Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Mijitu ipo inasubiri nianze masimulizi ianze kutukana,simulizi zipo za kutosha mkuu kutoka kwangu ila sasa nawaza kupoteza bando,pesa na muda kwa baadhi ya watu wajinga wasiokuwa na shukurani
Hao achana nao mkuu, wasikutoe kwenye reli. Kama unaamini dunia ina majaribu basi hao ndiyo akina majaribu wenyewe.
Kama safari yako ya maisha itakosa watu wa aina hiyo nakushauri ujifinye kwa nguvu, maana huenda utakuwa either upo ndotoni unaota au utakua umeshakufa😃.
Ukikutana na wato hao basi shukuru Mungu kwamba kumbe bado upo hai na kuna watu wanakufuatilia.
Ikiwa unaandika hadithi unafikisha readers milions na watu wanao comment wanafika 6K, unahitaji ni cha zaidi hapo, ili kikuthibitishie kuwa kazi zako zinakubalika?
 
Nashauri tuitishe "MAANDAMANO YA AMANI" JamiiForums ya kumtaka ndugu Santos06 kusimamimia ahadi yake! Au awajibike!

Tutatoa muongozo wa maandamano hayo ya amani, ambayo yataanza viwanja vya JF Entertainment kupitia mitaa ya JF Story, JF Jukwaa La Sheria na kumalizikia mitaa ya JF Intelligence!
 
Nashauri tuitishe "MAANDAMANO YA AMANI" JamiiForums ya kumtaka ndugu Santos06 kusimamimia ahadi yake! Au awajibike!

Tutatoa muongozo wa maandamano hayo ya amani, ambayo yataanza viwanja vya JF Entertainment kupitia mitaa ya JF Story, JF Jukwaa La Sheria na kumalizikia mitaa ya JF Intelligence!
Nafunga mkono hoja

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
ILIPOISHIA:
“Nimepata salamu zako kwamba umechagua kuwa tajiri, ombi lako limekubaliwa lakini kuna masharti inatakiwa kabla siku zako saba hazijaisha, uwe umeshaanza kuyafuata, vinginevyo utakufa,” alisema yule mwanamke, macho yakanitoka pima.
SASA ENDELEA...
Nilijiweka vizuri pale chini nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kusikia ataniambia nini, akanitazama machoni kisha akashusha pumzi ndefu na kunisogelea.
“Kwa nini umeamua kupita njia hii?” aliniuliza kwa sauti ya upole, nikashindwa kuelewa alikuwa anamaanisha nini.
“Unalingana na kijana wangu ambaye mwezi wa kumi na mbili angekuwa anatimiza miaka 21, makosa yangu yamesababisha niishi maisha ya kujuta kila siku, sitaki mtu mwingine apite njia kama niliyowahi kupita mimi na kusababisha nimpoteze mwanangu kipenzi,” alisema lakini wala maneno yake hayakuniingia akilini.
“Umeshawishiwa na mtu yeyote au ni maamuzi yako mwenyewe?”
“Nimeamua mwenyewe, wala hakuna aliyenishawishi.”
Kwa jinsi majibu yangu yalivyokuwa, yule mwanamke alishindwa kuendelea kunihoji maana nilishafikia uamuzi ndani ya moyo wangu na hakukuwa na jinsi yoyote ambayo ningebadilisha uamuzi huo.
“Unatakiwa kuwa makini sana na aina ya maisha utakayokuwa unaishi, hutakiwi kunywa pombe wala kuvuta sigara, hutakiwi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke yeyote mpaka utakapooa, hutakiwi kulala kitandani, utakuwa unalala chini na hutakiwi kula nyama nyekundu, mengine ni ya vitendo zaidi, nisubiri,” alisema mwanamke huyo na kutoka.
Nilibaki nayatafakari yale masharti aliyonipa, sikuona jambo lolote la kunizuia kwa sababu kama ishu ya ulevi, sikuwa nakunywa pombe wala kuvuta sigara, achilia mbali bangi ingawa katika makuzi ya ujana, kuna wakati nimewahi kujaribu na kuishia kudhalilika.
Suala la uhusiano wa kimapenzi, nilichokuwa nimekiamua kutoka ndani ya moyo wangu, ni kwamba kama Rahma akikubaliana na mimi, nitamuoa awe mke wangu wa ndoa maana alikuwa na kila kitu nilichokuwa nakihitaji, achilia mbali tofauti yetu ya umri. Suala la kutolala kitandani, nalo pia halikuwa tatizo kwangu kwa sbaabu maisha yetu ya kule kijijini, tulishazoea kulala kwenye vitanda vya kamba au kulala chini kwenye mkeka kwa hiyo hilo pia halikuwa tatizo kwangu.
Suala la kula nyama nalo sikuona kama ni shida kwa sababu maisha ya kule kijijini kwetu, nyama tulikuwa tunakula siku za sikukuu au mara chache tunapoenda kuwinda, mboga yetu kubwa ilikuwa ni samaki.
Kimsingi masharti hayo aliyonipa, yalinifanya ile hofu yote niliyokuwa nayo kuhusu kumiliki utajiri, iyeyuke kama theluji iyeyukavyo juani, hamu ya kutamani kuwa na utajiri mkubwa, ikazidi kunijaa.
Moyoni nilijiambia kama masharti yenyewe ndiyo hayo, kwa nini wachawi wanaogopa kuwa matajiri? Wanachokiogopa ni nini hasa? Akilini nilianza kuvuta picha ya jinsi nitakavyokuwa ‘tajiri mtoto’, nikiendesha magari ya kifahari na kuishi kwenye majumba ya gharama kubwa.
Hata ule ushauri alionipa Mkuu pamoja na baba yake Rahma, kwamba kama nataka mambo yasiwe magumu kwangu, nisitamani kuwa na utajiri mkubwa, bali fedha za kawaida tu za kuniwezesha kuishi bila shida, niliutupilia mbali, tabasamu pana likachanua kwenye uso wangu.
Dakika kadhaa baadaye, yule mwanamke alirejea, nikashtuka kumuona akiwa na kisicho cha kawaida. Shingoni alikuwa amebeba nyoka mdogo aliyejiviringisha huku kichwa chake akiwa amekielekezea mbele, akamshika na kumshusha chini, akajiviringisha na kuinua kidogo kichwa chake.
Nilishtuka sana, kama nilivyowahi kueleza, pamoja na ujanja wangu wote, hakuna kitu nilichokuwa naogopa kama nyoka.
“Unashtuka nini? Huyu itabidi umzoee tu,” alisema yule mwanamke, nikawa nimekaa kwa tahadhari kubwa, nikimtazama kwamba akinisogelea tu nikimbie kuelekea nje. Cha ajabu, nilipomchunguza vizuri yule nyoka, alikuwa na madoadoa sawasawa na ya yule nyoka ambaye Mkuu alinichanja na kumlambisha damu yangu.
“Itabidi umtunze na kumheshimu kwa moyo wako wote, huyu ndiye atakayeamua hatima ya utajiri unaoutaka, kadiri anavyozidi kuwa mkubwa ndivyo unayoyataka yatakavyokuwa yanatimia,” alisema mwanamke huyo, bado nikawa najiuliza maswali mengi yasiyo na majibu.
“Unamshangaa kwani ndiyo mara yako ya kwanza kumuona? Hebu vua shati huko,” alisema mwanamke yule, ni hapo ndipo nilipoamini kwamba ni kweli nyoka yule ndiyo yuleyule aliyelambishwa damu yangu na Mkuu.
Nilivua shati, yule mwanamke anachukua wembe na kusogelea, akanichanja kwenye mbavu upande wa kushoto, damu zikaanza kunitoka kwa sababu alivyonichanja alikandamiza mkono, akamchukua yule nyoka ambaye sasa alikuwa akitoa ulimi wake na kuchezesha.
Akamsogeza mpaka pale kwenye jeraha langu, hofu niliyokuwa nayo ilikuwa haielezeki. Simulizi kuhusu nyoka nilizowahi kuzisikia, achilia mbali matukio niliyowahi kushuhudia jinsi watu na mifugo inavyopoteza maisha baada ya kung’atwa na nyoka, vilinifanya niwe mwoga sana kwa viumbe hawa.
Alipomsogeza tu kwenye jeraha, alijikunjua na kunigusa kwa ulimi wake, akaanza kuilamba ile damu kwa kasi kubwa. Muda mfupi tu baadaye, jeraha lilibaki kuwa alama tu, damu zote alizilamba nyoka yule na wala nyingine hazikuendelea kunitoka.
“Utamzoea tu wala usijali, si umeamua mwenyewe?” alisema yule mwanamke huku akitingisha kichupa chenye dawa ya majimaji, akanipaka pale kwenye jeraha kisha akamchukua yule nyoka, safari hii alimuingiza kwenye mfuko uliotengenezwa kwa kipande cha gunia, akatoka na kuniacha nikiwaza sana.
Nimewahi kusikia simulizi za watu waliokuwa wakifuga nyoka wakubwa ndani ya nyumba zao kwa ajili ya imani za kishirikina, sikutaka kuamini kwamba na mimi ndiyo naelekea kwenye maisha hayo, nikaanza kuelewa hatari iliyokuwa mbele yangu.
Hata hivyo, bado shauku ya kuwa tajiri haikuniisha, nilijipa moyo kwamba kama wapo watu ambao wanaweza, kwa nini mimi nishindwe? Muda mfupi baadaye, yule mwanamke alirejea na kuendelea kunielekeza mambo mbalimbali, yaani alivyokuwa akiongea na mimi ni kama tayari nimeshakuwa tajiri maana alikuwa akinipa masharti ya namna ya kutumia fedha.
Aliniambia hata niwe na fedha nyingi kiasi gani, sitakiwi kutoa kumpa mtu yeyote fedha siku za Jumatatu, Jumanne na Jumapili, akaniambia hata kama kuna mtu amepatwa na dharura kubwa na kiwango kidogo tu cha fedha kinaweza kumsaidia, sitakiwi kabisa kutoa hata shilingi kumi kwenye siku hizo alizonitajia.
Akaniambia pia kwamba katika siku hizo nilizokuwa na uwezo wa kutoa fedha, muda wa kutoa fedha kumpa mtu yeyote au kufanya kitu chochotye kinachohusiana na fedha, ni saa kumi na mbili jioni, kabla jua halijazama. Maelezo hayo yalinishangaza sana, nikawa najiuliza maswali mengi kichwani yaliyokosa majibu.
Baadaye, aliniambia kwamba natakiwa kurudi tena nyumbani kwake hapo baada ya siku sita kwa ajili ya kwenda kukamilisha baadhi ya mambo. Alinipa mkono na kunitakia maisha mema ya utajiri, mimi bado macho yangu yakawa kwenye ule mfuko aliomuweka yule nyoka mdogo.
Baadaye baba na baba yake Rahma walikuja kunichukua, wakamshukuru mwanamke huyo, tukatoka na safari ya kurejea nyumbani ikaanza. Tayari ilishagonga saa nane za usiku, tukawa tunatembea kwa miguu kuelekea kwenye barabara kubwa ya lami.
Kutoka nyumbani kwa mwanamke huyo mpaka kwenye barabara ya lami, kulikuwa na umbali mrefu sana na kibaya zaidi, ni kwamba tulikuwa tunapita kwenye pori kubwa ambalo kwa usiku ule lilikuwa likitisha sana.
Tukiwa tunaendelea kuchanja mbuga, baba akiwa mbele na baba yake Rahma akiwa nyuma, mara tulianza kusikia sauti za ajabu kutoka ndani ya pori lile, huku kukiwa na purukushani kubwa, mapigo ya moyo wangu yalilipuka na kuanza kunienda mbio kuliko kawaida.

Usikose sehemu inayofuata...🙏🙏🙏
 
ILIPOISHIA:
“Nimepata salamu zako kwamba umechagua kuwa tajiri, ombi lako limekubaliwa lakini kuna masharti inatakiwa kabla siku zako saba hazijaisha, uwe umeshaanza kuyafuata, vinginevyo utakufa,” alisema yule mwanamke, macho yakanitoka pima.
SASA ENDELEA...
Nilijiweka vizuri pale chini nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kusikia ataniambia nini, akanitazama machoni kisha akashusha pumzi ndefu na kunisogelea.
“Kwa nini umeamua kupita njia hii?” aliniuliza kwa sauti ya upole, nikashindwa kuelewa alikuwa anamaanisha nini.
“Unalingana na kijana wangu ambaye mwezi wa kumi na mbili angekuwa anatimiza miaka 21, makosa yangu yamesababisha niishi maisha ya kujuta kila siku, sitaki mtu mwingine apite njia kama niliyowahi kupita mimi na kusababisha nimpoteze mwanangu kipenzi,” alisema lakini wala maneno yake hayakuniingia akilini.
“Umeshawishiwa na mtu yeyote au ni maamuzi yako mwenyewe?”
“Nimeamua mwenyewe, wala hakuna aliyenishawishi.”
Kwa jinsi majibu yangu yalivyokuwa, yule mwanamke alishindwa kuendelea kunihoji maana nilishafikia uamuzi ndani ya moyo wangu na hakukuwa na jinsi yoyote ambayo ningebadilisha uamuzi huo.
“Unatakiwa kuwa makini sana na aina ya maisha utakayokuwa unaishi, hutakiwi kunywa pombe wala kuvuta sigara, hutakiwi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke yeyote mpaka utakapooa, hutakiwi kulala kitandani, utakuwa unalala chini na hutakiwi kula nyama nyekundu, mengine ni ya vitendo zaidi, nisubiri,” alisema mwanamke huyo na kutoka.
Nilibaki nayatafakari yale masharti aliyonipa, sikuona jambo lolote la kunizuia kwa sababu kama ishu ya ulevi, sikuwa nakunywa pombe wala kuvuta sigara, achilia mbali bangi ingawa katika makuzi ya ujana, kuna wakati nimewahi kujaribu na kuishia kudhalilika.
Suala la uhusiano wa kimapenzi, nilichokuwa nimekiamua kutoka ndani ya moyo wangu, ni kwamba kama Rahma akikubaliana na mimi, nitamuoa awe mke wangu wa ndoa maana alikuwa na kila kitu nilichokuwa nakihitaji, achilia mbali tofauti yetu ya umri. Suala la kutolala kitandani, nalo pia halikuwa tatizo kwangu kwa sbaabu maisha yetu ya kule kijijini, tulishazoea kulala kwenye vitanda vya kamba au kulala chini kwenye mkeka kwa hiyo hilo pia halikuwa tatizo kwangu.
Suala la kula nyama nalo sikuona kama ni shida kwa sababu maisha ya kule kijijini kwetu, nyama tulikuwa tunakula siku za sikukuu au mara chache tunapoenda kuwinda, mboga yetu kubwa ilikuwa ni samaki.
Kimsingi masharti hayo aliyonipa, yalinifanya ile hofu yote niliyokuwa nayo kuhusu kumiliki utajiri, iyeyuke kama theluji iyeyukavyo juani, hamu ya kutamani kuwa na utajiri mkubwa, ikazidi kunijaa.
Moyoni nilijiambia kama masharti yenyewe ndiyo hayo, kwa nini wachawi wanaogopa kuwa matajiri? Wanachokiogopa ni nini hasa? Akilini nilianza kuvuta picha ya jinsi nitakavyokuwa ‘tajiri mtoto’, nikiendesha magari ya kifahari na kuishi kwenye majumba ya gharama kubwa.
Hata ule ushauri alionipa Mkuu pamoja na baba yake Rahma, kwamba kama nataka mambo yasiwe magumu kwangu, nisitamani kuwa na utajiri mkubwa, bali fedha za kawaida tu za kuniwezesha kuishi bila shida, niliutupilia mbali, tabasamu pana likachanua kwenye uso wangu.
Dakika kadhaa baadaye, yule mwanamke alirejea, nikashtuka kumuona akiwa na kisicho cha kawaida. Shingoni alikuwa amebeba nyoka mdogo aliyejiviringisha huku kichwa chake akiwa amekielekezea mbele, akamshika na kumshusha chini, akajiviringisha na kuinua kidogo kichwa chake.
Nilishtuka sana, kama nilivyowahi kueleza, pamoja na ujanja wangu wote, hakuna kitu nilichokuwa naogopa kama nyoka.
“Unashtuka nini? Huyu itabidi umzoee tu,” alisema yule mwanamke, nikawa nimekaa kwa tahadhari kubwa, nikimtazama kwamba akinisogelea tu nikimbie kuelekea nje. Cha ajabu, nilipomchunguza vizuri yule nyoka, alikuwa na madoadoa sawasawa na ya yule nyoka ambaye Mkuu alinichanja na kumlambisha damu yangu.
“Itabidi umtunze na kumheshimu kwa moyo wako wote, huyu ndiye atakayeamua hatima ya utajiri unaoutaka, kadiri anavyozidi kuwa mkubwa ndivyo unayoyataka yatakavyokuwa yanatimia,” alisema mwanamke huyo, bado nikawa najiuliza maswali mengi yasiyo na majibu.
“Unamshangaa kwani ndiyo mara yako ya kwanza kumuona? Hebu vua shati huko,” alisema mwanamke yule, ni hapo ndipo nilipoamini kwamba ni kweli nyoka yule ndiyo yuleyule aliyelambishwa damu yangu na Mkuu.
Nilivua shati, yule mwanamke anachukua wembe na kusogelea, akanichanja kwenye mbavu upande wa kushoto, damu zikaanza kunitoka kwa sababu alivyonichanja alikandamiza mkono, akamchukua yule nyoka ambaye sasa alikuwa akitoa ulimi wake na kuchezesha.
Akamsogeza mpaka pale kwenye jeraha langu, hofu niliyokuwa nayo ilikuwa haielezeki. Simulizi kuhusu nyoka nilizowahi kuzisikia, achilia mbali matukio niliyowahi kushuhudia jinsi watu na mifugo inavyopoteza maisha baada ya kung’atwa na nyoka, vilinifanya niwe mwoga sana kwa viumbe hawa.
Alipomsogeza tu kwenye jeraha, alijikunjua na kunigusa kwa ulimi wake, akaanza kuilamba ile damu kwa kasi kubwa. Muda mfupi tu baadaye, jeraha lilibaki kuwa alama tu, damu zote alizilamba nyoka yule na wala nyingine hazikuendelea kunitoka.
“Utamzoea tu wala usijali, si umeamua mwenyewe?” alisema yule mwanamke huku akitingisha kichupa chenye dawa ya majimaji, akanipaka pale kwenye jeraha kisha akamchukua yule nyoka, safari hii alimuingiza kwenye mfuko uliotengenezwa kwa kipande cha gunia, akatoka na kuniacha nikiwaza sana.
Nimewahi kusikia simulizi za watu waliokuwa wakifuga nyoka wakubwa ndani ya nyumba zao kwa ajili ya imani za kishirikina, sikutaka kuamini kwamba na mimi ndiyo naelekea kwenye maisha hayo, nikaanza kuelewa hatari iliyokuwa mbele yangu.
Hata hivyo, bado shauku ya kuwa tajiri haikuniisha, nilijipa moyo kwamba kama wapo watu ambao wanaweza, kwa nini mimi nishindwe? Muda mfupi baadaye, yule mwanamke alirejea na kuendelea kunielekeza mambo mbalimbali, yaani alivyokuwa akiongea na mimi ni kama tayari nimeshakuwa tajiri maana alikuwa akinipa masharti ya namna ya kutumia fedha.
Aliniambia hata niwe na fedha nyingi kiasi gani, sitakiwi kutoa kumpa mtu yeyote fedha siku za Jumatatu, Jumanne na Jumapili, akaniambia hata kama kuna mtu amepatwa na dharura kubwa na kiwango kidogo tu cha fedha kinaweza kumsaidia, sitakiwi kabisa kutoa hata shilingi kumi kwenye siku hizo alizonitajia.
Akaniambia pia kwamba katika siku hizo nilizokuwa na uwezo wa kutoa fedha, muda wa kutoa fedha kumpa mtu yeyote au kufanya kitu chochotye kinachohusiana na fedha, ni saa kumi na mbili jioni, kabla jua halijazama. Maelezo hayo yalinishangaza sana, nikawa najiuliza maswali mengi kichwani yaliyokosa majibu.
Baadaye, aliniambia kwamba natakiwa kurudi tena nyumbani kwake hapo baada ya siku sita kwa ajili ya kwenda kukamilisha baadhi ya mambo. Alinipa mkono na kunitakia maisha mema ya utajiri, mimi bado macho yangu yakawa kwenye ule mfuko aliomuweka yule nyoka mdogo.
Baadaye baba na baba yake Rahma walikuja kunichukua, wakamshukuru mwanamke huyo, tukatoka na safari ya kurejea nyumbani ikaanza. Tayari ilishagonga saa nane za usiku, tukawa tunatembea kwa miguu kuelekea kwenye barabara kubwa ya lami.
Kutoka nyumbani kwa mwanamke huyo mpaka kwenye barabara ya lami, kulikuwa na umbali mrefu sana na kibaya zaidi, ni kwamba tulikuwa tunapita kwenye pori kubwa ambalo kwa usiku ule lilikuwa likitisha sana.
Tukiwa tunaendelea kuchanja mbuga, baba akiwa mbele na baba yake Rahma akiwa nyuma, mara tulianza kusikia sauti za ajabu kutoka ndani ya pori lile, huku kukiwa na purukushani kubwa, mapigo ya moyo wangu yalilipuka na kuanza kunienda mbio kuliko kawaida.

Usikose sehemu inayofuata...🙏🙏🙏
63 Hiyo
 
#64

ILIPOISHIA:
Tukiwa tunaendelea kuchanja mbuga, baba akiwa mbele na baba yake Rahma akiwa nyuma, mara tulianza kusikia sauti za ajabu kutoka ndani ya pori lile, huku kukiwa na purukushani kubwa, mapigo ya moyo wangu yalilipuka na kuanza kunienda mbio kuliko kawaida.
SASA ENDELEA...

“Nakufaaa! Naku...fa...aa,” sauti ya mwanamke ilisikika, aliporudia mara ya pili kuimba msaada, sauti yake ilikuwa ikikwamakwama na muda mfupi baadaye akaanza kukoroma kuonesha kwamba mtu au watu waliokuwa wakitaka kumdhuru tayari walishafanikisha lengo lao.
Tofauti na hali niliyokuwa nayo mimi, baba na baba yake Rahma hawakuonesha kushtuka chochote, yaani ilikuwa ni kama hakuna kilichotokea na wala hakuna aliyeshughulika kwa chochote.
Muda mfupi baadaye, harufu ya damu mbichi ilitawala eneo lote lile, milio ya bundi na midege mingine ya ajabu ikazidi kuifanya hali iwe ya kutisha mno. Baba aliendelea kupiga hatua ndefundefu, hukumoyo wangu ukiwa umepondwapondwa kwa hofu na mshtuko, na mimi nikawa naongeza mwendo, miguu yangu ikitetemeka kuliko kawaida.

“Unaogopa nini? Hili linaitwa pori la kafara, huku ndiyo watu wanakokuja kutolea makafara ili mambo yao yafanikiwe,” alisema baba yake Rahma huku tukiendelea kusonga mbele, sikumjibu chochote maana bado nilikuwa natetemeka sana.
Jambo ambalo mpaka leo huwa silipatii majibu, ni kwa nini watu wenye imani za giza hawaoni hatari kabisa kuyakatisha maisha ya mtu mwingine? Ni kweli kwamba sote tutakufa na kifo hakiepukiki lakini kwa nini uyakatishe maisha ya mtu mwingine kwa sababu zako binafsi?
Japokuwa na mimi nimefanya sana huo mchezo, natamani kama utokee muujiza nguvu zote za giza zipotee. Ukweli ambao watu wengi hawaujui, katika vifo vinavyotokea kila siku, iwe ni kwa ajali, magonjwa, watu kujinyonga au kuuana, nguvu za giza zinahusika kwa asilimia kubwa sana.
Kuna matukio mengine unaweza kuona kama ni kifo cha kawaida tu lakini mtu mwenye uwezo wa kuona mambo kwa jicho la tatu, anakuwa anaelewa mchezo mzima ulivyotokea. Si kila kifo kinachotokea kipo kama unavyoweza kudhani, humu duniani kuna mambo mengi sana yaliyojificha na kuna watu wanawaonea sana wenzao na kundi kubwa linaloonewa sana, ni wale watu wasio na imani thabiti ndani ya mioyo yao.
Basi tulifika mpaka barabarani, kwa kuwa muda ulikuwa umeenda sana, hakukuwa na magari yoyote yaliyokuwa yakipita, barabara ilikuwa kimya kabisa. Nilitegemea baba atasema tutafute sehemu ya kuondokea kama kawaida yetu maana nilikuwa nimchoka sana lakini safari hii alizungumza kitu cha tofauti.
Alisemakwa sababu tulikuwa tumebeba kitu cha muhimu sana, ilikuwa ni lazima tufike nyumbani kwa njia za kawaida. Aliposema tumebeba kitu muhimu sikumuelewa kwa sababu kiukweli hakuna hata mmoja kati yetu aliyekuwa na mzigo wowote. Tulianza kutembea pembezoni mwa barabara ileile ya lami tuliyojia, huku wote tukiwa kimya kabisa. Utaratibu wetu ulikuwa uleule, baba mbele, mimi katikati na baba Rahma nyuma.
Kwa bahati nzuri, tulipofika mbele kidogo, kuna Fuso lilikuwa likitokea upande wa mashambani, likiwa na shehena ya mananasi, kama ujuavyo tena Bagamoyo kunalimwa sana matunda.
Harakaharaka baba alimpungia mkono dereva, akasimamisha gari kabla hajaingia kwenye barabara ya lami, akamfuata na kuzungumza naye ambapo sekunde chache baadaye, baba alitupa ishara kwamba tupande.
Nadhani walishakubaliana, ikawa ahueni maana nilikuwa nikiiwazia sana ile safari. Gari lilikuwa limejaza mananasi mpaka juu kabisa, ikabidi tupande na kukaa juu ya mabomba na kujishikilia vizuri, dereva akaliingiza gari kwenye barabara ya lami na safari ikaendelea.
Japokuwa kule juu kulikuw ana upepo mkali unaochoma mpaka ndani ya kifua, ilibidi tuvumilie maana ilikuwa bora kuliko kutembea kwa miguu. Baada ya kama dakika hamsini hivi, tuliwasili jijini Dar, tukateremka kwenye kituo cha Mwenge, tukamshukuru sana yule dereva, yeye akaendelea na safari yake na sisi tukaanza kutembea kuelekea nyumbani.
Kitu kingine ambacho nilijifunza lakini nisingependa kukizungumzia sana leo, maduka mengi, hasa yale makubwa, yanakuwa na ulinzi wa nguvu za giza hasa nyakati za usiku ambapo kama una uwezo wa kuona mambo yaliyojificha, unaweza kustaajabu sana.
Hii dunia ina mambo mengi sana yaliyojificha, kama nioivyosema, sitaki kuelezea sana kuhusu hili. Basi tuliendelea na safari yetu mpaka tulipofika nyumbani, tayari ilishagonga saa tisa na nusu.
“Unatakiwa kuwa mtulivu na msiri, hakuna kitu cha ajabu tena kwako, umenielewa,” baba aliniambia kwa kauli ya msisitizo wakati tukiagana kwa ajili ya kila mmoja kwenda kulala lakini sikumuelewa anamaanisha nini.
“Kuanzia leo utakuwa unalala peke yako, chumba chako kinatakiwa kuwa kimefungwa muda wote na usiruhusu watu kuingiaingia, hata awe nani, umenielewa?” alisema baba, baba yake Rahma akawa anatingisha kichwa kuonesha kwamba anaunga mkono kile alichokisema baba.
Bado sikuwa naelewa kwa nini wananiambia vile, baba akahitimisha kwa kuniambia kwamba eti hategemei kunisikia nikifanya jambo lolote la ajabu. Tuliagana, nikaingia chumbani kwangu, kweli yule ndugu yangu niliyekuwa nalala naye siku mojamoja hakuwepo, kwa hiyo nilikuwa peke yangu.
Kwa jinsi nilivyokuwa nimechoka, sikutaka hata kufanya kitu kitu chochote, nikavua nguo zote, nikazima taa na kujilaza kitandani. Mwili wangu ulikuwa na maumivu sehemu mbalimbali, lakini pale yule mwanamke aliponichanja usiku huo palikuwa na maumivu makali zaidi.
Nikiwa bado natafakari mambo chungu nzima yaliyotokea kwa siku nzima, nilisikia kitu kilichonishtua sana. Chini ya kitanda changu kulikuwa kama na purukushani fulani hivi kwa mbali, ikabidi harakaharaka niinuke na kwenda kuwasha taa.
Nikainama chini kwa tahadhari kubwa na kuchungulia uvunguni, katika hali ambayo sikuitegemea kabisa, nilikiona kile kimfuko kilichotengenezwa kwa kipande cha gunia, nilichokionakule kwa yule mtaalamu kikiwa chini ya kitanda changu.
Ni kimfuko hichohicho ndicho yule mtaalamu tuliyetoka kwake usiku huo, alichomuweka yule nyoka mdogo baada ya kumlambisha damu yangu. Kilichonishtua zaidi, kimfuko kilikuwa tupu, kwa akili za harakaharaka nikahisi kwamba lazima zile purukushani nilizokuwa nazisikia, zilikuwa ni za yule nyoka akihangaika kutoka.
Sasa kimfuko kimefikaje chumbani kwangu? Na kama kile nilichokuwa nakihisi ni kweli, yule nyoka alikuwa mle ndani, ningelalaje? Nilijikuta usingizi wote ukiniisha, harakaharaka nikapanda juu ya kitanda na kukaa kwenye uchago wa kitanda ili hata akipanda kitandani, asiweze kunifikia.
Ni hapo ndipo nilipoanza kuelewa kauli za baba zilikuwa na maana gani, kuanzia ile ya kule njiani kwamba ‘tumebeba kitu muhimu sana’, mpaka yale maneno aliyoyazungumza muda mfupi uliopita kabla kila mmoja hajaenda kulala.
Nilijiapiza kwamba sitalala mpaka kupambazuke, na ukizingatia tayari muda ulishaenda sana, niliona isiwe tabu. Lakini waliosema usingizi ndugu yake kifo hawakukosea, hata sijui nini kilitokea, nilipokuja kushtuka baadaye, nilijikuta nimelala kitandani na kibaya zaidi, hata taa ilikuwa imezimwa.
Mshtuko nilioupata ulikuwa hauelezeki, nikafumbua macho na kuyakodoa kama nitaona chochote lakini nilijitahidi nisitingishike hata sehemu moja kwenye mwili wangu. Nikiwa nimejikausha kama gogo, nilihisi hali fulani kwenye ile sehemu yule mwanamke aliponichanja usiku huo.
Nilihisi kama kuna kitu kinanilamba hivi, nikaanza kutetemeka huku nikiendelea kujikausha nisisababishe mtikisiko wa aina yoyote, nilipozidi kuvuta utulivu, nikahisi kuna kitu cha baridi kinatingishikatingisha upande ule niliokuwa nalambwa, mapigo ya moyo yakawa yanadunda kama nimetoka kukimbia mbio za mita mia moja.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
#65

ILIPOISHIA:
Nilihisi kama kuna kitu kinanilamba hivi, nikaanza kutetemeka huku nikiendelea kujikausha nisisababishe mtikisiko wa aina yoyote, nilipozidi kuvuta utulivu, nikahisi kuna kitu cha baridi kinatingishikatingisha upande ule niliokuwa nalambwa, mapigo ya moyo yakawa yanadunda kama nimetoka kukimbia mbio za mita mia moja.
SASA ENDELEA...
Nilitulia tuli huku nikiendelea kutetemeka, mara nikaanza kuhisi kile kitu kikitambaa na kunivuka mwili, kutoka upande mmoja kuelekea upande mwingine. Japokuwa kulikuwa na giza niliweza kukitambua vizuri kiumbe hicho kuwa alikuwa ni nyoka. Hata sijui ushujaa wa kutulia vile niliupata wapi maana kama nilivyowahi kusema, hakuna kitu nilichokuwa nakiogopa maishani mwangu kama nyoka.
Basi yule nyoka mdogo alinitambuka na kupotelea upande wa pili wa kitanda, nikashusha pumzi ndefu kisha kwa tahadhari kubwa nikainuka pale nilipokuwa nimelala, nikasimama kwenye uchago wa kitanda na kujivuta mpaka kwenye swichi ya taa, nikaiwasha.

Japokuwa kulikuwa na baridi kali ya usiku, mwili wote ulikuwa umelowa jasho, nikajitazama kwenye lile jeraha langu ubavuni, nikashtuka kugundua kwamba lilikuwa limeanza kujichimba na kutengeneza kidonda. Kumbe wakati yule nyoka akinilamba, alikuwa akitoa ganda la juu ambalo lilikuwa likiashiria kuanza kupona, nikashtuka mno huku nikiwa sielewi nini hatma yangu.
Cha ajabu ni kwamba safari hii sikuwa nasikia maumivu kabisa. Nikageuka na kutazama pale kitandani, hapakuwa na kitu zaidi ya shuka, nikalivuta na kujaribu kujikung’uta nikihofia kwamba yule nyoka anaweza kuwa bado yupo lakini hakukuwa na chochote.
Nikashuka na kuchungulia chini ya kitanda, pale palipokuwa na ule mfuko uliotengenezwa kwa kipande cha gunia. Cha ajabu, ulikuwa umefungwa vilevile, nikashusha pumzi ndefu na kurudi kitandani.
Kama ingekuwa amri yangu, siku hiyo nisingelala kabisa lakini usingizi ulikuwa ukinitesa sana. Nilichoamua, ilikuwa ni kufungua mlango na kuuegesha ili kama hali ikitokea tena, nitoke mbio mpaka nje. Sikuzima tena taa kama mwanzo, nikataka kuona nini kitatokea tena.
Nilipojiegesha kitandani tu, usingizi mzito ulinipitia, nilipokuja kuzinduka, tayari kulishakuwa kumepambazuka kabisa, harakaharaka nikashuka kitandani na kuchungulia kule chini ya kitanda.
Cha ajabu ni kwamba ule mfuko haukuwepo, niliangaza kila kona lakini sikuuona, nikahisi labda yule nyoka alitambaa nao na kujifuicha kwenye nguo zilizokuwa chini, nikapekua kila sehemu lakini sikuona dalili zozote.
“Unatafuta nini?” sauti ya baba ilinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo, nikashusha pumzi ndefu na kumtazama usoni, naye akawa ananitazama.
“Kuna kitu kimenitokea usiku sijakielewa.”
“Kitu gani?” baba aliniuliza kwa mkato, ikabidi niinue shati na kumuonesha pale ubavuni palipokuwa na kidonda, nikaanza kumueleza jinsi nilivyoshtuka na kukutana na mauzauza ya yule nyoka chumbani kwangu na jinsi alivyokuwa akinilamba pale kwenye kidonda.
Tofauti na nilivyotegemea, baba alicheka kwa dharau, akaniambia kama naipenda pepo kwa nini naogopa kufa? Sikumuelewa anamaanisha nini, ikabidi nimhoji, akanijibu kwa mafumbo na kutoka zake, akaniacha nikiwa na mawazo tele kichwani mwangu.
Baadaye nilitoka na kwenda kuoga, nikarudi na kujiandaa kisha nikatoka na kwenda kibarazani ambako baba yake Rahma alikuwa amekaa akisoma kitabu. Nilipomsalimia, aliacha kila alichokuwa anakifanya na kuitikia salamu yangu kwa uchangamfu.
Kwa jinsi alivyonipokea, nilipata nguvu ya kumuuliza kwa kina kuhusu mambo mbalimbali ambayo nilikuwa siyaelewi, akaniambia jambo ambalo lilinishtua sana. Aliniambia kwamba usiku wakati tukirejea nyumbani kutoka Bagamoyo, kuna sehemu tulipita na kusikia mwanamke akipiga kelele za kuomba msaada.
Akaniambia kwenye msitu ule ndipo mahali watu waliochagua njia kama yangu, ya kuwa na utajiri wa kichawi, wanapoenda kutolea makafara yao, akaniambia hata mimi mambo yakichanganya nitakuwa naenda kutoa kafara kwenye msitu huo. Nilishtuka sana kutokana na maneno aliyoniambia, nikawa nahisi kama nipo ndotoni.
“Ukiwa mwanachama wa kawaida, unatoa kafara za kawaida, kama ambazo tayari wewe umeshazitoa, si unakumbuka umeshatoa mara ngapi?” aliniuliza baba yake Rahma huku akigeuka huku na kule kuhakikisha hakuna anayetusikiliza.
“Mara mbili!” Nilimjibu. Kiukweli mpaka wakati huo tayari nilikuwa nimesababisha matukio yaliyoondoa nafsi za watu wasio na hatia wawili, la kwanza lilikuwa ni lile la ajali iliyoyakatisha maisha ya yule mtoto wa Mlandizi na ya pili ikiwa ni ile ya bodaboda aliyepata ajali mbaya baada ya kugongana na mimi, mita chache kutoka pale kwenye msiba wa yule mtoto.
Jaribio lingine la kumtoa kafara Sadoki, rafiki yangu kipenzi wa Chunya lilikuwa limegonga mwamba huku ikibakia kidogo nidhalilike kutokana na nguvu ya upako aliyokuwa nayo Sadoki na mama yake.
“Sasa ka njia uliyochagua, utatakiwa kuwa unatoa sadaka za damu mara nyingi kadiri iwezekanavyo, ndiyo maana kuanzia mwanzo nilikwambia kwamba utajiri huo ni mgumu sana, bora ubaki maskini,” alisema baba yake Rahma.
Japokuwa kweli niliogopa kwa kiasi fulani, lakini tamaa ya utajiri ilishawaka ndani ya moyo wangu kiasi kwamba sikuwa nataka kusikia jambo lingine lolote la kunirudisha nyuma. Nilimkatisha kijanja na kumuuliza kuhusu kile kilichotokea usiku kuhusu yule nyoka.
Alinifafanulia kwamba ni kawaida ya mtu yeyote anayemiliki au anayetaka kumiliki utajiri kwa nguvu za giza, kufuga mnyama huyo na kuongeza kwamba chakula chake kikubwa, ukiachana na vyakula vya kawaida ambavyo nyoka hupewa, ni lazima kila siku awe anakunywa damu yangu.
“Mungu wangu!” nilishtuka sana na kujikuta nimelitaja jina la Mungu. Kwa maneno hayo ya baba yake Rahma, ni kwamba kile kilichotokea usiku haukuwa muujiza na kwamba ni jambo ambalo litakuwa linatokea kila siku kwa kipindi chote cha maisha yangu, nilijikuta nikichoka.
“Kadiri utakavyokuwa unamtunza vizuri na kumpa mahitaji yake yote, ndivyo atakavyokuwa anaongezeka ukubwa na kadiri atakavyokuwa anaongezeka ndivyo utajiri wako utakavyokuwa unaongezeka kwa hiyo ukiwa mvumilivu, unaweza kufika mbali,” alisema baba yake Rahma, nikawa na shauku kubwa ya kuendelea kumuuliza, hasa kuhusu nyoka huyo lakini mazungumzo yetu yalikatishwa na Rahma.
“Kaka Togo za asubuhi? Naomba unisindikize dukani mara moja,” alisema Rahma kwa heshima, baba yake akanipa ishara kwamba niende, nikainuka na kutoka naye.
Tofauti na siku zote, pale nje palikuwa peupe kabisa, wale madereva Bajaj na bodaboda hawakuwepo, Rahma akaniambia eti walikuwa wameamua kuhamisha kituo chao na kukipeleka sehemu nyinginekwa sababu pale hakuna abiria.
Nilijikuta nikicheka tu maana ukweli haukuwa hivyo, moyoni nilibaki nikijiuliza, ina maana nimekuwa na nguvu kiasi cha kuwatisha watu kiasi kile?
“Mlikuwa mnazungumza nini na baba? Maana naona mnaelewana sana, sijawahi kumuona baba yangu akiwa karibu na mtu kama ilivyo kwako, siku hizi hata mimi hanipendi kama anavyokupenda wewe,” Rahma alisema wakati tukitembea taratibu kuelekea dukani.
Sikumjibu kitu chochote cha maana zaidi ya kuleta masihara kwa sababu jana yake nilipotaka kumweleza ukweli aliniona kama nimechanganyikiwa.
“Mbona mimi nakuuliza maswali ya msingi wewe unanijibu kimasihara?” Rahma alinihoji, ikabidi niache kuchekacheka na kuvaa ‘usiriasi’, nikamwambia hata mimi mwenyewe sielewi.
“Tunaenda wapi kwani?”
“Nataka twende pale tulipokaa jana, nahitaji kuzungumza na wewe,” aliniambia, moyo wangu ulisita kwani niliamini naweza kukutana na hali kama ya jana Rahma akaendelea kuniona mwendawazimu. Hata hivyo nilishindwa kumkatalia, tukaelekea mpaka pale dukani.
Cha ajabu, tulipofika tu, yule dada tuliyemkuta jana yake, aliponiona tu alikurupuka kwa kasi na kukimbia huku akiacha mlango wazi. Hakuwa amevaa nguo na nadhani hiyo ndiyo sababu iliyomfanya akimbie, Rahma akawa anashangaa akiwa haelewi kinachoendelea.
“Mbona unavuja damu nyingi hapo, umepatwa na nini?” alisema Rahma, nilipojitazama pale ubavuni, nilishtuka sana baada ya kuona damu nyingi nzito zikiwa zimenitoka bila mimi mwenyewe kujua chochote na kulowanisha kabisa shati langu.
Je, nini kitafuatia?
Usikose next issue.
 
#66

ILIPOISHIA:
“Mbona unavuja damu nyingi hapo, umepatwa na nini?” alisema Rahma, nilipojitazama pale ubavuni, nilishtuka sana baada ya kuona damu nyingi nzito zikiwa zimenitoka bila mimi mwenyewe kujua chochote na kulowanisha kabisa shati langu.
SASA ENDELEA...

Sikujua nini cha kufanya, nilitamani nirudi haraka ndani kabla mambo hayajazidi kuharibika lakini Rahma akaning’ang’ania, kwanza akitaka kujua kwa nini yule muuzaji alikuwa akinikimbia lakini pili nini kimetokea mpaka shati langu lilowe damu kiasi kile.
Kiukweli sikuwa na majibu, nikawa naendelea kuhangaika kuzuia damu isiendelee kunitoka. Rahma alivua kitenge chake na kunipa, naye akawa ni kama haelewi kilichokuwa kinaendelea.
Tukiwa tunaendelea kuhangaika, mara nilisikia ile hirizi yangu mkononi ikinibana sana, nikajua mambo yameshaharibika. Nilishaambiwa kwamba nikiona inanibana ghafla, ujue mahali nilipo kuna mtu mwenye nguvu za giza na kuna jambo baya anataka kulifanya.

Harakaharaka nilifanya kama nilivyokuwa nimeelekezwa, niliunganisha kidole gumba na kidole kidogo kwenye mkono wa kushoto, nikafanya hivyo kwenye mkono wa kulia, nikaviminya kwa nguvu huku nikigeuka huku na kule kuangalia ni nani atakayeonesha dalili zisizo za kawaida.
Nilifundishwa kwamba kama kuna mtu yeyote anataka kukujaribu kwa nguvu za giza, ukifanya hivyo basi umemkomesha na kama nguvu zake ni ndogo, anaweza kuumbuka hadharani.
“Mmefuata nini hapa?” sauti ya mwanaume ilisikika kutoka kwenye lile duka, wote tukageuka kutazama ni nani aliyekuwa akitusemesha.
“Shikamoo mzee!” Rahma alimsalimu mwanaume mzee aliyekuwa ndani ya duka hilo kwa uchangamfu. Ilionesha wanafahamiana. Badala ya kujibu, yule mzee alimuuliza Rahma mimi ni nani na nimefuata nini pale.
“Ni kaka yangu, anaitwa Togo, tuna mazungumzo ya kifamilia tulitaka tunywe soda huku tukiendelea kuzungumza.”
“Hapana! Hatuuzi soda hapa, ukitaka huduma uje peke yako, siyo na huyo,” alisema mwanaume huyo huku akiwa amenikazia macho, Rahma akashtuka na kunigeukia. Kadiri yule mzee alivyokuwa akizidi kunitazama, na mimi ndivyo nilivyozidi kuminya vidole huku nikiwa nimemkazia macho kwani nilihisi ndiye mbaya wangu mwenyewe.
“Ondokeni! Ondokeni,” alisema mzee huyo kwa kupaza sauti, wateja wengine waliokuwa pembeni wakawa wanashangaa kwa sababu hakukuwa na jambo lolote baya tulilofanya. Rahma aligeuka na kutaka kuondoka huku akishangaa iweje mzee huyo atubadilikie kiasi hicho lakini mimi wala sikutishika kwa sababu nilishaanza kuiona hofu ilivyomjaa ghafla.
Niliendelea kumtazama huku nikiendelea kuminya vidole vyangu kwa nguvu, nikashangaa kumuona akianza kutokwa na jasho jingi huku akitingisha kichwa kama kunipa ishara kwamba niache nilichokuwa nakifanya. Mara alianza kutetemeka, jasho likazidi kumtoka na kufumba na kufumbua, akaanza kutapatapa kama anayetaka kupandwa na kifafa, akadondoka chini kama mzigo, puh!
Kitendo hicho kilinishtua sana kwani alipodondoka tu, ile hirizi nayo iliacha kunibana, sijui nini kilinituma niangalie juu ya mlango wa kuingilia kwenye duka hilo ambalo lilikuwa limejaza vitu vingi vya thamani, nikashtuka mno kuona kitu kama fuvu la mtoto mdogo likiwa limeninginizwa juu ya mlango.
Nikiwa bado nimepigwa na butwaa, nilisikia sauti ya baba kutokea nyuma. Kumbe wakati nikiendelea kuvutana na yule mzee, Rahma alikimbilia nyumbani na kwenda kumuita baba yake pamoja na baba, harakaharaka wakaja.
“Unafanya nini Togo?” baba aliniuliza kwa sauti ya chini, nadhani hakutaka asikike kwa watu ambao walishaanza kukusanyika kwa lengo la kutoa huduma ya kwanza na kutaka kujua nini kimetokea.
“Hamna kitu baba, tulikuwa tunataka kuagiza soda, hakuna kingine,” nilisema huku nikiendelea kukitazama kile kitu kama fuvu.
“Ondoka haraka, hili eneo si salama, fanya haraka,” alisema baba, nikageuka na kukutana ana kwa ana na Rahma ambaye naye alikuwa ananionesha ishara ya kutaka tuondoke haraka eneo hilo maana tayari watu walishajaa.
Nikarudi kinyumenyume, nikajichanganya kwenye umati wa watu waliokuwa wakiendelea kujaa, Rahma akanishika mkono na kuanza kunivuta haraka tuelekee nyumbani.
“Togo, kuna kitu unanificha si ndiyo? Nataka leo unieleze ukweli, ngoja kwanza nikaangalie kinachoendelea, nakuomba usitoke, baba amesema ikibidi nikufungie chumbani kwako na funguo,” Rahma aliniambia huku akipumua kwa kasi, akarudia kunisisitiza kwamba nisitoke kisha harakaharaka akaondoka.
Nilikaa kitandani na kuvua shati ambalo lilikuwa limelowa damu, nikawa najitazama pale damu ilipokuwa inanitoka. Ilikuwa ni kwenye kile kidonda changu, nikawa nashangaa iweje nitokwe na damu nyingi kiasi kile wakati sikuwa nimejitonesha? Nilijiuliza maswali mengi ambayo yote hayakuwa na majibu.
“Ina maana yule ndiyo mmiliki wa lile duka? Kwa nini anatumia uchawi kwenye biashara yake? Kile pale mlangoni ni fuvu kweli? Ina maana alimuua mtoto ili kuvutia wateja kwenye biashara yake?
“Kwa nini yule mdada amekimbia tena kwa mara nyingine, tena akiwa mtupu? Ina maana ndiyo mchezo wake kuuza akiwa hana nguo mwilini?” niliendelea kujiuliza kwa sauti ya chini, maswali yalikuwa mengi sana ndani ya kichwa changu, hata sikujua ni nani atakayenipa majibu.
Dakika kadhaa baadaye, niliwasikia baba na baba yake Rahma wakirejea wakiwa wanazungumza kwa sauti za chinichini. Muda mfupi baadaye, Rahma naye akarejea na kuja moja kwa moja mpaka chumbani kwangu.
“Vipi, nini kimeendelea?” nilimuuliza Rahma huku nikisimama, nikiwa kifua wazi, akashusha pumzi ndefu na kabla hajanijibu chochote, macho yake yakatua kwenye ile hirizi niliyokuwa nimeivaa mkononi, akashtuka kidogo kisha akahamishia macho pale kwenye jeraha dogo ambalo bado lilikuwa likichuruzika damu.
“Hapo umefanya nini?” alisema huku akinisogelea na kuinama kunitazama vizuri, nikarudi nyuma huku nikimuonesha ishara kwamba asiniguse. Akanitazama usoni na kuyagandisha macho yake, tukawa tunatazamana.
“Hizo damu zimetoka wapi?” sauti ya baba ndiyo iliyotuzindua. Kumbe wakati nikipita pale koridoni kuelekea chumbani kwangu, matone ya damu yalikuwa yakidondoka chini mpaka kwenye mlango wangu.
Alipoingia na kunikuta nipo kifua wazi, tukitazamana na Rahma, alinisogelea na kitu cha kwanza, macho yake yalitua pale kwenye jeraha langu, akapatazama kwa sekunde kadhaa kisha akanitazama usoni, naye tukawa tunatazamana.
“Rahma hebu kamuite baba yako haraka,” alisema baba, harakaharaka Rahma akatoka.
“Haya ndiyo mambo niliyokuwa siyataki mimi, umeona huo utajiri unaoutaka ulivyo na mambo magumu? Hutakiwi kutembeatembea mpaka zipite siku saba, siku nyingine utakutana na magwiji watakuua, una bahati yule mzee bado hajakomaa kwenye haya mambo,” alisema baba, akaingiza mkono mfukoni na kutoa karatasi alilokuwa amelikunja, akalifungua na kutoa ungaunga mweusi, akachukua kidogo na kunipaka huku akinitaka kuwa makini.
“Naona na wewe umeanza kuonesha ukidume wako, unawaona watu si ndiyo?” alisema baba huku akiachia tabasamu hafifu. Ilikuwa ni nadra sana kwa baba kutabasamu, akanipigapiga mgongoni huku akiendelea kutabasamu.
Muda mfupi baadaye, baba yake Rahma aliingia, nikashangaa wote wanacheka na kugongesheana mikono, naye akarudia kuniambia kwamba niwe makini na nisiende tena kwenye lile duka, kama nahitaji soda ni bora niagize niletewe nyumbani. Hawakukaa sana, wakatoka na kuniacha mle chumbani, sekunde chache Rahma akaingia tena.
“Nataka uniambie ukweli Togo, nini kinachoendelea?”
“Hujanijibu swali langu kuhusu kilichotokea.”
“Watu wanasema eti yule mzee ni mchawi na biashara zake amekuwa akiziendesha kwa uchawi sasa leo amekutana na kiboko yake, wamempeleka kwa mganga lakini hali yake siyo nzuri,” alisema rahma, nikashusha pumzi ndefu na kukaa vizuri, Rahma akanisogelea huku bado akionesha kuwa na shauku kubwa ndani ya moyo wake.
“Togo wewe ni mchawi?” Rahma aliniuliza swali ambalo lilinishtua mno moyo wangu, nikamtazama, akarudia tena swali lake huku akisisitiza kwamba anataka mimi mwenyewe ndiyo nimweleze ukweli kama kweli nampenda.
Nikashusha pumzi ndefu huku nikijiuliza, nimweleze ukweli? Uamuzi niliofikia, ilikuwa ni kumweleza tu maana hayo ndiyo yalikuwa malengo yangu tangu jana yake, sikutaka kujali ataupokeaje ukweli, nikameza mate na kumtazama.
Je, nini kitafuatia? Usikose muendelezo
 
Back
Top Bottom