Wana-JF naomba tutoe uzoefu wetu kwenye hii topic ili tu-share kitu/vitu maana ndoa za siku hizi ni kama ujio wa bwana wetu yesu kristo yaani hujui siku wala saa ndoa itakapo kuwa haipo.
Ni kipi bora baada ya kutoka katika ndoa(Divorced) ukiwa bado na umri mdogo tu wa let say, mid-thirties or below,ukiwa na watoto,ubaki bila kuoa au uoe mwanamke wa aina gani,mwenye mtoto/watoto kama wewe/divorced kama wewe/umri mnaokaribiana au ulomzidi sana.
Lengo likiwa unataka the best for your children and keeping in mind your happiness as well.
This is one of the areas that I normally become speechless when it comes to what to say. Hakuna jibu la moja kwa moja. Kama ingewezekana hizi ndoa zikabaki ndoa hilo lingekuwa jambo la maana sana.
Wacha kusema ndoa za siku hizi mbona sisi tumeoa na hatuna matatizo, mnao waza mambo ya kuwachana kwanini mlioa??
Hivi mtu anaoa kwa sababu gani??
Sijawahi kusikia ndoa zikafananishwa na ujio wa Yesu, naona wewe unataka kukufuru sasa :cool2:
Yaani unaoa ili udivorse, uwe single parent afu ili uanze kutafuta mke tena??
Duh, mbona unagawanya kwa njia ndefu sana?
Ni kipi bora baada ya kutoka katika ndoa(Divorced) ukiwa bado na umri mdogo tu wa let say, mid-thirties or below,ukiwa na watoto,ubaki bila kuoa au uoe mwanamke wa aina gani,mwenye mtoto/watoto kama wewe/divorced kama wewe/umri mnaokaribiana au ulomzidi sana.
hakuna ubora wowote katika divorce, na chaguo la kuoa/kuolewa au la ni vema likazingatia feelings zako baada ya divorce. Je uko tayari kupenda? na umejiandaa vipi kuhakikisha hutamsumbua huyo mwenzi wako kutokana na yale uliyotendwa na ex wako?? hili ni muhimu sana kuhakikisha uimara wa hiyo ndoa mpya. Wanawake kwa mfano tukitendwa na mwanaume mmoja huwa kosa litawatesa wanaume wengine wote watakaokupenda pia wanaume baadhi wana hiyo kitu ambayo ni mbaya sana na ndio hasa husababisha ndoa nyingi za pili zishindwe. Pia kikubwa ni kwa huyo mwenzi wako mpya je amekuamini kwa dhati na anaamini unaweza kuwa mume/mke bora? au kila ukifanya kitu kidogo atakuwa anakuambia ndio maana uliachwa! ndoa baada ya ndoa yaweza kuwa ngumu na sidhani ni jambo lakuliendea haraka haraka, umakini na mungu anatakiwa ahusishwe sana hapo. yeyote anaweza kuwa mume/ mke bora bila kujali alishawahi kuoa/kuolewa au la, watoto ni baraka siku zote hiyo haijalishi sana japo mipaka na jinsi ya kuwalea watoto wenu inatakiwa kuzingatiwa sana kwani inaweza kuleta tabu pindi mnapokuwa hamna utaratibu uliosahihi wa malezi.
Swali lako halina jibu la moja kwa moja hasa hapo penye red!
Kwanza: Hapo penye red kabla ya hata hujafikiria kuoa/kuolewa tena ni vzr kuzitafakari njia zako na mwenendo wa awali na kujua sababu iliyokuletea divorce (solve root cause ya tatizo lako kwanza), vinginevyo unaweza ukaoa/kuolewa tena na talaka zikaendelea kama kawa na mwisho ukatuchosha na kuomba ushauri kila siku!
Pili: Ukishagundua kuwa wewe binafsi haukuwa sababu ya talaka, au umeplan sasa kutulia baada ya kusababisha talaka, then linakuja hilo swala la kuoa/kuolewa na nani. Ktk hili, kama ni kijana, ni vigumu kuishi pakee yako maana itakufanya uwe na tabia zisizo nzuri pindi mwili utakapokuwa na mahitaji. Ushauri ni vzr kuoa/kuolewa na mtu unayempenda (awe na watoto au hana) na yeye pia anayekupenda na kumshirikisha mapema kuwa tayari kutunza familia yako (yenu kama wote mna watoto). Ni vzr kuwa karibu na wanao/wanenu baada ya ndoa kuhakikisha kuwa ndoa yako mpya haileta mateso na majuto kwenye familia yako.
Mara nyingi baadhi ya wadada wameonyesha mienendo na tabia mbaya za kuwalea vibaya watoto wanaowakuta kwa waume zao hususan mume anapokuwa muongo kwa kutokumwambia ukweli. Transparency ni muhimu sana ili kuwa na familia yenye amani. Kama unaona familia yenu (watoto) wanasumbua, peleka boarding wakachape shule, itakusaidia muda wa kutulia na kujenga familia. Wakirudi likizo watakuta mmeimarika kwenye ndoa.
Kikungu.... Kwanza naomba niseme kua mtazamo wa namna hio (looking towards a divorce) kama upo katika ndoa sio mzuri.... Ina maana kama upo ndani ya ndoa na ina matatizo badala ya kutafuta suluhu ya kuweza weka sawa wewe unaangalia a way out. That is not advisable kumbuka waweza toka hapo ukaoa mwanamke mwingine ukawa umeruka majivu na kukanyaga moto... However haya mambo katika jamii yapo; Hivo kweli ni msingi kutafakari kuhusu hilo swala.... Bahati mbaya ni moja ya sehemu ambayo inaumiza saana kichwa..
Kwa upande wangu naona kama you are young na una watoto, mara nyingi a good candidate wa kuoa kweli kabisa nia mwanamke ambae nae kesha zaa.... (Sio lazima) ila ni muhimu kwa mambo mengi sana. Hakuna mahala wanafundisha upendo na jinsi ya kulea watoto.. hayo ni mambo tunajifunza pale unapokua umebahatika kua mzazi na wawalea... Na hapa realistically speaking ukifuate zile propaganda za mradi umpende ndio uoe... Waweza poteza direction ya familia yako yote daima. Waweza kuta in the long run watoto ulo nao wakawa na msingi mbaya sana wa maisha ila hao mtakao kua nao kwa huyo mwana mama..... For believe me you hata kama wote ni wafanya kazi mtu ambae ana control nyumba na yupo responsible on house keeping ni mama.... na bahati mbaya sana wanawake wengi suala la kumpenda mtoto wa mwenzio limetushinda saana... Hivo kama ni mama hopefully ataelewa ni jinsi gani hao watoto alokuta hapo wanamhitaji kama mama na mlezi wako mpya... na ukikosea tu kuchagua mwanamke then furaha kuwepo ndani ya ndoa yako hio mpya ni ndoto.
Swali lako halina jibu la moja kwa moja hasa hapo penye red!
Kwanza: Hapo penye red kabla ya hata hujafikiria kuoa/kuolewa tena ni vzr kuzitafakari njia zako na mwenendo wa awali na kujua sababu iliyokuletea divorce (solve root cause ya tatizo lako kwanza), vinginevyo unaweza ukaoa/kuolewa tena na talaka zikaendelea kama kawa na mwisho ukatuchosha na kuomba ushauri kila siku!
Pili: Ukishagundua kuwa wewe binafsi haukuwa sababu ya talaka, au umeplan sasa kutulia baada ya kusababisha talaka, then linakuja hilo swala la kuoa/kuolewa na nani. Ktk hili, kama ni kijana, ni vigumu kuishi pakee yako maana itakufanya uwe na tabia zisizo nzuri pindi mwili utakapokuwa na mahitaji. Ushauri ni vzr kuoa/kuolewa na mtu unayempenda (awe na watoto au hana) na yeye pia anayekupenda na kumshirikisha mapema kuwa tayari kutunza familia yako (yenu kama wote mna watoto). Ni vzr kuwa karibu na wanao/wanenu baada ya ndoa kuhakikisha kuwa ndoa yako mpya haileta mateso na majuto kwenye familia yako.
Mara nyingi baadhi ya wadada wameonyesha mienendo na tabia mbaya za kuwalea vibaya watoto wanaowakuta kwa waume zao hususan mume anapokuwa muongo kwa kutokumwambia ukweli. Transparency ni muhimu sana ili kuwa na familia yenye amani. Kama unaona familia yenu (watoto) wanasumbua, peleka boarding wakachape shule, itakusaidia muda wa kutulia na kujenga familia. Wakirudi likizo watakuta mmeimarika kwenye ndoa.