Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Nakubaliana na wewe kabisa. Ila nikuulize swali moja. Hivi unawafahamu watanzania kweli... Hawajali hata chembe. Wazo lako ili lifanikiwe, lazima liratibiwe, ni mchakato mrefu hasa wa kifikra. Sasa nani aratibu?! Mbowe!? Au hao waliokwenda ikulu wakiinama na kuinuka kama wanoingia mbinguni...? Wanasiasa wa upinzani wote hawafai kabisa kwa kuwa wameshindwa kurithisha madaraka kwa vijana, na kwa utu uzima wao (in fact uzee wao) hawawezi kutupatia mbinu bora hata chembe...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilichogundua hii haikuwa vita kama inavyoitwa, vita kwa uelewa wangu huwa ni pande mbili zinapigana.
Ila haya yalikuwa mauaji.
Na ndiyo maana siku zote yamekuwa yakiitwa mauaji tena mauaji ya kimbari. Kwa sababu asimilia kubwa kabisa ya waliouwa walikuwa ni wa upande mmoja yaani watutsi. Siyo vita wala nini.
 
wahutu walikuwa na mpango wakutokomeza kizazi cha watutsi, yaani kuua watutsi wote, ili enterahamwe wakose sapoti ya kuchukua nchi. Kagame anafanya vizuri sana kumaliza nguvu za wahutu. wahutu ni makatili sana bora kagame awauwe wale wakorofi. i hate hutus
 
Raia wa kitutsi na kihutu walikuwa adui.hivyo wale raia wa kitutsi walioko ndani ya rwanda walikuwa wanapenda wanajeshi wa kitutsi ( kina kagame) washinde vita ili nao wawe na power.maana walikuwa wanateseka na manyanyaso ya wahutu.ndio maana hapo msimuliaji alisema kwamba kulikuwa na watutsi wanatoroka kimya kimya wanakwenda msitunni kukutana na waasi.wanapewa mafunzo kisha wanarudi mtaani.na katika hizo safari walikuwa wanatoa siri ya mambo yaliyokuwa yanaendelea ndani ya nchi.hivyo hutu wakaona kuwa wanaishi na wasaliti mtaani.wakaona tutsi wote lao moja na waasi..ndio maana wakapanga kuwapoteza wote ...( mfano ikitokea jirani hakupendi anaenda kwa balozi wa kihutu..anamwambia mzee fulani wiki nzima hayupo mtaani ..ndio karudi leo naskia alienda polini kwa waasi..balozi atawasiliana na kiongozi wa jeshi..hapo watakuja home kukuchomoa na ndio unakufa hivyo.) ...samahani kwa kuingilia simulizi..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu! wakati raia wanauawa hovyo hawa askari wa UNAMIR walikuwa kimya tu bila kufanya kitu?
Walikuwa walinda amani hivyo hawakuwa na order ya kuingilia hiyo vita...lakini pia hao inasemekana walikuwa na mambo yao...mabeberu kama kawaida yao...kwahiyo walikuwa kama wale chatu wa ngoma za asili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na ndiyo maana siku zote yamekuwa yakiitwa mauaji tena mauaji ya kimbari. Kwa sababu asimilia kubwa kabisa ya waliouwa walikuwa ni wa upande mmoja yaani watutsi. Siyo vita wala nini.
Wahutu wengi pia waliuwawa hasa kama muhutu umeoa mtutsi halafu hutaki kuwauwa mkeo na wanao hivyo intrahamwe wanawaua wote kwakua ni mwiko mwanaume wa kihutu kuoa mke wa kitutsi..na ni hivyohiyo kwa wanawake..pia kuna wale ambao hawakujiunga na wahutu wenzao kuua watutsi hivyo unaonekana hampo pamoja..unakumbana na mtiti kama mtutsi..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante sana mkuu kwa hoja zako maridhawa, natamani kila mwanaJF awasilishe mawazo yake pasipo matusi na kejeri. Najiuliza kwa nini mtu anakuwa bize kuandika matusi tu, ina maana watu wetu wengi vichwani hamna fikra njema!! Hawataki kuumiza vichwa kidogo wakajenga hoja??!

Anyway!! Nikirudi kwenye hoja yako mkuu, hawa watusi waliteswa mno na wahutu. Ukimsoma mtoa post, attack ziliwalenga watusi, hivyo mikakati ya kujikomboa ilikuwa ni sawa kabisa. Shida ya ukombozi wà namna hiyo haudumu. Inasemekana kwa sasa ambapo watusi ndo wenye nchi, wahutu wako magerezani wanaozea huko. Hivyo, amani ya Rwanda nina mashaka nayo iwapo itadumu baada ya Kagame.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilichogundua hii haikuwa vita kama inavyoitwa, vita kwa uelewa wangu huwa ni pande mbili zinapigana.
Ila haya yalikuwa mauaji.
Vita vilikuwepo awali kati ya waasi (RPF) na Serikali ya Habyarimana ndio maana hata mazungumzo ya amani yalifanyika hapa Tz.

Ila mauaji yaliibuka baadae baada ya Rais Habyarimana kuuawa, japo inawezekana mauaji yalipangwa toka kitambo.
 
Kweli mzee kizazi kipya cha kihutu bado wana kisasi na unyonge, inaonekana wakipata backup toka kwa wakongwe walio magerezani lazima wakamilishe mission yao iliyozimwa hapo mwanzo
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na namna kagame anafanya sasa anakuwa kama ametega time bomb! Muda wake ukiisha au akifa ...it will be time.. the bomb to explode..mauaji ya kimbari yatatokea tena..hutu ni wengi sana kwa population 80%.hivyo kama tutsi wajanja wakiona kagame anakwenda halijojo..inabidi wakimbie vibaya sana[emoji23][emoji23].

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vita vilikuwepo awali kati ya waasi (RPF) na Serikali ya Habyarimana ndio maana hata mazungumzo ya amani yalifanyika hapa Tz.

Ila mauaji yaliibuka baadae baada ya Rais Habyarimana kuuawa, japo inawezekana mauaji yalipangwa toka kitambo.
Hutu militia (interahamwe )na baadhi ya maofisa top rank wa jeshi la rwanda.hawakukubaliana na mazungumzo ya amani..hawakuwa tayari kushea uongozi na waasi kina kagame..na ajenda kuu ya mkutano wa arusha ilikuwa kusitisha vita na kisha kushea madaraka kwa mgawanyo sawa kati wa hutu na tutsi.sasa top rank wa jeshi wote ambao waliunga mkono mazungumzo ya amani waliuwawa kwa nyakati tofauti..pia ndani ya ndege iliyouwa wale marais kulikuwa na maofisa wa juu wa jeshi la rwanda.nao walifia humo.jeshi liliteuwa wakubwa wengine ambao waliendana na mpango wa yale mauaji.kama sijakosea top rank alikuwa augustin bizimungu ( general) na theonette bagosora (kanali).

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yan nasikitika watanzania wenyewe wanaanza kushirikisha serikali kuhusika na mipango ya Rwanda pia hata Kama ilkua hvyo Basi mjue ilkua n kwasababu za kimaslai dhidi ya bongoland nasio vinginevyo Mana naona kunawatu wanakuja na swaga za bongoland ilihusika hvyo mjue hata Kama ilkua hvyo n kwa usalama wa baba zenu enz zile ndomana Leo unakatiza mikoa unayotaka bila wasiwasi na chezo ukitaka unapewa kwa ukarimu mkubwa.

Hata ukusikia nchi flan imepeleka wanajeshi wa Aman taifa flan jua Kuna kitu taifa lililopeleka hao njemba litanufaika na kitu kutoka huko.

Ila leo Jamaa kauchuna leo Mie naona aje yule jamaa aliemkumbusha kuwa ubaloz ulkua sehemu gan sijui ile, Mana hapa tunalishana mawazo mema kwa taifa Bora la kesho
 
''Wengi wape" kwanini Tutsi hawataki kutawaliwa na Wahutu walio wengi?

alafu mbona stori nyingi inaonekana wahutu ndio makatili na wakorofi?

kwani watutsi ni innocent kwa Wahutu tangu kizazi na kizazi?

Vipi kwa sasa utawala wa kagame, jeshi lina Wahutu pia?

Wakuu stori hii inasikitisha , hasa nikifikiria watanzania wenzangu waliokuwa na familia huko, Nahisi watanzania wengi waliuwawa ila mtoa mada alipona ndio maana leo anasimulia
RIP watanzania wenzetu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dikteta Mobutu alikuwa mshikaji wake Habyarimana wa kufa na kuzikana. Ukifika eneo hilo yalipokuwa makazi ya Habyarimana nyuma ya nyumba kwenye bustani utaona kibwawa kidogo ambacho simulizi iliyopo ni kwamba enzi za Habyarimana kuliwekwa chatu mwenye urefu na uzito mkubwa sana ambaye alikuwa akitumika kwa mambo ya kishirikina ikiwa ni pamoja na kufanyia kafara. Na huyo chatu alikuwa kapewa na rafikie Mobutu ili kufanyia huo ushirikina. Usiku ule ule Habyarimana alipouawa hilo chatu nalo lilipotea katika mazingira yasiyoeleweka na hadi leo halijawahi kuonekana tena.

Kingine ni kwamba mara baada ya Habyarimana kuuawa mwili wake ulichukuliwa kwa siri na kupelekwa huko Zaire (kwa sasa DR Congo) na Mobuto kuuhifadhi huo mwili wa best yake nyumbani kwake kwa miaka kama mitatu hivi hadi pale na yeye alipokaribia kupinduliwa na waasi wa nchini mwake ndipo akaamua kuuchoma moto!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…