Single mother amtamkia maneno mabaya Baba wa kufikia

Mjanja M1

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2018
Posts
4,058
Reaction score
14,382
Hii imetokea mtaani kwetu, kuna Single Mother alikuwa ameolewa na Jamaa anaepiga vibarua vya kutengeneza simu mtaani.

Sasa Jamaa wakati akiwa ofisini na mtoto wa kufikia mwenye umri wa miaka 14 yule dogo akaidondosha chini simu ya mteja.

Ikumbukwe kuwa jamaa huwa anamkatazaga Dogo asiwe anachezea simu za watu.

Jamaa akampiga Dogo kakofi kadogo dogo PAAH! πŸ‘‹

Dogo akaanza kulia kwa Nguvu, Mama yake akasikia Aisee!

Kilichotokea baada ya hapo ni maneno makali na kumwambia UNAMPIGA HUYU MTOTO NI WAKO?

Aisee! Nilisikitika sana kuona yule Jamaa anaambiwa maneno yale na ilhali ni yeye ndio anatoa huduma kwa Mama na mtoto wa Single mother.


JAMAA ANAJUTA SASAIVI KUOA SINGLE MOTHER!
 
Leona rumisho, si sawa kumpiga mtoto wa miaka hiyo kofi. Haituhusu.
 
Kastori ka uongo haka....
 
Hapo ilitakiwa jamaa aunganishe makofi mazito mazito na kwa single maza
 
Huyo jamaa wala hajuti. Maadam anaendelea kuishi nao hao ajiandae kumuona Mola mapema kabla ya muhulaπŸ˜€
 
Ulilipapatikia mwenyewe fupa lililomshinda fisi kulila, usituchoshe, tusikuchoshe, tusichoshane.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…