Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #161
133.
“Ni Mmarekani, na kuhusu swali la pili, ndio nilikuwa nakuja huko.” Akajibu kifupi Rais na kuendelea. “Kwanza kabisa, ni mwanajeshi ambaye aliwahi kufa. Na baada ya kufa, ndipo Dokta mmoja ambaye naye ni marehemu, aliweza kumfufua kwa kumuingizia kemikali za C.O.D.EX.” Akakatishwa maelezo yake na Agent.
“Hizo kemikali si ndizo zile zilifungiwa miaka kumi iliyopita kwa sababu ya kuwaathiri sana Alex na Alex Junior ambao walikuwa wanajeshi tishio sana duniani.” Akaongea Agent.
“Wewe hayo umeyajuaje wakati yalikuwa ni ya siri kubwa?” Akauliza Rais.
“Kuna vitabu, kaviandika Tariq Haji na kaviita C.O.D.EX, vipo vitatu. Vinaelezea kinagha ubagha yote hayo. Ni kama riwaya, lakini nilipofuatilia, haya mambo ni kweli yalitokea.” Akajibu Agent.
“Okay. Ni kweli ulichoongea. Lakini CIA na FBI pamoja na serikali nzima ya Marekani, walifungua tena ile maabara na safari hii walikuwa wanachukua watu waliokwisha kufa hasa wanajeshi wa Kimarekani ambao walifia vitani au wananchi wenye IQ kubwa ili wawasaidie katika kutengeneza silaha.”
“Kwa hiyo huyo mwanajeshi yupo vipi?” Rais akavuta bahasha fulani na kutupa mezani ambapo Agent aliifungua na kuanza kuangalia baadhi ya picha ambazo zilionesha wanajeshi wa C.O.D.EX wakiwa katika mazoezi yao. Walikuwa wanatisha sana kwa wanachokifanya lakini walionekana kutojali wala kuhisi maumivu.
Baada ya picha hizo, Rais pia akampa kijana anayemuamini simu matata sana na kumchezeshea video ambayo ilionesha wale wanajeshi wakiungua na baadae kurudi katika hali yao ya kawaida. Na picha kadhaa za video zile, zilionesha ukatili na silaha zao hatari wanazotumia. Mwili ukamsisimka Agent.
“Hapa kuna kazi kubwa Mkuu.” Akaongea Agent huku anarudisha vile vitu alivyopewa.
“Ndio maana wanajeshi wetu hawawezi. Anahitajika mtu mjanja na mwenye uelewa wa kuwazuia hata kwa sayansi zake. Naye ni wewe.” Rais akatoa jukumu zito.
“Nahitaji kusoma kwanza na sehemu ambapo nitatengeneza baadhi ya silaha zangu.” Akaongea Agent na Rais akamuelekeza kwenye maabara fulani iliyopo ndani ya Ikulu yake. Kisha akamtolea mafaili baadhi ambayo alitumiwa na CIA kwa ajili ya kumtambulisha mtu wanayetakiwa kukamata. Baada ya hapo, akaanza kumuelekeza mambo mengine mengi ambayo alipewa na CIA. Hadi nusu saa inakatika, Agent alikuwa kashiba maneno mengi ambayo yangemuongoza kwenye msako wake.
****
Ndani ya maabara ambayo ilikuwa ndani ya Ikulu, Agent alikuwa kavaa mawani kubwa myeusi na alikuwa anachanganya vitu kadhaa kwenye chungu cha chuma na ambacho kilikuwa kimepata joto kali na kuwa chekundu sana. Kila alipotupia baadhi ya vitu alivyovijua yeye, moto mkali ulifumuaka na kuzidisha joto ndani ya maabara ile ya Kisayansi.
Baada ya kuridhika, alimwagia mchanganyiko ule kwenye sahani moja kubwa na ya bati. Pini ndo go ndogo nyingi sana zikaonekana ndani ya sahani, naye Agent akatabasamu baada ya kufanikisha zoezi lake la kwanza lakini hakuishia hapo, alizimwagia kemikali fulani ambazo zilifanya pini zile zisimame kwenye sahani na kuchongoka zaidi.
Akabofya kiparaza cha kompyuta yake ambayo alikuwa anatembea nayo, na ile sahani ikaanza kuzunguka taratibu kisha kuhama na kwenda sehemu moja ambayo kulikuwa na kijumba kidogo alichokibuni Agent kwa ajili ya shughuli zake za Kisayansi. Kijumba hicho yeye mwenyewe alikiita UHAI. Akimaanisha ni kijumba kinachoweza kuvipa uhai vitu ambavyo havina uhai.
****
Asubuhi iliyofuata, Agent alionana na Rais na kumuelezea kazi yake ilivyokwenda na alimwambia yupo tayari kwa kazi ambayo kamtuma.
“Sawa kijana wangu. Nakuamini.” Rais aliongea kwa tabasamu na kisha akampa simu yake ambayo safari hii, alimtaka aende kuitazamia chumbani kwake kwa sababu yeye hakai tena ofisi sababu ziara ya siku hiyo ya kwenda Tabora kufungua miradi ya treni za angani. “Humo utaona ni wapi mtuhumiwa wako unatakiwa kumpata. Fanya yako leo hii, apatikane. Nishawaambia kuwa kazi ni leo.” Akaongea Rais baada ya kumkabidhi ile simu.
“Sawa Mkuu.” Agent alikubali na kusimama tayari kwa kuondoka ofisini.
“Agent Zero.” Kijana wa Rais akageuka na kumtazama Rais wake. “Kuna zawadi pia kwa ajili yako ukifanikisha hilo, Dola Milioni Moja inakusubiri na yawezekana ikapanda hadi hamsini.” Akampa taarifa mwanana kijana wake na kumfanya Agent atabasamu na kupiga saluti ya kikakamavu. “Nikutakie kheri katika kazi yako.” Akamaliza na Agent Zero kama alivyomuita, akatoka nje ya ofisi.
****
Furaha kubwa ilikuwa imemtawala Idris ambaye kila wakati alijiona mwenye bahati kukutana na Limasi ambaye kama mapenzi alimpa yote mwanaume yule aliyeficha siri nyingi juu yake. Idris akiwa anarudi nyumbani na zawadi kadhaa alizomnunulia mke wake, alisimama njia panda moja ambayo ilikuwa ina mataa ya usalama barabarani. Ilikuwa yapata saa tatu na robo usiku wakati mataa hayo ya usalama yaliposimamisha gari lake.
Aliamua kutumia muda ule mdogo kupekua zawadi kadhaa alizokuwa amemnunulia mpenzi wake. Wakati anafanya hayo akiwa ndani ya gari lake lingine la gharama, kuna gari moja kubwa aina ya scania lilikuwa linatokea upande wa kushoto kwa kasi ya ajabu na ghafla lilikumba gari la Idris na kulipasua katikati kisha ile sehemu inapokaa injini, ililipuka na kusababisha taflani eneo zima la barabara.
Furaha kubwa ilikuwa imemtawala Idris ambaye kila wakati alijiona mwenye bahati kukutana na Limasi ambaye kama mapenzi, alimpa yote, mwanaume yule aliyeficha siri nyingi juu yake. Idris akiwa anarudi nyumbani na zawadi kadhaa alizomnunulia mke wake, alisimama njia panda moja ambayo ilikuwa ina mataa ya usalama barabarani. Ilikuwa yapata saa tatu na robo usiku wakati mataa hayo ya usalama yaliposimamisha gari lake.
“Ni Mmarekani, na kuhusu swali la pili, ndio nilikuwa nakuja huko.” Akajibu kifupi Rais na kuendelea. “Kwanza kabisa, ni mwanajeshi ambaye aliwahi kufa. Na baada ya kufa, ndipo Dokta mmoja ambaye naye ni marehemu, aliweza kumfufua kwa kumuingizia kemikali za C.O.D.EX.” Akakatishwa maelezo yake na Agent.
“Hizo kemikali si ndizo zile zilifungiwa miaka kumi iliyopita kwa sababu ya kuwaathiri sana Alex na Alex Junior ambao walikuwa wanajeshi tishio sana duniani.” Akaongea Agent.
“Wewe hayo umeyajuaje wakati yalikuwa ni ya siri kubwa?” Akauliza Rais.
“Kuna vitabu, kaviandika Tariq Haji na kaviita C.O.D.EX, vipo vitatu. Vinaelezea kinagha ubagha yote hayo. Ni kama riwaya, lakini nilipofuatilia, haya mambo ni kweli yalitokea.” Akajibu Agent.
“Okay. Ni kweli ulichoongea. Lakini CIA na FBI pamoja na serikali nzima ya Marekani, walifungua tena ile maabara na safari hii walikuwa wanachukua watu waliokwisha kufa hasa wanajeshi wa Kimarekani ambao walifia vitani au wananchi wenye IQ kubwa ili wawasaidie katika kutengeneza silaha.”
“Kwa hiyo huyo mwanajeshi yupo vipi?” Rais akavuta bahasha fulani na kutupa mezani ambapo Agent aliifungua na kuanza kuangalia baadhi ya picha ambazo zilionesha wanajeshi wa C.O.D.EX wakiwa katika mazoezi yao. Walikuwa wanatisha sana kwa wanachokifanya lakini walionekana kutojali wala kuhisi maumivu.
Baada ya picha hizo, Rais pia akampa kijana anayemuamini simu matata sana na kumchezeshea video ambayo ilionesha wale wanajeshi wakiungua na baadae kurudi katika hali yao ya kawaida. Na picha kadhaa za video zile, zilionesha ukatili na silaha zao hatari wanazotumia. Mwili ukamsisimka Agent.
“Hapa kuna kazi kubwa Mkuu.” Akaongea Agent huku anarudisha vile vitu alivyopewa.
“Ndio maana wanajeshi wetu hawawezi. Anahitajika mtu mjanja na mwenye uelewa wa kuwazuia hata kwa sayansi zake. Naye ni wewe.” Rais akatoa jukumu zito.
“Nahitaji kusoma kwanza na sehemu ambapo nitatengeneza baadhi ya silaha zangu.” Akaongea Agent na Rais akamuelekeza kwenye maabara fulani iliyopo ndani ya Ikulu yake. Kisha akamtolea mafaili baadhi ambayo alitumiwa na CIA kwa ajili ya kumtambulisha mtu wanayetakiwa kukamata. Baada ya hapo, akaanza kumuelekeza mambo mengine mengi ambayo alipewa na CIA. Hadi nusu saa inakatika, Agent alikuwa kashiba maneno mengi ambayo yangemuongoza kwenye msako wake.
****
Ndani ya maabara ambayo ilikuwa ndani ya Ikulu, Agent alikuwa kavaa mawani kubwa myeusi na alikuwa anachanganya vitu kadhaa kwenye chungu cha chuma na ambacho kilikuwa kimepata joto kali na kuwa chekundu sana. Kila alipotupia baadhi ya vitu alivyovijua yeye, moto mkali ulifumuaka na kuzidisha joto ndani ya maabara ile ya Kisayansi.
Baada ya kuridhika, alimwagia mchanganyiko ule kwenye sahani moja kubwa na ya bati. Pini ndo go ndogo nyingi sana zikaonekana ndani ya sahani, naye Agent akatabasamu baada ya kufanikisha zoezi lake la kwanza lakini hakuishia hapo, alizimwagia kemikali fulani ambazo zilifanya pini zile zisimame kwenye sahani na kuchongoka zaidi.
Akabofya kiparaza cha kompyuta yake ambayo alikuwa anatembea nayo, na ile sahani ikaanza kuzunguka taratibu kisha kuhama na kwenda sehemu moja ambayo kulikuwa na kijumba kidogo alichokibuni Agent kwa ajili ya shughuli zake za Kisayansi. Kijumba hicho yeye mwenyewe alikiita UHAI. Akimaanisha ni kijumba kinachoweza kuvipa uhai vitu ambavyo havina uhai.
****
Asubuhi iliyofuata, Agent alionana na Rais na kumuelezea kazi yake ilivyokwenda na alimwambia yupo tayari kwa kazi ambayo kamtuma.
“Sawa kijana wangu. Nakuamini.” Rais aliongea kwa tabasamu na kisha akampa simu yake ambayo safari hii, alimtaka aende kuitazamia chumbani kwake kwa sababu yeye hakai tena ofisi sababu ziara ya siku hiyo ya kwenda Tabora kufungua miradi ya treni za angani. “Humo utaona ni wapi mtuhumiwa wako unatakiwa kumpata. Fanya yako leo hii, apatikane. Nishawaambia kuwa kazi ni leo.” Akaongea Rais baada ya kumkabidhi ile simu.
“Sawa Mkuu.” Agent alikubali na kusimama tayari kwa kuondoka ofisini.
“Agent Zero.” Kijana wa Rais akageuka na kumtazama Rais wake. “Kuna zawadi pia kwa ajili yako ukifanikisha hilo, Dola Milioni Moja inakusubiri na yawezekana ikapanda hadi hamsini.” Akampa taarifa mwanana kijana wake na kumfanya Agent atabasamu na kupiga saluti ya kikakamavu. “Nikutakie kheri katika kazi yako.” Akamaliza na Agent Zero kama alivyomuita, akatoka nje ya ofisi.
****
Furaha kubwa ilikuwa imemtawala Idris ambaye kila wakati alijiona mwenye bahati kukutana na Limasi ambaye kama mapenzi alimpa yote mwanaume yule aliyeficha siri nyingi juu yake. Idris akiwa anarudi nyumbani na zawadi kadhaa alizomnunulia mke wake, alisimama njia panda moja ambayo ilikuwa ina mataa ya usalama barabarani. Ilikuwa yapata saa tatu na robo usiku wakati mataa hayo ya usalama yaliposimamisha gari lake.
Aliamua kutumia muda ule mdogo kupekua zawadi kadhaa alizokuwa amemnunulia mpenzi wake. Wakati anafanya hayo akiwa ndani ya gari lake lingine la gharama, kuna gari moja kubwa aina ya scania lilikuwa linatokea upande wa kushoto kwa kasi ya ajabu na ghafla lilikumba gari la Idris na kulipasua katikati kisha ile sehemu inapokaa injini, ililipuka na kusababisha taflani eneo zima la barabara.
Furaha kubwa ilikuwa imemtawala Idris ambaye kila wakati alijiona mwenye bahati kukutana na Limasi ambaye kama mapenzi, alimpa yote, mwanaume yule aliyeficha siri nyingi juu yake. Idris akiwa anarudi nyumbani na zawadi kadhaa alizomnunulia mke wake, alisimama njia panda moja ambayo ilikuwa ina mataa ya usalama barabarani. Ilikuwa yapata saa tatu na robo usiku wakati mataa hayo ya usalama yaliposimamisha gari lake.