangu, hata kama mimi sio binti yake ila anakosa hata ubinadamu je nikimfia hapa hatalaumiwa kweli?” Niliwaza sana lakini sikupata jibu.

Sasa usiku kwenda kulala maumivu niliyosikia sio ya mchezo, ule mzigo ulikua umeniumiza sana, pia ukizingatia nilikua naumwa kwa kweli nilijua nitakufa siku hiyo.

Kwenye kulala nililala kifudi fudi, yani huwezi kuamini nikilala chali au kulalia ubavu nikua nahisi maumivu makubwa mnoo mwilini ikawa kupiga yotwe tu.

Sasa jambo lililokuja kunishangaza ni asubuhi nilivyoamka nikajikuta NIMEJIKOJOLEA hapo hapo kitandani, sasa Frida akagundua

“Wewe Hesha Tabia gani hii, yani unajikojolea msichana mzima khaah!”

Kilikua kitendo cha aibu sana kwangu na ukizingatia nipo kwa watu, harafu hata huko mtaani na shuleni naonekana mchafu.

Hapo nikaona nipo kwenye wakati mgumu ila kwasababu ni bahati mbaya nikamuomba Frida kuwa

“Frida naomba usimwambie Mama Kwasababu nikutokana naumwa na sijwahi kufanya kitendo hiki”

Nikashukuru Mungu akanielewa, sasa maajabu ikwa ni tabia endelevu yani nakojoa hata bila kubanwa mkojo. Maisha sasa yakabadilika nikawa najichukia mnoo! Nikakosa amani, sina furaha aibu kama yote, Nikawa najiuliza mengi sababu ni nini? Msichana kama mimi kidato cha kwanza najikojolea, je ikijulikana itakuaje!?

Nikawa namuomba Frida asimwambie mama yake kila siku lakini mwishoe akagundua aisee daah!.

“Khee! Mwanamke mzima unakojoa kitandani, haya chumba kinanuka mikojo ya mtu na maziwa yake huna hata aibu looh! Sasa hakuna sabuni ya kufulia ukikojoa utajua mwenyewe”

Ooh my God!!! Huyu mama alivyokua na kiherehere akaenda kuwambia wale wa kaka, ambao mmoja ni mtoto wa yule mwanaume wa mama yangu na rafiki yake. Mungu wangu! Wakawa wananitania sasa

“Kikojozi kikojozi”

Hapo kila muda nililia yani, nikajichukia mnoo na ukizingatia sina nguo ndio nikawa rafu kama nimeokotwa.

Kipindi chote hicho bado naumwa sijapona na hali ni hiyo, harafu pia mama yangu mzazi bado hajui kitu....... ITAENDELEA.

Unadhani kipi kitatokea, Aisee mengi yanakuja. Kumbuka ni Kisa Cha kweli.
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA! (Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA KUMI (10)
MTUNZI: Man Middo Tz +255 655 969 973

Sasa kutokana na kujikojolea ikabidi nishushwe chini, nikapewa kipande cha godoro na mabox. Kwa kweli sikujaribu kukataa au kuleta ubishi kutokana na aibu niliyokua nimekutana nayo.

Sasa shida kubwa ikawa kwenye kufua, nikikojoa sikupewa sabuni harafu DAAH! Hadi machoz yanatoka! Nilikua na chupi moja tu nikikojolea kama ni shule nitaenda nayo hivyo hivyo.

Aisee niliumizwa sana na ile hali sikujua ni kitu gani kile kwasababu hata niseme nilale macho huo muda nitakaopitiwa tu hata dakika ngap basi hapo hapo nitaharibu, Kuna wakati nikawa sinywi maji kabisa nikijua nitatua tatizo lakin wapi.

***
Sasa siku niliyopona kufika shule sikutegemea kabisa kumbe taarifa zimefika shule nzima, sasa wakaka wa form four wale wakorofi wa darasa wakaunga mstari wakaniongoza, sasa na vile mimi ni kibonge aisee daah wakanza kunikimbiza mchaka mchaka huku wanaimba

“kibonge kikojoozi eeh… Kibonge kikojooz eeh”

Yani wameniimbisha huku maneno kibao ya kashfa na kunibeza, aisee siku hii nililia sana yani kila hatua nikawa nalaani wale waliomuua baba yangu.

Kwasababu kama sio kifo chake naamini kabisa masaibu yale nisingekutana nayo. Basi baadae nikarudishwa hadi maeneo ya shule wanafunzi wote ni kunishangaa tu aisee nilichokifanya nilikimbilia chooni nikajifungia huku nalia tu.

Baadae Dada mkuu na wadada wengine wakanifuata kunibembeleza

“Nakuomba ufungue mimi dada mkuu, hapa kuna wasichana wenzako usiogope hatukufanyi chochote tunataka kukusaidia”

Sikujibu nikawa naendelea tu kulia, wakaendelea kunibembeleza ila mwenyewe nikajisemea kuwa

“Sasa nitakaa humu chooni mpaka muda gani”

Ikabidi nitoke wakanishika huku wakiniomba nisilie wkanipeleka hadi kwenye ofisi ya dada mkuu aibu kama yote yani nilitamani ardhi ipasuke.

Ila kiukweli nilikuana harufu ya mkojo kidogo sasa wakawa wananidharu baada ya kufika

“Anna (Hesha) wewe ni msichana saivi unatakiwa uwe msafi, ukirudi shule unafua nguo zako vizuri zikikauka unapass vizuri ukija shule umependeza, si unatuona wenzako tulivyo eeh sasa kwanini wewe usijipende mpaka wavulana wakufanyie hivi? Jipende bhn mbona mwenzako Frida anapendeza na mnakaa wote”

Sasa niliwasikiliza huku nabubujikwa na machozi kwa kweli niliumizwa na ushauri wao kwasababu wao walijua mimi nafanya makusudi tu.

Kila nilipofikiria mazingira ninayoishi kule na kazi ninazopewa huku hata sabuni yenyewe nanyimwa, tatizo lenyewe la kujikojolea limetokea tu hata sijui sababu ni nini haswa aisee ndio nikazidi kulia.

Kilichoniumiza ni wao kumuona Frida anang’aa, anapendeza bila kujua yeye anapewa kila anachokitaka wakati huo mimi nanyimwa.

Sasa baadae ikabidi niwambie kwa ufupi ninavyoishi pale, waliumizwa sana na yale maisha.

Sasa baadae wakanikagua nakugundua sikuwa nimevaa chupi ndani, Aisee waliniogesha wakaniweka ofisini kwa Madam mmoja kisha wakanifulia na nguo zote, nikapewa khanga nijifunge nikasubiri hadi nguo zikauke.

Nguo zilivyokauka wakazinyoosha na pasi kumbe walienda kuninunulia chupi na tight wakanipa nikavaa…………ITAENDELEA.

JE HIYO NDIO SIKU YA MWISHO KWA ANNA A.K.A BI HESHA KUACHA UCHAFU?

JE NI LIPI LITATOKEA BAADA YA HILI?

ASEE YAJAYO YANAFURAHISHA NA KUSIKITISHA?

NUKUU “Katika maisha ya shule kuna watu wanakili harafu wanamuonekano wa ajabu sana, wengi wetu tumetumia midomo yetu kuwazihaki, kuwabeza kuwaona kama mazoba yasiojiweza bila kujua kumbe wengi wao hawakupenda kuwa hivyo.

Kuna watu wengi wanaishi katika haya maisha,

FUNZO kamwe usimdharau wala kumjaji yoyote kutokana na muonekano wake huwezi kujua ni yapi anayapitia. “Usitamni viatu vyangu, ukivivaa hautembei”

kamwe usitamani kuishi maisha ya mwenzako.

Like na comments ukishasoma
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA!(Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA 11
MTUNZI: Man Middo Tz +255 655 969 973

Baada yakupata chupi moja na tight nilibadilika kwa kiasi ingawa sio sana kwasababu nguo nyingine za kubadilisha sikua nazo.

Sasa ikawa navaa kwa zamu ile chupi na ile tight, maisha yakasonga hivyo ila havikuweza kuleta mabadiliko kwasababu kazi nilizokua nafanya muda wa kupunzika hakuna, kingine sikupewa sabuni pale.

Kule kukojoa kulianza kulipotea baada tu ya kupona lile homa, hapo nikawa na amani moyoni kiasi ingawa ilikua inaenda huku inarudi.

Sasa maisha yakasonga vile vile majukumu kama yote, sasa ishu ya kusoma peke yangu iliniumiza sana pamoja na kwamba sikupata muda wa kutosha lakini kwa huo muda nilioupata nilijitahidi kujisomea ila sasa kusoma peke yangu sebleni niliogopa sana.

Basi kuanzia mwezi wa 3 hadi kipindi cha mitihani nikakubaliana na hali ile ya maisha kuw haya ndio maisha yangu, shuleni na uchafu wangu wakawa washanizoea sasa hakukua na wakusema sema ingawa kejeli na vijembe havikuisha.

Baada ya kufunga shule yule mama akaniambia

“Anna itabidi usirudi likizo ili utusaidie parizi, nitamtafuta mama yako nitampa taarifa kuwa hutorudi likizo kuna kazi utusaidie kidogo”

Kweli nikabaki nikawasaidia pale kazi, Aisee hapo ndio unaweza sema nilikua kwenye mafunzo ya JKT lakini sikua na namna.

Baadae shule zikafunguliwa nikaendelea na masomo kama kawaida. Ilipofika mwezi wa 8 nikapata mdada mmoja hivi akawa rafiki yangu, huyu dada nimepatana nae kwasababu ya dada yangu Julieth.

Kipindi dada anasoma hapo huyu alikua rafiki yake sasa akawa ananiomba nikaishi nae kwao.

Huyu Dada anaitwa Matrona alikua kidato cha pili mimi cha kwanza.

Wadogo zake watatu walikua primary, Mama yake aliondoka muda na kuwaacha akaenda kuishi visiwani na baba yake anaishi wilaya nyingine na baba yake mdogo.

Kwa hivyo ilikua ni familia ya watoto tu, wakike watatu na wakiume mmoja alikua mdogo umri kati ya miaka 5 au 6.

Basi kabla ya kuniambia hivyo siku hiyo nilikua na mawazo sana, siku nzima nilikua nawaza kuhusu maisha niliyokua naishi kuanzia kwetu hadi pale kwa yule mama.

Sasa wakati huo tupo shule yule dada ndio akaniambia kuwa

“Hesha leo nakuona upo na mawazo sana ila kama unawaza kuhusu kuishi kule kwa yule mama, mimi nilikua naomba uje tuishi kwetu kwanza tunaishi wenyewe tu, harafu pili utajisomea vizuri na hakuna kazi za kusema mpaka uchoke”

“Da Matrona huoni kuwa nitawaletea mzigo usiowahusu?”

“Khee! Yani kuishi na wewe ni mzigo! Hapana Hesha kuwa huru sisi tunaishi kawaida tu kama familia nyingine harafu pia tushazoea hivyo tutakochokula na wewe utakula hicho hicho wala usiogope”

“Mmh! Basi ngoja nitakujibu maana siwezi tu kutoka kule kuja kuishi huku bila sababu ya msingi”

“Sawa lakini zingatia sana mustakabari wa maisha yako”

Ilinichukua mwezi mzima kukaa kimya bila kumjibu kwasababu nilijua nikimwambia mama lazima atanikatalia harafu ilikua ni lazima niondoke pale.

Basi siku moja nikamwambia yule mama

“Samahani mama kuna sehemu nataka niende nikakae, huko kuna wanafunzi wengi ambao nasoma nao tutakua tunasoma kwasababu hapa kukaa peke yangu kusoma sebleni naogopa, kwa ninavyoona sisomi”

“Khee! Kwahiyo hapa husomi! Maajabu haya umesoma toka mwezi wa kwanza mpaka sasa harafu useme unaona kama vile hapa husomi! Kweli shukrani ya punda ni mateke…”............ ITAENDELEA.

JE HESHA ATAFANIKIWA KUONDOKA?
USIKOSE KIFUATACHO.

SOMA LIKE NA COMMENT?

WHATSAPP 0655 969 973
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA!
(Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA 12
MTUNZI: Man Middo Tz +255 655 969 973
[emoji1427][emoji1427][emoji1427]

Siku hiyo alinisimanga sana na maneno kibao, sasa maajabu toka nimwambie kuwa nataka kuondoka zilipita siku nne bila kupewa kazi ngumu wala kupewa matusi maana kutukanwa ilikua kama sheria kwake. Siku ya 5 asubuhi niliamkia kufua harafu jioni nikabeba vikabrasha vyangu nikahama nikanza maisha mapya sehemu nyingine.

Maisha mapya yakanza yenye furaha na upendo mkubwa tu, kwanza Dada Matrona alikua ni mtu aliyejenga ukaribu na mimi, alikua anapiga stori na mimi tofauti na nilivyokua naishi kule kwa yule mama.

Lakini pia kama kuna kazi za pale tulikua tunambiana na kujadiliana tuzifanyeje na muda gani, ikifika asubuhi tunamshana kwenda kama ni shamba au kama ni siku ya shule hivyo hivyo. Pia usiku tulikua tunaamshana kusoma, ikawa kipindi cha furaha sana kwangu.

Dada Matrona pia alijenga ukaribu na familia yangu, sasa ikawa anaenda kwetu anawasalimia anarudi akawa ananisaidia kumwambia mama juu ya hali yangu. Muda mwingine tunaenda wote, kuna siku alivyoenda mama kamuliza

“Anaendeleaje mwenzako?”
Akajibu kuwa

“Anaendelea vizuri kiafya ila ana hali mbaya kimuonekano, hana mavazi shule nzima kawa gumzo kwa muonekano wake sketi imechakaa kwasababu muda mwingine anaitumia hadi nyumbani”

“MMH! Sasa mbona hasemi muda wote huo?’

“Mimi nahisi labda anakuogopa, na inawezekana ikawa hivyo”

“Sasa anawezaje kumuogopa mama yake jamani kha!”

Basi mama akampa hela Da Matrona alivyokuja akaenda kunishonea sketi mpya, viatu vilikua vimechoka akaninunulia vipya pia.

Na wakati namkuta alikuaga amenunua nguo ya ndani ikawa haimtoshi akanipa hivyo nikongeza idadi zikawa mbili maana ile yangu ilikua ishalegea kwa kuvaliwa kila siku.

Basi maisha ya furaha yakaendelea hivyo hivyo kwa wiki mbili mbeleni nikiwa na furaha, kwanza ule mji ulikua unavijana wengi wa rika letu.

Da Matrona pia alikua na marafiki zake wengi wakiume na wakike hivyo walikua wanakuja pale tunapiga stori usiku au mchana kwasababu mji ulijaa wanafunzi wengi wakiwa wamepanga kama ujuavyo shule ya kata kwa vijiji viitano vyote walikuja kupanga eneo hilo.

Sasa katikakupiga stori mimi nisikua naongea kitu ila nilikuaga mchekaji mzuri na mkosoaji kwa wale wanaochapia lugha. Kwenye mtaa ule nilizoeleka sana kwa wamama na akina baba walinipenda sana kwanza nilikua mcheshi lakini Dah! Baadae maisha yakabadilika……………ITAENDELEA.

KIPI KINAKUJA KUBADILIKA TENA WAKATI YUPO KWENYE FURAHA? JE UMEWAHI KUISHI MAISHA KAMA HAYA? TUAMBIE KWEYE COMMENT YAKO YALIKUAJE?

NUKUU “Siku zote msaidie anaehitaji msaada kwasababu unaweza kuwa ni wewe pekee unaefanya hivyo kwake, saidia bila kutarajia malipo”

Siku zote furahia maisha uliyonayo unaweza kuyaona ni maisha magumu nay a hovyo lakini kumbe maisha hayo hayo unakuta ni ndoto ya melfu ya watu.

Ndio kuna watu wanatamani waishi maisha unayoishi wewe ambayo wewe unayadharau, Hebu Jifunze kumshukuru Mungu na kuomba msamaha kwasababu unakosea kwa kujua na kutokujua.

SIMULIZI HII INAMAFUNZO MENGI SANA, USIACHE HATA EPISODE MOJA IKUPITE.

KAMA UNAHITAJI MWENDELEZO NICHEKI WAHATSAPP 0655 969 973.
 
JINA LA SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA!
(Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA 13
MTUNZI: Man Middo Tz

Kweli nikafagia uwanja nilipomaliza nikaenda kuchota maji ni mbali kidogo, sasa nilivyorudi nikakuta ashaosha vyombo harafu ameshadeki sebleni nilishangaa sana aisee sikutemea! Hakuishia hapo akaita mtoto fulani wa jirani yule mtoto alikua na baiskeli sikujua amemuagiza nini mimi ikawa yangu macho tu. Sasa aliporudi ndani akaniambia

“Kapige mswaki kisha kaoge”
Kweli nikafanya hivyo, nikajipakaa mafuta nikavaa, sasa niliporudi sebleni tukawa tunatazamana tu………..

“Naomba usogee hapakaribu yangu kuna jambo nataka nikwambie”
Kwa jinsi nilivyokua namfahamu Ostadh Othman hakuwa mtu wa wanawake maana hata wambea wa pale mtaani walishasema hajaoa lakini anajiheshimu sana hana muda na wanawake, kwahiyo nilijua hawezi kunitamani kwa jinsi nilivyo. Basi muda huo yule mtoto aliyetumwa karudi akampa mfuko, Othman akatoa chapatti na halfcake na juisi ya embe, aisee nilishangaa sana. Sasa muda wote nilikua nimesimama akanimbia

“Njoo basi ukae jaman unaogopa nini?”

Nikaanza kuzoea mazingira pale nikasogea alipo nikakaa, nikashangaa sana unajua ni kwanini? Ni kwasababu ni mara ya kwanza kuonyeshwa upendo tangu baba yangu afariki. Basi tukawa tunapiga stori za hapa na pale akaniuliza

“Sasa mbona ulikua unaogopa?”
“Hapana ni kwasababu nimekua nakuona hapa lakini sina mazoea yoyote na wewe hivyo ni lazima niogope”

“Ndio ni kweli unachokisema, unajua kwanini nimekuja hapa?”

“Hata sijui!” nikajibu akasema

“Ni kwasababu Kila siku nakosa nafasi ya kuongea na wewe hivyo jana nilikusikia ukisema huendi shule leo nikafurahi nitapata nafasi ya kuongea na wewe, harafu pia wewe ni binti wa kipekee sana kabla ya yote unaweza kunisimulia stori ya maisha yako mpaka kuja kuishi hapa?” muda wote alikua ananilisha huku akiongea, nikamwambia

“MMH! Kwasasa sio muda sahihi wa kukwambia maisha yangu ya nilivyoishi hadi kufika hapa, ipo siku utajua tu”

Basi tukapiga stori hadi saa 8 akaniaga ingawa alionyesha kutoridhika kabisa alitamani tuendelee kuongea sana. Kwa muda mfupi niliokaa nae Nikagundua kuwa anafurahia zaidi kuongea na mimi kuliko hata wengine, basi akanitonya kuwa

“Ngoja nikuache muda umeenda kwasababu wakinikuta hapa na wewe ni lazima watanihisi vibaya, ila ombi moja tu naomba usionyeshe kuwa unanifahamu wala usiwambie chochote kuhusu mimi kuja kupiga stori na wewe”

“Sawa usijali siwezi kuwambia”
****

Basi maisha yakasonga tukaendelea na urafiki na Ostadh Othman ingawa kwa siri, sasa katika kipindi hicho hicho pale nyumbani palikua na mganga wa kienyeji ni baba tu mtu mzima ana mke na mtoto mmoja.

Huyu mzee alikua akitupenda wote pale yani kuonyesha kujali kama ndugu zake bila kubagua, sasa huyu mganga akaanza kunitongoza aisee nikashangaa sana, nikajawa hofu na uoga wa hali ya juu, sikua na amani kabisa. Sasa ikawa hata kujisomea sijisomei nawaza tu watu wananichukuliaje hadi kutongozwa na mganga! Aisee hapo nikakosa hadi ujasiri wa kutoka nje najifungia ndani tu kwa kukosa amani.

Sasa nakumbuka zilipita wiki mbili hivi tangu nitongozwe na mganga, sasa pale kwake akaja kijana hivi wa makamo yetu akitokea Dar es salaam, majirani tukatambulishwa kuwa ni mtoto wa kwanza wa mganga anaitwa Justin. Sasa Justin akakutana na dogo mmoja wa pale mtaani anaitwa Side wakawa marafiki sana lakini ishu zao zote zilikua wasichana.

Justin alikua ni mcheshi sana akawa anakuja kule nyumbani tunapiga stori anatuchekesha kisha anaondoka.

Sasa sifa yake iliharibika ndani ya wiki moja maana ndani ya wiki kila mtu alijua Justin kamaliza kila wanafunzi wote hadi wanaomzidi umri pale kwasababu tu Msafi, anakiswahili cha Dar (Sisi tnaongea cha MARA) harafu anatumia pafumu, anapamba kali ingawa hakukua na ukweli wowote, lakini mimi pia sikua na muda nao kwasababu mimi sifanani na watu wote.

Sasa yule side akaanza kunitongoza eti niwe na Justin, yani kwa kule Musoma vijijini ilikua eti kutongozwa na kijana anaetokea Dar ilionekana kama bahati ya kipekee

“Wewe Hesha Justin ujue anakupenda sana hiyo ni bahati kubali kuwa nae”

“Mimi sitaki kuwa na mpenzi yoyote, mwambie sitaki”

Sasa akawa anilazimisha ila nikakataa, akanishawishi kwa maneno mengi mara Justin msafi, ammetokea Dar sijui nini yani maneno mengi. Sasa kipindi hicho nikawa mkali mnoo kilichoniumiza ni baada ya kuona baba na mtoto wote wananitaka, Hata pale nyumbani nikabadilika kwenye makundi ya stori usiku nikawa sishiriki.

Ukaribu wangu na Ostadh Othman ukaendelea, akawa beneti na mimi. Othman akawa anipa sifa nyingi ambazo nilihisi mimi sina. Akiniambia kuwa

“Unajua wewe ni Genious, wewe ni mjanja, ooh Hesha wewe ni mrembo”

Sasa akawa kila akija pale haondoki bila kuniona kaonyesha kunijali sana mara anibebe eti ananifanyisha zoezi kwakua mimi kibonge au anipeleke msituni eti kubadilisha mazingira. Sasa ikafikia hatua kule kwenda kupikiwa na kufanya usafi hataki waende akina Rahma, basi siku moja akaniita kwake kufika akaniambia

“Unajisiaje kuwa hapa?”
“Najisikia furaha tu yani”
"Kuanzia leo nitakuwa nakuita Bi.hesha, la Anna silitaki”
"Mmh kwanini?”
"Nimelipenda tu harafu ujue nini?”
"Nambie”…………………..ITAENDELEA.

JE USTADH OTHMAN ANATAKA KUMWAMBIA NINI HESHA? JE WAMEPENDANA NINI USIKOSE KUJUA ALICHOMWAMBIA, SOMA SEHEMU IJAYO KWA SH 200 TU.

NUKUU “Katika maisha hujui kesho yako na ya jana yalishapita hivyo ifurahie leo kwasababu ndio siku uliyobakiwa nayo tu. Hakuna haja kumchukia anaekuchukia wewe muda wote kuwa bize kumpenda anekupenda (Hivyo tu)” Anna sasa naona yupo bize kumpenda anaempenda, Hisia za mapenzi hazionekani lakini kila mmoja anahisi tu ndani ya moyo wake jinsi alivyo na hisia kwa mwenzake na hapo lazima uzionyeshe tu"
 
JINA LA SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA!
(Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA 14
MTUNZI: Man Middo Tz
INSTAGRAM: @middotz_
"Kuanzia keo nitakuwa nakuita Bi.hesha, la Anna silitaki”
"Mmh kwanini?”
"Nimelipenda tu harafu ujue nini?”
"Nambie”…………………..Songanayo.

"Hapa ni nyumbani kwako uwe huru”
"😲Kwangu??
"Yaap kuanzia leo usipokuja kupika wewe nitalala njaa au nitakula kwa mama lishe.
"Sikuelew Othman”
"Huelewi nini?”
"Tangu nikufahamu sijawahi kukuelewa”
"🤣🤣Acha papara utaelewa..twende nikurudishe nyumbani.
"Sitaki"
"Kwanini"
"Sijaridhika"
"Hapan wewe ni mwanafunzi twende"
"Othman "(huku nalia)
"Naam"
"Kwanini umekuja maishani mwangu?"
"Hahhaaa Bi hesha bwana…. mambo si hayo sasa hebu ngoja nikuoneshe”

Akaanza kuimba nachi nyingi nying huku akicheza vizuri kama walivokuwa wanacheza pale huku amemipa simu niangalie video zile huku anafuatisha kuimba, Aisee nilihisi kulegea nilihisi raha mno. Nikamwambia

“Unajua kucheza kesho uje kule ucheze” akasema

"Hapana kule siwezi hadi wewe uje huku” nikaguma mhh.
"Aya twende"

"Nikasimama" Tukaanza kurudi nilikua na furaha hatari yani, njiani sasa ilikuwa vituko tu sitamani tufike...tulifka kam saa 2 kasoro. Basi kufika yeye akasalimia pale akaondoka mimi nilisalimia tu kwa pamoja “mambo”nikapitiliza ndani.

Kitendo cha Othuman kuondoka wakaja madogo wakorofi wa mtaa..wanaimba na kupiga makopo, kila mtu pale siku ile aliamini nimetoka kufanya mapenzi na Ustadh Othman, sasa wakawa wanaimba

"Heeyyuuu heyyu ameliwa Heeyuuu ana mimba Heyuu...tumuogope Hesha anamimba ..amepewa ukimwiii”

Khaa!! wakaja kugonga mlango nitoke cha ajabu hadi wale wenyeji wangu na kina Justin wapo wanacheka. Asee nikashangaa sana ilionekana kama vile ni kitu wamekipanga au wanachokifurahia aisee nilipata aibu ambayo pengine sikuwahi kupata, lakini sikujua kama ule ni mwanzo tu makubwa yanafuatia, Sasa uku machozi yananitoka nikajifumgia mlango sikutoka mpaka asubuhi.

Ilipofika asubuhi sikwenda shule wenzangu wakawa wameenda, nikaanza kukumbuka yale matukio ya jana kule kwa Othman (Ochu) alivokuwa ananifanya niwe happy, sauti yake nzuri anavodance asee nikasahau yote niliyoaibishwa usiku, nikawa natabasamu kwa furaha mara mlango wa chumbani ukagongwa nikafunga kanga nikatoka kwenda kuangalia nikafungua mara Ochu akajaa mikononi kwangu akanikumbatia

"Khaa wewe!!"
"Nini sasa."
"Umefika sasa ngapi hapa" akacheka
"Hahahaaah! Nililala hapa"
"Mhh! Ochu acha uongo bhn!"
"True bibie"
"Aya subiri nivae nije sebuleni"

Akanchum kwenye paji la uso akatoka, Nikamfuata sebleni tukakaa kupiga stori mambo mengi mengi dini elimu na vitu vingine...sasa akaniuliza swali

“Hesha samahan”
"Bila samahani Ochu"

“Mbona hupendi kwenda shule na nimejaribu kukuchunguza sana watu wanakudharau sana, hakuna mtu yuko tayari kuongelea habari yoyote kuhusu wewe. Lakini pia upo lafu sana, shule hushirikiani na watu,hujijali na kwa ninavyokufahamu mbona upo tofauti na watu wengine wanavyoamini. Kwanza sijawahi ona msichana mdogo mwenye upeo kamaa wako lakini hakuna anaelitambua hili”

Yaan mpaka anamaliza swali lilelenye maelezo marefu mimi huku napambana na moyo nilikuwa najiambia “Moyo wangu leo hakuna kudondosha chozi mbele ya Othman tulia hivyo hivyo leo onesha tabasamu la kinafiki siku ipite”
Aliyvonitaka nijibu kwanza nilicheka, yes kicheko kilitoka nikamwambia

“Nitazame vizuri”
Akanigeukia akanishika mikono Nikamwambia

“Napenda kusoma mno napenda kuitwa msomi sana, siku za mbele lakini nachukia shule sana sipendi kwenda shule hata kidogo, kuna siku nitakuelezea” nikaendelea kumwambia kuwa

“Kuhusu kujijali mimi ni mtu smart sana, siku za mbele tena nitaitwa mrembo, ila kwasasa acha iwe hivyo..nashindwa kujiweka smart maana nitaitwa mwizi au nitachekwa pia...na zaidi naomba usiifuatilie historia yangu kwa watu kama mimi ambavyo sijawahi kujua wewe ni nani kwa kuambiwa na mtu, ukitaka chochote niulize mimi, kwa leo tuishie hapo”

Mpaka nafunga mdomo nafumbua macho nilikuta mtoto wa kiume mashavu yanatiririka chozi, nikainuka nikamfuta kwa mikono yangu...akanichumu akanimbia

“Twende kwangu” Weeee tukio la jana usiku la...”amegongwa, ana mimba Malaya, ana ukimwi, anatok na cheusi” likajirudia mara mia kichwani………………ITAENDELEA

JE ATAKUBALI KWENDA KWA OCHU? JE OCHU ANAZAWADI GANI KAMUANDALIA HESH(ANNA)?JE ATAISHI KWA AMANI NA WENZAKE WASHANZA KUONYESHA KUMCHUKIA? USIKOSE KIFUATACHO.

NUKUU “Katika maisha unaweza kukosa furaha kwa miaka harafu ukaja kupata faraja kutokwa kwa mtu ambae hukuwahi kurajia kama angekuja katika maisha yako. Hivyo Kumbuka kuwa: Siku zote akiondoka yule ambae hukudhania angeondoka katika maisha yako, Atakuja yule ambae hukurajia angekuja katika maisha yako. Kila tukio katika maisha yako linakusudio lake, Kamwe usiache kuchukua Funzo katika kila tukio la maisha yako”

Sh 200 tu kupata mwendelezo, MALIPO 0655 969 973.
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA!
(Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA 15
MTUNZI: Man Middo Tz
instagram @middotz_
.
.
.
ILIPOISHIA…………Aliyvonitaka nijibu kwanza nilicheka, yes kicheko kilitoka nikamwambia
“Nitazame vizuri”
Akanigeukia akanishika mikono Nikamwambia

“Napenda kusoma mno napenda kuitwa msomi sana, siku za mbele lakini nachukia shule sana sipendi kwenda shule hata kidogo, kuna siku nitakuelezea” nikaendelea kumwambia kuwa

“Kuhusu kujijali mimi ni mtu smart sana, siku za mbele tena nitaitwa mrembo, ila kwasasa acha iwe hivyo..nashindwa kujiweka smart maana nitaitwa mwizi au nitachekwa pia...na zaidi naomba usiifuatilie historia yangu kwa watu kama mimi ambavyo sijawahi kujua wewe ni nani kwa kuambiwa na mtu, ukitaka chochote niulize mimi, kwa leo tuishie hapo”

Mpaka nafunga mdomo nafumbua macho nilikuta mtoto wa kiume mashavu yanatiririka chozi, nikainuka nikamfuta kwa mikono yangu...akanichumu akanimbia
“Twende kwangu” Weeee tukio la jana usiku la...”amegongwa, ana mimba Malaya, ana ukimwi, anatok na cheusi” likajirudia mara mia kichwani………………SONGANAYO

Basi nikamwambia tu kwa upole kuwa “Ochu naomba leo nisiende kwasababu ya tukio la jana” bahati nzuri akanilewa, akasema

“Nikuletee zawadi gani?” nikajibu
“Glucose na Jojo” akacheka kisha akanichum akatoka.

Sasa siku hiyo wakati Ochu anatoka akakutana na Rahma mlangoni mmh! Hata Ochu alipomsalimia Rahma hakuitikia! Nikajisemea kuwa leo ni siku mbaya kwangu na maisha yangu hapa yatakua magumu kuanzia sasa.

Rahma hata alipoingia hakunisemesha chochote, usoni alionyesha kukarisirika na mimi nikaona nikijishaua kunyanyua mdomo wangu hapa italeta shida nikanyuti zangu. Sasa maajabu hata Da Matrona alipokuja hawakunisemesha mmh! Mguno ndio kitu kilikua kimebaki. Basi usiku wakasema

“Kuna kikao watu wote wawepo sebleni”
Mmh! Nikaguna tena ila nikatii wito, kufika kwenye kikao Da Matrona akaanza kusema kuwa

“Tumeitana hapa ili kuongea tabia za baadhi ya watu kati yetu kuwa mbaya, watu wamebadilika. Hesha umebadilika sana mdogo wangu kuna tabia unaonyesha sio nzuri” mara Rahma akadakia

“Ni kweli maana mchana nimemkuta akifanya mapenzi na Ochu hapa sebleni hiyo tabia sijapenda”

“Khee! Yani hapa sebleni! Ndio maana siku ile kina side walikuja kuimba vile kumbe unatembea na Ustadhi Othuman”

Sasa kila mtu akawa naongea la kwake hata nafasi ya kujitetea nikakosa, kwakua yasemwayo si ya kweli machozi yalikua yamenilenga tu na kudondoka ye nyewe mashavuni mwangu. Rahma alionyesha dhahiri kuwa anampenda Ustadh Ochu hivyo alichukia sana ukaribu wangu na Ochu, ingawa shida ipo kwa Ustadh Ochu yeye hampendi kabisa Rahma.

Sasa kila nikifikiria nihame sikujua nihamie wapi, nikifikiria visa hivi nitaviepukaje sikujua na ukizingatia siwezi kuvunja ukaribu na Othman ambae ndio mtu pekee anaejua kuhusu furaha yangu, ndio mtu pekee anaenijali kwa dhati na ndio mtu pekee anaenionyesha upendo wa kweli, hapo moyoni nikajiambia tu kuwa vumilia yataisha haya.

Kitu kingine ikawa kumwambia Ochu nikaona sio sahihi ingawa anapaswa kujua ila shida akijua hata vumilia atawauliza na itakua ugomvi na mimi nitafukuzwa sasa nitaenda wapi!? Hapo ikanibidi ninyamaze kimya huku machozi yakiwa ndio majibu yangu.

Sasa tukiwa tunaendelea na kikao pale akaja Side na Justin wakamwambia Da Matrona kuwa “Tunamuomba Anna”

“Huyo hapo nazani mwenyewe amewasikia”

Basi nikainuka kuwafuata nje, kwanza niliona ni bora niinuke kujinusuru na yale masimango pale ndani. Kufika nje nikawasalimia wakaitikia nashangaa wakaniambia

“Twende Getho”

“Getho! Hapana jaman siwezi kwenda usiku huu harafu naumwa”

Niligoma lakini safari hii kiustaarabu kwasababu hata wao waliniona naumwa, sasa hapo nyumba jinsi zilivyo iko hivi kwetu (Kwa akina matron) kwao na Side harafu kwao na Justin. Sasa nikashangaa kuwambia sitoenda wakacheka sana mmh! Nikaona dharau nikamua kuondoka, sasa ile napiga hatua tu nikapigwa mtama si wakitoto mimi huyo hadi chini tena nimeanguka bila hata balansi nikawauliza

“Mbona nyie wakarofi, ustaarabu gani huu na nimewakosea nini” nikaanza kuwaita ndani

”Da matronaa…. Rahama…” lakini hakuna hata mmoja aliyesikia walishaingia chumbani.

Sasa nikizani ni uatani kumbe wapo siriasi, nikiwa pale chini sina hili wala lile wakanivua yebo zangu(Hrafu zilikua hizo hizo nazitegemea kama viatu vyangu na siku hiyo asubuhi nilivaa nguo nzuri ili kujiweka smart kidogo kwa Ochu zikawa zimechafuka) sasa nikajaribu kupiga kelele nikashangaa nakula ngumi mabuti ikabidi nitulie. Nikiwa pale chini mmoja alinishika miguu wakanivua hizo yebo, blauzi na kitenge nikabaki na sketi tu na vest harafu wakaniambia.

“Kama unavitaka vitu vyako uvifuate Getho”

Machozi yakawa yanatiririka tu nisijue kipi chakufanya, nikawaza nikiwa pale chini kuwa “Nina mikosi gani mie, nimekosea nini mimi kwa Mungu hadi kila siku majanga hayaniishi! Mapungufu yangu ni yapi hadi haya yote yanitokee” lakini sikupata jibu.

Baadae nikajikongoja hadi ndani huku naugulia maumivu ya kipigo, kufika nikawaelezea wenzangu kilichonikuta, wakaonyesha kushangaa ingawa sio sana ila Rahma kasema

“Justin katuambia kuwa eti wewe ni mpenzi wake na ushakula pesa zake sana ila unamzingua kwahiyo ndio maana wamekufanyia hivyo”

“Jaman Justin yeye amenitongoza tu na sijamkubalia chochote harafu aseme mi ni mtu wake, sasa nimewakosea nini hadi kunipiga” niliongea kwa kwi kwi za kilio, siku hiyo nililia hadi nilipopitiwa na usingizi.

Sasa ikawa sijaenda kuchukua vitu vyangu, nikawa nadandia ndala za watu, nikiwaona nikawa naogopa sana kwasababu ya kipigo walichonipa. Na kipindi hicho mama yake Side alikua amesafiri hivyo akawa amepageuza nyumbani kwao kama gesti, kazi ikawa kuingiza mademu tu kila kukicha kwakua yupo huru tu pale. Niliendelea kumficha Othuman asijue chochote kwasababu uadui ndio ungezidi na wenzangu pale ndani wangechukia zaidi.Ustadh Ochu kwa wakati huo ndio alikua ndugu yangu, rafiki japo nilikua sijamwambia chochote kuhusu maisha yangu.

***

Sasa siku zilisonga hivyo nikiwa bado sijapata yebo zangu na ile blauzi, nikaendelea kuvaa za wenzangu kama wakiwa hawapo. Sasa siku moja nikapokea simu kutoka kwa mama akasema

“Nimekutafuta sana hampatikani, kuna mjomba yako amekuja amekusubiri sana hivyo jitahidi kesho uje ili uonane nae kisha urudi shule”

Mmh! Sasa nikawaza naendaje wakati sina viatu, kitenge ninachojifunga nacho wamekichukua kina Side na Justin! Nikahisi kufa nikawa nahisi maumivu makubwa, sasa ikabidi nimueleze dada Matrona

“Dada matron, Pale mama alivyopiga ameniambia niende nyumbani kuna mjomba kaja anataka anione kwakua nina muda sijawahi kuonana nae, sasa kitenge nitegemeacho na viatu ndio wamebeba akina Side sijui hata nafanyaje” akaniambia kuwa

“Subiri niongee nao wakurudishie” akaongea nao baadae akaniambia kuwa “Justin kakubali baadae twende ukupe” nikamwambia

“Da Matrona samahani lakini naomba ukanichukulie” Kwa huruma nilimuomba lakini mwenzangu akawa mkali akisema

“Yani nimekuombea harafu nakuchukua tena unataka niende mimi kwani nilipeleka mimi”

Mmh!! Ikabidi niwe mpole tu, na kwa jinsi nilivyomnyonge sikua na jinsi. Basi jioni tukawa tumetoka matembezi yani siku hiyo sikua na raha kabisa, tulivyorudi njian Da Matrona akaniambia

“Tupite hapo uchukue vitu vyako”

Kweli akabisha hodi wakasema “ingieni” mimi nikasita Da Matrona akaingia wakapiga stori kidogo na Justin mimi bado nipo nje baadae akatoka akasema “Nenda kaangalie vitu vyako uko ndani” sasa ikawa nawaza “MMh! Humu ndani itakuaje kama sio kubakwa tu”……..ITAENDELEA.

JE UNADHANI HESHA ATAPONA HUMO NDANI? JE WATAMUACHA SALAMA NA KUMPATIA VITU VYAKE? USIKOSE EPISODE YA 16.

NUKUU “Usiwaaminiwatu ambao hisia zao hubadilika kila wakati. Waamini watu ambao hisia zao zinabaki vile vile hata wakati unapo badilika” “Watalaumu na kulalamika kwanini umebadilika, lakini hawataona kamwe ni tabia zao ndizo zilizokufanya ubadilike”

Chukua hii “OGOPA rafiki au ndugu anayejaribu kushinda moyo wako, kwa lengo la kuwa mshinani wako. Kuwa makini usiamini mtu yoyote. Hapa HESHA anatakiwa awe makini kwa Rahma kwasababu Rahma Hisia zake kwa Othuman zinampelekea kutaka kuushinda moyo wa Hesha huku akimlaumu Hesha kuwa Amebadilika kumbe yeye ndio amebadilika, Zingatia sana”

Kwa sh 200 tu nakupatia mwendelezo wa stoti hii pendwa nakutumia whatsapp 0655 969 973 man Middo.
 
SIMULIZI: SABABU NI KIFO CHAKO BABA!
(Kisa cha kweli cha kusisimua)
SEHEMU YA 16
MTUNZI: Man Middo Tz

ILIPOISHIA…………….Akaniambia kuwa “Subiri niongee nao wakurudishie” akaongea nao baadae akaniambia kuwa “Justin kakubali baadae twende ukupe” nikamwambia

“Da Matrona samahani lakini naomba ukanichukulie” Kwa huruma nilimuomba lakini mwenzangu akawa mkali akisema

“Yani nimekuombea harafu nakuchukua tena unataka niende mimi kwani nilipeleka mimi”

Mmh!! Ikabidi niwe mpole tu, na kwa jinsi nilivyomnyonge sikua na jinsi. Basi jioni tukawa tumetoka matembezi yani siku hiyo sikua na raha kabisa, tulivyorudi njian Da Matrona akaniambia

“Tupite hapo uchukue vitu vyako”
Kweli akabisha hodi wakasema “ingieni” mimi nikasita Da Matrona akaingia wakapiga stori kidogo na Justin mimi bado nipo nje baadae akatoka akasema “Nenda kaangalie vitu vyako uko ndani” sasa ikawa nawaza “MMh! Humu ndani itakuaje kama sio kubakwa tu”………..SONGANAYO.

“Mlango wa chumbani upo wazi harafu uko ndani kuna vitu vya wadada wengi kwahiyo ingia uchukue na Side hayupo”
Nikajpa ujasiri nikaingia Khee! Kumbe Side yupo waliponiona tu wakapeana ishara ya ushindi Side akamwambia Justin

“Piga kazi dogo, mtoto mdogo kama huyu anakusumbua hivi”

Wakapeana 5 nikazibiwa njia, Side akatoka nje, Sasa Side alivyotoka tu Justin akanionyesha kufuli na funguo akaanza kunitukana sasa matusi yanguoni mengine hata hayaelezeki

“Malaya mkubwa wewe unajifanya keki wakati hujui hata kuoga unaliwa na waislam mpumbavu wee…”

Yani matusi kibao, kweli akafunga mlango akaja kunipalamia mwilini, lakini nikagundua kwamba namzidi nguvu, yeye ni mtoto wa Dar mayai tu. Njia iliyokuepo ni kuwa yeye anasimu kwahiyo nikizingua tu anampigia Side, Sasa akataka nivue nguo mwenyewe kwa hiari nikaanza kujenga nae urafiki kwa muda ule.

“Justin hii sio njia sahihi, kama unanipenda upo muda sahihi tutafanya usifanye hivi niamini” akasema

“Kama hutaki humu umefuata nini?”
Hapo nikahamaki inamaana huyu hajui kuwa kuna nguo zangu! Hapo nikajsemea moyoni

“Yani Usichana wangu nilioutunza na nilioahidi kumpatia atakaenipenda leo hii nimpe kibaka! Aisee hapana!”

Harafu sasa wakati huo nikawa nawaza je wakitufuma humu itakuaje, wakati huo nilikua nimevalia khanga nimeifunga shingoni, na kakibodi ka mkanda mweusi na taiti nyeusi tena katikati inaning’nia imeshachanika muda tu sasa nikawaza

“Sasa hivi nilivyovaa nikimvulia si atanitangaza huyu? Naje wakitufuma si itaonekana nimekubali mwenyewe humu ndani?” aisee hapo nikachoka balaa.

Sasa mwanaume muda huo Justin mzuka ushampanda ameshavua nguo zote amebaki na boksa tu harafu akinishika anatumia nguvu sana, nilipoona namzidi nguvu amepoa nikachukua simu nikamuomba password kisimu cha batani tu lakini aliweka password basi akanipa nikatumia akili zakuzaliwa nikamtumia Side sms nikijdai ni Justin kuwa

“Oya njo tayari nimemaliza” lakini wakati huo huo nikamsikia mama yake Justin akiita

“Justin… Justin …Justin… weweee Justin.....”
Asee Justin aliishiwa nguvu akaanza kuomba Side aje lakini nikamnyima password maana nilizibadilisha kuhofia Side akija atanipiga, sasa hapo ndani purukushani ndio zikazidi kila mtu anafikiria namna natokaje pale ndani ili kujinusuru. Ila mama Justin alionekana kama kuna kitu anakijua kuhusu mimi na Mwanae maana nikamsikia ameenda pale ninapoishi kwa akina Da matron kuuliza

“Hodi humu, Matrona Hesha yupo ndani” akajibwa

“Hapana yupo na Justin ila hatujui wapo wapi”

Mmh! Nilihisi mkojo kabisa unakaribia kutoka, nje kukatawala kimya ingawa kuna minong’ono niliisikia walionekana kuteta jambo uko nje, basi baada ya dakika 5 mlango ukaanza kugongwa kwa nguvu uku wanaita

“Hesha….. Justin…… weee Heshaa….. Justin…”

Hatukuitika asee ila sikua na wa kumlaumu ingawaje Da Matrona ni kama alitengeneza mazingira kwa akina Justin juu yangu. Sasa nikawa sina jinsi zaidi ya kukumbuka matukio yote yaliyonitokea kwa muda mfupi vile.

Hatimae nje kote wakajaa wanafunzi waliopangisha mtaa ule wote, watu wote wazima wakajaa, harafu Mganga hakuwepo alikua kwa mke mdogo akapigiwa akaja, mama Side mwenye Nyumba nae hakua mbali sana alikua ameenda kumuuguza mgonjwa ndani ya kata hiyo hiyo nae akapigiwa simu akaja. Sasa pale ikawa mimi na Justin ndio hatupo Daah haya mambo usiombe yakukute simuliwa tu, ikawa huko ndani kulia sio kulia sijui nini ila machozi yanatiririka tu. Tukawasikia wakisema

“Humu ndani kuna wawili harafu mmoja ndio kabana mlango kaondoka, ila mwanamke atakua ndani”

Sasa wakawa hawajui kuwa ndani nipo na Side au Justin, namba ya Side ikatafutwa akawa hapokei wakatumwa watu kwend akumtafuta akaja huku anapiga mkwara balaa kama ujuavyo wakurya.

“Mimi nimefanyaje mpaka mnanitumia watu uko” wazee akamtuliza kwa kumpiga mkwara

“Acha kututisha tunakupeleka polisi sasaivi, hebu fungua mlango huo haraka”

Kweli akaja kafungua kwa nguvu.. Aisee wakati huo nilikua nimejinyoosha kwenye mavi ya mbuzi humo ndani kama nimekufa kuepuka aibu kumbe hata kupoteza fahamu sikupoteza. Sasa wakaingia wamama watu wazima kama wanne wakanikuta nimelala Justin akatolewa nje wakapigishwa magoti na mwenzake Side. Basi wale wamama kakasema

“Mmh! Jaman mtoto mdogo hivi mara hii ushaanza ngono tena kwenye nyumba za wakubwa, tulikua tunakutetea sana lakini kumbe wewe ndio wa hovyo, binti umetutia aibu sana”

Nilijikunyata nilipopata tu balansi sijui nilikurupukaje huyo hadi ndani kwetu ninapoishi, watu wengi hawa kuniona, nikachukua sweta la shule na kitenge nikavaa nikazunguka nyuma ya nyumba nikatulia. Baadae wakanza kunitafuta huku wanaimba wanapiga madumu kuzunguka nyumba aisee nilikimbia porini mbali sana siku hiyo nililala kichakani hadi asubuhi………………..ITAENDELEA.

JE HESHA HAKUPATA MATIZO HUKO PORINI? JE KULIVYOKUCHA ALIRUDI WAPI KULE KWA AKINA MATRONA AU ALIENDA KWAO KUOGOPA AIBU?


NUKUU “Inawezekana maisha unaoishi leo ni ndoto ya mamilioni ya watu, Hivyo muda wote katika maisha yako ridhika na maisha yako, kuwa na furaha kila wakati. Kuna watu kama Hesha anatamani awe na furaha uliyonayo, uhuru ulionao, mavazi uliyonayo, marafiki ulionao, ndugu ulionao lakini hakipati anaishia kupatwa na matatizo kila siku.
Kama umebarikiwa furaha, Uhuru, unavaa vizuri, unakula vizuri, unafamilia inakupenda, ndugu wanakupenda, marafiki wanakupenda basi mshukukuru Mungu kwasababu wewe ni tajiri ila hujui tu, hebu acha kulalamika kuhusu pesa unamkufuru Mungu, ishi ukifurahia neema alizokupatia Mungu”
 
Back
Top Bottom