Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Hv ni kwanini yanafahamika kama mauaji ya kimbari?? Kimbari ni jina la eneo au nini hasa??

Sent using Jamii Forums mobile app
Kimbari nadhani neno lilitumika kumaanisha" azimio la kuua idadi kubwa ya watu hasa wenye mlengo wa aina fulani..mfano nchi.dini.kabila.e.tc..kwa rwanda waweza sema ni azimio la kuua idadi kubwa ya watu wa kabila la kitutsi.( hii ni tafsiri yangu..niko " teyari" kusahihishwa.).

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na namna kagame anafanya sasa anakuwa kama ametega time bomb! Muda wake ukiisha au akifa ...it will be time.. the bomb to explode..mauaji ya kimbari yatatokea tena..hutu ni wengi sana kwa population 80%.hivyo kama tutsi wajanja wakiona kagame anakwenda halijojo..inabidi wakimbie vibaya sana[emoji23][emoji23].

Sent using Jamii Forums mobile app

Dah nimecheka [emoji3] jamaa tayari yuko halijojo


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukweli mwingi umefichwa na serikali ya KAGAME.Ni ukweli usiopingika kuwa tusi waliuawa wengi.ILA ukweli usiosemwa ni kwamba mara baada ya RPF kushika dola wahutu wenye mlengo wa kushoto na RPF walikipata cha mtema kuni.jeshi la intelahamwi lilisambazwa hivyo ikabidi wapiganaji wakimbilie zaire(DRC) RPF wakawafata huko huko na kilichowapata huwa hakisemwi sana.yaani waliuliwa kikatili sana.walikuwa wanafungwa mikono na miguu na wanawekwa kwenye magogo kama yale ya bucha zetu za kwa mtogole au manzese then kichwa kinawekwa kwenye gogo unashushiwa nyundo ya kilo 12 na jitu lenye miraba minne.ukweli ni kwamba inasadikika kuwa wahutu walioaga dunia baada ya RPF kushika dola ni wengi kushinda watusi waliouaw enzi za mapigano
Hiki ndio ninachokijua slim shade anatembelea kick ya genocide sympathy wakat yeye anafanya unyama maradufu ya ule na hausemwi inasikitisha sana
 
Hawa wahutu na watusi wana bifu la vizazi kadhaa huko nyuma ni kama waisraeli na wenzao wapalestina, ndomaana hata akina kagame wamekulia kwenye nchi za watu hasa uganda na zaire/kongo. Hataivo ni suala la muda lazima watakuja kuchapana tena huko mbeleni, ni ishu ya muda tu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hii anayosimulia jamaa ni genocide ya pili kwao. Iliwahi kutokea miaka ya nyuma sana, ndo ikatokea tena 1994. Tuombe Mungu kwa kweli awasimie Jirani zetu


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Bossless,
Heshima kwako. Katika umri huu wa 55 napenda kukupa pole na dhoruba za maisha ya kiutafutaji. Kiukweli umepitia mengi...umeona mengi, mazuri, mabay na habari za kutisha kama hizo hapo. Mungu azidi kukunemeesha uishi siku nyingi.

Dunia haijawahi kua eneo lenye isawa wa viumbe hai (binadamu) kuishi. Habari za mlango wa nyuma zinatisha sana...dunia ina matukio makubwa ya kutisha na kuogofya.

Mkuu napenda kukupa hongera nyingi sana kwa kutuletea simulizi ya uhakika kabisa. Mm tu niseme usiyumbishwe na maneno ya watu. Waty tumeumbiwa kuongea, kwa hiyo vinywa vyetu usivipe nafasi kabisa...ww fanya liipendezayo nafsi yako. Nasfsi zetu sisi ni kuona haufanikiwi kweny malengo yako..ukituskiliza sisi walimwengu utapote. Shusha nondo mkuu wangu...tema cheche...tema nyongotukusaidie kubeba huo mzigo ulipo kwenye kifua chako angalau ubaki na furaha uweze kulionanjua siku nyingi kadrii alivokujaalia maulana.

Kudos mkuu. 🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿
 
Hawa wahutu na watusi wana bifu la vizazi kadhaa huko nyuma ni kama waisraeli na wenzao wapalestina, ndomaana hata akina kagame wamekulia kwenye nchi za watu hasa uganda na zaire/kongo. Hataivo ni suala la muda lazima watakuja kuchapana tena huko mbeleni, ni ishu ya muda tu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Soma historia yao, mwaka 1959-1964 waliuana pia japo hawakua watu wengi. Watutsi wengi walikimbilia uhamishoni.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uchawi upi? Ule ni ushauri tu nimempa maana yake sio kwamba aikatishe hapa ili aitolee kitabu, hapana, nadhani utakua hujanielewa point yangu.. Unajua hizi issue za history history ni asset kubwa sana hasa kwa wenzetu wazungu wanaopenda mambo ya kufanya tafiti na documentary..

Sent using Jamii Forums mobile app
andika story yako ukauze kama unaona ni rahisi
 
Muanze kujiandaa kisaikilojia Sasa mmesikia ndo wanaingia Burundi Zen Tanzania uwanja wa Vita n Rwanda ndo washaondoka hvyo.

Sio mje muanze ooh mbona imeisha, jiandaen kisaikolojia
Nliwaambia tokea Jana mjiandae kisaikolojia Mana Uzi unasema mauaji ya Rwanda na msimulizi kaadithia yote ya Rwanda na mwisho kasema wapo border to Burundi Sasa mnajiuliza nn Tena.
 
Haya mauaji yalifumbiwa macho na kila mtu hata nchi na mashirika ya kimataifa walikuwa kimya utafkir hawaoni au kuskia kinachotokea.

Haikuwa siri kila mfuatiliaji wa habari hasa za kimataifa alisikia hizo habar za jamaa kuchinjana.

Nakumbuka redio kama bbc, channel afrika ile redio ya sauzi zilitangaza sana hii ishu lakini cha ajabu hakuna aliyeonekana kusikia wala kuingilia ni kama watu walitiwa ganzi hivi kuingilia nazan kwa sabab ya ugeni wa aina yenyewe ya vita kwa sabab tumezoea vita za nch na nchi.hawa walikua wanachapana wenyew kwa wenyew.

Ila kiukweli kipindi hicho dunia ilikua ya moto sana hata ulaya kwenyewe kuna maeneo walikuwa wanachapana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nliwaambia tokea Jana mjiandae kisaikolojia Mana Uzi unasema mauaji ya Rwanda na msimulizi kaadithia yote ya Rwanda na mwisho kasema wapo border to Burundi Sasa mnajiuliza nn Tena.
Kwa jinsi tulivyo na wakat uliopo sishangai kama atakua hajaambiwa awape version watu flani waihakiki maana mjamaa ujue alikua ubalozini kabisa na ni nguli so wenyewe wanaifanyia editing.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwili wote unasisimka [emoji119][emoji119][emoji119][emoji119].
Inaendelea...................... 49k viewers si mchezo.

Haya sasa tusonge mbele tarehe, saa, sekunde za malaika mtoa roho zikawadia 6/04/1994. Saa tisa usiku tukaashuhudia kitu kama kimondo kikishuka ardhini ila kikapotelea vichakani kwa mbali nje ya mji. kutokana na kishindo chake pale ubalozini kila mtu aliamka lakini hakuna aliejua hasa ni nini, tukachukulia kawaida tukajua ni yale yale kila siku si tumeshaanza kuzoea watu wakaendelea kuchapa usingizi nawanaume wakaendelea kulinda getini.
Asubuhi mapema tukashudia hali ya ajabu ambayo sijawahi kuiona katika maisha yangu, yani kukatokea kitu kama wingu hivi yanii mtu akisimama mitaa tano au kumi kutoka ulipo huwezi mtambua vizuri hadi awe karibu sanaa. Wenye redio wakafungulia redio zao kusikiliza , ikumbukwe kuwa kipindi chote wapiga mayowe wa propaganda redioni walikuwa hawaongee ulikuwa unapigwa tu muziki wa chama ila alfajiri ikasikika wimbo wa taifa ndo unapigwa watu wakabaki wanashangaa halafu unakuwa unajirudia .dalili ya kitu kibaya ikaanza kuhisiwa kigali yote kimyaa.....

Tukawa sasa tunaingia tarehe yenyewe 7/04/1994 harufu ya damu ikawa inasikika kigali nzima, makelele ya maumivu ya watu yakawa yanasikika kwa mbali kutoka hapo ubalozini ,balozi ndo akawa ametoka kututangazia kuwa sasa hali si nzuri rais habyarimana ameuawa ile kusema tu vile watu wote akili zilituruka wengine wakawa kama wanataka kukimbia hovyo wanaume ikabidi wafanye kazi ya ziada kwani kitendo cha kutoka nje ya ubalozi kingeleta maafa makubwa sanaa. Ila wote pale picha iliyotujia kichwani ni kwamba sasa tunakufa hakuna tena msalie mtume.

Swali likaja nani kamuua rais? Hakuna mwenye jibu. Aise kuna wimbo moja hivi ukiimbwa unakuwa kama vile unaomboleza unafanafana na ile ya Kimasai ukawekwa kwenye radio ukawa unapigwa huku unamtaja rais kuwa ameuliwa na Ng'otanyi(waasi wa kitusi) aisee vita ikawa imeanza rasmi hata balozi sasa akawa hatoki tena tukakaa wote mle ndani hakuna kutoka kufuata chakula wala nini.

Siku ya kwanza mitaa kelele kila upande, sasa interahamwe wakaanza kuvamia hadi balozi za jirani ambao walikuwa wameondoka walinzi wao wakakimbia watu wakazidi kuuawa. chakula pale kwa ni uji tu hakuna sukari wala nini, unajua kama upo vitani mara nyingi unakuwa husikii hamu ya kula na unajiona uko powa tu kumbe unazidi kuisha ( kama kuna mtu alipigana vita humu ya kagera atadhibitisha hilo) halafu unaweza shanga kumekucha ghafla kiza kimeingia ghafla usiku mnalala usingizi wenye wa mang'amung'amu tu.

Balozi zikawa zinaendelea kuvunjwa siku zinaenda magrounet yanarushwa hovyo hovyo risasi zinalia zikitulia labda nusu saa zinaanza tena,unajua rwanda ni milima sasa unaweza kaa usiku unaona roketi inarushwa kutoka upande moja kwenda upande mwingine vimulimuli tu vya moto hadi kuna kucha kelele na risasi zinaanza tena. Sasa ikawa dhahiri kuwa hakuna namna tumuachie mungu tu.

Lakini wakati huo balozi alikuwa kwenye chumba kimoja kati vile vyumba vya sili nilivyosema hapo awali sijui alikuwa anafanya nini , ikafika ya kumi sasa ikawa hakuna kitu tena njaa tupo katikati ya vita mjini umezungukwa na wanajeshi wanapigana live bila chenga jiona ya siku hiyo ndo wakaja wanajeshi wa rwanda ,na toka siku ile ndo niliwaona live wanajeshi wa rwanda majitu yamepanda sura ngumu macho mekundu wakaja na maroli yale 24 na ile defender nyeupe ila waliokuwa kwenye ile defender hawakushuka tukaitwa uwani ubalozini .balozi akatoa tamko akasema SAFARI YA KUWAONDOA KIGALI WATANZANIA NDO IMEFIKA NA KAMA HUNA PAPER ( PASSPORT ) TAFADHARI USIPANDE KWENYE ROLI UKIPANDA LIKALOKUTOKEA MBELE USILAUMU MTU. hii kauli aliitoa kwa uchungu na kwa msisitizo sanaa huwa siisahau maishani mwangu. .

Hapo sasa ndo ngoma ikawa ngumu kila mtu akamkimbilia balozi kuomba amsaidie mkewe na watoto wake, balozi akagoma kabisa wengine akawa anawajibu kama unampenda mkeo baki nae hapa aisee watu wakawa kama vile wamepagawa maroli yapo nje lakini unashindwa kwenda kulipanda paper huna , sasa kuna kisa kimoja kilichojitokeza sintokuja kukisahau.kuna mama wa kinyarwanda mtusi alikuwa na bwanake mtanzania amezaa nae ila yeye kipindi cha vita alikuwa ameleta mzigo tanzania ,hivyo ikabidi mama ajitoe mhanga akamuita balozi awachukue wale mabinti wake mapacha wawili walikuwa kama na miaka 14 hivi weupe pua za kitusi kabisa balozi akakubali mama akabaki ,sasa tutaona mbele walivyotaka kuleta kizaazaa nusu tuchapwe RPG kwa sababu yao.

Sasa tukawa tumejipakia kwenye roli wengine wasio na vibali wakawa wamebaki pale hapo ubalozini, hapo hakuna kusikitikiana mnapeana mkono wa kwaheri basi safari ikawa imeanza na escot ya wanajeshi wa rwanda ,vizuizi kibao tukifika kwenye vizuizi wanashuka wanaenda wanajeshi wenyewe wanavitoa tunapita ,cha ajabu vizuizi vingine vilikuwa havina hata watu sijui walikuwa wakajificha au vipi.

Sasa wakati vita imepamba moto Tanzania wakawa wamefunga mpaka wake na rwanda Ikatulazimu kupitia boda ya burundi sasa kimbembe ndo kikaanza hapo, kuna wilaya kama tatu inabidi upite ndo ufike boda ya Burundi na rwanda kama sijakosea kwa kutokea kigali lazima upitie province ya butare halafu ya Gitarama ya mwisho nimeisahau kitambo sanaa. Sasa province Butare (wenyewe wanaita) ili ufike lazima uvuke mto fulani mkubwa unaitwa Nyabarongo kuna daraja kubwa hivi linalounganisha kigali na hiyo wilaya hapo sasa ndo niliona mchezo wawale jamaa saba wa defender hapo tunaenda lakini magari yanakanyaga maiti barabarani maiti zimezaga kila kona. Ile tunashuka kilima kidogo inakaribia kuulifikia kama kilomita tatu hivi wale wanajeshi wa rwanda wakageuka na gari lao ghafla wakarudi nyuma moyo ukapiga paaahhh nikahisi kuna kitu si chakawaida unageuzaje gari ghafla unarudi kwanini usituache tuvuke ndo urudi aisee.

Mbele tena kidogo ile defenda ikasimama katika ya barabara hakuna gari kuendelea kupita magali yakawa yamesimama tu ile defenda ikawa inaendelea kusogea mbele sisi tumeambiwa tusimame hapo hapo hadi Difenda itakaporudi kutoruhusu tuendelee tukawa tu pale na madereva kila mtu kwenye Kibini wengine kwenye bodi nyuma kimyaaaaaa...


Kama lisaa hivi tukasikia risasi zinalindima vibaya Sanaaa yani ikawa dhahiri kama mbele yetu kama kilomita moja watu wanapigana lisasi live ila hatuoni tatizo la rwanda mapori na vichaka vingii ila risasi zikawa zinalia kama zipo chumbani nikasema sasa huu ndo mwisho wetu.

Mwisho lisasi zikakoma tumekaa kama nusu saa hivi defenda hairudi na risasi hazisikiki tena Mwisho balozi akaamuru tuendelee na safari bila defenda dahhh ile tunafika darajani maiti kibao zimelala hapo ila hakuna defenda tukawa tunaendelea na safari tu.

Sasa tukawa tunakaribia kuimaliza province ya Butare sasa hapo ndo kulitokea kizaazaa cha wale mabinti aise tulikuta bonge la kizuizi...... Na maenterahamwe mchanganyiko na wanajeshi wa rwanda aise........ Nikasema. Sasa tunakufa.................................

Itaendelea...........................................

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakumbuka hata wakati Mobutu anapinduliwa radio za kimataifa zilikuwa zinatangaza kuwa wanajeshi wa banyamulenge walikuwa wanaongea kiswahili safi!

Baada ya mapinduzi General Mboma mkuu wa JWTZ na Jakaya ndio walikuwa watu wa kwanza kuunga mkono yale mapinduzi kupitia BBC! Ndio maana pamoja na Mobutu kupewa msaada kijeshi na marafiki zake bado alichezea kichapo cha nguvu! Tuiheshimu sana nchi yetu! Hii nchi ina watu, Nyerere alipanda mbegu vyema!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya mauaji yalifumbiwa macho na kila mtu hata nchi na mashirika ya kimataifa walikuwa kimya utafkir hawaoni au kuskia kinachotokea.

Haikuwa siri kila mfuatiliaji wa habari hasa za kimataifa alisikia hizo habar za jamaa kuchinjana.

Nakumbuka redio kama bbc, channel afrika ile redio ya sauzi zilitangaza sana hii ishu lakini cha ajabu hakuna aliyeonekana kusikia wala kuingilia ni kama watu walitiwa ganzi hivi kuingilia nazan kwa sabab ya ugeni wa aina yenyewe ya vita kwa sabab tumezoea vita za nch na nchi.hawa walikua wanachapana wenyew kwa wenyew.

Ila kiukweli kipindi hicho dunia ilikua ya moto sana hata ulaya kwenyewe kuna maeneo walikuwa wanachapana

Sent using Jamii Forums mobile app
Wakati hii vita inatokea kule Soviet napo kulikuwa na mapigano ya kujitenga na urusi, nadhan ndo yalipewa sana airtime , Rwanda zilikua siku 90 tu za Hofu na mashaka , na inasemekana watu zaidi ya milioni moja waliuwawa ndani ya siku hizi tisini.

Sent from my SM-A207F using Tapatalk
 
Back
Top Bottom