Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Barrier hazikuwa nyingi kihivyo zilikuwa mbili tu na maaskari walikuwa wanahangaika na malori kuliko hivyo vigari vidogo vya abiria.
Halafu napata mashaka kama kweli ulikuwa nimwanabarozi,kujua vizuizi vilivyopo kasumbalesa mpaka Lubumbashi kote huko ulifuata nini tena na gari wakati ubalozi upo kinshasa maelfu ya km kutoka mpaka wa Zaire(Kongo) na Zambia.
Mi nadhani useme ukweli tu kwamba wewe ni wa malori mwenzangu sio dhambi.
Na sisi watu wa malori tuna exposure kubwa zaidi kuliko wapanda ndege hivyo usione haya kusema wewe ni dereva.
Pia wakati wa machafuko nyie mnaojiita mabalozi mlijifungia ktk balozi zenu sisi baadhi yetu ndio tuliotekwa nyara tukazuiwa,bidhaa zikaibwa na baadhi ya nyakati tulishuhudia live watu wakiuawa. Na ukiruhusiwa kurudi kwenu unakuta maiti zimezagaa barabarani,mwanzoni tulikuwa tunazisogeza kwa kuzipa heshima ya kibinadamu lakini kwa jinsi zilivyokuwa nyingi tukawa tunazikanyaga tu.


Sent using Jamii Forums mobile app
Basi tunasubiri story yako mkuu ikiisha hii asante sana kumbe na wewe ulikuwa huko
 
Na Chisekedi anaungwa mkono na PK? Au historia imeishia kwa Joseph Kabila?
Nachoamini mimi hizi zote ni consipiracy theories. Nimewahi kusoma makala fulani ilikuwa inamuelezea Kabila Jr, na inaonesha kabila aliishi Tanzania na mdogo wake wa kike. Makala hiyo imeeleza jinsi Kabila Jr alivokuwa akienda msituni mara kadhaa kuungana na waasi.

Halafu pamoja na jinsi USA anafaidika na DRC mbona USA huyo huyo alimkodolea macho sana Kabila ili aondoke madarakani.
 
wewe nawe babu zima unakua na mishebeduo kama demu.
Ukiambiwa fact kubali, wengi tumeshakushtukia tangu mwanzo.

Ulikua unabwabwaja ukidhani hakuna wanaojua story ya Rwanda kuliko wewe imekula kwako 😅😅😅😅😅
Kwani yeye kasema Rwanda alikuwa peke yake.
Wewe ni mtusi umetumwa kuchafua uzi hapa sio Rw .
 
Nilichopenda kwenye story yote ya huyu bwana ni personal account kwa jicho la mgeni that perspective made it interesting to me na nilijikuta jumamosi na jumapili yote nasoma kuanzia mwanzo hadi mwisho that is rare for me kufuatilia thread hivyo.

I wasnt disappointed either because he is a very good storyteller with much use of imagery unasoma kama vile na yeye unamuona na character zingine walivyokuwa wanapambana na hizo changamoto there are couple of established novelist haven’t reached the level of his art ukisoma vitabu vyao.

Lakini kuhusu nini kilichojiri lets not get carried away there are hundreds of journals, first hand interviews and books which provides different perspectives and the role of various stakeholders labda kinachouzi nchi iliyokuwa mstari wa mbele kwenye usuluhishi kama Tanzania wahusika did not bother to give their accounts kwa ivyo kwa wafuatiliaji utakutana na perspective za west on the whole saga na hakuna information isiyokuwepo.

Vilevile hakuna kilicho siri balozi kuokoa watu wake aliwezi kuwa swala la national security baada ya incident kupita kwanini umfiche heroin kama huyu wakati wenzake hao hakina ‘Ami Mpungwe’ ata kama sisi atutatumbui mchango wao S.A wamempa huyo mtu medal ya juu wanayoweza toa ya ushujaa ndani ya nchi yao kwa raia na amepokea recognition kibao za kimataifa kama Tanzania diplomat kwenye masuala ya Rwanda.

Mwisho kabisa kwa mtu aliyeenda shule kusoma kitu bila ya kutafuta credibility ya story yenyewe inaonesha huyo kwenye elimu alikuwa msindikizaji au mfumo wa elimu aliyopitia una utata na hakuna sababu ya kufundisha wanafunzi namna ya kuchambua credibility sources na pumba kwenye kufanya research.

Kama elimu airuhusu kumeza kila kitu na facts zinaonyesha atukuwa na balozi Rwanda wala Burundi kuanzia 1992 mpaka 1995 bila ya kutaja huyo balozi pamoja na uzuri wa maelezo yake na reality resembleness sijui kwako ila kwangu itabaki kuwa na elements za fictitious story.

mkuu kwanza nikushukru kwa uchambuzi, isivyo bahati mambo ya diplomatic ethics yanamlolongo mrefu sanA, kiasi kwamba ukitizama kwa makini Bossless amejarb tu kuelezA yale mambo kwa juujuu sana....

hvyo upo ukwel lakin si ukwel wote ila tukio au matukio ni hAlisi.... wakati mwingin maadili ya kazi yAnazua kusemA kitu maana ukikisemA hicho kitu hAtA kama una id iliyojificha waki track wanajua ni nani kasema.....

b
 
Inaendelea ..............

Sasa nimelazimika kuandika hii mapema Sanaa asubuhi ili kumpa mwenyewe simu yake andelee na mambo yake .(simu ya wife)

Sasa tuendelee tukafika province ya GITARAMA tukashudia Jambo la ajabu Sanaa yani kumepowaa watu wachache Sanaa wanatembea mtaani Ila maduka yako wazi biashara inaendelea tu Kama hakuna kitu kinachoendelea Rwanda nikashangaa Sanaa huwezi amini ilibidi tusimame hapo kwanza kwa muda magari yote yakasimima tukawa tunashuka tumepumzika wengine wanaenda dukani lakini hakuna anaerudi na kitu ikawa ni Yale Yale nipe kitu nikupe kitu ,yani una hela nyingi za manyarwansa unaenda dukani mwenye duka anakwambia Kama unataka labda soda nipe Hilo jacket lako aise ikawa pale watu wanauza majaketi na masweta njaaa............ni hatariii.

Unajua ule mji wa GITARAMA Kuna baridi hatari naifananisha na baridi ya njombe na tunduma mwezi wa sita .yani unavaa jacket ili baridi isiingie kwenye mifupa lakini bado inakuchapa tu Kama kawaida ,watu wakawa wanabadilishana na saa za mikononi kwa biskuti daa njaaa....

Gari zikawashwa tukaanza Sasa safari ya kuelekea province nyingine(nimeisahau jina) tukawa tunaendelea tu na safari Kama kilomita 150 tunamaliza Sasa ndo live tunayakuta majeshi ya hayajulikani Ila baadae niliambiwa ni ni batalio ya PK yanii wapo full vijana wembamba warefu wa kitusi ,Ila nchi ya Rwanda niyakipumbavu Sanaa,Sasa katika kuchunguza kwangu nikagundua Kuna baadhi yao wanahaiba ya kihutu kabisa Sasa nikawa najiuliza hii Vita gani? Mbona sielewi ni yakikabila au ya kimaslahi nikawa nikaaachana na Hilo wazo wakatusimamisha lakini kiistarabu Kama traffic hawa wa kwetu wanavyosimamisha magari ya tukasimama .

Sasa ikawa wanaongea na balozi wetu Ila baadae ilikuja julikana kuwa walikuwa wanadai kipande kilichobaki Cha kuingia mpakani Kati ya Burundi na rwanda Kuna mtanange unaendelea( Wanaume wanachapana risasi ikumbukwe mpaka mda huo Kuna miji ambayo tayari ikishakuwa chini udhibiti wa majeshi ya kagame akitafuta mbinu za kuingia Kigali ) tukashauriwa tusubiri kwanza hali itakapokuwa imetulia Hali tutaendelea na safari

Tukatulia hapo inaelekea saa kumi na mbili ya jioni muda ukawadia tukaruhusiwa Sasa Cha ajabu wale wanajeshi wote walikuwepo wakapanda kwenye yale maroli tukawa tunaelekea njia moja kila roli na wanajeshi Kama nane hivi au kumi nyuma ya bodi safarii ikaanza wazee wapo tayari tayari kwa Hali ile nikasema Sasa hapa tunaingia vitani rasmi safarii ikawa inasonga ,Kuna kitu nilijifunza vitani Mara nyingi vitani wanajeshi wanaongea kwa ishara na Kama wakiamua kuongea Basi huongea kwa sauti ya chini Sanaa.

Sasa tukawa Kama tumeshatembea Kama kilomita 30 hivi Sasa tukaanza kusikia risasi zinarushwa hovyo hovyo kutokea maeneo ya polini wale wanajeshi wakastukia kiongozi wao nikasikia anatoa sauti flani hivi ya kutaka Kama kujibu mashamulizi hivi wale wanajeshi nao wakawa wanarusha risasi hivyo hivyo msituni yani AK 47 zinanguruma kwenye masikio yetu live huku magari yanaendelea tu kutembea Ila kwa mwendo mkali Sanaa jamaa wakawa wanajibu Kuna askali alikuwa amesimama upande wangu alikuwa ana RPG na bunduki akawa anaweka vizuri rocket Ili alivurumishe kwenye vile vichaka akinipa Ak47 halafu ananionyesha niendelee kufyatua risasi kwa mbali kupitia tundu la bodi ya gari (yani nilivyoishika ile chuma Kama dakika mbili tu nikajikuta yani nimepata ujasiri mkubwa bila kutarajia hapo ndo nilisema mwanzo nami nikawa nimepigana angalau Vita kidogo yule mwanajeshi akavurumisha lile li rocket Polini mle ndo risasi zikawa zimepoa safari ikawa inaendelea kwa kasi .

Tukaenda tukafika mbele kidogo Kuna Kijiji kimoja wakashuka wakabaki wanajeshi wachache tu tukaendelea na safari hapo wakatwambia kazi imeisha Sasa tunaweza kwenda Hadi boda tukawa nao wale wachache Hadi boda tukafika Kama saa mbili usiku hivi.

Sasa angalia chakushangaza tukalikuta lile defenda jeupe na wanajeshi wale njemba Saba walioshuka ubalozini siku ile yani wamechafuka vibaya sanaa yani vumbi Hadi kwenye kope wamevaa combati hizi hizi za jeshi letu lakini hazina majina yao wala begi ya bendera ya Tanzania wakasalimiana na wale tuliowa wachukua njiani hapo Sasa nikajiongeza nikajua Hawa wazee ,tofauti na pale ubalozi hawakutaka kuongea na mtu pale wakawa wanasaidia watu kushuka halafu wanatupa na pole kabisa huku wanatabasamu ,majitu yameshiba

Sasa Kuna Jambo pembezo ya mpaka likawa linawashangaza watu ,kwenye ukingo wa Barbara wa daraja watu wakawa wanakimbilia pale kwa wingi kuangalia majini usiku wa mbalamwezi huo( kwa taarifa tu Mpaka wa Burundi na rwanda unatenganishwa na mto au niseme maporomoko Kama Yale ya rusumo sijui jina lake) namimi nikawa nimesogea pale lahaulaaa maiti zinatoka upande wa Burundi wa mto zinaingia upande wa Rwanda wakiwa wamechomwa na miti tumboni nasehemu za sili nikasema hii ni Sasa na burundi kimechafuka au ? Sasa nikawa najiuliza tunaenda wapi tunaluka majivu tunakanyaga Moto .
.
Ukisikia kukataa tamaa ya kuishi ndo ikawa Sasa nimekata tamaa nilijua tukifika Burundi ndo ntakuwa sasa nimepona Sasa nao wamaenza kuchinjana Tena ....watu wa boda usiku huo wakaruhusu magari tu kuvuka upande wa pili wakasema watu Hadi kesho tukalala chini pale boda.....maishaaa

Itaendelea..............


(Narudisha simu kwa wife nikipata muda Tena ntamuomba niendelee sijaenda kwa fundi Leo mvua inanyesha, halafu watu wengi wanajua naishi Dar, japo nimezaliwa Ilala nimekulia Magomeni mapipa mtaa wa kizingo nyumba namba Siri yangu Ila kwa Sasa Mimi naishi Morogoro -wilaya mpya ya Mlimba .tarafa,kata,Kijiji Siri yangu najishughurisha na kilimo Cha mpunga na biashara ya mchele) jumapili njema .

Sent using Jamii Forums mobile app
Daah yan wewe nakujua kbs
Mimi bi mkubwà wangu kakulia wazani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
I concur.. Ila one thing is certain mtoa mada amewahi kuishi Rwanda maana kwa jins anavyotofautisha haiba, tabia na tofauti kati ya wahutu na watutsi ni pasi na shaka kwamba amewah kuishi Rwanda. Anatoa vivid naration ya yaliyojiri na yeye akiwa part ya yaliyotokea since 1989 mpaka 1994 ambayo siwezi pinga most of the details zinareflect kiukweli yaliyotokea ambayo ni good thing kushare na kutoa mwangaza kwa waliokuwa hawafaham yaliyojiri pia kutoa precaution kuhusu madhara ya ukabila na utengano wa kikanda hasa Tanzania inapoelekea katika uchaguzi mkuu 2020... Kiukweli ukabila ni mbaya sana na athari kubwa sana panapoibuka Civil/tribal wars. History ni mwalimu mzur kuhusu madhara yake tunapoangazia vita mbalimbali za kikabila zilizowah tokea duniani

Lakin pia niseme kuna discrepancies nyingi katika story yake, siondoi credibility ya maudhui ya story hii ila niseme tu;

1. Hakuna province mbili katika nchi ya Rwanda zinazotenganishwa na zaid ya km 150 kama anavyosimulia mtoa mada kwamba wakati wana evacuate toka kigali baada ya vita kuanza kuna kipind walisafiri km 150 toka province moja mpaka nyingine, hii si kweli. Rwanda ni nchi ndogo sana hakua mkoa unaotenganishwa na mkoa mwingine kwa zaidi ya km 150

2. Anasema walitoka province ya butare then wakaenda province ya Gitarama siku iliyofuata then wakafika border ya burundi the next day. Si kweli maana ukitoka Kigali unaenda province ya Gitarama then ndo unaenda Butare(Huye) na si vice versa ndo unafika Border ya Rwanda na burundi. Kwa route hii kutoka kigali mpaka border ya burundi ni only 154km.

3. Kama waliondoka Kigali kwenda border ya Burundi kuna short route ya kupitia Kinazi then Nyamata mpaka Border ya Burundi. Njia hii ni rougly 36km kutoka Kigali unakua umefika border ya Burundi. Ndo njia ya haraka zaidi, Why hawakupita njia hii sijui.

4. Furthermore kutoka kigali kuja Tanzania directly ilikua rahisi zaidi kupitia border ya Rusumo. Ambapo route hii ya kutoka Kigali mpaka rusumo ni umbali wa 156km tu.
Why walienda bujumbura kwanza ndo waje Tanzania mtoa mada anaweza fafanua zaidi.

5. Pia kwa nini aliacha a very lucrative, noble diplomatic job na kuturn into bussiness bila kufukuzwa kazi na kuturn into bussiness za chuma chakavu Zambia itabaki kuwa mystery kwangu. Uache kazi inayolipa vizur na yenye future na heshima ubalozini uende uza vyuma chakavu zambia inatatanisha. Maybe anaweza fafanua zaidi.

6. Evacuation ya Kutoka Kigali kwenda mipaka yote iwe Uganda, Tz, Burundi au ata Goma DRC kwa gari haipaswi kuchukua more than 1 day maana kigali ni katikati kabisa ya nchi. Na umbali wa kutoka kigali kwenda mipaka yote ya Ug,Tz, DRC, Burundi haizidi km 170. Ambayo kama ni kwa hapa Tanzania ni umbali wa kutoka Dar city centre mpaka Morogoro na morogoro hufiki, Rwanda ni nchi ndogo sana.

Yapo mengi ila kwa sasa ni hayo tu.

Hujafuatilia simulizi vizuri kumbe

Amesema wakati wanarudi Mpaka wa Tanzania na Rwanda ulikuwa umefungwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
I concur.. Ila one thing is certain mtoa mada amewahi kuishi Rwanda maana kwa jins anavyotofautisha haiba, tabia na tofauti kati ya wahutu na watutsi ni pasi na shaka kwamba amewah kuishi Rwanda. Anatoa vivid naration ya yaliyojiri na yeye akiwa part ya yaliyotokea since 1989 mpaka 1994 ambayo siwezi pinga most of the details zinareflect kiukweli yaliyotokea ambayo ni good thing kushare na kutoa mwangaza kwa waliokuwa hawafaham yaliyojiri pia kutoa precaution kuhusu madhara ya ukabila na utengano wa kikanda hasa Tanzania inapoelekea katika uchaguzi mkuu 2020... Kiukweli ukabila ni mbaya sana na athari kubwa sana panapoibuka Civil/tribal wars. History ni mwalimu mzur kuhusu madhara yake tunapoangazia vita mbalimbali za kikabila zilizowah tokea duniani

Lakin pia niseme kuna discrepancies nyingi katika story yake, siondoi credibility ya maudhui ya story hii ila niseme tu;

1. Hakuna province mbili katika nchi ya Rwanda zinazotenganishwa na zaid ya km 150 kama anavyosimulia mtoa mada kwamba wakati wana evacuate toka kigali baada ya vita kuanza kuna kipind walisafiri km 150 toka province moja mpaka nyingine, hii si kweli. Rwanda ni nchi ndogo sana hakua mkoa unaotenganishwa na mkoa mwingine kwa zaidi ya km 150

2. Anasema walitoka province ya butare then wakaenda province ya Gitarama siku iliyofuata then wakafika border ya burundi the next day. Si kweli maana ukitoka Kigali unaenda province ya Gitarama then ndo unaenda Butare(Huye) na si vice versa ndo unafika Border ya Rwanda na burundi. Kwa route hii kutoka kigali mpaka border ya burundi ni only 154km.

3. Kama waliondoka Kigali kwenda border ya Burundi kuna short route ya kupitia Kinazi then Nyamata mpaka Border ya Burundi. Njia hii ni rougly 36km kutoka Kigali unakua umefika border ya Burundi. Ndo njia ya haraka zaidi, Why hawakupita njia hii sijui.

4. Furthermore kutoka kigali kuja Tanzania directly ilikua rahisi zaidi kupitia border ya Rusumo. Ambapo route hii ya kutoka Kigali mpaka rusumo ni umbali wa 156km tu.
Why walienda bujumbura kwanza ndo waje Tanzania mtoa mada anaweza fafanua zaidi.

5. Pia kwa nini aliacha a very lucrative, noble diplomatic job na kuturn into bussiness bila kufukuzwa kazi na kuturn into bussiness za chuma chakavu Zambia itabaki kuwa mystery kwangu. Uache kazi inayolipa vizur na yenye future na heshima ubalozini uende uza vyuma chakavu zambia inatatanisha. Maybe anaweza fafanua zaidi.

6. Evacuation ya Kutoka Kigali kwenda mipaka yote iwe Uganda, Tz, Burundi au ata Goma DRC kwa gari haipaswi kuchukua more than 1 day maana kigali ni katikati kabisa ya nchi. Na umbali wa kutoka kigali kwenda mipaka yote ya Ug,Tz, DRC, Burundi haizidi km 170. Ambayo kama ni kwa hapa Tanzania ni umbali wa kutoka Dar city centre mpaka Morogoro na morogoro hufiki, Rwanda ni nchi ndogo sana.

Yapo mengi ila kwa sasa ni hayo tu.
Kuhusu swali lako namba 5 Diplomats wengi huwa ni watu wa Usalama wa Taifa kama utakuwa mfuatiliaji wa mambo utakuwa unalijua hili

Na nikufichulie siri nyingine moja ya style ya maisha ya Usalama wa Taifa huwa wanasafiri sana nje ya nchi na hawafanyi kazi moja tu huwa wanakuwa attached maeneo mengi tofauti tofauti

Rejea post alizokuwepo mkurugenzi mkuu wa usalama wa taifa wa sasa Diwani Msuya (alipanda vyeo haraka na huko Polisi mara akawa ADC wa IGP mara akaja kuwa RPC, akapanda fasta kuwa DCI, akaenda kuwa RAS Kagera, akaja kuwa mkurugenzi mkuu wa Takukuru mara amekuwa mkurugenzi mkuu wa Usalama wa Taifa)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Iko hivi...Congo War 1 ilikua kati ya mwaka 1996-1997. Kuna makundi manne( Mobutu Sseseko, Laurent Kabila, Paul Kagame, Yoweri Musseveni) yaliyopigana vita hii na kila kundi lilikua na interest zake tofauti.
Vita hii ilitokea DRC kipindi hicho ikiitwa Zaire ilianzia pronvince za kaskazini mashariki Nord na Soud Kivu, ikaelekea Kisangani mpaka DRC magharibi then Kinshasha ilipoisha na kuondolewa madarakani kwa Rais wa kipind hicho Mobutu Seseko, nchi ikatwaliwa na Laurent Kabila aliyebadili jina la nchi kutoka Zaire na kuwa Democratic Republic of Congo.

Kwa kifupi ni kwamba wakati vita hii inaanza Mobutu ndiye alikuwa rais halali wa DRC na Laurent Kabila Sr ndiye alikuwa muasi akipigana kutoka msituni mashariki ya Kongo. Kabila alipata msaada wa kijeshi kutoka kwa majeshi ya Rwanda na Uganda chini ya Kagame na Mseveni. Lengo la Kagame si kwamba alikua sympathizer wa movement au uasi wa Kabila bali lengo lake lilikua ni kuwamalizia mbali wahutu na interahamwe wote waliokimbilia Congo baada ya genocide ya 1994 na pia aliona fursa kwenye madini adhimu ya Congo.

Museveni ye hakua interested na wahutu bali ye pia aliona fursa kwenye madini. Sasa basi majeshi ya Rwanda chini ya Gen James Kabaerebe, uganda pamoja na vikosi vidogo vya waasi wa congo wakiongozwa na Laurent Kabila walivamia Congo mwaka 1996 na kuanza kuuwa interahamwe , kushambulia majeshi halali ya Congo ya Mobutu, wakasonga mbele Toka Goma, kwenda Kisangani, kindu, kinanga mpaka walipofanikiwa kuuzingira mji mkuu wa DRC Kinshasha na kumuondoa madarakani Mobutu Seseko, na kufanikiwa kumuweka kibaraka wao Laurent Kabila kama rais mpya wa DRC. Kabila aliwatunuku vyeo jeshi maafisa waandamizi wa majeshi ya Rwanda ilhali hawakua raia wa Congo.

Ambapo Gen wa kitutsi James Kabarebe aliyeongoza vikosi upande wa Rwanda akipewa cheo cha mkuu wa majeshi CDF. Kilichofuata hapo ni historia ilikua ni kuchota madini tu na kuuwa wahutu/interahamwe wote waliokua wakionekana kama threat kwa serikali ya Rwanda chini ya Kagame. Na pia ndipo kipindi hiki wakasimikwa waasi wa Kitutsi mashariki ya DRC wanaoisumbua serikali ya DRC mpaka leo hii.
Madini yalichotwa na wahutu waliuuwawa mpaka sense ilipomuingia Laurent Kabila ambapo katika kujaribu kutokomeza hali hii akamfukuza na kumvua vyeo vyote CDF wake wankinyarwanda Gen Kabarebe mwaka 1997.

Hali hii ilimchukiza Kagame na swahiba wake Museveni ndipo mikakati ikaanza ya kumng'oa madarakani Laurent Kabila iliyopelekea vita iliyokuja kupewa jina ya Congo War 2.
Ni historia ndefu ila kwa kifupi tu ni kwamba zilitafutwa mbinu nyingi za kivita na za kiinteligensia za kumuondoa Kabila Sr mpaka walipofanikiwa kwa msaada wa CIA ambapo mwaka 2001 Laurent Kabila akiwa ofiain kwake Ikulu Kinshasa alipigwa Risasi na Bodyguard wake karibu, na Bodyguard wake pia akapigwa risasi na mpambe wa Rais (ADC) Eddy Kapend, naye pia kabla ya kuwekwa nguvun katika ile taharuki akapigwa risasi na mlinz mwingine aliyetokomea kusikojulikana. Mpaka leo mauaji ya Rais Kabila Sr yanabaki kuwa ni mystery maana walioshuriki katika kufyatua risasi nao pia waliuawa kama cover up.

Baada ya kufanikiwa katika mauaji haya, Joseph Kabila ambaye ni mtoto wa kambo wa Kabila( si mtoto wake by birth) mwenye asili ya kitutsi akakabidhiwa madaraka ya DRC kama Rais. Joseph kabila ni mtusti, mzaliwa wa Rwanda na ni mpwa wa Gen Kabarebe. Alilelewa na Kabila Sr toka akiwa mdogo baada ya baba yake ambaye alikua member wa jeshi la waasi wa Kabila mashariki ya Kongo alipofariki katika umri mdogo, Laurent Kabila Sr akamchukua Joseph na kumlea kama mwanaye, ila Joseph Kabila si mtoto wa kuzaliwa na Laurent Kabila .

Toka mwaka 2001 baada ya Rais Joseph Kabila Jr kuchukua madaraka rasmi kama Rais, plunder na looting ya madini kutoka DRC na kusafirishwa kinyemela kwenye mataifa ya magharibi kupitia Rwanda Kigali inaendelea na itaendelea mpaka kesho as long as Kagame yuko madarakani.

Pichani chini ni Joseph Kabila akiwa na Uncle ake Gen James Kabarebe (ambae amehudumu kama CDF na minister of defence katika serikali ya Kagame kwa miaka mingi toka 2000 mpaka 2018).
Huyo mrefu katikati mwenye sare ya Jeshi ndo Gen Kabarebe na kulia kwake ni Joseph Kabila , hapo walikua Kigali 1998.

View attachment 1384017
Kabisa mkuu,kabarebe yuko chini ya uangalizi mpaka sasa. Vyeo vyote vya kijeshi hana
 
Nilipewa story na mtu aliyeenda Rwanda kipindi wanakumbuka hayo mauaji. Kwanza wameweka kumbukizi kama mauaji ya watutsi pekee kitu ambacho binafsi nakiona kama kinachochea mgawanyiko maana hata familia za kihutu zilipoteza pia wapendwa wao. Hii inawanyima haki

Kingine wanachukua muda mrefu zaidi ya wiki kama kumbukumbu zangu zipo sawa na familia hukusanyika kuomboleza na wanashea stories za yaliyotokea. Hii naona kama kuwarithisha kizazi kipya hili bifu maana nao wanakuwa wanafeel yale machungu kama walikuwepo

Rwanda nilivyoelezwa ipo katika tension na siku mkuu wetu akiondoka while hajaweka succession plan ya kueleweka bhasi outbreak ya genocide ingine inaweza kutokea
Hapo mwishoni unamaanisha mkuu wetu yupi akiondoka?
 
Ni hivi...Laurent Desiré Kabila Sr alikua ni loverboy au tuseme player kwani alikua na wake official 13 na watoto zaidi ya 25.. alikua na wanawake kila kona ya nchi hizi za africa mashariki na kati..Kama muasi wa serikali halali ya Mobutu aliishi maisha ya kujificha katika misitu ya Congo, muda mwingine alikua Uganda, ku kipind alikua Tanzania Lake Tanganyika na kwingineko hii yote ni kuukwepa mkono wa chuma wa dikteta Mobutu Sseseko..maisha yake yalikua ya ki guerrilla warfare akistage attacks toka msituni huku akiomba msaada toka nchi jiran za Tanzania, Uganda rwanda na Burundi. Kwa hiyo katika harakati hizi alikua akizaa hovyo na wanawake kila anapokwenda. Idadi halisi ya watoto wake haijulikani na idadi halisi ya wake zake haijulikani pia. Na hadi anakua Rais wa DRC 1998-2001 hakua na mke mmoja rasmi. Hakuwah kuwa na first lady wala hakuwajali kabisa watoto wake. Inasemekana Joseph Kabila ni mtoto wake aliyempata alipokuwa Tanzania wengine wanasema ni mtoto wa rafiki yake wa Kitutsi aliyezaliwa south Kivu Congo mashariki. Baba yake halisi Kabila, mzee Kanambe alikua rafiki wa Kabila na walikuwa pamoja kama waasi wa AFDL dhidi ya serikali ya Mobutu. Alipofariki vitani Kabila anamchukua Joseph Kabila ( Jina lake halisi Hipolite Kanambe) na kumlea kama mwanae. Asili ya Joseph kabila ni debatable ila kwa mwonekano wake wa uso na pua ana asili ya Kitutsi na hafanani kabisa na Laurent Kabila.
Tunachojua for fact ni kwamba Joseph Kabila Jr kakulia Tanzania, Kasoma Shule ya Msingi Msasani Dar es salaam, sekondari kasoma hapa hapa Tanzania, chuo kikuu kasoma Makerere Uganda na katika kutafuta maisha amewah kuwa dereva taxi Dar es salaam, baadae akaelekea Rwanda na Congo kuungana na majeshi ya baba yake ya AFDL pamoja na RPF akiwa kama commander of the 'kadogos'( child soldiers) mpaka alipokuja kurithi mikoba ya baba yake mwaka 2001 kama rais wa DRC akiwa na umri mdogo tu wa miaka 29.

Pichani chini ni Baba yake mzazi Joseph Kabila, Adrien Kanambe, wa mwisho Kulia akiwa na Laurent Kabila katikati wa tatu toka kulia, hapa walikua msituni Congo mashariki wakiongoza vikosi vya waasi dhidi ya serikali ya Mobutu Sseseko.
View attachment 1384412
View attachment 1384468View attachment 1384470View attachment 1384473
Laurent Kabila akiwa Tanzania makazi yake na familia yalikuwa pale Mzinga way, Oysterbay jirani kabisa na zilipo ofisi za United Nations Umoja House.
 
It’s a believable story kwa sababu kuna mambo mengi aliyoelezea unaona kama kuna vinasaba vya mtu alieishi huko kipindi icho na binafsi nimepata ideas za nini kilianza kutokea siku mwanzo kupitia kwake tatizo chumvi nyingi kwenye kuchangamsha genge.

Lakini huyu mtu anakipaji cha uandishi hapo ndipo alipotunasa wengi kutaka kuona nini kilimkuta mbele na alichomoka vipi.
Mkuu isijekuwa msimuliaji alinusa harufu ya "yajayo yanafurahisha" kama hizi comments za sasa zilivyo hivyo akaona njia ya kukwepa aibu ni kusababisha simu yake "kuharibika" na kuamua kutumia ya mamsap wake ili kumalizia stori kwa kulipualipua? Ila kama sehemu kubwa katulisha matango Mungu anamwona maana wengine tuliamini kwa 95%.
 
Kuna siku nilikuwa natoka Bujumbura naelekea Bukoba, nilipanda gari na wacongo man aisee ziliibuka story za kagame sijui vita vya congo, wale wacongo wanamchukia Kagame mpaka kupitiliza, leo ndio nimepata mwanga kamili kwann wacongoman hawampend Kagema
Kwa stori hii kumbe wanovuruga amani Congo ni Museven na Kagame.

Kenya, Tz, Congo na nchi zingine zinazozunguka maziwa makuu inabidi ziungane kuwaangamiza Kagame na Museven

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Iko hivi...Congo War 1 ilikua kati ya mwaka 1996-1997. Kuna makundi manne( Mobutu Sseseko, Laurent Kabila, Paul Kagame, Yoweri Musseveni) yaliyopigana vita hii na kila kundi lilikua na interest zake tofauti.
Vita hii ilitokea DRC kipindi hicho ikiitwa Zaire ilianzia pronvince za kaskazini mashariki Nord na Soud Kivu, ikaelekea Kisangani mpaka DRC magharibi then Kinshasha ilipoisha na kuondolewa madarakani kwa Rais wa kipind hicho Mobutu Seseko, nchi ikatwaliwa na Laurent Kabila aliyebadili jina la nchi kutoka Zaire na kuwa Democratic Republic of Congo.

Kwa kifupi ni kwamba wakati vita hii inaanza Mobutu ndiye alikuwa rais halali wa DRC na Laurent Kabila Sr ndiye alikuwa muasi akipigana kutoka msituni mashariki ya Kongo. Kabila alipata msaada wa kijeshi kutoka kwa majeshi ya Rwanda na Uganda chini ya Kagame na Mseveni. Lengo la Kagame si kwamba alikua sympathizer wa movement au uasi wa Kabila bali lengo lake lilikua ni kuwamalizia mbali wahutu na interahamwe wote waliokimbilia Congo baada ya genocide ya 1994 na pia aliona fursa kwenye madini adhimu ya Congo.

Museveni ye hakua interested na wahutu bali ye pia aliona fursa kwenye madini. Sasa basi majeshi ya Rwanda chini ya Gen James Kabaerebe, uganda pamoja na vikosi vidogo vya waasi wa congo wakiongozwa na Laurent Kabila walivamia Congo mwaka 1996 na kuanza kuuwa interahamwe , kushambulia majeshi halali ya Congo ya Mobutu, wakasonga mbele Toka Goma, kwenda Kisangani, kindu, kinanga mpaka walipofanikiwa kuuzingira mji mkuu wa DRC Kinshasha na kumuondoa madarakani Mobutu Seseko, na kufanikiwa kumuweka kibaraka wao Laurent Kabila kama rais mpya wa DRC. Kabila aliwatunuku vyeo jeshi maafisa waandamizi wa majeshi ya Rwanda ilhali hawakua raia wa Congo.

Ambapo Gen wa kitutsi James Kabarebe aliyeongoza vikosi upande wa Rwanda akipewa cheo cha mkuu wa majeshi CDF. Kilichofuata hapo ni historia ilikua ni kuchota madini tu na kuuwa wahutu/interahamwe wote waliokua wakionekana kama threat kwa serikali ya Rwanda chini ya Kagame. Na pia ndipo kipindi hiki wakasimikwa waasi wa Kitutsi mashariki ya DRC wanaoisumbua serikali ya DRC mpaka leo hii.
Madini yalichotwa na wahutu waliuuwawa mpaka sense ilipomuingia Laurent Kabila ambapo katika kujaribu kutokomeza hali hii akamfukuza na kumvua vyeo vyote CDF wake wankinyarwanda Gen Kabarebe mwaka 1997.

Hali hii ilimchukiza Kagame na swahiba wake Museveni ndipo mikakati ikaanza ya kumng'oa madarakani Laurent Kabila iliyopelekea vita iliyokuja kupewa jina ya Congo War 2.
Ni historia ndefu ila kwa kifupi tu ni kwamba zilitafutwa mbinu nyingi za kivita na za kiinteligensia za kumuondoa Kabila Sr mpaka walipofanikiwa kwa msaada wa CIA ambapo mwaka 2001 Laurent Kabila akiwa ofiain kwake Ikulu Kinshasa alipigwa Risasi na Bodyguard wake karibu, na Bodyguard wake pia akapigwa risasi na mpambe wa Rais (ADC) Eddy Kapend, naye pia kabla ya kuwekwa nguvun katika ile taharuki akapigwa risasi na mlinz mwingine aliyetokomea kusikojulikana. Mpaka leo mauaji ya Rais Kabila Sr yanabaki kuwa ni mystery maana walioshuriki katika kufyatua risasi nao pia waliuawa kama cover up.

Baada ya kufanikiwa katika mauaji haya, Joseph Kabila ambaye ni mtoto wa kambo wa Kabila( si mtoto wake by birth) mwenye asili ya kitutsi akakabidhiwa madaraka ya DRC kama Rais. Joseph kabila ni mtusti, mzaliwa wa Rwanda na ni mpwa wa Gen Kabarebe. Alilelewa na Kabila Sr toka akiwa mdogo baada ya baba yake ambaye alikua member wa jeshi la waasi wa Kabila mashariki ya Kongo alipofariki katika umri mdogo, Laurent Kabila Sr akamchukua Joseph na kumlea kama mwanaye, ila Joseph Kabila si mtoto wa kuzaliwa na Laurent Kabila .

Toka mwaka 2001 baada ya Rais Joseph Kabila Jr kuchukua madaraka rasmi kama Rais, plunder na looting ya madini kutoka DRC na kusafirishwa kinyemela kwenye mataifa ya magharibi kupitia Rwanda Kigali inaendelea na itaendelea mpaka kesho as long as Kagame yuko madarakani.

Pichani chini ni Joseph Kabila akiwa na Uncle ake Gen James Kabarebe (ambae amehudumu kama CDF na minister of defence katika serikali ya Kagame kwa miaka mingi toka 2000 mpaka 2018).
Huyo mrefu katikati mwenye sare ya Jeshi ndo Gen Kabarebe na kulia kwake ni Joseph Kabila , hapo walikua Kigali 1998.

View attachment 1384017
Hata mazingira ya Joseph Kabila kupewa urais mara tu baada ya kifo cha "baba yake" yalikuwa na utata sana kwa wengi ambao hatukuujua ukweli uliojificha.
 
Hujafuatilia simulizi vizuri kumbe

Amesema wakati wanarudi Mpaka wa Tanzania na Rwanda ulikuwa umefungwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Sikumbuki Kama alisema hivyo katika simulizi yake Ila ninachojua mimi ambacho ni FACT ni kwamba maelfu na maelfu ya wakimbizi wahutu kwa watutsi walivuka border ya Rusumo toka rwanda na kupokelewa Tanzania kati ya Apr mpaka July 1994, ambapo zilianzishwa kambi za wakimbizi chini ya Uangalizi wa UNHCR, kulikua na kambi za wakimbizi Benako, Kyerwa Karagwe, Ngara pamoja na Rulenge.

Pia ikumbukwe kwamba hakuna border ya nchi kavu kati ya Rwanda na Tanzania zaid ya Daraja la Rusumo, kwingine kote tanzania na rwanda inatenganishwa na maji ya mto kagera. Border ni moja tu pale Rusumo darajani.

Sipingani na simulizi ya mtoa mada. Ni kweli anayosema yalitokea. Na anatoa anaglizo ili tuwe makini yasije yakajirudia tena either rwanda au nchi yoyote ile ya jirani. Siko hapa kupingana nae ila kusupport alichosimulia ila pale nilipoona kuna utofauti ndipo nilipohighlight. Tofauti ni ndogo sana ambazo pia anaweza zitolea maelezo zikaeleweka otherwise kila kitu kiko sawa. Historia na vizazi vijavyo vitatuhukumu tusipoweka haya mambo sawa.
 
Bonge la story aisee.. mkuu hongera sana
Inaendelea...........

EeeeMRND ......eeeeee...MRND..eeeee..MRND ....eeeeee...MRnd.. ishaka rya banyarwanda , eeeee...eeee
Eeee MRN ishaka ryubumng'e na mahoro na majambele ya rubanda tweshe turagushigikie ...eeeeMRNd ikomera.×2

Huo hapo ni wimbo wa kinyarwanda wa chama tawala Cha MRND nikaona kabla hatujamalizana na rwanda wote muujue huu wimbo ,Kama nilivyosema mwanzoni kipindi hicho ulikuwa unapigwa redioni masaa 24 kwa siku hakuna kupumzika .nachotaka kusema hapa ni kwamba wimbo huo ulipigwa maksudi ili kuwakaririsha watu waamini kuwa hakuna chama kingine Cha kuwaletea maendeleo zaidi ya chama cha MRND na hakuna mbadala ,huu wimbo ulipigwa redioni Hadi wazungu wakawa wanaujua achilia mbali watoto ukabadilika ukawa Kama wimbo wa taifa yani unaweza kukamatwa na interahamwe ukalazimishwa uimbe huo wimbo Kama ukishimdwa unakula vibao vya kufaa mtu ikalazimika Sasa lazima kila mtu aukariri uujue angalau beti hiyo moja huwa si usahau Hadi Leo (matumiz mabaya ya redio yakawa yameniathiri ) haijalishi we ni mwenyeji au mgeni.imbaaa

Haya Sasa tumalize na Rwanda.......

Tukawa tumelala pale boda usiku asubuhi tukawa tunasogea kwenye kidirisha Ila uongo mbaya sikumbuki sawasawa Kama siku ile nililala usingizi au vipi huwa sina kumbukumbu sawasawa nilistukia tu kumekucha watu Wana nawa nyuso nami nikaenda kunawa uso tukawa foleni kugonga passports zetu kuwahi kupanda maroli upande wa pili ,taratibu zikakamilika

Saa mbili kamili nikawa tumeiacha ardhi ya Rwanda rasmi tunaingia ardhi ya Burundi nikasema ASANTE MUNGU ,safari ikaanza kwenda bujumbura safari ikaanza huku tukiwa na baadhi ya warundi tukawa tunapiga stori kuhusu zile maiti za mtoni usiku Ila wao wakawa wanasema zile maiti zimetoka mbali Sanaa vijiji vya mbali Burundi bado Hali sio mbaya Sanaa japo kulikuwa na tension kubwa rais wao nae alikuwa kwenye ndege iliyomuua rais wa Rwanda Habyarimana. nikajiapiza kuwa kamwe haitotokea Mimi nikanyage ardhi ya Rwanda Tena hadi nakufa hata Kama Vita itaisha nikaambiwa nirudi kazini tena ,hata ningeteuliwa kuwa balozi kamili na ndo ingekuwa mwisho wa hiyo kazi siko hiyo .( Ila miaka ya 2000' ) nilitembelea Kigali tena zaidi ya Mara mbili kibiashara lakini mwenyewe.)

tukaingia Burundi MAROLI yakaenda kupaki eneo la Gitega Kama sijakosea Ila ise nako kulikuwa na kituko ambacho kiliniacha hoi yani niliona magari kadhaa yanapishana mjini yakiwa na matundu ya risasi na polisi hawana time nayo magari ya raia tu nikawa nawaza hapaNapo sipo.tukalala asubuhi safari ikaanza rasmi kuelekea boda ya Tanzania tukavuka boda nikawa ndani ya motherland nikavuta pumzi ndefuu nikasema uuuuaaahhhhhh Asante mungu.
Kuna kitu sitaki kumaliza bila kukisema baada ya kumaliza kuvuka boada ya tanzania Kuna kamwendo kakutoka boda Hadi kuna sehemu madereva huwa wanakula na Kama kupumzika kunaitwa kwa MAMA SHILINGI Sina uhakika Kama bado kupo Kuna mgahawa hivi Sasa pale watu tukawa tunashuka ili kula nikakosa sahani ya kulia ya kuwekea ubwabwa ikabidi yule mama muuzaji anipe kikombe cha chai ili nitumie Kama Sahank na kweli nikachotewa ubwabwa nikawekewa nikawa na kula huwa nikikumbuka nachekaa sanaAaaaa...ubwabwa kwenye kikombe duuuhhh.

Nafikiri Sasa nikawa ndani ya Tanzania ..rasmi ya Rwanda yakawa yameishia hapo.

Sasa kwakuwa niliahidi kuwaletea stori yangu hadi kufika Tanzania,kuacha kazi,kujiingiza katika biashara ya chuma chakavu huko Zambia ,kufungwa jera Ndola n.k Basi niwaombe Kwanza nitengeneze simu yangu kwanza ikiwa imepona Basi ntaiendeleza Kama sehemu ya pili ya maisha yangu kujifunza tu.

Mwisho naomba niwashukuru wote kwa kunifuatilia,kunikumbisha,hata wale mliinidhihaki lakini mkawa mnanifuatilia Kiaina,Asante Sanaa..

Stori hii naamini itakuwa imewavutia wengi sio mbaya kuipeleka kokote Kama sehemu ya kujifunza lakini usisahau kutoa credit kwa Bossless mwenyewe ambae ndo mmiliki wake halali.

Asante kwa viewers na comments za kutosha. USIKU MWEMA.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata mazingira ya Joseph Kabila kupewa urais mara tu baada ya kifo cha "baba yake" yalikuwa na utata sana kwa wengi ambao hatukuujua ukweli uliojificha.
Alishaandaliwa muda kuchukua madaraka toka Kigali, na wakati Baba yake anauawa hakuwepo DRC. 10 days baada ya baba yake kufariki alitua Kinshasa na ndege toka Kigali Rwanda na kukabidhiwa nchi. Rwanda ina mikono mrefu sana katika siasa za Congo
 
Back
Top Bottom