Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Kuna comment zina chekesha Kuna watu wako radhi kulia ili story iendelee..wana comment kwa hisia zote najua wame ku PM wengi sana ulipo taka kui hairisha[emoji81][emoji81][emoji81]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na wewe tupia tupia matukio kadhaa unayokumbuka wakati tunasubir mleta mada kama kuchangamsha tu.
Akifanya hivyo ataharibu uzi. Bora asubirie hadi mwenye simulizi yake amalize kabisa ndiyo aongezee hayo ya kwake. Hata sisi wengine tunayo baadhi ya mambo ya kusimulia kuhusu mauaji hayo lakini tumempa nafasi mwenye mada yake anogeshe mambo.
 
Yani nasoma hadi mwili unasisimka...but naona umejitahidi sana kuna codes( classified info) nyingi kwenye hii hadithi...funguka tu ni zaidi ya miaka ishirini sasa.
Lile wingu lilisababisbwa na nini?ama ndege iliyotunguliwa ilikua karibu na eneo la ubalozini?
 
Acha tu
Yani nasoma hadi mwili unasisimka...but naona umejitahidi sana kuna codes( classified info) nyingi kwenye hii hadithi...funguka tu ni zaidi ya miaka ishirini sasa.
Lile wingu lilisababisbwa na nini?ama ndege iliyotunguliwa ilikua karibu na eneo la ubalozini?

Sent using komputa mpakato
 
Habari zenu wakubwa kwa wadogo.

Kwanza napenda kutoa pole na shughuli za kutwa kwa wale wahangaikaji wote kama mimi ambao kila siku lazima tutoke ili tuweze kujipatia riziki halali kila siku iendayo kwa mungu. Tuseme wote asante mungu.

Nisiwachoshe niende moja kwa moja kwenye mada,mdaa huu wakati naandika huu ushuhuda wangu binafsi ambayo nimeishuhudia kwa macho yangu mawili nchini rwanda wakati wa vita ya kikabila ,wenyewe hupenda kuiita mauji ya halaiki.

Stori inaanza wakati ndo nimemaliza masomo yangu ya uhasibu ngazi ya stashahada mwaka 1989 (sintotaja chuo hicho) nikajaribu kuomba kazi wizara ya mambo ya njee mungu si Athumani nikapata kazi ubalozi lakini nikapaangiwa kituo changu cha kazi kigali-Rwanda, kama sijasahau ubalozi Tanzania ulikuwa maeneo yanaitwa KICHUKIRO ,kwa sasa sijui kama bado upo palepale au vipi sina uhakika.

basi mwezi wa sita baada ya kukamilisha taratibu zote nikaanza safari ya kwenda Rwanda kituo changu cha kazi kipya,ajira mpya na mara ya kwanza kusafiri nje ya Tanzania... Safari ikaanza kwenda kuanza maisha mapya nchi ya watu ,mbali na ndugu jamaa na marafiki nikiwa sijui chochote kuhusu nchi hiyo..

Angalizo. naomba tuvulimiliane ni long stori kidogo na yanaweza jitokeza makosa ya kiundishi na kifasihi.... Ntaelezea mambo mengi sana ya kutisha ambayo niliyashuhudia kwa macho yangu mwenyewe ambayo hadi leo nimejitahidi kuyasahau lakini imeshindika kabisa.

Safari inaanza pale Mnazi moja nakumbuka enzi zile kulikuwa hakuna mambo ya Booking. unawahi alfajiri na mapema unatafuta basi lako unapanda tu unasubiri safari ianze.

Basi nikiwa na mabegi yangu na shilingi za kitanzania 60 elfu(nilipewa kwa ajili safari na kujikimu na passport ) tu ,naianza safari ya kwenda Kahama, safari ikaanza midaa ya kama saa moja kamili asubuhi (jina la basi lile nimelisahau ila nakumbuka lilikuwa rayland) kipindi hicho barabara ni vumbi tupu changarawe la vumbi hadi linaingia kupitia madirishani, baada ya safari ya uchovu mwingi hatimae saa nane usiku tunaingia singida stand. Mimi mgeni sijui niende uelekeo gani ikumbukwe miaka ile nyumba za wageni zilikuwa za kuhesabu basi ikabidi tushuke pale stand tukawa tunakula mikate na chai na wengine chai na kahawa.

Basi mimi nikarudi kulala kwenye gari,alfajiri na mapema gari likaanza safari tena nakumbuka tulifika stand kuu Kahama kana saa tatu usiku hivi. yani tulitumia kama siku mbili hivi Dar-kahama .leo hii dar - Kahama unatumia siku moja umefika halafu utasikia mtu anasema nchini hii bwana hakuna maendeleo kabisa daa!!!

Tumefika Kahama stand tumepokelewa na wapiga debe enzi hizo wao ndo walikuwa kama mawakala wa magari makubwa anakubebea mzigo hadi kwenye gari unalipa nauli yeye anachukua chake mnaachana hapo hapo hapo ni usiku inabidi kupata gari ya kwenda boda ya Rwanda na Tanzania Rusumo hapo unavuka Mpaka, kuna mto mkubwa unaitwa mto Rusumo unapita kwenye daraja la chuma kama lile lile liloejengwa na wanajeshi pale njia panda Kawe unavuka ng'ambo ukagonga passport ,cha kuchekesha pale kulikuwa hakuna magari ya abiria makubwa.

Magari ya abiria kutoka boda hadi kigali mjini yalikuwa hakuna, ilikuwa inakubidi upande roli la mizigo au abiria mjichange kwa makundi mkodi magari madogo kama tax ila mnabananishwa humo hatari na mizigo juu, kutoka boda hadi kigali ilikuwa kama mwendo wa masaa nane hivi kuingia kigali mjini.
Hatimae baada ya kubadilisha fedha zetu kuwa mafaranga tukapata usafiri wa kutufikisha kigali nakumbuka kundi langu kwenye gari tulilokodi nilipanda na wazaire watupu hivyo kelele zilikuwa nyingi hadi tunaingia kigali wanaimba nakuongea sanaa ubishi mwingi mara mpira mara siasa ili mradi makelele tu.

Saa tisa mchana nikawa tumewasili kigali town enzi hizo sijui lolote kuhusu mji huo zaidi ya address na namba za simu ikabidi niangaze angalau kupata simu lakini wapi,aise kinyarwanda sijui na wao kiswahili kigumu kila nae mujliza ila kupata mawasiliano sikupata msaada ikabidi nikasogolea kwenye stand ya mabus madogo nikamuulize konda kuwa nataka kwenda ubalozi wa Tanzania akaishia kucheka tu niligundua hakunielewa lugha .

Nakumbuka nilikaa stand pale hadi saa kumi na mbili bila bila ikabidi niulizie sehemu pakulala hapo nikaeleweka nikaambiwa lazima upande bus nipelekwe sehemu inaitwa NYAMIRAMBO na nikaambiwa pia kuwa kuna waswahili wengi nikapanda bus hadi nyamirambo nikashushwa tu stand konda akanionyesha kuna hoteli moja ilikuwa imeandikwa nakumbuka inaitwa kama sijasahau ilikuwa inaitwa IMHALA ila nyamirambo ilichanganya kigodo naweza fananisha Magomeni enzi zile.


Nikaenda nikalipia chumba nikaomba kuelekezwa eneo la kula nikaelekezwa, nikaenda nikala halafu nikarudi kujilaza nikipanga namna ya kuingia kesho u abalozi wa Tanzania kuanza majukumu mapya .

Itaendelea...........





Sent using Jamii Forums mobile app
Uje utuambie huyu Mnyarwanda anayetuendesha hapa nyumbani kama alikuja nchini na hayo Mabasi

Sent from my SM-A207F using Tapatalk
 
Hapo waweza tazama movie moja inaitwa "Rules of Engagement" kwa kusindikizia hii story...
Naona wazee wa defender walitangulia kufanya yao..
 
Inaendelea.........

Wandugu habari mchana sasa tuendelee tulipoishia, ubalozini. Sasa maisha yakawa yamehamia ubalozini maisha yakawa changanyikeni maisha yakawa hayana thamani tena, wanaume wajasiri wakajitolea kukaa zamu kulinda geti la ubalozi, maji yakakata watu wanalala njee kwenye nyasi hakuna cha mume wala mke wa mtu kama una mkeka mnalala chini familia mbili, ile mandhari ya ubalozi ikageuka kuwa kama kambi ya wakimbizi majani ya kukauka yote, maua yakafaa vyoo vikaanza kuzidiwa maji hamna daaahhh watoto vilio usiku kucha, ukichanganya na milio ya risasi ya mara kwa mara ikawa ni kusubiri siku ifike tuone nini kitakachotokea .

Sasa kuna mambo yalikuwa yanaendelea huku tanzania, kulikuwa sijui kuna vikao vya mazungumzo sijui ya amani kati ya serikali ya rwanda na waasi kama sijakosea alikuja habyarimana mwenyewe na baadhi ya mawaziri wake na wakati tunasikiliza redio bbc jioni anatoka kwenye kikao kuna maneno Aliyatamka hakika kuanzia siku hiyo niliwachukia Wanyarwanda wote, mungu anisamehe.

Alisema hivi watanzania na wageni wote nchini rwanda wako salama wala hakuna lolote linaloendelea baya kwao na serikali inaendelea kuwalinda, na maneno kuwa nchi imeingiwa na machafuko ni propaganda za waasi wa Kagame kujaribu kuishawishi dunia ili imuunge mkono katika hatua yake ya kuivamia rwanda na apuuzwe. Na siku hiyo ndo ilikuwa mwisho wa kusikiliza redio maishani mwangu, utamaduni ambao nimeendelea nao hadi sasa huwa sisikilizi redio kabisa,yani nikija kwako kukutembelea ukitaka kunifukuza kwako washa redio naondoka hapo hapo.

Watu wakawa wengi chakula kikawa kimeisha.tukafanya mawasiliano na balozi,sasa kuna kitu kilikuwa kinaendelea ambacho tulikuwa hatujui. unawakumbuka wale jamaa saba alikuwepo moja kama mpemba hivi siku hiyo alikuja na balozi, pale akaangalia hali halisi wakaingia ndani walichoengea na balozi hatujui ila wakatoka wakaondoka hapo wote tukabaki tunatazamana hakuna anaejua nini kinaendelea.

Sasa ipo hivi hakuna watu wabaya kama wafanyabiashara lakini walikuwa na msaada mkubwa unajua kama sio wafanyabishara wa maroli tungekuwa tumeondoka mda mrefu ila kukawa na zuio kuwa maroli yote ya watanzania ambayo yalikuwa bandari kavu eneo la MAGERWA (tamka majerwa) lazima yarudi na madereva wake wote sasa ikawa kuna mengine yalikuwa hayajapakua ililazimu yapakue na, ndo walipokuwa wale manjemba saba waliokuja na defender nilikuja kuambiwa baadae na dereva moja hivi lakini nae alikuwa anawaona tu wanazungukazunguka mle ndani ya bandari ila wakiwa makini kweli kweli na mabegi yao.

Siku zikayoyoma ikawa kila siku lazima balozi awashe gari lake aende Majerwa( bandari kavu) Peke yake anapakia tambi, majani ya chai maziwa ya kopo, na mazagazaga mengine waliyokuwa wanashusha kwenye maroli ya watanzania analeta tunakula siku imeisha mlo moja tu hakuna cha mama anayenyonyesha wala wala mtoto ni mlo moja tu basiii.siku zikawa zinakwenda ikawa sasa inakaribia siku yenyewe sasa ambayo iliweka historia nchini rwanda....................

Mwanzo wa safari ya mateso, kutembea katika njia ya mauti, kushuhudia maiti zimezaga barabarani kama nzige ,unyama mbaya kuwahi kuushudia maishani mwangu.....

Itaendelea............. Leo leo.



Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna dada mmoja humu anaitwa Jestkilla ni mnyarwanda tena mtusti amekuwa akitoa maneno ya kashifa na dharau kwa watanzania humu ndani...

Amesahau, jinsi tulivyowasaidia ndugu zao hadi kufikia ku-force ndoa ili kuwaupusha na vifo maana walikua wanachinjana kama mijusi...

Kuanzia leo naomba awaombe radhi Watanzania walioko humu kwa lugha chafu alizokua akiitolea Tanzania...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaendelea...................... 49k viewers si mchezo.

Haya sasa tusonge mbele tarehe, saa, sekunde za malaika mtoa roho zikawadia 6/04/1994. Saa tisa usiku tukaashuhudia kitu kama kimondo kikishuka ardhini ila kikapotelea vichakani kwa mbali nje ya mji. kutokana na kishindo chake pale ubalozini kila mtu aliamka lakini hakuna aliejua hasa ni nini, tukachukulia kawaida tukajua ni yale yale kila siku si tumeshaanza kuzoea watu wakaendelea kuchapa usingizi nawanaume wakaendelea kulinda getini.
Asubuhi mapema tukashudia hali ya ajabu ambayo sijawahi kuiona katika maisha yangu, yani kukatokea kitu kama wingu hivi yanii mtu akisimama mitaa tano au kumi kutoka ulipo huwezi mtambua vizuri hadi awe karibu sanaa. Wenye redio wakafungulia redio zao kusikiliza , ikumbukwe kuwa kipindi chote wapiga mayowe wa propaganda redioni walikuwa hawaongee ulikuwa unapigwa tu muziki wa chama ila alfajiri ikasikika wimbo wa taifa ndo unapigwa watu wakabaki wanashangaa halafu unakuwa unajirudia .dalili ya kitu kibaya ikaanza kuhisiwa kigali yote kimyaa.....

Tukawa sasa tunaingia tarehe yenyewe 7/04/1994 harufu ya damu ikawa inasikika kigali nzima, makelele ya maumivu ya watu yakawa yanasikika kwa mbali kutoka hapo ubalozini ,balozi ndo akawa ametoka kututangazia kuwa sasa hali si nzuri rais habyarimana ameuawa ile kusema tu vile watu wote akili zilituruka wengine wakawa kama wanataka kukimbia hovyo wanaume ikabidi wafanye kazi ya ziada kwani kitendo cha kutoka nje ya ubalozi kingeleta maafa makubwa sanaa. Ila wote pale picha iliyotujia kichwani ni kwamba sasa tunakufa hakuna tena msalie mtume.

Swali likaja nani kamuua rais? Hakuna mwenye jibu. Aise kuna wimbo moja hivi ukiimbwa unakuwa kama vile unaomboleza unafanafana na ile ya Kimasai ukawekwa kwenye radio ukawa unapigwa huku unamtaja rais kuwa ameuliwa na Ng'otanyi(waasi wa kitusi) aisee vita ikawa imeanza rasmi hata balozi sasa akawa hatoki tena tukakaa wote mle ndani hakuna kutoka kufuata chakula wala nini.

Siku ya kwanza mitaa kelele kila upande, sasa interahamwe wakaanza kuvamia hadi balozi za jirani ambao walikuwa wameondoka walinzi wao wakakimbia watu wakazidi kuuawa. chakula pale kwa ni uji tu hakuna sukari wala nini, unajua kama upo vitani mara nyingi unakuwa husikii hamu ya kula na unajiona uko powa tu kumbe unazidi kuisha ( kama kuna mtu alipigana vita humu ya kagera atadhibitisha hilo) halafu unaweza shanga kumekucha ghafla kiza kimeingia ghafla usiku mnalala usingizi wenye wa mang'amung'amu tu.

Balozi zikawa zinaendelea kuvunjwa siku zinaenda magrounet yanarushwa hovyo hovyo risasi zinalia zikitulia labda nusu saa zinaanza tena,unajua rwanda ni milima sasa unaweza kaa usiku unaona roketi inarushwa kutoka upande moja kwenda upande mwingine vimulimuli tu vya moto hadi kuna kucha kelele na risasi zinaanza tena. Sasa ikawa dhahiri kuwa hakuna namna tumuachie mungu tu.

Lakini wakati huo balozi alikuwa kwenye chumba kimoja kati vile vyumba vya sili nilivyosema hapo awali sijui alikuwa anafanya nini , ikafika ya kumi sasa ikawa hakuna kitu tena njaa tupo katikati ya vita mjini umezungukwa na wanajeshi wanapigana live bila chenga jiona ya siku hiyo ndo wakaja wanajeshi wa rwanda ,na toka siku ile ndo niliwaona live wanajeshi wa rwanda majitu yamepanda sura ngumu macho mekundu wakaja na maroli yale 24 na ile defender nyeupe ila waliokuwa kwenye ile defender hawakushuka tukaitwa uwani ubalozini .balozi akatoa tamko akasema SAFARI YA KUWAONDOA KIGALI WATANZANIA NDO IMEFIKA NA KAMA HUNA PAPER ( PASSPORT ) TAFADHARI USIPANDE KWENYE ROLI UKIPANDA LIKALOKUTOKEA MBELE USILAUMU MTU. hii kauli aliitoa kwa uchungu na kwa msisitizo sanaa huwa siisahau maishani mwangu. .

Hapo sasa ndo ngoma ikawa ngumu kila mtu akamkimbilia balozi kuomba amsaidie mkewe na watoto wake, balozi akagoma kabisa wengine akawa anawajibu kama unampenda mkeo baki nae hapa aisee watu wakawa kama vile wamepagawa maroli yapo nje lakini unashindwa kwenda kulipanda paper huna , sasa kuna kisa kimoja kilichojitokeza sintokuja kukisahau.kuna mama wa kinyarwanda mtusi alikuwa na bwanake mtanzania amezaa nae ila yeye kipindi cha vita alikuwa ameleta mzigo tanzania ,hivyo ikabidi mama ajitoe mhanga akamuita balozi awachukue wale mabinti wake mapacha wawili walikuwa kama na miaka 14 hivi weupe pua za kitusi kabisa balozi akakubali mama akabaki ,sasa tutaona mbele walivyotaka kuleta kizaazaa nusu tuchapwe RPG kwa sababu yao.

Sasa tukawa tumejipakia kwenye roli wengine wasio na vibali wakawa wamebaki pale hapo ubalozini, hapo hakuna kusikitikiana mnapeana mkono wa kwaheri basi safari ikawa imeanza na escot ya wanajeshi wa rwanda ,vizuizi kibao tukifika kwenye vizuizi wanashuka wanaenda wanajeshi wenyewe wanavitoa tunapita ,cha ajabu vizuizi vingine vilikuwa havina hata watu sijui walikuwa wakajificha au vipi.

Sasa wakati vita imepamba moto Tanzania wakawa wamefunga mpaka wake na rwanda Ikatulazimu kupitia boda ya burundi sasa kimbembe ndo kikaanza hapo, kuna wilaya kama tatu inabidi upite ndo ufike boda ya Burundi na rwanda kama sijakosea kwa kutokea kigali lazima upitie province ya butare halafu ya Gitarama ya mwisho nimeisahau kitambo sanaa. Sasa province Butare (wenyewe wanaita) ili ufike lazima uvuke mto fulani mkubwa unaitwa Nyabarongo kuna daraja kubwa hivi linalounganisha kigali na hiyo wilaya hapo sasa ndo niliona mchezo wawale jamaa saba wa defender hapo tunaenda lakini magari yanakanyaga maiti barabarani maiti zimezaga kila kona. Ile tunashuka kilima kidogo inakaribia kuulifikia kama kilomita tatu hivi wale wanajeshi wa rwanda wakageuka na gari lao ghafla wakarudi nyuma moyo ukapiga paaahhh nikahisi kuna kitu si chakawaida unageuzaje gari ghafla unarudi kwanini usituache tuvuke ndo urudi aisee.

Mbele tena kidogo ile defenda ikasimama katika ya barabara hakuna gari kuendelea kupita magali yakawa yamesimama tu ile defenda ikawa inaendelea kusogea mbele sisi tumeambiwa tusimame hapo hapo hadi Difenda itakaporudi kutoruhusu tuendelee tukawa tu pale na madereva kila mtu kwenye Kibini wengine kwenye bodi nyuma kimyaaaaaa...


Kama lisaa hivi tukasikia risasi zinalindima vibaya Sanaaa yani ikawa dhahiri kama mbele yetu kama kilomita moja watu wanapigana lisasi live ila hatuoni tatizo la rwanda mapori na vichaka vingii ila risasi zikawa zinalia kama zipo chumbani nikasema sasa huu ndo mwisho wetu.

Mwisho lisasi zikakoma tumekaa kama nusu saa hivi defenda hairudi na risasi hazisikiki tena Mwisho balozi akaamuru tuendelee na safari bila defenda dahhh ile tunafika darajani maiti kibao zimelala hapo ila hakuna defenda tukawa tunaendelea na safari tu.

Sasa tukawa tunakaribia kuimaliza province ya Butare sasa hapo ndo kulitokea kizaazaa cha wale mabinti aise tulikuta bonge la kizuizi...... Na maenterahamwe mchanganyiko na wanajeshi wa rwanda aise........ Nikasema. Sasa tunakufa.................................

Itaendelea...........................................

Sent using Jamii Forums mobile app
Dah! Inatisha na inasikitisha Sana
 
Kuna dada mmoja humu anaitwa Jestkilla ni mnyarwanda tena mtusti amekuwa akitoa maneno ya kashifa na dharau kwa watanzania humu ndani...

Amesahau, jinsi tulivyowasaidia ndugu zao hadi kufikia ku-force ndoa ili kuwaupusha na vifo maana walikua wanachinjana kama mijusi...

Kuanzia leo naomba awaombe radhi Watanzania walioko humu kwa lugha chafu alizokua akiitolea Tanzania...

Sent using Jamii Forums mobile app
Hao wengi wao walizaliwa 96 kwenda chini....hawezi jua kitu msamehe tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akifanya hivyo ataharibu uzi. Bora asubirie hadi mwenye simulizi yake amalize kabisa ndiyo aongezee hayo ya kwake. Hata sisi wengine tunayo baadhi ya mambo ya kusimulia kuhusu mauaji hayo lakini tumempa nafasi mwenye mada yake anogeshe mambo.
Nimekupata mkuu
 
Nashindwa nikujibu je.ila nikuombe hebu angalia move za mauaji ya kivita kuna hali inakuwa kama vile haiko sawasawana kama vile nchi inapokuwa na amani. Angalia move kama diamond blood,tears of the sun, au hata angalia vita ya kagera Tanzania na Uganda. Yanii angani kuna wingu jeupe linashuka karibia ardhi sijaweza kujua ni nini.
Mkuu ufafanuzi kidogo lile wingu lilisababishwa na nn

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom