Hi,
Nimeshika ujauzito ila nimeshindwa kuelewa kama ni wa Rafiki yangu au Mr..
Nilikutana na Rafiki jioni ya siku ya kumi na nne ya mzunguko wangu, usiku nikakutana na mr, baada ya hapo sijakutana na wote hadi siku ya 21 ya mzunguko nilipokutana na hubby tena.
Msinielewe vibaya, sijapenda, iko hivi. Nina Rafiki yangu ambae ni Mume wa mtu, tumetoka mbali, yeye ndio aligharamia elimu yangu ya chuo kwa 80%, Diploma 2 yrs na Degree 3 yrs, sikufaulu vizuri form six nikalazimika kuunga unga.
Hakuishia hapo amenisaidia kupata kazi pia, alioa kabla hatujafahamiana, si mtu mzima kiviile, nadhan ana 40+ kwa sasa. Nlipoanza kazi akajitokeza mchumba tukafunga ndoa, niligundua ana matatizo makubwa kuhusu unyumba kabla hata ya ndoa ila nilidhani with time litaisha ila tatizo liliendelea na kuzidi baada ya ndoa, ejaculation inachukua less than two minutes hadi 4 to 5 days ndipo anapata erection tena. I promised myself never to be unfaithful, lakini imeshindikana.
Somehow, i don't know how tukaanza upya mawasiliano na yule ex wangu ambae nilikua nikimkwepa tangu nimeolewa ingawa hakukata tamaa.
Tatizo lenyewe ni hili:-
Nilikutana na hubby siku ya 6 ya mzunguko mpya, hatukufanya tena hadi siku ya 10 ya mzunguko nikakutana na yule Rafiki yangu, sikufanya tena maana Mr alikua safari, hadi siku ya 14 ya mzunguko nikafanya tena na Rafiki yangu. Ilikua jioni after work, usiku bila kutarajia Mr angekua amerudi akanihitaji tukafanya usiku, sikufanya tena na yeyote hadi siku ya 21 ya mzunguko nilipofanya tena na hubby. Na ninahisi mimba iliingia siku hiyo ila ndio sijui ni ya rafiki jioni au Mr usiku.
Kwa mahesabu haya naomba mnaojua mnisaidie kuona ni lini hapo mimba iliingia na inaweza kuwa ya nani?
Nahitaji ushauri kuhusu hilo eneo la mimba, hayo mengine mwachieni ngoswe.
Asante..