Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Mkuu bossless tafadhali tupe kwa ufupi.Vyumba vya siri ubalozini vinahusiana na nn.Usijari toa japo mistar miwili tuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Nafurahi tu hapa maana kama jamaa alifanya kazi ubalozini na miaka ndio kama hiyo aliyoitaja kuna uwezekano mkubwa jamaa wakamfahamu

Sasa hiyo kusema tu kua ubalozini kuna vyumba vya siri hata kama hajasema ni siri gani naona kama ameshatoa siri, wanaweza wakamtafuta labda
 
Mtoa post haya masimulizi mazuri sana japo yanafuatiliwa na wenda wazimu wengi, ndo maana comments nyingi ni za kukatishana tamaa (hayo ni matokeo ya mnyukano wa maisha huku mtaani).

Jambo zuri nimeliona ni pale unapotahadharisha uwepo wa vikundi vya usalama visivyo tambulika kisheria, kujipa mamlaka ya kiusalama kuliko hata polisi. Na umetoa mifano kwa Tanzania bila kupepesa, rejea kile kinachoendelea huko Kilimanjaro kwenye mikutano ya Mbowe anapovamiwa na vijana wasio polisi, mauaji ya baadhi ya watanzania ambao hatima ya matukio hayo haijulikani na haifanyiwi kazi yoyote.

Pengine kwa uliyoyashuhudia huko Rwanda, unaanza kuona dalili zake hapa kwetu... Tunayo mengi ya kujifunza kutokana na story hii. Endelea kutupa uhondo, hatubanduki hadi tukutane kwenye biashara yako ya chuma chakavu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Story ingeandikwa kwa pamoja ingekuwa ndefu mno. Bora alete episode hata mbili kwa siku ila avumilie baadhi ya vichwa vimepinda.
Na watu wangelalamika, ungesikia aliyesoma mpaka mwisho anisumulie....
 
Inaendeleaaa...........

Nilipoishia nikiwa IMhala hoteli najiandaa sasa namna ya kuwahi kuamka mapema kuwahi kituoni kwangu kuripoti asubuhi. Mapema tu nikaamua nikajianda safi kabisa nikaanza safari ya kuelekea kituoni kwangu, nikashudia kitu cha ajabu ambacho sikukizoea .Dar ukiamka saa kumi na moja alfajiri kwa miaka hiyo hata kwa sasa ukifika stand utakaa tu kidogo hadi saa kumi na mbili au nani nusu hivi unaweza kuwa umepata usafiri na kuondoka iwe kwa texi au daladala wanyarwanda swala la kuamka mapema hilo kwao hapana labda sijui kama wamebadilika kipindi hiki, basii mtu mzima nikawa stand barabarani nasubiri daladala huwezi amini hadi saa moja moja kamili asubuhi hakuna cha daladala wala nini nikamuuliza jirani yangu pale stand hii ukoje akaniambia mabasi yanaanza kufika saa mbili kamili au na nusu nikamuomba anionyeshe texi nipande akaniambia hakuna stand ya texi Unachotakiwa kufanya unasimama barabarani unapungua gari lolote dogo mkono itakayosimama basi hiyo ndo taxi mnaelewana bei anakupeleka, mimi nikafanya hivyo kweli nikawa nimepata usafiri tukaelewana (sikukumbuki tulikabiliana bei gani ila alipeleka hadi ubalozini getini) nilishuka nikajitambulisha kwa mlinzi akiniruhusu kuingia ndani nikaingia hadi mapokezi nikatoa barua yangu ya ajira nikapokelewa safii kabisa na watumishi wenzangu sasa hapo nikawa majihisi nipo nyumba tunaongea lugha moja tunaelewana safii mzee nikapumzishwa sebule ndogo kumsubiri balozi afike nijitambulishe ili sasa taratibu zingine zifuatwe.

Muda si mrefu balozi akafika alikuwa mwanamama mweupe kama mpemba mama mtu mzima( naomba nisilitaje jina lake) akanikaribisha tukaongea maeneo ya hapa na pale ikawa baadae akaaga nikabaki na wasaidizi wake sasa ndo nikawa nimeingia mzigoni rasmi nikiwa na mabegi yangu yote( ikumbukwe kule hotelini niliaga kuwa sirudi hivyo niliondoka na kila siku changu hadi ubalozi).

Iko hivi ubalozi wowote lazima uwe na baadhi ya vyumba vya siri na wazi hivyo vya siri( naomba nisivizungumzie na kazi yake ni nini kwa kuwa sio lengo) basi katika vile vyumba viwili nikakabidhiwa chumba kimoja kwa ajili ya kupumzika mimi na mizigo yangu nikawa naishi pale ubalozini kwa muda kama week mbili hivi nalala naamka nafanya shughuli ndogondogo za ofisi mda wa kazi ukiisha watumishi wenzangu wananitembezA mjini ,taratibu nikaanza kuzoea mjii mawazo ya kupanga uswahili yakaanza kuingia akilini mwangu ,baada ya muda nikaomba kuhamia mtaani nikakubaliwa bila shaka ( hili niliweka sawa kwanza madhumuni ya vyumba vy pale ubalozini sio kufanya kuwa makazi ya kudumu unakaa kwa muda unajipanga kidogo then unaanza kuishi mtaani) .

Basi mzee mzima nikapa nyumba yangu pale Gikondo karibu na bandari kavu huwa wanakuita MAGERWAA kama sijakosea speeling basi nikawa nimepata nyumba nakuanza maisha nikiwa single kabisa sina hata mtoto wa kusingiziwa nje maisha ya kaanza hapo ( RWANDA hadi sasa hakunaga mambo ya kupanga chumba kimoja kule ukipanga unatakiwa upange nyumba nzima ) maisha yakawa yanaendelea ni kazini nyumbani taratibu vijana wakaanza kunizoea majirani wote wakaanza kunizoea pia sasa sikujua walikuwa wanavutiwa na nini kwangu ila baadae niligundua kuwa walikuwa wananipenda kwasababu naongea kiswahili hivyo nikiwa naongea wanafurahi japo sikuwa na uhakika kama wananielewa au vipi? Akafikia hata wakifanya sherehe zao majirani lazima wamletee barua ya mwaliko mimi nikihudhuria wanafurahi sanaa walikuwa wananiita mswahili. Neno la kwanza kujifunza la kinyarwanda ilikuwa salama AMAKURU yani habari yako.

Maisha yakaendelea pale kazini, ikawa ni mwendo wa kazi kwenda mbele hadi kufikia mwaka 1990 hapo yani nikawa na miezi sita na siku kadhaa kigali miezi yote hiyo nilikuwa sijatoka nje ya mji wa kibali.

Niseme mwaka huo ndo nilianza kupata ufahamu juu ya maisha halisi ya Wanyarwanda mtaani kwangu ikawa nikialikwa kwenye sherehe nakuta watu wale wale (naomba nieleweke hapo kwa mfano unaishi mtaa moja kuna kaya nyingi tu lakini ule mtaa ukawa kama kuna mgawanyiko flani hivi yani ukiitwaa kwa mzee john unamkuta mzee Amosi yupo hivyo kwa mzee Amosi unakuta mzee john yupo halafu mtaani kuna watu wengine hawashirikishwi kabisa japo wapo mtaani hapo.) hii ikawa unanitatiza ikabidi nianze kufanya utafiti wangu kwa siri ikiwemo kuwauliza watumishi wenzangu pale ubalozini.

Pale ubalozi kulikuwa na dereva ambao alikuwa anasaidia anahudumu pale ubalozini,siku moja nikamuuliza kuhusu hilo jambo alichonijibu ni kuwa hicho kinachotokea na ndo maisha halisi ya Wanyarwanda yani Watusi na Wahutu hawafungamani katika mambo mbalimbali akasema kuwa kuna hali ya ubaguzi wa hali ya juu hasa Wahutu kuwabagua Watusi ambao ni wachache sanaa na hilo ndo nilipokuwa nilishuhudia kwa takribani kipindi cha mwanzoni ila nikawa siajelewa mtusi yupo na mhutu yupo na unamtambuaje mtusi na mhutu unamtambua aje ukawa mtihani sasa kwangu.

Baada ya kulielewa hilo sawasawa ndo ikawa sababu ya mimi kukacha tena kwenda kwenye sherehe za majirani kwani nilihisi kinachotengezwa hapo si jambo jema ikafikia mahala jirani akiniiona nimesimama na jirani mwingine ana nuna au ananipita bila hata kutusalimia ikawa inanishangaza kwakweli CHUKI YA UKABILA NI MBAYAA SANAA.usiombe.

Maisha yakaendelea kama kawaida ila nikaona Nihamie mtaa mwingine kuwakomoa wale majirani, nikawa nimehama pale nikahamia mtaa mwingine nikajitahidi nisiwe na mazoea kama ya awali nikawa ni kazi ,nyumba ,matembezi mjini kurudi nyumbani na kulala.

Hatimae mwaka ukapita ukaingia mwaka wa pili ya ni 1992 hapo ndipo kuna kipindi rwanda kukawa na mambo ya ajabu sanaa yani mnaweza mkawa mmelala wanakuja watu wana silaha, mapanga na mashoka usiku wanawamsha wote mnawekwa kwenye foleni unasikia huyu ni ing'otanyi ukiambiwa hivyo ujue jamaa watakuchukua wanaondoka na wewe ndo kwa heri na ukujifanya kubisha pale pale unageuzwa asusa yani unakataa katwa mapanga watu wanakuona ,ila niligundua waliokuwa wanafanyiwa hivyo wengi wao waikuwaWatusi wakawa wanadai kuwa huwa wanatoroka kwenda kupata mafunzo ya kijeshi polini na wanarudi kimya kimya uraiani kuchora ramani ya uvamizi kuisaidia kikundi cha waasi wa RPF.kwa miaka hiyo uvamizi wa RPF maeneo ya mipakani ulikuwa wa mara kwa mara hadi kufikia jeshi la rwanda kuhamia mipakani kulinda ila mashambulizi hayakukomaa japo majeshi ya serikali yalikuwa tunajitahidi kuzima uasi

Sasa turudi kwa wale watu wanaokuja usiku na bunduki na magruneti na mapanga kusaka watu wanaowaita ing'otanyi ,badaae nikagundua kuwa wale jamaa wanaitwa interahamwe yani kwa kiswahili wavamizi wa pamoja hapa naomba niongelee jambo moja muhimu sanaa kwa faida ya wasomaji, dalili ya kwanza kabisa ya uvunjifu wa amani au vurugu za kikabila au vita ni pale utakapo ona vikundi vya kisiasa, au vya kidini vinakuwa na walinzi au vikundi vya ulinzi halafu wanamilishwa bunduki halafu mkuu wa jeshi la polisi au majeshi anakaa kimyaa hakemei wala kutoa katazo lolote ukiona hivyo Unachotakiwa kufanya uza mali zako zote hamia nchi unapoona wewe ni salama kwako mapema sanaa.

Kilichotokea interahamwe walikuwa kwa mfano kama green gard wa Ccm au red bregard wa chadema , mara ghafla wakawa wanaonekana mtaani wamevaa nguo za chama chao cha MRND wakiwa na silaha kabisa za kivita wanatembea mtaani wanaimba nyimbo za kujipamba chama chao na rais wao hii maanake nini ukiona hivi juu chama tawala hakina imani tena na jeshi hivyo wakaona bora silaha zinaoagizwa na serikali wapewe makada wa chama wajilinde wenyewe, makada wakawapa interahamwe, interahamwe wakawa wNaogopeka kuliko hata polisi au jeshi wakiingia dukani kwako wakichukua mkate au siagi haruhusiwi kuhoji, kuhoji tu umekula kwako utachakazwa kwa kipigo vibaya sanaa sasa ikawa ukiwa na kesi hata kama aliekuonea ni interahamwe ukipeleke kesi polisi hakuna kitakachoemdelea ,kama umemkariri nenda kwa bosi wake huwa anakuwa Kada wa chama mfano mabalozi unamuelezea pale kwa kutia huruma ndani ya dakika sufuri anaitisha gwaride kama huyo aliokuonea ni wa eneo hilo ukimtambua anamcharaza vibaya fimbo mbele za watu ata kama kakupora kitu lazima arudishe hapo hapo ikawa inankishangaza sanaa binafsi nikiwa eneo la nyehere-gikondo kuna moja alinipora saa nikaenda kwa kada akaitwa akanirudishia tena bila ubishi kama kauza au katupa analipa pesa atakayoitaja kada (balozi) haijalishi hicho alichokupola kina dhamana gani.


Leo nimejitahidi kuandika ndefu nitaendelea kesho nimechoka sanaa........itaendelea.

Sent using Jamii Forums mobile app
Inaendelea.........

Habari za mchana wandugu ,sasa tuendelee leo ntajikita kuelezea matukio mbalimbali ya unyanyasaji, uonevu, mauji, uporaji ulianza kujitokeza . nitajitahidi kuelezea niliyoyashuhudia kwa macho yangu ya yaliyotutokea sisi kama sisi maoneo ya kazi... (ubalozini). Haya matukio yamejaa kichwani kwangu kwa kipindi cha mda wa miaka mingi hadi huwa yananikoseha raha wakati mwingine naota kabisa hadi na weweseka vibaya ndugu zangu msiombe vita narudia tena usiombe vita ( utasikia kijana humu anasema bora kinuke aise tema mate chini).

Tukio la kwanza -: hii ilikuwa kipindi hicho hicho mwaka 1992 kama sijasahau mwezi wa nne hivi kama unavyojua mpaka hapo tayari nimeshakuwa na Demu mweupe mfupi kiasi ila alikuwa mzuri ( hapo naona vijana wa mambo yetu wanaanza kutabasamu hhhhaaaa ...) nikiwa nae kwenye mahusiano kama miezi minne hivi sasa kukawa kuna sehemu moja hivi town kulikuwa linapigwa disco kama lile lilokuwa linapigwa pale mikocheni (blue palm eneo dogo lakini weekend wanakaa watu nyomi hatari mziki unapigwa balaa,kwaa taarifa tu eneo lile lilikuwa haliguswi na Askali yeyote yule au interahamwe au kwenda pale kuanzisha vurugu unajua kwanini? Eneo lile ni la Kada wa eneo lile mtemi na msumbufu aliitwa Nyihibilazi (balozi) na disko la kwake sasa mnanza aje? Kwanza mlangoni ukiingia unakuta Askali wake wana AK 47 na magrouneti yapo nje nje.

Basi disko likapigwa kufika mida kama saa kumi hivi nikamwambia demu wangu tuondoke enzi hizo tunakula Mai hatari (pombe) kwa kwenda mbele mzee unakula primus hadi unazima watu wanakubeba kukurudisha nyumbani, basi mtu mzima nikashika chombo( demu) yangu kiuno nikawa nashuka nayo lami kutokea ukumbini kama kuna kilima unashika unaenda lami kuu ndo unasimamisha texi ya kurudi home ,ile namalizia tu kilima kile kwa mbele kidogo nikaona Toyota hilux inakuja wamejaa interahamwe tupu na mabunduki i yao .
Kufika tu mbele wakasimama wakawa wanarudi nyuma aise asikwambie mtu pombe inaleta ujasiri,nikamwambia demu wangu hakuna kuongea chochote hata akiuliza jina lako labda aulizwe kwa kiingereza au kiswahili ndo ajibu, siku hiyo alivaa tisheti yangu zile za watalii zimeandikwa HAKUNA MATATA zilikuwa sinatengenezwa kenya kama sijasahau, basi majama yakawa yamefika pale kwanza wakaanza kukoki mibhnduki yao ebwaanae nikasema sasa tumekwisha lakini niwaambie mwanaume kama una mapenzi na demu wako aise hata itokee hatari gani lazima unamtetea tu hata kama kuna hatari kiasi gani basi swala la kwanza wakatuuliza tulipitokea niliwajibu disko wakasikia refudhi yangu ya kiswahili wakasema nyinyi ni waswahili? Nikamjibu ndio wakauliza watz yani watanzania wanafupisha nane tz nikasema ndo kumbuka nilimwambia demu asiongie hata akipigwa kibao, moja anaiuliza na huyu mugole? (Mugole-ni mwanamke nikamjibu mke wangu) kumbuka hapo kinyarwanda nimeshaanza kukipata pata ila kuongea ikawa shida kidogo, sasa ikatokea ubishi miongoni mwao baadhi yao wakawa wanahisi yule si mtz ni mnyarwanda wengine wakawa wanananiamini mimi hapo sasa ndo kimbembe kilipoanza

Vuta ni kuvute kumlazimisha demu aongee demu anasem na mimi nawaambieni huyu hawaelewi nyinyi huyu ni mtz kwanza haelewi mnaongea nini wakaomba ID ninatoa passport jina moja wakaomba ID ya demu ikiwaambia ipo ubalozini kama vipi twende nikawaonyeshe wakagoma ,demu waNgu yupo kimyaa, sasa ipo hivi yule demu naweza mfananisha na kama msanii Menina ya ni mweupe ana sifa zote za kitusi ila pua lake tu ni pana kidogo kama unavyomuona Menina ,sasa wakawa wanashindwa wafanye nini kumchukua hawawezi wanahisi ni mtz sasa mimi wakati huo nachapa kiswahili hatari na vijimaneno vya hapa na pale ghafla ukaingia ujumbe kwenye redio call yao nikasikia maneno flani nikaona wanaitana wakapakiana kwenye gari na kuondoka pale pale nikawahi texi tukarudi nyumbani na sikumpeleka kwao nilienda kulala( ikawa furaha tosha kwetu kwa usiku huo naona vijana wanatabasamu hapa hhhaaaaa.....) hakika yule demu alinipenda sanaa kwa lile tukio akaja akawa anawahadithia ndugu zake pale mtaani tukawa vile mke na mume aise anakuja nyumbani anytime mungu amsaidie huko aliko kwani tulipoteana tu uenda simu zingekuwepo au mitandao tungetafutana ( jina kapuni) ntaalezea baadae tulivyopoteana vita.. vita ...vita ..baba mbaya sanaa sasa sijui yuko hai au alishakufa ? Maisha yakaendelea...

Tukio la pili-: nilishuhudia saa nane mchana eneo la birjogo( tamka bijogo) hiace nzima ya abiria watu wakashushwa wanapigwa fimbo wakachambuliwa wakatolewa INYEZI ( inyezi maanake mende yani Watusi) wakatandikwa virungu vya kufaa mtu sasa hapo niliona kada (balozi )hilo analisimamia mwenyewe, sasa utamtambuaje balozi katikati ya interahamwe? Yeye anakuwa amevaa belleti nyekundu na shati la chama aisee wale watu walipigwa walikatwakatwa na mapanga huku watusi wakipata mateso makali sanaa ,unajua kwanini ?nilikuja kugundua baadae sanaa kwanini Watusi wanateswa. Sasa ipo hivi wakati Rpf wanaanza chokochoko walikuwa wanapewa taarifa na Watusi wa ndani n baadhi ya ndugu zao wanaume walikuwa wanaenda kwa siri kupata mafunzo maeneo mbali mbali karibu na walipokuwa waasi sasa taarifa hizo zikawa zinawafikia mabalozi mbalimbali nao wanazisambaza kwa interahamwe sasa usiku unashangaa unavamiwa na hao jamaa wanakula kisago halafu wanaondoka na wewe ni ndo imetoka hakuna anaejali basi wakawakatakata mapanga wale Watusi pale shell kituoni cha mafuta hadi leo picha hii huwa hainitoki akilini kuua kwa mapanga zaidi ya watu 12 wanauawa machoni mwangu kweupe pakavu jua la saa saba mchana then nobody care .

Nimesema hapa leo naweka matukio....ya kinyama.

Itaendelea jioni hii......................... Msichoke.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari zenu wakubwa kwa wadogo.

Kwanza napenda kutoa pole na shughuli za kutwa kwa wale wahangaikaji wote kama mimi ambao kila siku lazima tutoke ili tuweze kujipatia riziki halali kila siku iendayo kwa mungu. Tuseme wote asante mungu.

Nisiwachoshe niende moja kwa moja kwenye mada,mdaa huu wakati naandika huu ushuhuda wangu binafsi ambayo nimeishuhudia kwa macho yangu mawili nchini rwanda wakati wa vita ya kikabila ,wenyewe hupenda kuiita mauji ya halaiki.

Stori inaanza wakati ndo nimemaliza masomo yangu ya uhasibu ngazi ya stashahada mwaka 1989 (sintotaja chuo hicho) nikajaribu kuomba kazi wizara ya mambo ya njee mungu si Athumani nikapata kazi ubalozi lakini nikapaangiwa kituo changu cha kazi kigali-Rwanda, kama sijasahau ubalozi Tanzania ulikuwa maeneo yanaitwa KICHUKIRO ,kwa sasa sijui kama bado upo palepale au vipi sina uhakika.

basi mwezi wa sita baada ya kukamilisha taratibu zote nikaanza safari ya kwenda Rwanda kituo changu cha kazi kipya,ajira mpya na mara ya kwanza kusafiri nje ya Tanzania... Safari ikaanza kwenda kuanza maisha mapya nchi ya watu ,mbali na ndugu jamaa na marafiki nikiwa sijui chochote kuhusu nchi hiyo..

Angalizo. naomba tuvulimiliane ni long stori kidogo na yanaweza jitokeza makosa ya kiundishi na kifasihi.... Ntaelezea mambo mengi sana ya kutisha ambayo niliyashuhudia kwa macho yangu mwenyewe ambayo hadi leo nimejitahidi kuyasahau lakini imeshindika kabisa.

Safari inaanza pale Mnazi moja nakumbuka enzi zile kulikuwa hakuna mambo ya Booking. unawahi alfajiri na mapema unatafuta basi lako unapanda tu unasubiri safari ianze.

Basi nikiwa na mabegi yangu na shilingi za kitanzania 60 elfu(nilipewa kwa ajili safari na kujikimu na passport ) tu ,naianza safari ya kwenda Kahama, safari ikaanza midaa ya kama saa moja kamili asubuhi (jina la basi lile nimelisahau ila nakumbuka lilikuwa rayland) kipindi hicho barabara ni vumbi tupu changarawe la vumbi hadi linaingia kupitia madirishani, baada ya safari ya uchovu mwingi hatimae saa nane usiku tunaingia singida stand. Mimi mgeni sijui niende uelekeo gani ikumbukwe miaka ile nyumba za wageni zilikuwa za kuhesabu basi ikabidi tushuke pale stand tukawa tunakula mikate na chai na wengine chai na kahawa.

Basi mimi nikarudi kulala kwenye gari,alfajiri na mapema gari likaanza safari tena nakumbuka tulifika stand kuu Kahama kana saa tatu usiku hivi. yani tulitumia kama siku mbili hivi Dar-kahama .leo hii dar - Kahama unatumia siku moja umefika halafu utasikia mtu anasema nchini hii bwana hakuna maendeleo kabisa daa!!!

Tumefika Kahama stand tumepokelewa na wapiga debe enzi hizo wao ndo walikuwa kama mawakala wa magari makubwa anakubebea mzigo hadi kwenye gari unalipa nauli yeye anachukua chake mnaachana hapo hapo hapo ni usiku inabidi kupata gari ya kwenda boda ya Rwanda na Tanzania Rusumo hapo unavuka Mpaka, kuna mto mkubwa unaitwa mto Rusumo unapita kwenye daraja la chuma kama lile lile liloejengwa na wanajeshi pale njia panda Kawe unavuka ng'ambo ukagonga passport ,cha kuchekesha pale kulikuwa hakuna magari ya abiria makubwa.

Magari ya abiria kutoka boda hadi kigali mjini yalikuwa hakuna, ilikuwa inakubidi upande roli la mizigo au abiria mjichange kwa makundi mkodi magari madogo kama tax ila mnabananishwa humo hatari na mizigo juu, kutoka boda hadi kigali ilikuwa kama mwendo wa masaa nane hivi kuingia kigali mjini.
Hatimae baada ya kubadilisha fedha zetu kuwa mafaranga tukapata usafiri wa kutufikisha kigali nakumbuka kundi langu kwenye gari tulilokodi nilipanda na wazaire watupu hivyo kelele zilikuwa nyingi hadi tunaingia kigali wanaimba nakuongea sanaa ubishi mwingi mara mpira mara siasa ili mradi makelele tu.

Saa tisa mchana nikawa tumewasili kigali town enzi hizo sijui lolote kuhusu mji huo zaidi ya address na namba za simu ikabidi niangaze angalau kupata simu lakini wapi,aise kinyarwanda sijui na wao kiswahili kigumu kila nae mujliza ila kupata mawasiliano sikupata msaada ikabidi nikasogolea kwenye stand ya mabus madogo nikamuulize konda kuwa nataka kwenda ubalozi wa Tanzania akaishia kucheka tu niligundua hakunielewa lugha .

Nakumbuka nilikaa stand pale hadi saa kumi na mbili bila bila ikabidi niulizie sehemu pakulala hapo nikaeleweka nikaambiwa lazima upande bus nipelekwe sehemu inaitwa NYAMIRAMBO na nikaambiwa pia kuwa kuna waswahili wengi nikapanda bus hadi nyamirambo nikashushwa tu stand konda akanionyesha kuna hoteli moja ilikuwa imeandikwa nakumbuka inaitwa kama sijasahau ilikuwa inaitwa IMHALA ila nyamirambo ilichanganya kigodo naweza fananisha Magomeni enzi zile.


Nikaenda nikalipia chumba nikaomba kuelekezwa eneo la kula nikaelekezwa, nikaenda nikala halafu nikarudi kujilaza nikipanga namna ya kuingia kesho u abalozi wa Tanzania kuanza majukumu mapya .

Itaendelea...........





Sent using Jamii Forums mobile app
Inaendelea.........

Habari za mchana wandugu ,sasa tuendelee leo ntajikita kuelezea matukio mbalimbali ya unyanyasaji, uonevu, mauji, uporaji ulianza kujitokeza . nitajitahidi kuelezea niliyoyashuhudia kwa macho yangu ya yaliyotutokea sisi kama sisi maoneo ya kazi... (ubalozini). Haya matukio yamejaa kichwani kwangu kwa kipindi cha mda wa miaka mingi hadi huwa yananikoseha raha wakati mwingine naota kabisa hadi na weweseka vibaya ndugu zangu msiombe vita narudia tena usiombe vita ( utasikia kijana humu anasema bora kinuke aise tema mate chini).

Tukio la kwanza -: hii ilikuwa kipindi hicho hicho mwaka 1992 kama sijasahau mwezi wa nne hivi kama unavyojua mpaka hapo tayari nimeshakuwa na Demu mweupe mfupi kiasi ila alikuwa mzuri ( hapo naona vijana wa mambo yetu wanaanza kutabasamu hhhhaaaa ...) nikiwa nae kwenye mahusiano kama miezi minne hivi sasa kukawa kuna sehemu moja hivi town kulikuwa linapigwa disco kama lile lilokuwa linapigwa pale mikocheni (blue palm eneo dogo lakini weekend wanakaa watu nyomi hatari mziki unapigwa balaa,kwaa taarifa tu eneo lile lilikuwa haliguswi na Askali yeyote yule au interahamwe au kwenda pale kuanzisha vurugu unajua kwanini? Eneo lile ni la Kada wa eneo lile mtemi na msumbufu aliitwa Nyihibilazi (balozi) na disko la kwake sasa mnanza aje? Kwanza mlangoni ukiingia unakuta Askali wake wana AK 47 na magrouneti yapo nje nje.

Basi disko likapigwa kufika mida kama saa kumi hivi nikamwambia demu wangu tuondoke enzi hizo tunakula Mai hatari (pombe) kwa kwenda mbele mzee unakula primus hadi unazima watu wanakubeba kukurudisha nyumbani, basi mtu mzima nikashika chombo( demu) yangu kiuno nikawa nashuka nayo lami kutokea ukumbini kama kuna kilima unashika unaenda lami kuu ndo unasimamisha texi ya kurudi home ,ile namalizia tu kilima kile kwa mbele kidogo nikaona Toyota hilux inakuja wamejaa interahamwe tupu na mabunduki i yao .
Kufika tu mbele wakasimama wakawa wanarudi nyuma aise asikwambie mtu pombe inaleta ujasiri,nikamwambia demu wangu hakuna kuongea chochote hata akiuliza jina lako labda aulizwe kwa kiingereza au kiswahili ndo ajibu, siku hiyo alivaa tisheti yangu zile za watalii zimeandikwa HAKUNA MATATA zilikuwa sinatengenezwa kenya kama sijasahau, basi majama yakawa yamefika pale kwanza wakaanza kukoki mibhnduki yao ebwaanae nikasema sasa tumekwisha lakini niwaambie mwanaume kama una mapenzi na demu wako aise hata itokee hatari gani lazima unamtetea tu hata kama kuna hatari kiasi gani basi swala la kwanza wakatuuliza tulipitokea niliwajibu disko wakasikia refudhi yangu ya kiswahili wakasema nyinyi ni waswahili? Nikamjibu ndio wakauliza watz yani watanzania wanafupisha nane tz nikasema ndo kumbuka nilimwambia demu asiongie hata akipigwa kibao, moja anaiuliza na huyu mugole? (Mugole-ni mwanamke nikamjibu mke wangu) kumbuka hapo kinyarwanda nimeshaanza kukipata pata ila kuongea ikawa shida kidogo, sasa ikatokea ubishi miongoni mwao baadhi yao wakawa wanahisi yule si mtz ni mnyarwanda wengine wakawa wanananiamini mimi hapo sasa ndo kimbembe kilipoanza

Vuta ni kuvute kumlazimisha demu aongee demu anasem na mimi nawaambieni huyu hawaelewi nyinyi huyu ni mtz kwanza haelewi mnaongea nini wakaomba ID ninatoa passport jina moja wakaomba ID ya demu ikiwaambia ipo ubalozini kama vipi twende nikawaonyeshe wakagoma ,demu waNgu yupo kimyaa, sasa ipo hivi yule demu naweza mfananisha na kama msanii Menina ya ni mweupe ana sifa zote za kitusi ila pua lake tu ni pana kidogo kama unavyomuona Menina ,sasa wakawa wanashindwa wafanye nini kumchukua hawawezi wanahisi ni mtz sasa mimi wakati huo nachapa kiswahili hatari na vijimaneno vya hapa na pale ghafla ukaingia ujumbe kwenye redio call yao nikasikia maneno flani nikaona wanaitana wakapakiana kwenye gari na kuondoka pale pale nikawahi texi tukarudi nyumbani na sikumpeleka kwao nilienda kulala( ikawa furaha tosha kwetu kwa usiku huo naona vijana wanatabasamu hapa hhhaaaaa.....) hakika yule demu alinipenda sanaa kwa lile tukio akaja akawa anawahadithia ndugu zake pale mtaani tukawa vile mke na mume aise anakuja nyumbani anytime mungu amsaidie huko aliko kwani tulipoteana tu uenda simu zingekuwepo au mitandao tungetafutana ( jina kapuni) ntaalezea baadae tulivyopoteana vita.. vita ...vita ..baba mbaya sanaa sasa sijui yuko hai au alishakufa ? Maisha yakaendelea...

Tukio la pili-: nilishuhudia saa nane mchana eneo la birjogo( tamka bijogo) hiace nzima ya abiria watu wakashushwa wanapigwa fimbo wakachambuliwa wakatolewa INYEZI ( inyezi maanake mende yani Watusi) wakatandikwa virungu vya kufaa mtu sasa hapo niliona kada (balozi )hilo analisimamia mwenyewe, sasa utamtambuaje balozi katikati ya interahamwe? Yeye anakuwa amevaa belleti nyekundu na shati la chama aisee wale watu walipigwa walikatwakatwa na mapanga huku watusi wakipata mateso makali sanaa ,unajua kwanini ?nilikuja kugundua baadae sanaa kwanini Watusi wanateswa. Sasa ipo hivi wakati Rpf wanaanza chokochoko walikuwa wanapewa taarifa na Watusi wa ndani n baadhi ya ndugu zao wanaume walikuwa wanaenda kwa siri kupata mafunzo maeneo mbali mbali karibu na walipokuwa waasi sasa taarifa hizo zikawa zinawafikia mabalozi mbalimbali nao wanazisambaza kwa interahamwe sasa usiku unashangaa unavamiwa na hao jamaa wanakula kisago halafu wanaondoka na wewe ni ndo imetoka hakuna anaejali basi wakawakatakata mapanga wale Watusi pale shell kituoni cha mafuta hadi leo picha hii huwa hainitoki akilini kuua kwa mapanga zaidi ya watu 12 wanauawa machoni mwangu kweupe pakavu jua la saa saba mchana then nobody care .

Nimesema hapa leo naweka matukio....ya kinyama.

Itaendelea jioni hii......................... Msichoke.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaendelea.........

Habari za mchana wandugu ,sasa tuendelee leo ntajikita kuelezea matukio mbalimbali ya unyanyasaji, uonevu, mauji, uporaji ulianza kujitokeza . nitajitahidi kuelezea niliyoyashuhudia kwa macho yangu ya yaliyotutokea sisi kama sisi maoneo ya kazi... (ubalozini). Haya matukio yamejaa kichwani kwangu kwa kipindi cha mda wa miaka mingi hadi huwa yananikoseha raha wakati mwingine naota kabisa hadi na weweseka vibaya ndugu zangu msiombe vita narudia tena usiombe vita ( utasikia kijana humu anasema bora kinuke aise tema mate chini).

Tukio la kwanza -: hii ilikuwa kipindi hicho hicho mwaka 1992 kama sijasahau mwezi wa nne hivi kama unavyojua mpaka hapo tayari nimeshakuwa na Demu mweupe mfupi kiasi ila alikuwa mzuri ( hapo naona vijana wa mambo yetu wanaanza kutabasamu hhhhaaaa ...) nikiwa nae kwenye mahusiano kama miezi minne hivi sasa kukawa kuna sehemu moja hivi town kulikuwa linapigwa disco kama lile lilokuwa linapigwa pale mikocheni (blue palm eneo dogo lakini weekend wanakaa watu nyomi hatari mziki unapigwa balaa,kwaa taarifa tu eneo lile lilikuwa haliguswi na Askali yeyote yule au interahamwe au kwenda pale kuanzisha vurugu unajua kwanini? Eneo lile ni la Kada wa eneo lile mtemi na msumbufu aliitwa Nyihibilazi (balozi) na disko la kwake sasa mnanza aje? Kwanza mlangoni ukiingia unakuta Askali wake wana AK 47 na magrouneti yapo nje nje.

Basi disko likapigwa kufika mida kama saa kumi hivi nikamwambia demu wangu tuondoke enzi hizo tunakula Mai hatari (pombe) kwa kwenda mbele mzee unakula primus hadi unazima watu wanakubeba kukurudisha nyumbani, basi mtu mzima nikashika chombo( demu) yangu kiuno nikawa nashuka nayo lami kutokea ukumbini kama kuna kilima unashika unaenda lami kuu ndo unasimamisha texi ya kurudi home ,ile namalizia tu kilima kile kwa mbele kidogo nikaona Toyota hilux inakuja wamejaa interahamwe tupu na mabunduki i yao .
Kufika tu mbele wakasimama wakawa wanarudi nyuma aise asikwambie mtu pombe inaleta ujasiri,nikamwambia demu wangu hakuna kuongea chochote hata akiuliza jina lako labda aulizwe kwa kiingereza au kiswahili ndo ajibu, siku hiyo alivaa tisheti yangu zile za watalii zimeandikwa HAKUNA MATATA zilikuwa sinatengenezwa kenya kama sijasahau, basi majama yakawa yamefika pale kwanza wakaanza kukoki mibhnduki yao ebwaanae nikasema sasa tumekwisha lakini niwaambie mwanaume kama una mapenzi na demu wako aise hata itokee hatari gani lazima unamtetea tu hata kama kuna hatari kiasi gani basi swala la kwanza wakatuuliza tulipitokea niliwajibu disko wakasikia refudhi yangu ya kiswahili wakasema nyinyi ni waswahili? Nikamjibu ndio wakauliza watz yani watanzania wanafupisha nane tz nikasema ndo kumbuka nilimwambia demu asiongie hata akipigwa kibao, moja anaiuliza na huyu mugole? (Mugole-ni mwanamke nikamjibu mke wangu) kumbuka hapo kinyarwanda nimeshaanza kukipata pata ila kuongea ikawa shida kidogo, sasa ikatokea ubishi miongoni mwao baadhi yao wakawa wanahisi yule si mtz ni mnyarwanda wengine wakawa wanananiamini mimi hapo sasa ndo kimbembe kilipoanza

Vuta ni kuvute kumlazimisha demu aongee demu anasem na mimi nawaambieni huyu hawaelewi nyinyi huyu ni mtz kwanza haelewi mnaongea nini wakaomba ID ninatoa passport jina moja wakaomba ID ya demu ikiwaambia ipo ubalozini kama vipi twende nikawaonyeshe wakagoma ,demu waNgu yupo kimyaa, sasa ipo hivi yule demu naweza mfananisha na kama msanii Menina ya ni mweupe ana sifa zote za kitusi ila pua lake tu ni pana kidogo kama unavyomuona Menina ,sasa wakawa wanashindwa wafanye nini kumchukua hawawezi wanahisi ni mtz sasa mimi wakati huo nachapa kiswahili hatari na vijimaneno vya hapa na pale ghafla ukaingia ujumbe kwenye redio call yao nikasikia maneno flani nikaona wanaitana wakapakiana kwenye gari na kuondoka pale pale nikawahi texi tukarudi nyumbani na sikumpeleka kwao nilienda kulala( ikawa furaha tosha kwetu kwa usiku huo naona vijana wanatabasamu hapa hhhaaaaa.....) hakika yule demu alinipenda sanaa kwa lile tukio akaja akawa anawahadithia ndugu zake pale mtaani tukawa vile mke na mume aise anakuja nyumbani anytime mungu amsaidie huko aliko kwani tulipoteana tu uenda simu zingekuwepo au mitandao tungetafutana ( jina kapuni) ntaalezea baadae tulivyopoteana vita.. vita ...vita ..baba mbaya sanaa sasa sijui yuko hai au alishakufa ? Maisha yakaendelea...

Tukio la pili-: nilishuhudia saa nane mchana eneo la birjogo( tamka bijogo) hiace nzima ya abiria watu wakashushwa wanapigwa fimbo wakachambuliwa wakatolewa INYEZI ( inyezi maanake mende yani Watusi) wakatandikwa virungu vya kufaa mtu sasa hapo niliona kada (balozi )hilo analisimamia mwenyewe, sasa utamtambuaje balozi katikati ya interahamwe? Yeye anakuwa amevaa belleti nyekundu na shati la chama aisee wale watu walipigwa walikatwakatwa na mapanga huku watusi wakipata mateso makali sanaa ,unajua kwanini ?nilikuja kugundua baadae sanaa kwanini Watusi wanateswa. Sasa ipo hivi wakati Rpf wanaanza chokochoko walikuwa wanapewa taarifa na Watusi wa ndani n baadhi ya ndugu zao wanaume walikuwa wanaenda kwa siri kupata mafunzo maeneo mbali mbali karibu na walipokuwa waasi sasa taarifa hizo zikawa zinawafikia mabalozi mbalimbali nao wanazisambaza kwa interahamwe sasa usiku unashangaa unavamiwa na hao jamaa wanakula kisago halafu wanaondoka na wewe ni ndo imetoka hakuna anaejali basi wakawakatakata mapanga wale Watusi pale shell kituoni cha mafuta hadi leo picha hii huwa hainitoki akilini kuua kwa mapanga zaidi ya watu 12 wanauawa machoni mwangu kweupe pakavu jua la saa saba mchana then nobody care .

Nimesema hapa leo naweka matukio....ya kinyama.

Itaendelea jioni hii......................... Msichoke.

Sent using Jamii Forums mobile app
Dah! Aiseee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaendelea.........

Habari za mchana wandugu ,sasa tuendelee leo ntajikita kuelezea matukio mbalimbali ya unyanyasaji, uonevu, mauji, uporaji ulianza kujitokeza . nitajitahidi kuelezea niliyoyashuhudia kwa macho yangu ya yaliyotutokea sisi kama sisi maoneo ya kazi... (ubalozini). Haya matukio yamejaa kichwani kwangu kwa kipindi cha mda wa miaka mingi hadi huwa yananikoseha raha wakati mwingine naota kabisa hadi na weweseka vibaya ndugu zangu msiombe vita narudia tena usiombe vita ( utasikia kijana humu anasema bora kinuke aise tema mate chini).

Tukio la kwanza -: hii ilikuwa kipindi hicho hicho mwaka 1992 kama sijasahau mwezi wa nne hivi kama unavyojua mpaka hapo tayari nimeshakuwa na Demu mweupe mfupi kiasi ila alikuwa mzuri ( hapo naona vijana wa mambo yetu wanaanza kutabasamu hhhhaaaa ...) nikiwa nae kwenye mahusiano kama miezi minne hivi sasa kukawa kuna sehemu moja hivi town kulikuwa linapigwa disco kama lile lilokuwa linapigwa pale mikocheni (blue palm eneo dogo lakini weekend wanakaa watu nyomi hatari mziki unapigwa balaa,kwaa taarifa tu eneo lile lilikuwa haliguswi na Askali yeyote yule au interahamwe au kwenda pale kuanzisha vurugu unajua kwanini? Eneo lile ni la Kada wa eneo lile mtemi na msumbufu aliitwa Nyihibilazi (balozi) na disko la kwake sasa mnanza aje? Kwanza mlangoni ukiingia unakuta Askali wake wana AK 47 na magrouneti yapo nje nje.

Basi disko likapigwa kufika mida kama saa kumi hivi nikamwambia demu wangu tuondoke enzi hizo tunakula Mai hatari (pombe) kwa kwenda mbele mzee unakula primus hadi unazima watu wanakubeba kukurudisha nyumbani, basi mtu mzima nikashika chombo( demu) yangu kiuno nikawa nashuka nayo lami kutokea ukumbini kama kuna kilima unashika unaenda lami kuu ndo unasimamisha texi ya kurudi home ,ile namalizia tu kilima kile kwa mbele kidogo nikaona Toyota hilux inakuja wamejaa interahamwe tupu na mabunduki i yao .
Kufika tu mbele wakasimama wakawa wanarudi nyuma aise asikwambie mtu pombe inaleta ujasiri,nikamwambia demu wangu hakuna kuongea chochote hata akiuliza jina lako labda aulizwe kwa kiingereza au kiswahili ndo ajibu, siku hiyo alivaa tisheti yangu zile za watalii zimeandikwa HAKUNA MATATA zilikuwa sinatengenezwa kenya kama sijasahau, basi majama yakawa yamefika pale kwanza wakaanza kukoki mibhnduki yao ebwaanae nikasema sasa tumekwisha lakini niwaambie mwanaume kama una mapenzi na demu wako aise hata itokee hatari gani lazima unamtetea tu hata kama kuna hatari kiasi gani basi swala la kwanza wakatuuliza tulipitokea niliwajibu disko wakasikia refudhi yangu ya kiswahili wakasema nyinyi ni waswahili? Nikamjibu ndio wakauliza watz yani watanzania wanafupisha nane tz nikasema ndo kumbuka nilimwambia demu asiongie hata akipigwa kibao, moja anaiuliza na huyu mugole? (Mugole-ni mwanamke nikamjibu mke wangu) kumbuka hapo kinyarwanda nimeshaanza kukipata pata ila kuongea ikawa shida kidogo, sasa ikatokea ubishi miongoni mwao baadhi yao wakawa wanahisi yule si mtz ni mnyarwanda wengine wakawa wanananiamini mimi hapo sasa ndo kimbembe kilipoanza

Vuta ni kuvute kumlazimisha demu aongee demu anasem na mimi nawaambieni huyu hawaelewi nyinyi huyu ni mtz kwanza haelewi mnaongea nini wakaomba ID ninatoa passport jina moja wakaomba ID ya demu ikiwaambia ipo ubalozini kama vipi twende nikawaonyeshe wakagoma ,demu waNgu yupo kimyaa, sasa ipo hivi yule demu naweza mfananisha na kama msanii Menina ya ni mweupe ana sifa zote za kitusi ila pua lake tu ni pana kidogo kama unavyomuona Menina ,sasa wakawa wanashindwa wafanye nini kumchukua hawawezi wanahisi ni mtz sasa mimi wakati huo nachapa kiswahili hatari na vijimaneno vya hapa na pale ghafla ukaingia ujumbe kwenye redio call yao nikasikia maneno flani nikaona wanaitana wakapakiana kwenye gari na kuondoka pale pale nikawahi texi tukarudi nyumbani na sikumpeleka kwao nilienda kulala( ikawa furaha tosha kwetu kwa usiku huo naona vijana wanatabasamu hapa hhhaaaaa.....) hakika yule demu alinipenda sanaa kwa lile tukio akaja akawa anawahadithia ndugu zake pale mtaani tukawa vile mke na mume aise anakuja nyumbani anytime mungu amsaidie huko aliko kwani tulipoteana tu uenda simu zingekuwepo au mitandao tungetafutana ( jina kapuni) ntaalezea baadae tulivyopoteana vita.. vita ...vita ..baba mbaya sanaa sasa sijui yuko hai au alishakufa ? Maisha yakaendelea...

Tukio la pili-: nilishuhudia saa nane mchana eneo la birjogo( tamka bijogo) hiace nzima ya abiria watu wakashushwa wanapigwa fimbo wakachambuliwa wakatolewa INYEZI ( inyezi maanake mende yani Watusi) wakatandikwa virungu vya kufaa mtu sasa hapo niliona kada (balozi )hilo analisimamia mwenyewe, sasa utamtambuaje balozi katikati ya interahamwe? Yeye anakuwa amevaa belleti nyekundu na shati la chama aisee wale watu walipigwa walikatwakatwa na mapanga huku watusi wakipata mateso makali sanaa ,unajua kwanini ?nilikuja kugundua baadae sanaa kwanini Watusi wanateswa. Sasa ipo hivi wakati Rpf wanaanza chokochoko walikuwa wanapewa taarifa na Watusi wa ndani n baadhi ya ndugu zao wanaume walikuwa wanaenda kwa siri kupata mafunzo maeneo mbali mbali karibu na walipokuwa waasi sasa taarifa hizo zikawa zinawafikia mabalozi mbalimbali nao wanazisambaza kwa interahamwe sasa usiku unashangaa unavamiwa na hao jamaa wanakula kisago halafu wanaondoka na wewe ni ndo imetoka hakuna anaejali basi wakawakatakata mapanga wale Watusi pale shell kituoni cha mafuta hadi leo picha hii huwa hainitoki akilini kuua kwa mapanga zaidi ya watu 12 wanauawa machoni mwangu kweupe pakavu jua la saa saba mchana then nobody care .

Nimesema hapa leo naweka matukio....ya kinyama.

Itaendelea jioni hii......................... Msichoke.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante mkuu kwa mwendelezo,ila nna mawasali hivi kati ya hao wa tutsi na wahutu ni yupi alianza kumbagua/kuua mwenzie?na kati ya hao yupi ni mkatili kuliko mwenzie?
 
Kutokana na kashfa na matusi ya baadhi ya memebers humu napenda kusitisha ushuhuda huu, niwaombe radhi tena na samahani sintoweza kuendelea bora nihamishie ushuhuda wangu kwenye another social network lakini sio humu jf. Mtu hajamaliza kuandika unatukanwa, anakashifiwa,sijui huu utamaduni sijui wawapi? Cha ajabu modereta wanakausha tu bila kukemea mwisho jf inaonekana imekuwa kijiwe cha wahuni. Asante sanaa. Naomba nami nibaki kuwa msomaji wa mada za wengine humu.

Sent using Jamii Forums mobile app

We Bossless acha ufala nawe nae! Kisa hawa waropokaji ndio ukatishe uhondo, haya mangapi huko mtaani unakutana nayo, hebu leta stori mzee tusikerane dingii!!

Nimejitahidi kusoma nipate mwendelezo, halaf nakutana na hii comment yako, bila shaka we ni mkubwa wangu ila haki ya nani vile ungekuwa karibu ningekupiga mbonge wa mbichwaaa!! [emoji13][emoji23]🤣

Leta mambo bwana!
 
Back
Top Bottom