KERO Singida: Baadhi ya mitaa gari la taka halipiti kwa wakati, wiki ya 3 uchafu umezagaa mitaani

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Habari.

Kuna kero moja Manispaa ya Singida, kumekuwa na tabia ya uchelewaji wa kuchukua taka katika baadhi ya maeneo hasa Ginery.

Wananchi wanatoa taka nje siku ya kubeba hawaji kuchukua. Hii ni wiki ya tatu taka zimezagaa kwenye mitaa tu.

Na ni tatizo limeanza toka mwezi wa 12 Mwaka jana (2024). Huko mitaani taka zinatupwa ovyo sababu watu wameshajaza vifaa vyao vya kuwekea taka.


Hii picha chinii ni karibu na Chuo cha Uhasibu barabara ya kwenda Ginery.

Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.

Pia soma ~ Hatimaye gari la taka lapita kukusanya takataka mitaa ya Singida
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…