kallase
Member
- Mar 18, 2020
- 27
- 43
MESEJI MOJA...........(01)
Imeandikwa Na SALUM KALASE.
MAWASILIANO: 0625000557
SEHEMU YA KWANZA.
Kwa majina naitwa James Daudi ni kijana wa miaka ishirini na tano. Katika umri wangu huu sijawahi kuwa na mpenzi hata mara moja. Kwa lugha nyepesi naweza sema sijawahi kuijua radha ya mwanamke inavyofanana hadi kufikia umri huu.
Sababu hiyo imefanya washikaji zangu wawe wananicheka sana kwa kudai kuwa mimi ni domo zege, yaani sijui kutongoza kitu ambacho si cha kweli hata kidogo kwani kati ya vijana wenye Juhudi ya utongozaji nauhakika hauwezi kunitoa mie.
Kwa haraka haraka mimi huwa naweza kutongoza hata wadada ishirini kwa wiki moja lakini cha ajabu huwa naishia kukataliwa na wadada wote. Ni kama huwa nina gundu hivi ambayo sielewi imetokea wapi kwani nikijitazama najiona kabisa kuwa ni mwanaume niliyekamilika.
Namshukuru Mungu hakuniumba kuwa mfupi, nina urefu ule wa kunifanya niwe mwanaume ninayejiamini, mwili wangu ni wa mazoezi kiasi kwani kila ninapopata muda ni lazima niende gym kufanya mazoezi ili kujiweka sawa.
Rangi yangu si haba naweza kusema ni maji ya kunde na hata sura yangu nayo namshukuru Mungu inatazamika. Najua japo si vizuri kwa mtoto wa kiume kujisifia uzuri wa sura ila mimi ni mzuri bhana!!
Ukiachana na hayo, pia mimi napenda kupendeza, kila ninapotoka huwa najitahidi sana kuvaa vizuri na kupulizia pafyumu nzuri ili ninukie vizuri.
Lakini pamoja na juhudi zote hizo huwa naishia kuangukia pua kila ninapojaribu kuongea na wasichana. Kuna muda huwa nahisi labda nimerogwa maana kama ni kutongoza mimi ni fundi haswa. Natongoza kweli kweli yaani nikimuweka chini mtoto wa watu anisikilize huwa nahakikisha namweleza maneno matamu ambayo nina uhakika hajawahi kuyasikia kwingine kokote kule.
Sio kwamba najisifia lahasha! Ila huo ndio ukweli wenyewe kwani hata washikaji zangu kadhaa wale wanaonichekaga nimeshawahi kuwasaidia kupata mademu kwa kuwafundisha swaga zangu.
Swaga ambazo kwao huwa zinakubali ila kwangu huwa zinabuma sijui hata kwanini.
Nimeshajaribu njia kadhaa za kujaribu kuisafisha nyota yangu kwani kama ni kwa waganga nimeshakwenda kutazama nyota yangu, Na nikapewa dawa za kujisafisha nyota yangu lakini hakuna kilichobadilika.
Nikajaribu kwenda kanisani kufanya maombi, na kama haitoshi nikawa nafunga kabisa kula hata kwa siku tatu mfululizo kumuomba Mungu anisafishe nyota yangu lakini wapi kwani licha ya juhudi zangu zote hizo hakuna kilichobadilika.
Kwangu kila kukicha nilikuwa na kutana na mkatao mpya kila nilipojaribu kutongoza lakini pamoja na yote hayo sikukata tamaa.
Ndani mwangu, yaani moyoni mwangu kuna imani ilikua inaniambia zamu yangu itakuja tu hivyo hapakuwa na haja ya kukata tamaa. Niliamini kama nitakata tamaa ni kama nitakua naukubali uhalisia wa kuwa mie nimechafuliwa nyota yangu hivyo niliendelea kupambania kombe la kutaka kuingia kwenye mahusiano.
"Mambo!!"
Ujumbe wa meseji ulisomeka hivyo kwenye kioo cha simu yangu. Ujumbe ambao niliusoma mida ya saa kumi na mbili za asubuhi baada ya kuwa nimeamka kutoka usingizini.
Kwa haraka haraka niliwaza ujumbe kama huo hawezi kutuma mwanaume mwenzangu.
"Ni demu huyu!!" Niliwaza ila swali kichwani likawa ni nani huyo aliyenitumia ujumbe huo bila kujitambulisha na kwa nilivyoitazama ila meseji ilionekana kuingia usiku sana wa saa nane usiku.
Nikawaza haraka wacha nijifanye kama naitumia pesa namba ile ili kiona jina la usajili wa ile namba nitasoma nani,
"PRISCA PAULO PALESTINA"
Majina matatu ya usajili yalisomeka, na jina moja tu la PRISCA ndilo lililoiteka akili yangu,
"Ni manzi huyu!!" Nilijikuta natamka maneno hayo yaliyoufanya moyo wangu ujawe na furaha kiasi cha kunifanya nijikute naanza kuruka ruka kitandani kwangu kwa shangwe.
"Poa!! vipi mwenzangu mzima wewe?"
Niliijibu meseji ile kisha nikakaa kusubiri jibu langu. Japo ilikuwa ni asubuhi sana bado lakini nilikuwa naomba Prisca awe ameshaamka.
"Mie nipo salama kabisa James za tangu juzi"
Prisca alinijibu, jibu lake ndilo lililonichanganya zaidi, nikawaza "Inamaana Prisca ananifahamu kumbe!" Ila cha ajabu mie sikuwa namkumbuka, nadhani ni kwa sababu ya idadi za wanawake ninaokutana nao kwa siku. Isingekuwa rahisi kumkumbuka kila mdada niliyezungumza nae kwa upande wangu.
"Salama kabisa nimeisubiri sana simu yako ujue best" Nilimjibu Prisca kwa kujiamini japo sikuwa nakumbuka ni kitu gani nilichokuwa nimezungumza nae, sio hilo tu mbaya zaidi hata sura yake sikuwa naikumbuka kwani hata jina nililolitazama kwenye ule muamala lilikuwa jipya kabisa kwangu.
Lakini pamoja na yote hayo sikutaka kuipoteza bahati ya kumpoteza Prisca kwani tangu nimeanza kutongoza huyo ndiye aliyekuwa binti wa kwanza kunitafuta mwenyewe kwa ridhaa yake.
Hivyo kivyovyote vile nilihitaji kupata Prisca, kumpoteza ni kitu ambacho sikutaka kabisa kukisikia kwenye fikra za ubongo wangu.
ITAENDELEA TENA KESHO.
Ili kupata simulizi zangu nyingine nyingi kama hii karibu ujiunge kwenye group langu la WhatsApp kwa kubonyeza link hii hapa chini [emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]KAKA MKUBWA STORIES.
Imeandikwa Na SALUM KALASE.
MAWASILIANO: 0625000557
SEHEMU YA KWANZA.
Kwa majina naitwa James Daudi ni kijana wa miaka ishirini na tano. Katika umri wangu huu sijawahi kuwa na mpenzi hata mara moja. Kwa lugha nyepesi naweza sema sijawahi kuijua radha ya mwanamke inavyofanana hadi kufikia umri huu.
Sababu hiyo imefanya washikaji zangu wawe wananicheka sana kwa kudai kuwa mimi ni domo zege, yaani sijui kutongoza kitu ambacho si cha kweli hata kidogo kwani kati ya vijana wenye Juhudi ya utongozaji nauhakika hauwezi kunitoa mie.
Kwa haraka haraka mimi huwa naweza kutongoza hata wadada ishirini kwa wiki moja lakini cha ajabu huwa naishia kukataliwa na wadada wote. Ni kama huwa nina gundu hivi ambayo sielewi imetokea wapi kwani nikijitazama najiona kabisa kuwa ni mwanaume niliyekamilika.
Namshukuru Mungu hakuniumba kuwa mfupi, nina urefu ule wa kunifanya niwe mwanaume ninayejiamini, mwili wangu ni wa mazoezi kiasi kwani kila ninapopata muda ni lazima niende gym kufanya mazoezi ili kujiweka sawa.
Rangi yangu si haba naweza kusema ni maji ya kunde na hata sura yangu nayo namshukuru Mungu inatazamika. Najua japo si vizuri kwa mtoto wa kiume kujisifia uzuri wa sura ila mimi ni mzuri bhana!!
Ukiachana na hayo, pia mimi napenda kupendeza, kila ninapotoka huwa najitahidi sana kuvaa vizuri na kupulizia pafyumu nzuri ili ninukie vizuri.
Lakini pamoja na juhudi zote hizo huwa naishia kuangukia pua kila ninapojaribu kuongea na wasichana. Kuna muda huwa nahisi labda nimerogwa maana kama ni kutongoza mimi ni fundi haswa. Natongoza kweli kweli yaani nikimuweka chini mtoto wa watu anisikilize huwa nahakikisha namweleza maneno matamu ambayo nina uhakika hajawahi kuyasikia kwingine kokote kule.
Sio kwamba najisifia lahasha! Ila huo ndio ukweli wenyewe kwani hata washikaji zangu kadhaa wale wanaonichekaga nimeshawahi kuwasaidia kupata mademu kwa kuwafundisha swaga zangu.
Swaga ambazo kwao huwa zinakubali ila kwangu huwa zinabuma sijui hata kwanini.
Nimeshajaribu njia kadhaa za kujaribu kuisafisha nyota yangu kwani kama ni kwa waganga nimeshakwenda kutazama nyota yangu, Na nikapewa dawa za kujisafisha nyota yangu lakini hakuna kilichobadilika.
Nikajaribu kwenda kanisani kufanya maombi, na kama haitoshi nikawa nafunga kabisa kula hata kwa siku tatu mfululizo kumuomba Mungu anisafishe nyota yangu lakini wapi kwani licha ya juhudi zangu zote hizo hakuna kilichobadilika.
Kwangu kila kukicha nilikuwa na kutana na mkatao mpya kila nilipojaribu kutongoza lakini pamoja na yote hayo sikukata tamaa.
Ndani mwangu, yaani moyoni mwangu kuna imani ilikua inaniambia zamu yangu itakuja tu hivyo hapakuwa na haja ya kukata tamaa. Niliamini kama nitakata tamaa ni kama nitakua naukubali uhalisia wa kuwa mie nimechafuliwa nyota yangu hivyo niliendelea kupambania kombe la kutaka kuingia kwenye mahusiano.
"Mambo!!"
Ujumbe wa meseji ulisomeka hivyo kwenye kioo cha simu yangu. Ujumbe ambao niliusoma mida ya saa kumi na mbili za asubuhi baada ya kuwa nimeamka kutoka usingizini.
Kwa haraka haraka niliwaza ujumbe kama huo hawezi kutuma mwanaume mwenzangu.
"Ni demu huyu!!" Niliwaza ila swali kichwani likawa ni nani huyo aliyenitumia ujumbe huo bila kujitambulisha na kwa nilivyoitazama ila meseji ilionekana kuingia usiku sana wa saa nane usiku.
Nikawaza haraka wacha nijifanye kama naitumia pesa namba ile ili kiona jina la usajili wa ile namba nitasoma nani,
"PRISCA PAULO PALESTINA"
Majina matatu ya usajili yalisomeka, na jina moja tu la PRISCA ndilo lililoiteka akili yangu,
"Ni manzi huyu!!" Nilijikuta natamka maneno hayo yaliyoufanya moyo wangu ujawe na furaha kiasi cha kunifanya nijikute naanza kuruka ruka kitandani kwangu kwa shangwe.
"Poa!! vipi mwenzangu mzima wewe?"
Niliijibu meseji ile kisha nikakaa kusubiri jibu langu. Japo ilikuwa ni asubuhi sana bado lakini nilikuwa naomba Prisca awe ameshaamka.
"Mie nipo salama kabisa James za tangu juzi"
Prisca alinijibu, jibu lake ndilo lililonichanganya zaidi, nikawaza "Inamaana Prisca ananifahamu kumbe!" Ila cha ajabu mie sikuwa namkumbuka, nadhani ni kwa sababu ya idadi za wanawake ninaokutana nao kwa siku. Isingekuwa rahisi kumkumbuka kila mdada niliyezungumza nae kwa upande wangu.
"Salama kabisa nimeisubiri sana simu yako ujue best" Nilimjibu Prisca kwa kujiamini japo sikuwa nakumbuka ni kitu gani nilichokuwa nimezungumza nae, sio hilo tu mbaya zaidi hata sura yake sikuwa naikumbuka kwani hata jina nililolitazama kwenye ule muamala lilikuwa jipya kabisa kwangu.
Lakini pamoja na yote hayo sikutaka kuipoteza bahati ya kumpoteza Prisca kwani tangu nimeanza kutongoza huyo ndiye aliyekuwa binti wa kwanza kunitafuta mwenyewe kwa ridhaa yake.
Hivyo kivyovyote vile nilihitaji kupata Prisca, kumpoteza ni kitu ambacho sikutaka kabisa kukisikia kwenye fikra za ubongo wangu.
ITAENDELEA TENA KESHO.
Ili kupata simulizi zangu nyingine nyingi kama hii karibu ujiunge kwenye group langu la WhatsApp kwa kubonyeza link hii hapa chini [emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]KAKA MKUBWA STORIES.