Uchaguzi 2020 Singida Magharibi na Halmashauri ya Wilaya Ikungi msiachie lulu hii

Uchaguzi 2020 Singida Magharibi na Halmashauri ya Wilaya Ikungi msiachie lulu hii

Fundi Madirisha

Senior Member
Joined
Jun 30, 2020
Posts
184
Reaction score
988
Na Fundi madirisha,

Nawasalimu sana ndugu zangu wananchi wa jimbo la Singida Magharibi. Mwafanga naa! Amuchii!

Kwa ufupi ndugu zangu wa jimbo la Singida Magharibi hasa wapiga kura za maoni nataka niwadokezee kidogo, mna mtu mmoja mpambanaji na ni mtu wa kazi sana anaitwa HAMISI LISSU MAHANJU, huyu ni msomi wa chuo kikuu mwenye mipango yenye mafanikio makubwa katika taifa hili.

Huyu bwana ni mtia nia jimbo lenu la Singida Magharibi, huyu mtu namtazama kwa jicho la mbali anataka kulisaidia taifa hili na wananchi kwa ujumla kama mwakilihi wao. Huyu kwa maoni yangu ni mtu sahihi pengine kuliko watangulizi waliowahi kua wabunge katika jimbo hilo. Hiki kichwa ni balaa, nina kifahamu tangu tukiwa sekondari, Chuo cha Ualimu Mkwawa, JKT, UDSM na mpaka kwenye majukumu akiwa baraza la mitihani, mkaguzi mkuu wa shule kanda na Afisa Elimu wa mikoa ya Mara na Dar es Salaam, hakika kila alikopita aliacha alama kubwa sana. Ninyi Watani zangu hamlijui hili nisikilizeni mimi ambaye namjua kwa undani na hata yeye hanijui mimi kama ninavyomfahamu ingawa tumekua wote kwenye majukumu ya kujenga nchi.

Nataka niwaambie Watani zangu, mnaweza kuhisi ninapigia mtu kampeni lakini mimi natoa ya moyoni mwangu baada ya kusikia huyu bwana anagombea ubunge katika jimbo hilo, nimesisimkwa nikatamani angependa kugombea mkoani kwetu Mara maana huko pia aliacha alama akiwa kama Afisa Elimu wa mkoa kwa kuutoa kutoka kufanya vibaya hadi kua mkoa bora kielimu kitaifa kabla hajahamishiwa kuokoa jahazi Dar es Salaam.

Huyu bwana yawezekana hata hanijumbuki kwakua nilikua chini ya idara zake alizopitia lakini mimi ninamfahamu vizuri sana ndio maana nikaamua kutumia fursa hii kuwaeleza Watani zangu msiachie LULU hii. Sina sababu ya kumpigia kampeni ispokua natamani sana awawakilishe awasaidie kwa sababu ya uwezo wake mkubwa sana kiakili na kiuongozi.

Ninawatakia kila lakheri katika chaguzi zenu za kura za maoni lakini nina imani mmenielewa Watani zangu.Mungu awabariki sana.

Fundi Madirisha,
madirishafundi@gmail.com
 
Kama ni CDM anaweza kuwa wa maana lakini kama ni CCM hapana wana Singida msikubali kurudi nyuma enzi za ccm zinakwisha songeni mbele.
 
Tupo naye SAU kama kawaida tunapanga kila mtu ale kuku mzima sio vipande vipande
 
Ngoja TL arudi,hao wote wanafagiliwa mbali.Mgombea wa ccm hatoboi
 
Kama ni CDM anaweza kuwa wa maana lakini kama ni CCM hapana wana Singida msikubali kurudi nyuma enzi za ccm zinakwisha songeni mbele.
Ni CCM lakini siyo kama aliyepita. Huyu ni mtu wa kazi sio maneno tuu. Kama watampa ridhaa atawapaisha na ataweka alama
 
Na Fundi madirisha,

Nawasalimu sana ndugu zangu wananchi wa jimbo la Singida Magharibi. Mwafanga naa! Amuchii!

Kwa ufupi ndugu zangu wa jimbo la Singida Magharibi hasa wapiga kura za maoni nataka niwadokezee kidogo, mna mtu mmoja mpambanaji na ni mtu wa kazi sana anaitwa HAMISI LISSU MAHANJU, huyu ni msomi wa chuo kikuu mwenye mipango yenye mafanikio makubwa katika taifa hili.

Huyu bwana ni mtia nia jimbo lenu la Singida Magharibi, huyu mtu namtazama kwa jicho la mbali anataka kulisaidia taifa hili na wananchi kwa ujumla kama mwakilihi wao. Huyu kwa maoni yangu ni mtu sahihi pengine kuliko watangulizi waliowahi kua wabunge katika jimbo hilo. Hiki kichwa ni balaa, nina kifahamu tangu tukiwa sekondari, Chuo cha Ualimu Mkwawa, JKT, UDSM na mpaka kwenye majukumu akiwa baraza la mitihani, mkaguzi mkuu wa shule kanda na Afisa Elimu wa mikoa ya Mara na Dar es Salaam, hakika kila alikopita aliacha alama kubwa sana. Ninyi Watani zangu hamlijui hili nisikilizeni mimi ambaye namjua kwa undani na hata yeye hanijui mimi kama ninavyomfahamu ingawa tumekua wote kwenye majukumu ya kujenga nchi.

Nataka niwaambie Watani zangu, mnaweza kuhisi ninapigia mtu kampeni lakini mimi natoa ya moyoni mwangu baada ya kusikia huyu bwana anagombea ubunge katika jimbo hilo, nimesisimkwa nikatamani angependa kugombea mkoani kwetu Mara maana huko pia aliacha alama akiwa kama Afisa Elimu wa mkoa kwa kuutoa kutoka kufanya vibaya hadi kua mkoa bora kielimu kitaifa kabla hajahamishiwa kuokoa jahazi Dar es Salaam.

Huyu bwana yawezekana hata hanijumbuki kwakua nilikua chini ya idara zake alizopitia lakini mimi ninamfahamu vizuri sana ndio maana nikaamua kutumia fursa hii kuwaeleza Watani zangu msiachie LULU hii. Sina sababu ya kumpigia kampeni ispokua natamani sana awawakilishe awasaidie kwa sababu ya uwezo wake mkubwa sana kiakili na kiuongozi.

Ninawatakia kila lakheri katika chaguzi zenu za kura za maoni lakini nina imani mmenielewa Watani zangu.Mungu awabariki sana.

Fundi Madirisha,
madirishafundi@gmail.com
Okay
 
Wasomi wangapi wamewekwa kapuni na ''bwana heri'' sembuse huyo unayemnadi!!!!!!!!!!!
 
Bongo bado sana hata wasomi kusimama na elimu zao
 
huko pia aliacha alama akiwa kama Afisa Elimu wa mkoa kwa kuutoa kutoka kufanya vibaya hadi kua mkoa bora kielimu kitaifa kabla hajahamishiwa kuokoa jahazi Dar es Salaam.
Kam aliokoa jahazi Mara, hivi ni kwa nini alishindwa kuzirudisha kwenye chati zile shule kongwe ambazo mpaka leo zinachukua vichwa kama Mara Secondary, Musoma Technical na Tarime ? Alikwama wapi ?
 
Back
Top Bottom