Simulizi ya kweli: Niliishi kuzimu siku saba

Nimeanza kuingiwa na giza juu ya hii story umetolewa polisi kwenda kuleta wepesi wa mgonjwa kutoa ushirikiano na polisi hapo hapo umekimbia watu unao wahisi kuwa ni wabaya pasipo kuwataarifu polisi kwanza kuwa kuna watu wanafuatilia nyendo zenu, mpaka kuchukua boda boda. Hapa hapajakaa sawa hata kidogo.
 
it can't be true story aisee[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] ...umewaona kwenye gari ,na polisi wako maeneo hayo ukashindwa kuwashtua, bhac hata kushika plate no daaaah ....ila story tamuuu . Utunzi wako uko mahali pakee[emoji106] [emoji106]
 
nacopy na kupaste huku

SEHEMU YA 21.
ILIPOISHIA:
Nikiwa naendelea kulia, nilipaliwa na mate, hali iliyofanya nikohoe mfululizo, ajabu zaidi, na ule mwili wangu pale kitandani ukakohoa, madaktari wakazidi kupigwa na butwaa, wakawa wanatazamana wakiwa ni kama hawaamini kilichokuwa kinatokea.
SASA ENDELEA...
“Amerejewa na fahamu zake, amezinduka,” alisema daktari mmoja kwa sauti, nikaona pilikapilika zimeanza tena kupamba moto mle wodini. Daktari mmoja akaja kunipima mapigo ya moyo huku akiwatazama wenzake, nikamuona akitingisha kichwa.
Niliendelea kupewa matibabu ya uhakika, kila mmoja akawa anachakarika kwa nafasi yake. Nilimuona daktari mmoja akifungua mlango na kutoka nje, akasogea mpaka pale akina Raya walipokuwa wamekusanyika.
Nikamuona akizungumza nao mambo fulani, ghafla nikamuona Raya akimrukia mwilini kwa furaha, akamkumbatia kwa nguvu kisha akainua mikono juu kama ishara ya kumshukuru Mungu.
Japokuwa sikuwa nimesikia walichokuwa wanakizungumza, niliamini kwamba lazima yule daktari atakuwa ameenda kuwaambia kwamba sikuwa nimekufa kama wanavyofikiria. Nilijikuta nikisisimka sana, yale machozi yaliyokuwa yananitoka yakaacha, nikawa namtazama Raya alivyofurahi kama mwendawazimu.

Nilijikuta nikitabasamu kwa jinsi maichana huyo alivyokuwa amefurahi, nikamuona akimkumbatia kila mtu kwa furaha, huku tabasamu likichanua kwenye uso wake uliokuwa umeloweshwa na machozi. Kumbe vile nilivyokuwa nikitabasamu mwenyewe, hata ule mwili wangu pale kitandani ulikuwa ukitabasamu, nikawaona madaktari wote wakipeana mikono kama ishara ya kupongezana.
Ama kweli hii dunia ina maajabu, nilisema mwanzo na sitaacha kusisitiza, hii dunia ina mambo mengi sana ambayo kwa akili za kawaida ni vigumu sana kuyaelewa. Najua bado kuna watu wengi hawaelewi au hawaamini ninachokisema lakini napenda tu kuwaambia watu kwamba maisha yana siri kubwa sana.
Ni wale tu ambao wako tayari kujifunza vitu vipya kila siku wanaoweza kuendana na kasi halisi ya maisha. Ukitazama kwa juujuu, unaweza kuona kama maisha au uhai wa mtu ni jambo jepesi sana lakini haipo hivyo. Ukiijua thamani halisi ya maisha na uhai, kamwe huwezi kumtendea ubaya binadamu mwenzako, huwezi kuyakatisha maisha ya mtu wala huwezi kuwadharau wengine.
Basi wakati watu wote wakionesha kufurahishwa na maendeleo yangu pale kitandani, mimi mwenyewe nilikuwa nikijihisi hali tofauti kabisa. Japokuwa nilikuwa nimefungwa bandeji kubwa kwenye lile jeraha langu kubwa kifuani na mara kwa mara lilikuwa likisafishwa na kuwekwa dawa nyingine, huku katika ulimwengu wa peke yangu sikuwa nikihisi maumivu hata kidogo.
Hata watu walivyokuwa wakihangaika, nilibaki kuwashangaa tu kwa sababu sikuwa najihisi kama naumwa sehemu yoyote na hata pale walipokuwa wanasema kwamba nimekufa, mwenyewe bado nilikuwa na akili zangu timamu na nilikuwa naelewa kila kitu kilichokuwa kinaendelea.
Katika ukuaji wangu, nimewahi kusikia kwamba mtu anapokufa, anakuwa anaendelea kuishi kwa siku kadhaa, na hata siku ya mazishi yake, huwa mwenyewe anashuhudia anavyozikwa, anaangalia nani analia sana, nani halii, nani anafurahia kifo chake na watu wangapi wamehudhuria kwenye mazishi yake.
Kabla sijatokewa na mkasa huu, na mimi nilikuwa mgumu sana kuamini lakini leo naamini kwamba kumbe hata wafu huwa wanaishi, kwa hiyo usimtendee mtu ubaya ukiamini kwamba akishakufa huo ndiyo mwisho wake, unajidanganya!
Hata katika vitabu mbalimbali vya dini, vinaeleza kwamba kuna maisha baada ya kifo, natamani sana kila mtu awe anaishi maisha yake akielewa kwamba kuna maisha baada ya kifo!
Nikiwa bado nimesimama palepale nikijitazama mwili wangu pale kitandani na watu wote waliokuwa ndani ya wodi hiyo, kwa mara nyingine nilijikuta nikishikwa tena mkono na kuvutwa kwa nguvu na mtu ambaye sikumuona.
Safari hii alikuwa na nguvu pengine kuliko hata mara ile ya kwanza, kufumba na kufumbua nikajikuta nimerudishwa tena kule nilikokuwa mwanzo lakini tofauti yake, safari hii giza halikuwa nene sana wala hakukuwa na milio ya wanyama wa kutisha.
Jambo ambalo bado lilikuwa likifanana, ni kwamba kila nilichokuwa nikikiwaza moyoni, kilikuwa kikisikika kwa sauti ya mwangwi utafikiri nimekitamka mdomoni. Yule mtu hakunisemesha chochote, akaniacha mahali ambapo sipajui kisha akayeyuka kama upepo.
“Jamal! Nisamehe Jamal,” niliisikia sauti ambayo niliitambua kwamba ni ya Shenaiza ikinizungumzisha kwa mbali, ikawa inasikika kwa mwangwi kama sauti nyingine. Nilishtuka sana, kilichonishtua ni kugundua kwamba Shenaiza naye alikuwepo kwenye mazingira yale ya ajabu na kutisha kuliko kawaida.
“Nimekusamehe Shenaiza ila nataka kuufahamu ukweli wako,” nilitamka lakini kama ilivyokuwa mwanzo, sauti haikutoka kabisa, nikashusha pumzi ndefu na kuanza kuzungumzia moyoni, nikarudia maneno yaleyale, kweli sauti ikatoka.
“Mimi sina ubaya wowote na wewe Jamal, haya yote ameyasababisha baba yangu.”
“Baba yako amesababisha kivipi? Na hapa nilipo ni wapi? Nimefikaje?”
“Sijui chochote Jamal, mi nahisi kama nipo ndotoni ila nasikia wewe ulishakufa,” alisema Shenaiza na muda huohuo, nikajikuta nimehama pale nilipokuwepo na kutokezea sehemu nyingine tofauti kabisa. Nilijikuta nimetokezea kwenye chumba cha kifahari, kilichokuwa na kitanda kikubwa na vitu vingine vya thamani.
Juu ya kitanda hicho, alikuwa amelala msichana mrembo ambaye bila hata kuuliza, niligundua kuwa ni Shenaiza. Nilishindwa kuelewa pale ni wapi na imekuwaje nifike pale, pia nikawa najiuliza kuhusu kauli ya Shenaiza kwamba eti mimi nimekufa. Kama Shenaiza amelala, niliyekuwa nazungumza naye ni nani? Au ndiyo maana alisema anahisi kama yupo ndotoni?
“Shenaiza!” nilimuita lakini sauti haikutoka, nikamuita moyoni! Cha ajabu aliitika, nikamuona japokuwa alikuwa amelala, midomo yake ilikuwa ikichezacheza kuonesha kwamba ni yeye ndiye aliyekuwa akizungumza.
“Unasema baba yako ndiyo anahusika na haya yote, hebu niambie kivipi.”
“Siwezi kukwambia chochote Jamal kwa sababu wewe umeshakufa, ila kaa ukielewa kwamba baba yangu siyo mtu mzuri hata kidogo.”
“Nataka uniambia ukweli, ilikuwa ukaipata namba yangu na kuanza kuwasiliana na mimi wakati ukijua kabisa unanisababishia matatizo na kwa sababu gani unang’ang’ania kusema nimekufa?”
”Hayo hayana maana tena Jamal, nakuomba unisamehe kwa kukusababishia kifo.”
“Kifo? Mimi sijafa Shenaiza.”
“Najua naongea na mzimu wako Jamal, nakuomba sana msamaha, siku ya mazishi yako nitajitahidi kufika nikuage, nilikupenda sana lakini ndiyo hivyo tena, Mungu amekuchukua kipindi ambacho hata sijakufaidi, najisikia vibaya sana Jamal.”
“Unazungumza nini? Mimi sijafa Shenaiza! Sijafaaa,” nilisema kwa sauti kubwa huku nikimtingisha pale kitandani azinduke usingizini, ghafla nikashangaa msichana huyo akikurupuka usingizini na kupiga kelele kwa nguvu!
“Mzimuuu! Mzimu wa Jamal umenifuata, nisaidieni nakufaaa!” alisema Shenaiza na kuendelea kupiga kelele, muda mfupi baadaye, mlango wa chumba chake ukafunguliwa, wakaingia wanawake wawili ambao walikuwa wamefanana naye, wakamshika huku na kule na kuanza kumuuliza kilichotokea.
“Umepatwa na nini?”
“Nimetokewa na mzimu.”
“Mzimu? Mzimu gani wakati sasa hivi ni mchana?”
“Nilikuwa nimelala nikatokewa na mzimu wa marehemu Jamal!”
“Mh! Au unaanza kuchanganyikiwa mwenzetu? Jamal gani unayemzungumzia?”
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue
 
SEHEMU YA 22.

ILIPOISHIA:


“Mzimu? Mzimu gani wakati sasa hivi ni mchana?”

“Nilikuwa nimelala nikatokewa na mzimu wa marehemu Jamal!”

“Mh! Au unaanza kuchanganyikiwa mwenzetu? Jamal gani unayemzungumzia?”

SASA ENDELEA…

“Nimeota kabisa naongea na Jamal wakati ameshafariki. Ninachosema ni kweli kabisa, wala siyo kwamba nimeanza kuchanganyikiwa,” Shenaiza alizidi kusisitiza lakini hakuna aliyemuamini.

Tangu aende kuchukuliwa kwa nguvu na walinzi wa baba yake na kurejeshwa kwenye makazi ya siri ya familia yao, Kurasini, alikuwa ni kama amechanganyikiwa. Muda mwingi alikuwa ni mtu wa kulia na kuijutia nafsi yake huku akimlaumu baba yake kwamba alikuwa akimuonea kwa yote aliyokuwa akimfanyia.

Alipokuwa akizidi kusumbua, daktari maalum wa familia hiyo, alikuwa akipewa kazi ya kumdunga dawa za usingizi zilizomfanya alale muda mrefu. Hali hiyo ilimfanya kwa kiasi kikubwa akose hata nafasi ya kufuatilia kilichokuwa kinaendelea kuhusu Jamal, kitu pekee alichokuwa anakijua akilini mwake, ni kwamba kijana huyo alikuwa amefariki dunia baada ya lile tukio ambalo yeye ndiye aliyekuwa chanzo.

“Muiteni dokta.”

“No! I dont need any more sedatives please, im not out of my mind,” (Hapana! Sihitaji tena kuchomwa dawa za usingizi, mimi sijachanganyikiwa) alipiga kelele Shenaiza lakini haikusaidia kitu, muda mfupi baadaye, daktari wao aliingia akiwa na bomba la sindano na kichupa cha dawa mkononi kilichokuwa na maandishi yaliyosomeka Diazepam, akiwa ameongozana na wanaume wawili wenye miili mikubwa.

Shenaiza alijaribu kufurukuta lakini wapi! Akashikiliwa kwa nguvu na wale wanaume, daktari akatoa pamba iliyokuwa imepakwa ‘spirit’, akamsafisha sehemu ya ndani ya mkono wake, mahali kwenye mishipa ya damu na taratibu akazamisha sindano kwenye mshipa wake na kuisukumia ile dawa ndani, muda mfupi baadaye, Shenaiza alianza kuzungumza maneno yasiyoeleweka na kupitiwa na usingizi mzito.

Wakati yote hayo yakiendelea, nilikuwa nikishuhudia kila kitu, bado nikiwa katika hali ileile ambayo hakuna mtu ambaye aliniona ingawa mimi nilikuwa na uwezo wa kuona kila kitu. Kile kitendo cha kushuhudia Shenaiza akifanyiwa ukatili ule, kilinisikitisha sana ndani ya moyo wangu na kunifanya nianze kumtazama Shenaiza kwa sura tofauti kabisa.

Nisiseme uongo, baada ya mfululizo wa matukio yale, mpaka lile la mwisho ambalo liliyabadilisha kabisa maisha yangu na kunifanya nisieleweke kama mimi ni binadamu au maiti, nilikuwa nikimchukia sana kwa kuona kwamba yeye ndiye aliyeniingiza kwenye mtego huo kwa makusudi.

Hata hivyo, kwa kile nilichokishuhudia, nilianza kuamini kwamba huenda haikuwa dhamira ya Shenaiza kuniingiza kwenye matatizo makubwa kiasi kile, nikajikuta nikimuonea huruma na kuwalaani wale waliokuwa wakimfanyia kitendo kile.

Nilijikuta nikiwasonya kwa nguvu. Cha ajabu, ilionesha kwamba walisikia nilivyowasonya kwani wote waliokuwa ndani ya kile chumba, wakiwemo wale ndugu zake Shenaiza waliokuwa wamefanana naye sana, yule daktari na wale walinzi, waligeuka na kuanza kutazama huku na kule.

“Nimesikia kama mtu amesonya, au masikio yangu yamesikia vibaya,” aliuliza mmoja, kila mmoja wao akajibu kwamba na yeye amesikia lakini wakawa hawajui ni nani aliyefanya kitendo hicho. Japokuwa nilikuwa palepale jirani yao, kwenye moja ya kona za chumba hicho, hakuna aliyeniona, baadaye nikawaona wakianza kutoka mmoja baada ya mwingine, kila mmoja akionesha kuwa na hofu kubwa ndani ya moyo wake.

Nilichojifunza, katika maisha ya kawaida, ukijiona upo katika mazingira ambayo hakuna mtu lakini ghafla ukasikia mtu anakusonya kwa sauti lakini ukigeuka humuoni yeyote, jua kwamba eneo hilo hauko peke yako. Kuna mtu au watu wengine wanakuona na pengine hawafurahishwi na unachokifanya.

Ukiwa na akili, inabidi urekebishe kile unachokifanya kwa sababu unaweza kupata matatizo ambayo hakuna anayeweza kuyaelezea, hapa ndipo lile neno ‘katika mazingira ya kutatanisha’ linapotumika. Kwamba unafanya tukio au unapatwa na tukio ambalo katika akili ya kawaida, hakuna anayeweza kuelewa nini hasa kilichotokea.

Basi niliendelea kusimama palepale nikimtazama Shenaiza ambaye tayari alishapitiwa na usingizi mzito, nikawa na shauku kubwa ya kutaka kujua mambo mengi yaliyokuwa yamejificha nyuma ya maisha yake.

“Jamal! Jamal! Jamaaaal!” nilisikia sauti nzito, nene ya kutetemeka ikiliita jina langu kwa nguvu, kabla hata sijajibu chochote, nilishangaa nikichukuliwa pale na kitu kama kimbunga kikali, sekunde chache tu baadaye, nilijikuta nikiwa tena kulekule nilikokuwa mwanzo, giza nene likiwa limetawala kila upande lakini tofauti na awali, nilihisi kama nimesimama juu ya kokoto.

Ile sauti iliyoniita haikusikika tena, ila kwa mbali nikawa nasikia muungurumo kama wa treni likija kwa kasi kubwa pale nilipokuwepo. Muungurumo ulizidi kuongezeka, nikawa nageuka huku na kule kutazama ulikokuwa unatokea lakini sikuona chochote, nikahisi nikiendelea kusimama palepale huenda nikagongwa na treni hilo.

Nilipopiga hatua moja mbele, nilikanyaga kitu kama reli, nikagundua kwamba kumbe nilikuwa kwenye njia ya treni hilo ambalo sikuelewa ni la aina gani kwa sababu ninachojua mimi, treni huwa zinakuwa na taa na huwa haziendi kwa mwendo kasi kiasi hicho.

Ilibidi nichangamke, nikakimbia hatua kadhaa lakini kila nilipokuwa napita, bado nilikuwa nikikanyaga reli, ghafla nikasikia mlio mkali wa honi uliofuatiwa na mwanga mkali wa taa, ni hapo ndipo nilipogundua kuwa treni hilo lilikuwa limenikaribia mno na lilikuwa likija usawa wangu kabisa kiasi kwamba kama nisingefanya chochote kujiokoa, lingenigonga na kunisagasaga.

Cha ajabu zaidi, baada ya kunipigia honi na kunimulika, miguu yangu iliganda palepale nilipokuwa nimesimama, sikuweza hata kutingishika, nikawa nimeganda kama sanamu huku hofu kubwa ikiwa imenijaa moyoni, ilibidi nifumbe macho kwani nilijua huo ndiyo mwisho wa maisha yangu.

Nilisikia kelele za vyuma vikikwaruzana, nadhani ni matairi ya treni na reli baada ya kufunga breki kali, nikasikia nikipulizwa na upepo mkali na kudondokea mita chache mbele, nilipofumbua macho, lile treni lilikuwa limesimama mita chache kutoka pale nilipokuwa nimeangukia, ile taa ikiwa imezimwa lakin likiendelea kunguruma kwa nguvu.

“Panda twende,” ilisikika sauti nzito ya mwanaume, nilipoinua macho yangu, nilimuona mzee mmoja akiwa amekaa sehemu ya dereva, akawa ananipungia mikono akiniashiria nifanye vile alivyoniambia.

Harakaharaka niliinuka, nikalisogelea lile treni ambalo lilikuwa na joto kali, nadhani ni kwa sababu ya kasi liliyokuwa nayo, yule mzee akanionesha niendelee kuelekea nyuma mpaka sehemu ya kupandia, nilifanya hivyo lakini kutokana na giza nene lililokuwepo nilishindwa hata kuona sehemu ya kuelekea, nikashtukia nikishikwa mkono na mtu ambaye wala sikumuona, akanisukumia kwenye ngazi, nikapanda na kuingia ndani ya treni hilo.

Kilichonipa moyo, ndani ya treni hakukuwa na giza kama kule nje, kulikuwa na taa ndogo iliyokuwa na mwanga hafifu uliofanya angalau nione ndani ya lile treni kulivyokuwa. Treni hiyo ilikuwa chakavu sana, kuanzia viti vyake, sakafu na kila kitu ndani yake.

Kulikuwa na abiria kadhaa ambao wote walikuwa wameinamisha vichwa vyao kuonesha kwamba walikuwa wamelala, niliamini kwamba huenda watakuwa wametoka safari ya mbali sana ndiyo maana walichoka vile.

Muda huohuo, treni iliondoka kwa kasi kubwa, kelele za vyuma na muungurumo zikawa zinasikika kwa nguvu huku moshi mwingi ukiingia kupitia madirishani, nilitamani kuuliza tulikuwa tunaelekea wapi lakini hakukuwa na wa kumuuliza. Nilitamani hata kumuona yule mtu aliyenishika na kunisaidia kupanda lakini pia sikumuona, watu wote walikuwa kimya kabisa, nyuso zao wakiwa wameziinamisha.

Treni ilizidi kushika kasi, ikafika kipindi nikawa nahisi kwamba haikanyagi kwenye reli bali inapaa angani kwa jinsi ilivyokuwa ikienda kasi. Ghafla, nilipogeuka huku na kule, nilishtuka kugundua kwamba nilikuwa nimebaki peke yangu kwenye treni hilo, sikukumbuka kama kuna sehemu lilisimama, nikawa najiuliza wale abiria wengine wameenda wapi?

Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.

SEHEMU YA 23
ILIPOISHIA:


Treni ilizidi kushika kasi, ikafika kipindi nikawa nahisi kwamba haikanyagi kwenye reli bali inapaa angani kwa jinsi ilivyokuwa ikienda kasi. Ghafla, nilipogeuka huku na kule, nilishtuka kugundua kwamba nilikuwa nimebaki peke yangu kwenye treni hilo, sikukumbuka kama kuna sehemu lilisimama, nikawa najiuliza wale abiria wengine wameenda wapi?

SASA ENDELEA…

Kuna wakati nilihisi pengine huenda nilikuwa kwenye ndoto lakini bado sikuwa na uwezo wa kuthibitisha kwamba ile ilikuwa ni ndoto, maisha halisi au kitu gani, kila kitu kilikuwa gizani. Treni lilizidi kushika kasi, moshi mwingi ukiwa unazidi kuingia ndani na kufanya hata ule mwanga hafifu niliokuwa nauona awali nao umezwe na moshi huo mweusi.

Ghafla, nilihisi kama naguswa na mtu pembeni yangu, nikajikuta nikiruka kwa hofu kubwa, nilipogeuka na kumtazama aliyenigusa, alionesha ni mwanamke kwa jinsi alivyokuwa amevaa lakini uso wake alikuwa ameuinamisha chini.

“Jamal! Jamal, ni wewe?” alisema yule mtu kwa sauti ya chini lakini ambayo ilisikika vizuri licha ya kelele ya vyuma vya treni lile, muungurumo mkubwa na upepo uliokuwa unavuma.

*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

Badala ya kuitikia, niligeuka na kumtazama kwa hofu kubwa mno, yeye wala hakugeuka kunitazama zaidi ya kuendelea kujiinamia vilevile, akisubiri majibu kutoka kwangu. Licha ya zile kelele na yeye mwenyewe kuzungumza kwa sauti ya chini, bado niliweza kuitambua vyema sauti hiyo, haikuwa ngeni kabisa masikioni mwangu.

“Mbona hunijibu!” aliuliza tena lakini tofauti na mwanzo, sauti yake ilisikika kwa nguvu ikiambatana na mwangwi ambao uliyaumiza masikio yangu.

“Wewe ni nani?” nilimuuliza lakini nikashangaa sauti haitoki, nikakumbuka sheria za huko ambapo haraka nilifumba mdomo na kuzungumzia moyoni, sauti kubwa ikasikika lakini badala ya kunijibu, nikamuona akiinua uso wake taratibu na kunigeukia.

“Mungu wangu!” nilijisemea kwa hofu kubwa. Kwa msaada wa mwanga hafifu uliokuwepo ndani ya treni hiyo, niliweza kumtambua kwamba yule mtu alikuwa ni Shenaiza lakini tofauti na yule ninayemfahamu, maeneo yake ya kwenye macho yalionesha kutokuwa na macho ya kawaida kama binadamu wengine, yalikuwa meusi tii ambayo hata sijui niyafananishe na nini.

“Ni mimi Shenaiza, au umenisahau? Nataka kukufuata huko uliko, nimechoka maisha ya duniani, nichukue Jamal!” alisema na kuanza kugugumia kwa kilio kilichoonesha kwamba yupo kwenye maumivu makali mno.

*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

Nilishindwa kuelewa kilichokuwa kinaendelea, muda mfupi uliopita nilikuwa nikizungumza naye katika kile mwenyewe alichoeleza kwamba yupo ndotoni na ameniona mimi kama mzimu, lakini muda huo tulikuwa tukizungumza kwa kawaida, akiniambia kwamba anahitaji nimchukue!

Kwanza nilishangaa, nimchukue kumpeleka wapi? Na hapo tulipokuwepo ni wapi? Na yeye alitokea wapi kwa sababu wakati mimi napanda kwenye treni hilo la ajabu, hakuwepo, aliingiaje? Nilijiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu.

“Mbona unanishangaa hivyo Jamal?” aliniuliza huku mkono wake mmoja akinishika shingoni, nikashangazwa na jambo jingine kwamba mwili wake ulikuwa wa baridi kuliko kawaida. Nilitamani kupiga kelele kwa hofu niliyokuwa nayo, nilihisi kama nimekutana na kiumbe wa ajabu mwenye sura ya kibinadamu na sasa alikuwa anataka kuyakatisha maisha yangu.

“Usiniogope Jamal! Hata mimi mwanzo nilikuwa nakuogopa lakini hushangai sikuogopi tena?”

“Kwani hapa ni wapi Shenaiza na wewe umefikaje huku?”

“Mh! Hata mimi sielewi hapa ni wapi lakini nafikiri tunaelekea sehemu nzuuuri ambayo ndiyo itakuwa makazi yetu ya milele, si unajua duniani tunapita tu?”

“Sijakuelewa, kwa hiyo hapa siyo duniani?”

“Siyo duniani Jamal, duniani si kule tulikokuwa tunaishi siku zote? Kwani unaona hapa kunafanana na kule?”

“Sasa kama siyo duniani ni wapi na wewe imekuwaje uje huku?”

“Sijui hapa ni wapi, mimi nimekuja huku kwa sababu nimechoka kuishi, yaani kila siku wananichoma dawa za usingizi, nikiamka tu wananichoma tena, leo nimeamua kujiovadozi kwa makusudi ili nife?”

“Niniii? Shenaiza, unazungumzia nini mbona sikuelewi?”

“Nimeamua kukufuata Jamal, kwa kuwa wewe ulikufa na mimi nikiwa ndiyo chanzo, nimeamua na mimi nife tu.”

“Lakini mimi sijafa Shenaiza, mimi niko hai.”

“Ungekuwa hai ndiyo ungekuwa huku? Acha kujidanganya Jamal!”

“Hapana sijafa! Mimi sijafa! Niko haiii,” nilisema kwa sauti kubwa iliyofuatiwa na kilio.

***

Hali ilikuwa ya patashika nguo kuchanika ndani ya makazi ya siri ndani ya jumba la kifahari la baba yake Shenaiza, lililokuwa Kurasini. Hakuna ambaye alielewa nini kimetokea kwa sababu kama ilivyo kawaida, Shenaiza alizinduka kutoka usingizini baada ya dawa alizokuwa amedungwa awali kuisha nguvu.

Tofauti na awamu zote, safari hii alipozinduka usingizini, alijikokota na kuinuka kutoka kitandani kwake, akasogelea mpaka kwenye kabati lililokuwa ndani ya chumba hicho. Mfanyakazi maalum aliyepewa jukumu la kuhakikisha anapata huduma zote muhimu, alishtuka kumuona akiwa amefungua kabati, ikabidi amuwahi na kumlaza kitandani.

“Nasikia njaa sana, kaniletee chakula,” alisema Shenaiza, harakahara yule mhudumu akatoka kwenda kumletea chakula kwani tayari kilishaandaliwa kwa ajili yake. Alipotoka tu, Shenaiza alisimama na kurudi tena pale kabatini.

*Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi

Muda mfupi baadaye, alichukua kichupa kidogo pamoja na bomba la sindano, harakaharaka akarudi pale kitandani kwake na kujilaza, akavificha vile vitu chini ya mto. Mhudumu alipoingia akiwa na sinia lililokuwa limejaa vyakula vya kila aina, Shenaiza alitulia kimya kama hajui kinachoendelea.

Yule mhudumu alimuandalia chakula ambapo tofauti na alivyotegemea kwamba atakula kwa sababu alikuwa na njaa kama mwenyewe alivyodai, Shenaiza alishikashika tu kisha akamwambia atoe.

“Mbona sasa hujala?”

“Hamu ya kula imeniisha ghafla, weka nitakula baadaye.”

“Lakini dada, mimi nilikuwa na ushauri mmoja juu yako. Unajua baba anakupenda sana ila anase…”

“Shiii! Ishia hapohapo, we toa vyakula vyako kisha uondoke, sitaki kusikia kitu chochote kwa sasa, niache,” alisema Shenaiza kwa sauti iliyoonesha kutokuwa na masihara hata kidogo.

Yule mhudumu alikusanya vyombo vyake na kutoka nje, akawaacha walinzi wakiwa mlangoni hapo kumlinda Shenaiza kama walivyoelekezwa na baba yake.

Baada ya mhudumu huyo kutoka, harakaharaka Shenaiza alichukua kile kichupa kilichokuwa na maandishi yaliyosomeka Diazepam, akakitingisha na kuchukua bomba la sindano, akavuta dawa nyingi kiasi cha kulifanya bomba lote lijae, akachukua mtandio wake na kujifunga mkononi kwa nguvu, akatafuta mshipa mkubwa wa damu.

Akajichoma na kuanza kuisikumia ile dawa ndani ya mshipa wake wa damu. Hakuweza kuimaliza yote, aliposukuma kiasi cha nusu ya bomba kuingia mwilini mwake, usingizi mzito ulimpitia, akalala huku bomba hilo likiwa bado linaning’inia mkononi.

Yule mhudumu aliporudi kwa mara ya pili kuja kumalizia vyombo vichache vilivyosalia, alishtuka kupita kiasi baada ya kuona damu nyingi ikiwa inatoka kwenye mkono wa Shenaiza na kulowanisha shuka lake huku mwenyewe akitapatapa kama anayetaka kukata roho, mapovu yakimtoka kwa wingi mdomoni na puani.

Harakaharaka, huku akilia, aliwaita walinzi ambao nao walimuita daktari wa familia hiyo, muda mfupi baadaye wote wakawa wamejaa ndani ya chumba hicho wakijaribu kuokoa maisha ya msichana huyo lakini ilionesha kwamba tayari walikuwa wamechelewa.

Je, nini kitafuatia? Usikose next issue au bofya Simulizi za Majonzi.
 
Hadithi yako nimeipenda pale tuu kwenye ulimwengu wa dunia na huyo shenaiza.. Ila mambo ya giza giza.. Yananishindaga kusoma kabisa... Nimeisia pale unaposogea kwa mbele kidogo... Huku watu wakilia kwa uchungu...

Mwenye anajua sehemu ya ngapi ulivyorudi ulimwengu wa kawaida ili nisome namna shenaiza mlivyo ishiana naye..

Na yule dem ulofanya naye kazi ulivyo mgegeda
 
Karibu dunian... Vp wazee wa fursa akina gwajima na nwenzie hujawapa hii habari ili iwe topic kanisani kwao??
 
Malizia jmn mpka naogopa, hivi ni ya kweli au??
 
Mkuu ingia kwenye link iliyotolewa na Dafu na Ndimu imeandikwa "Simulizi za Majonzi" kwa rangi ya blue click hapo itakupeleka kwenye page ya hiyo story. Hapo utaweza kupembua mchele na pumba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…