Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nimeanza kuingiwa na giza juu ya hii story umetolewa polisi kwenda kuleta wepesi wa mgonjwa kutoa ushirikiano na polisi hapo hapo umekimbia watu unao wahisi kuwa ni wabaya pasipo kuwataarifu polisi kwanza kuwa kuna watu wanafuatilia nyendo zenu, mpaka kuchukua boda boda. Hapa hapajakaa sawa hata kidogo.SEHEMU YA 14.
ILIPOISHIA:
“Tuondoke!” nilisema huku nikiinuka pale nilipokuwa nimekaa kwani tayari kengele ya hatari ililia ndani ya kichwa changu, Raya naye akainuka, tukaanza kuelekea kwenye lango la kutokea nje ya hospitali hiyo lakini cha ajabu zaidi, tukiwa getini tunataka kutoka, nililiona lile gari nalo likija kule tulipokuwepo.
SASA ENDELEA…
“Bodaboda! Bodaboda!” niliita kwa sauti huku tukitembea kwa haraka kuelekea nje ya hospitali, lile gari nalo likizidi kuja kwa kasi kule tulipokuwepo. Ilibidi nimshike mkono Raya kwani kwa jinsi alivyokuwa ‘mayai’ ningeweza kumuacha pale na kumsababishia matatizo.
Kwa bahati nzuri, dereva mmoja wa bodaboda alituona na harakaharaka akawasha pikipiki yake na kutufuata, mwenyewe akijiona amewazidi wenzake ujanja kwa kuwahi abiria.
“Tupeleke Kijitonyama,” nilisema huku nikimsaidia Raya kupanda, na mimi nikapanda lakini dereva wa bodaboda hakutaka kuondoka mpaka tukubaliane kwanza.
“Twende bwana nitakupa kiwango chochote unachotaka.”
“Lakini siku hizi haturuhusiwi kupakiza mishikaki nitakamatwa.”
“Twendeee,” nilisema kwa sauti ya juu, yule dereva akaondoa pikipiki, kabla hajafika popote wote tulishtukia bodaboda ikikoswakoswa kugongwa kwa nyuma na lile gari lililokuwa linatufuata kwa kasi. Dereva wa bodaboda alitaka kusimama pembeni kulipisha gari hilo lakini nilimsisitiza kuongeza mwendo na kuhakikisha analipoteza kabisa lile gari.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Akiwa haelewi kinachoendelea, hofu kubwa ikiwa imemkumba moyoni, yule dereva bodaboda alikata kona ya ghafla na kuingia kwenye uchochoro mita chache mbele, hali iliyosababisha lile gari ambalo lilikuwa likijiandaa kutugonga kwa nyuma lipitilize kwa kasi, likaenda kusimama mita chache mbele.
Raya alikuwa akipiga kelele kwa nguvu huku akilitaja jina la Mungu wake, hakuelewa kilichotokea kiasi cha kujikuta katikati ya mtego wa kifo kama ule, nikawa nambembeleza na kumtaka atulie.
Lile gari lilirudi kinyumenyume na kujaribu kupita kwenye ule uchochoro kuifuata ile bodaboda lakini sehemu ilikuwa ndogo, likashindwa. Nikawa namsisitiza dereva kuzidi kuongeza kasi, tukatokeza mtaa wa pili na kuingia kwenye barabara ya lami, safari ikazidi kupamba moto.
“Usipite barabara kubwa, wanaweza kuwa wanatufuatilia, ingia kushoto hapo mbele,” nilimwambia, wazo ambalo dereva huyo alilifuata, tukawa tunazidi kukata mitaa tukitumia njia za uchochoroni.
“Nataka twende nyumbani kwetu Jamal,” alisema Raya huku akiwa bado na hofu kubwa moyoni.
“Ok sawa,” nilimjibu kwa kifupi kwa sababu kiukweli sikuwa nataka kupata muda wa kukaa peke yangu na Raya kama ilivyotokea usiku uliopita lakini kwa jinsi hali ilivyokuwa sikuwa na ujanja.
Dakika kadhaa baadaye, tayari tulikuwa tumefika Kijitonyama lakini kwa kukwepa kuonekana tumeelekea wapi, tuliamua kushuka kwenye bodaboda, tukakubaliana bei na dereva huyo ambaye licha ya kulipwa fedha zake, alionesha kuwa na shauku kubwa ya kutaka kujua kilichokuwa kinaendelea.
Hata hivyo, sikuwa tayari kumueleza chochote, akaondoka kwa shingo upande huku akigeukageuka nyuma, kuna wakati alihisi huenda alikuwa ametubeba majambazi lakini alikosa ushahidi wa hilo.
Yule dereva bodaboda alipoondoka tu, mimi na Raya tulipanda kwenye Bajaj ambayo ilitupeleka mpaka nyumbani kwa akina Raya, tukawa na uhakika mkubwa kwamba hata kama wale watu wataamua kutufuatilia, haitakuwa rahisi kutupata.
“Naomba ukaoge kwanza wakati mimi nafanya utaratibu wa chakula,” alisema Raya baada ya kuhakikisha milango yote ya nyumba hiyo imefungwa kwa ndani, kuanzia geti kubwa la nje mpaka milango ya ndani.
Kwa kuwa wazazi wa Raya hawakuwa wamerejea safarini kama mwenyewe alivyonieleza, kwa mara nyingine tulijikuta tukiwa peke yetu ndani ya nyumba.
Wakati nikiendelea kujiuliza kuhusu mfululizo wa matukio yaliyokuwa yakiendelea kuniandama kiasi cha kunifanya nikose uhakika juu ya maisha yangu, Raya alikuwa akifikiria jambo jingine tofauti kabisa.
Niliingia kwenye chumba cha wageni ambacho ndicho nilicholala usiku uliopita na kubadilisha nguo, nikajifunga taulo na kuelekea bafuni, mawazo mengi yakiendelea kukisumbua kichwa changu.
*Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi
Bado nilishindwa kupata majibu kuhusu Shenaiza, sikuwa nikielewa kama Shenaiza alikuwa ni mtu wa namna gani, akina nani walikuwa wakiyawinda maisha yake na alikuwa na uhusiano gani nao. Kila swali nililojiuliza halikuwa na majibu.
“Shenaiza Petras Loris,” nililikumbuka jina kamili la msichana huyo alilolitaja wakati akihojiwa na yule mpelelezi.
“Kabila langu ni Aethikes… mimi siyo Mtanzania, natokea Greece (Ugiriki), asili yetu ni Attica, baba yangu amezaliwa na kukulia kwenye Jiji la Athens lakini mama yangu ni mpare wa Mtae, Lushoto mkoani Tanga,” maneno ya Shenaiza wakati akijieleza yalikuwa yakijirudiarudia ndani ya kichwa change kama mkanda wa video.
“Lazima niujue ukweli! Lazima!” nilisema wakati nikifungulia bomba la maji ya mvua, maji ya baridi yakawa yananimwagikia na kuufanya mwili wangu uliokuwa umechoka sana upate nguvu mpya.
Japokuwa msichana huyo hakuwa tayari kunieleza ukweli zaidi ya kuishia kuniambia nisubiri ataniambia, niliamua kuutafuta ukweli kwa njia nyingine ingawa bado sikuwa naijua ni njia gani na nitafanyaje kumfahamu Shenaiza.
Nilikaa muda mrefu bafuni, nikiwa naendelea kujimwagia maji huku akili yangu ikienda mbio kuliko kawaida. Nilikuja kushtuka baada ya kusikia Raya akiniita na kuugonga mlango wa bafuni.
“Mbona hutoki bafuni mpenzi wangu,” alihoji Raya kwa sauti ya kubembeleza, harakaharaka nikafunga bomba na kuchukua taulo, nikajifuta na kufungua mlango, macho yangu yakagongana na Raya ambaye naye alikuwa amejifunga khanga moja tu.
“Na mimi nataka kuoga, nisubiri tuondoke wote,” alisema msichana huyo huku akinitazama kwa macho yaliyojaa ujumbe mzito, taratibu akanirudisha bafuni, nilishindwa kumzuia, naye akaingia na kufunga mlango kwa ndani.
“Nataka leo na mimi nideke, naomba uniogeshe,” alisema Raya na kunifanya nijikute kwenye wakati mgumu kwa mara nyingine, nikiwa bado sijui nijibu nini, msichana huyo alifungua khanga na kuitundika nyuma ya mlango, akabaki kama alivyoletwa duniani, vifuu viwili vikiwa vimechomoza kwenye kifua chake na kunifanya nisisimke mwili mzima.
Akalishika taulo nililokuwa nimejifunga na kulivuta kisha akalitundika pale alipoweka khanga yake, tukabaki saresare maua! Akanisogelea jirani kabisa kiasi cha kila mmoja kuanza kuzisikia pumzi za mwenzake, tukawa tunatazamana machoni huku ‘Jamal’ wangu naye akianza kufura kwa hasira.
***
Baada ya kumaliza kumhoji Shenaiza, yule askari mpelelezi, alitoka hadi nje alikowaacha wenzake, akawavuta pembeni na kuanza kuwaeleza alichoelezwa na msichana huyo, kila mmoja akawa ametulia akimsikiliza. Maelezo aliyoendelea kuyatoa, yalimshangaza kila mmoja, wakawa wanatazamana wakiwa ni kama hawaamini walichokuwa wakiendelea kukisikia kutoka kwa mwenzao.
“Kwani amesema asili yake ni wapi?”
“Ni Athens, Greece! Na kubwa zaidi, amesema jina lake kamili ni Shenaiza Petras Loris.”
“Unataka kusema kwamba ni mtoto wa Petras Loris huyu tunayemjua?”
“Sijamuuliza lakini kwa maelezo yake, upo uwezekano mkubwa akawa ni mwanaye au wana undugu fulani.”
“Aisee! Mbona hii inaonekana kuwa ngoma nzito?”
“Ni ngoma nzito kwelikweli, halafu kuna huyu kijana ameingizwa kwenye mtego bila mwenyewe kujua chochote, mpaka namuonea huruma.”
Je, nini kitafuatia? Usikose
it can't be true story aisee[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] ...umewaona kwenye gari ,na polisi wako maeneo hayo ukashindwa kuwashtua, bhac hata kushika plate no daaaah ....ila story tamuuu . Utunzi wako uko mahali pakee[emoji106] [emoji106]SEHEMU 13.
ILIPOISHIA:
Ilibidi yule askari avunje ukimya na kurudia tena kumuuliza swali lile lakini badala ya kutoa majibu kama alivyokuwa akifanya kwa maswali yote, alikaa kimya huku machozi mengi yakimtoka na kulowanisha uso wake.
“Kijana hebu naomba utupishe mara moja, toka nje nitakuita,” alisema yule askari, ikabidi nitii, nikawaacha wenyewe wawili mle wodini.
SASA ENDELEA…
Nilihisi kichwa changu kikipata moto, nilikuwa na shauku kubwa mno ya kutaka kuufahamu ukweli wa kilichokuwa kimemtokea Shenaiza. Lile swali la awali kwamba yeye ni nani, tayari nilishapata majibu kwa kiasi fulani lakini bado nilitaka kujua nini hasa kilichomtokea.
Mazungumzo kati ya Shenaiza na yule mpelelezi kule ndani yaliendelea kwa muda na baada ya kama dakika kumi na tano kupita, mlango ulifunguliwa na yule mpelelezi akatoka, akanionesha ishara kwamba niingie ndani.
Nikaenda ambapo nilimkuta Shenaiza akiwa anajifuta machozi, macho yake yakiwa yamebadilika rangi na kuwa mekundu sana.
“Come to me Jamal, you are my comfort,” (Njoo Jamal, wewe ndiyo faraja yangu) alisema Shenaiza kwa sauti ya chini, nikamsogelea pale kitandani na kumkumbatia, akanibusu shavuni na kuniomba radhi kwa kilichotokea.
“Unaniomba radhi kwa nini Shenaiza?”
“Najua hujajisikia vizuri kwa mimi kuzungumza kilichonitokea wakati wewe ukiwa nje, nilitamani na wewe usikie lakini naona kwa sasa siyo muda muafaka lakini nakuahidi kwamba muda mfupi ujao nitakueleza wala usijali,” alisema Shenaiza huku akiendelea kunibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu.
Nilimtoa wasiwasi na kumtaka awe huru na mimi, akaniachia kisha nikakaa pembeni ya kitanda chake.
“Walitaka kuniua jana, yaani ni Mungu tu na naamini hata wao wanajua kwamba nimekufa, wamenipiga sana,” alisema Shenaiza na kuniambia anajisikia vibaya sana kuniingiza kwenye matatizo ambayo wala hayakuwa yakinihusu.
“Nakuomba sana nikishapata nafuu kidogo tu tuondoke, hata ikibidi kwenda kuishi hotelini mimi nitagharamia kila kitu maana wanaweza kurudi tena kule nyumbani kwako kwa sababu wanaamini kwamba nimeshakwambia kila kitu kinachoendelea.”
“Kwa hiyo unataka kusema wanaweza tena kurudi nyumbani kwangu?”
“Ndiyo! Wanaweza kurudi na kukudhuru bure wakati hauna hatia yoyote,” alisema Shenaiza, kauli ambayo ilinishangaza na kunijaza hofu kubwa moyoni. Kuna wakati nilikuwa najuta sana kwa kujiingiza kwenye mdomo wa mamba bila kujua.
Shenaiza aliendelea kuniongelesha mambo mbalimbali lakini wala akili yangu haikuwa pale, nilikuwa nikiwaza mambo tofauti kabisa. Baadaye nesi aliingia na kunieleza kwamba mgonjwa alikuwa anahitaji kupumzika kwa hiyo nitoke na kumuacha peke yake.
Shenaiza alikuwa mbishi kidogo lakini baadaye alikubali, akaomba kabla sijatoka nimbusu, nikamuinamia pale kitandani kwa lengo la kumbusu kwenye shavu lake lakini alinishika shingoni na kunivutia kwake, ndimi zetu zikagusana na kunifanya nipigwe na ganzi kwa sekunde kadhaa, aliponiachia, nilibaki nimeganda vilevile mpaka nesi aliponishtua.
“Inabidi uende nje kaka ili tumhudumie mkeo kisha apate muda wa kupumzika,” alisema yule nesi, nikashtuka kama mtu aliyekuwa usingizini, nikageuka na kumtazama Shenaiza pale kitandani, akanifinyia jicho lake moja na kunibusu kwa mbali, nikatoka mpaka nje huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wangu.
“Jamal! Uko salama mpenzi wangu? Nakupigia simu lakini sikupati mpaka imebidi nije huku,” alisema Raya ambaye aliponiona tu nikitoka wodini, alikuja na kunikumbatia kwa nguvu, akionesha kuwa na hofu kubwa na ukimya wangu.
Hata hivyo sikumtilia sana maanani, japokuwa nilitoka nikiwa natabasamu, nilipomuona nilikunja sura, nikaingiza mkono mfukoni na kutoa simu, nikagundua kuwa kumbe kweli ilikuwa imejizima bila mimi kufahamu, nikaiwasha na kusogea mpaka pembeni kulikokuwa na mabenchi, nikakaa. Raya naye akaja na kukaa pembeni yangu, akawa na shauku kubwa ya kutaka kusikia chochote kutoka kwangu.
“Niache kidogo Raya, akili yangu haijatulia kabisa, tutazungumza baadaye,” nilimjibu msichana huyo kwa kifupi, nikamuona akishusha pumzi ndefu na kutulia kimya. Maskini Raya! Alionesha kuwa na hisia nzito juu yangu lakini kwa bahati mbaya mwenzake nilikuwa namchukulia kawaida sana.
Sote tukiwa kimya kabisa, nilikumbuka kilichotokea kati yangu na Raya usiku na kujikuta nikishindwa kumeza chakula nilichotafuniwa, nikageuka na kumtazama usoni, naye akanitazama, nikagundua kwamba alikuwa akilengwalengwa na machozi.
“Najua hunipendi Jamal lakini hiyo isiwe sababu ya kuninyanyasa, nakupenda sana mwenzio kuliko mtu yeyote chini ya jua, naamini ipo siku utaujua ukweli,” alisema msichana huyo, nikarudia kumsisitiza kwamba aniache kidogo hayo mambo tutayajadili baadaye, safari hii nilizungumza kwa sauti ya chini nikiwa kama nambembeleza f’lani, nikamuona ametulia.
Nikiwa nimekaa pale, nilimuona yule askari mpelelezi akiwa na wenzake, nikamuomba Raya anisubiri hapohapo, nikainuka na kumfuata huku bado nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kujua alizungumza nini na Shenaiza.
Hata hivyo, licha ya kumfuata askari huyo na kumuomba anidokeze alichoelezwa na Samantha, alikataa katakata kwa maelezo kwamba atavuruga upelelezi, nikakosa cha kufanya. Nilirudi hadi pale nilipokuwa nimemuacha Raya, nikakaa pembeni yake huku nikiwa kimya kabisa.
“Nakushuru kwa jinsi ulivyojitoa kunisaidia katika haya matatizo yanayonikabili,” nilivunja ukimya na kumsemesha Raya, nikamuona akiinua uso wake ambao muda wote alikuwa ameuinamisha chini, akanitazama huku tabasamu hafifu likichanua kwenye uso wake.
“Usijali Jamal, nipo kwa ajili yako na kamwe sitakuacha peke yako hata iweje.”
“Yaani japokuwa ulikuwa unalia lakini macho yako yamezidi kuwa mazuri,” nilimtania Raya, akashindwa kujizua na kucheka kwa nguvu. Hakuna kitu alichokuwa anakipenda Raya kama kusikia kauli yoyote ya kumsifia kutoka kwangu. Ile huzuni aliyokuwa nayo, iliyeyuka kama theluji juani, akachangamka kabisa.
“Na leo si tutaenda kulala pamoja nyumbani kwetu?”
“Kwani wazazi wako bado hawajarudi?”
“Bado!”
“Ok, tutaangalia itakavyokuwa,” niliamua kumjibu hivyo Raya ili kumridhisha ingawa ukweli ni kwamba kauli hiyo haikuwa imetoka ndani ya moyo wangu. Wakati tukiendelea kuzungumza, niligundua jambo lisilo la kawaida.
Mita chache kutoka pale tulipokuwa tumekaa, kulikuwa na maegesho ya magari. Magari mengi yalikuwa yameegeshwa lakini miongoni mwa magari hayo, ndani ya gari moja kulionekana kuwa na watu zaidi ya mmoja ambao baadaye nilikuja kushtukia kwamba walikuwa wakitutazama sana mimi na Raya pale tulipokuwa tumekaa na zaidi walikuwa wakiniangalia mimi.
Nilipogeuka haraka na kuwatazama, macho yangu na yao yaligongana lakini wakazuga kwamba hawakuwa wakinitazama, wakawa wanaendelea na mazungumzo yao.
“Kwani nini wananitazama mimi?” nilijikuta nikizungumza kwa sauti, Raya akashtuka na kuniuliza nilikuwa namaanisha nini? Nikataka kumzuga lakini haikuwa rahisi, akafanikiwa kugundua kuwa nilikuwa nawatazama watu gani.
“Hata mimi nimewaona muda mrefu tu, tangu unatoka wodini walikuwa wakikutazama lakini sikuwatilia maanani.”
“Tuondoke!” nilisema huku nikiinuka pale nilipokuwa nimekaa kwani tayari kengele ya hatari ililia ndani ya kichwa changu, Raya naye akainuka, tukaanza kuelekea kwenye lango la kutokea nje ya hospitali hiyo lakini cha ajabu zaidi, tukiwa getini tunataka kutoka, nililiona lile gari nalo likija kule tulipokuwepo.
Je, nini kitafuatia? Usikose
karudi kuzimu kuna kitu alisahauhuyu jamaa kakimbia
[emoji23] [emoji23] [emoji23]karudi kuzimu kuna kitu alisahau
ahahahaaaaaa haaaaatatizo la mtoa hadithi siku moja yupo duniani wiki yupo kuzimu
Mkuu ingia kwenye link iliyotolewa na Dafu na Ndimu imeandikwa "Simulizi za Majonzi" kwa rangi ya blue click hapo itakupeleka kwenye page ya hiyo story. Hapo utaweza kupembua mchele na pumbaHadithi yako nimeipenda pale tuu kwenye ulimwengu wa dunia na huyo shenaiza.. Ila mambo ya giza giza.. Yananishindaga kusoma kabisa... Nimeisia pale unaposogea kwa mbele kidogo... Huku watu wakilia kwa uchungu...
Mwenye anajua sehemu ya ngapi ulivyorudi ulimwengu wa kawaida ili nisome namna shenaiza mlivyo ishiana naye..
Na yule dem ulofanya naye kazi ulivyo mgegeda
Link ishatolewa mkuu. Angalia sehemu ya 23 imeandikwa kwa rangi ya blue Simulizi za Majonzitatizo la mtoa hadithi siku moja yupo duniani wiki yupo kuzimu