- Thread starter
- #101
Tukashuka chini tukakubaliana twende na moto wa kuni tukapanda nao,tukaichoma dawa ikawaka na kuteketea wakati nainama kuchukua majivu,akatokea nyoka mweusi mkubwa akawa anatoka upande mmoja akawa kama anatufuata ,niliinuka ghafla nikawa nataka kurudi kwa nyuma nilistuka sana lakini yule msaidizi wa mganga alinishika mkono kwa nguvu na kunizuia kutoka eneo lile.
Nyoka alitupita kwa karibu sana akawa anaelekea chini ya mlima,nikazoa majivu tukashuka nayo,tukafika kwa mganga,mganga akamuuliza yule msaidizi je,
nyoka alitokea,msaidizi wake akajibu ndiyo...nilibaki na mshangao.
Mganga akaendeleza uganga wake akanipa majivu na madawa mengine aliyoyafunga pamoja akaniambia niende kuyafukia kwenye kaburi,kaburi LA MTU mzima mwenye umri zaidi ya miaka hamsini na awe amezikwa zaidi ya miaka kumi na nifukie kabla ya SAA saba mchana,nikishindwa kwa Siku hiyo nifanye kesho yake muda huo huo.
Nikaondoka nikaenda kutafuta kaburi lenye sifa.
Nilitafuta kaburi pale mjini kuanzia makaburi ya Mfaranyaki,Ruvuma,Mkuzo nikaenda hadi kwenye makaburi yaliyo karibu na Chuo cha ualimu Songea Matogoro lakini kote huko nilikuta watu kibao,jambo langu
lilikuwa haliwezi kufanyika.
Ikabidi nitoke nje ya mji nikapata makaburi yaliyokuwa yamejitenga na yaliyokuwa na miti mingi kwahiyo kulikuwa na Giza kidogo.
Nikaanza kupita kusoma tarehe za kuzaliwa na tarehe za kuzikwa nikapata moja lililokuwa limejengewa lakini lilibomolewa na mizizi mikubwa ya mti iliyokuwa imepita kwenye kaburi.
Nikaanza kuchimba shimo katikati ya kaburi udongo ulikuwa umetitia ardhi ilikuwa ngumu sana kuchimba lakini nikatumia kipande cha mti nikafanikiwa kuchimba shimo dogo nikafukia dawa nikaondoka zangu.
Hela hazikurudi ila baada ya miaka kama mitatu yule tajiri nilikutana naye Madaba anafanya kazi ya kupakia magunia ya tangawizi kwenye roli.
Itaendelea.
Imebakia kwa mganga mmoja na stori za kutengeneza radi na kuita na kufukuza mvua.
Nyoka alitupita kwa karibu sana akawa anaelekea chini ya mlima,nikazoa majivu tukashuka nayo,tukafika kwa mganga,mganga akamuuliza yule msaidizi je,
nyoka alitokea,msaidizi wake akajibu ndiyo...nilibaki na mshangao.
Mganga akaendeleza uganga wake akanipa majivu na madawa mengine aliyoyafunga pamoja akaniambia niende kuyafukia kwenye kaburi,kaburi LA MTU mzima mwenye umri zaidi ya miaka hamsini na awe amezikwa zaidi ya miaka kumi na nifukie kabla ya SAA saba mchana,nikishindwa kwa Siku hiyo nifanye kesho yake muda huo huo.
Nikaondoka nikaenda kutafuta kaburi lenye sifa.
Nilitafuta kaburi pale mjini kuanzia makaburi ya Mfaranyaki,Ruvuma,Mkuzo nikaenda hadi kwenye makaburi yaliyo karibu na Chuo cha ualimu Songea Matogoro lakini kote huko nilikuta watu kibao,jambo langu
lilikuwa haliwezi kufanyika.
Ikabidi nitoke nje ya mji nikapata makaburi yaliyokuwa yamejitenga na yaliyokuwa na miti mingi kwahiyo kulikuwa na Giza kidogo.
Nikaanza kupita kusoma tarehe za kuzaliwa na tarehe za kuzikwa nikapata moja lililokuwa limejengewa lakini lilibomolewa na mizizi mikubwa ya mti iliyokuwa imepita kwenye kaburi.
Nikaanza kuchimba shimo katikati ya kaburi udongo ulikuwa umetitia ardhi ilikuwa ngumu sana kuchimba lakini nikatumia kipande cha mti nikafanikiwa kuchimba shimo dogo nikafukia dawa nikaondoka zangu.
Hela hazikurudi ila baada ya miaka kama mitatu yule tajiri nilikutana naye Madaba anafanya kazi ya kupakia magunia ya tangawizi kwenye roli.
Itaendelea.
Imebakia kwa mganga mmoja na stori za kutengeneza radi na kuita na kufukuza mvua.