Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Inasikitisha Sana wanafikiria kabila ndo linaloleta msosi mezani ukiona mtu ame progress lazima ame hustle Sana. Kazi na ubunifu ni mkombozi wa umaskini, wengine hujiaminisha wengine wameiba wamefanikiwa kwanini na wao wasiibe wafanikiwe?
Hyo corona mbona imefika kwetu na idadi inaongeza Hadi wizara imekuwa kimya.
Kuna binadamu wa ajabu sana,mtu hataki kufanyakazi anakodolea macho ukabila.Majuzi nilikuwa mitaa ya Bondeni basi jamaa mmoja kawajaza watu ujinga eti corona inapukutisha wazungu mwakani lazima waje afrika kutuomba tuhamie Ulaya washabiki wakawa wanashangilia utafikiri majuha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
From: BOSSLESS TO BONGOMAN

SASA TUENDELEA NA STORY YETU ILA NAOMBA NIWATAKE RADHI KIDOGO KUTOKANA NA SHUGHURI ZA SHAMBA NILIVYOKUWA NI MEBANWA HAKIKA UKIJUMLISHA NA HAYA MASIKA HATA MUDA WA KUANDIKA MISTARI MIWIRI TU NILIKUWA NI KUDHINDA SHAMBA NA KULALA SHAMBA .
PLUS KUKIMBIZANA NA NDEGE NA KUTEGUA MAJARUBA PALE YANAPOJAA MAJI KUHUSUS SIMU HAIKUPONA VIZURI NIKAAMUA KUNUNUA NYINGINE TU NAWASHUKURU WALE MLIOKUWA NA NIA YA KUNICHANGIA SASA TUENDELEE NA STORY YETU.

Sasa baada ya kuvuka mpaka ndo nikahisi akili yangu ndo imakaa sawa nakumbuka nilisafiri kwa maroli kutoka mpakani hadi kahama tben nikakaa kahama mjini kama siku mbili hivi then nikakwea train kuingia kuja Dar (ikiwa ni mara ya kwanza kupanda train) ugeni wa kupanda train ukanipa somo fulani ila kuna kituko nilikifanya hadi leo huwa sikisahau na nikikumbuka macheka mwenyewe iko hivi nilipokuwa nimekaa nilikaa na jamaa moja hivi yeye alikuwa ametulia tu na konyagi yake mkononi anakunywa taratibu sasa sikumbuki kama tulibadilishana story kwa namna moja ama nyingine ila kwa asilimia kubwa alikuwa anaongea mwenyewe kilevilevi tu.

Tukafika sehemu hivi nakumbuka itakuwa ilikuwa Tabora train ikawa imesimama akina mama wanauza chakula na mambo mengine hivi sasa tukawa tumeagiza vyakula tunakula sasa wakati tunakula yule mlevi akaniuliza ndugu wewe unaelekea wapi nikamjibi naekea Tanzania halafu nikawa namjibi kwa kujiamini kabisa daaahhh ebwanae watu waliokaribu walicheka hatarii nikajistukia nikarekebisha kuwa naelekea Dar ila watu walibaki na kicheko hatariii. Safari ikaendelea

Hatimae tukafika station_ dar es salama nikashuka nikapanda texi hadi magomeni enzi zile kuna majamaa yalikuwa yanauza mitumba pale barabarani mitumba safi kabisa nikanunua tisheti mbili na jeans mbili zikawa ndo nguo zangu za mwanzo toka nirudi ikumbukwe tu kuwA niliach nguo nyingi na baadhi yamabegi yangu yalipoteana kwenye maroli sasa nikawa ndo naekea home .

Nikafika home nikakuta hakuna mtu ila nyumba iko wazi niakaingia nikaenda chumba cha madogo nikabadilisha nguo nikaenda bafuni kuoga nikarudi nikaingia ndani nikalala mpaka saa kumi na mbili jioni ndo nikaamka nikala sasa ndo nikaanza kupokea pole na maswali kibao toka kwa ndugu jamaa na marafiki wengine wakawa kama hawaamini .mzes asikwambie mtu bongo kuna amani sanaaa

Yani anaenda kuitwa jamaa w mtaa wa ng'ambo kuja kuniona tu jamaa wakawa wazidi kujaa tu nyumbani ikabidi mzee awaambie waje kesho waniache kwanza nipumzike maisha yakawa yanaendelea siku ikapita hadi week ikaisha ijumaa tatu mapema nikariport wizara ya mambo ya njee .

Taarifa zetu zilikuwa zimeshawafikia so kufika nikasaini kitabu nikamuona katibu muhtasi akanipa barua sikujua ina nini nikakaa benchi nikawa na isoma nikumbushe ni mwaka huo huo 1994 ilikuwa kama mwezi wa tano mwishoni au katika ya wa sita hivi ,nikawa nasoma nikakuta barua ya likizo ya miezi mitatu na barua ya malipo ya likizo ya mapumziko na laki 130 nikachukua barua yangu nikarudi home.

Ikimbukwe tu kuwa bado tulikuwa kwenye payroll na hela ilikuwa inaingia kila mwezi kama kawaida .sasa mzee mzima nimasema ngoja niangalie salio kipindi hicho mfumo wa kulipa mishahara kupitia akaunti za mabenk ulikuwa hakuna wewe kila mwisho wa mwezi nikupokea tu kwa mahasubu uwe dar au kigali , sijui taasisi kwaa taasisi nyingine.ulikuwa unaweza kumuuliza mhasibu kiasi au balance ua mshara wako bada ya muda akakwambia so mimi nilikuwa na kama nina miezi 2 hivi sijagusa mshahara nikauliza ikaonekana na kama US 600 hivi .

Nikaridi home maisha yakawa yanaendelea natokea home kila siku naenda pale kwa wauza mitumba napiga story jioni narudi nyumbani nakula nalala siku zikaenda likizo ikaisha nikareport wizarani nikakuta barua ya kupangiwa kituo makau kama mhasibu msaidizi ,

Nikumbishe maisha ya kukaa uraiani miezi ile mitatu ndo yslinifany sasa nikakutana na watu wengi walikuw wanafanya biashara tofauti pale kijiweni japo wengi hawakujua taaluma yangu lakini walitokea kunipenda akiweno mzes moja alikuwa wa kichagga alikuwa na anaitwa Mambosasa sina hakika kama ndo lilikusa jina lake halisi ila alikuwa na mabasi ya abiria ya ubungo_kariakoo alikuwa ameyaandika jina hilo Mambosasa na fiat moja hivi kukuu mzes alikuwa anaishi magomeni makanya na alikuwa ana nunua srepa na kuuza so nikawa nimeanza kupata IDEAR ya ile biashara yake.......

Itaendeleea .......POLE NA CORONA

Sent using Jamii Forums mobile app
Umenichekesha eti naelekea Tanzania

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watusi ni akina Kagame ambao leo ndo watawala, ukiconnect dots, ni kama vile kabla watusi hawajashika hatamu na kuonyesha ubabe wao kama malipizi, tayari walinyanyasika kiasi cha kutosha. Ngoja mzee wetu aendelee kumimina matukio...

Wenzangu na mimi mnaojifunza Kinyarwanda twende pamoja:
Mugore (mke/demu)
Amakuru (Mambo/habari yako)

Niliona Niyonzima wa Yanga ana binti mrembo, nitakuwa na pa kuanzia nikitupa ndoano.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mugabi= mwanaume (bibi na babu yangu wazaa mama ni warundi)
Mama yangu mzazi pia nae kazaliwa Burundi akifuatiwa na wajomba zangu wawili
Walikuja Tanzania kama MANAMBA (sijui tafsiri sahihi ya hili neno) Wajuzi naomba ufafanuzi
Nakumbuka nilipofuatilia kitambulisho cha uraia nilipata usumbufu fulani hivi haswa na majina yangu yote ninayotumia yana asili ya kitaliano na kikatoliki (na burundi kule wengi ni wakatoliki dhehebu ambalo makao makuu yake yapo Italy)
Mwaka 2014 uhamiaji walikuja kufanya uchunguzi kuhusu kesi ya binamu yangu ambaye alikua Diwani kigoma(kupitia chama cha zitto kabwe) ila alishinda kesi

Au basi wacha niishie hapa nisije fungua code bure mkaanza kunifuatilia na mimi
 
Mugabi= mwanaume (bibi na babu yangu wazaa mama ni warundi)
Mama yangu mzazi pia nae kazaliwa Burundi akifuatiwa na wajomba zangu wawili
Walikuja Tanzania kama MANAMBA (sijui tafsiri sahihi ya hili neno) Wajuzi naomba ufafanuzi
Nakumbuka nilipofuatilia kitambulisho cha uraia nilipata usumbufu fulani hivi haswa na majina yangu yote ninayotumia yana asili ya kitaliano na kikatoliki (na burundi kule wengi ni wakatoliki dhehebu ambalo makao makuu yake yapo Italy)
Mwaka 2014 uhamiaji walikuja kufanya uchunguzi kuhusu kesi ya binamu yangu ambaye alikua Diwani kigoma(kupitia chama cha zitto kabwe) ila alishinda kesi

Au basi wacha niishie hapa nisije fungua code bure mkaanza kunifuatilia na mimi
Manamba- wafanyakazi wa shambani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kagame hakujipanga "msituni" bali alikua na back up ya serikali za kitutsi za Uganda na Burundi ambao pia baada ya kushika hatamu walimsaidia kuwateketeza wahutu waliokimbilia huko DRC.

Wahutu changamoto ni kwamba hawapo organized wala kimkakati kila mtu anapambana kivyake sasa ambacho wanaweza ni kutumia back up ya serikali za kihutu mfano Nkuruzinza na walitakiwa wahakikishe DRC anashinda mtu ambaye hayuko puppet wa Kagame!! Wamechelewa sana.

Maana kagame wakimvamia tu Museveni na Magu watamsaidia so watafeli!! Hapo bado DRC itawafukuza..... Ila kagame na watutsi walikua makini kabla ya uvamizi wanahakikisha serikali za jirani zipo mfukoni.

Hata alopovamia wahutu DRC alihakikisha ameshaongea na kaunda wa Zambia na Dos santos wa Angola kuwa wasiingilie vita. Sasa wahutu hawana ushawishi huo kwenye serikali zetu hivyo vita itakua ngumu sana

Fursa yao pekee ni kuhakikisha Nkuruzinza hatolewi kwa gharama yoyote lasihivyo ndio utakua mwisho wa ndoto zao kurudi Rwanda.
 
Naomba kuuliza

Hivi wanafunzi wa Kinyarwanda huwa wanasoma hizi Rwanda Genocide na Civil Wars mashuleni?
Mtaala wa Rwanda tokea 2016 unaruhusu sio tu kuendelea kufundishwa kwenye somo la history ila hadi masomo mengine!!

Ila shida imehodhiwa kwa matakwa ya kuwatukuza watutsi na RPF. Kwamba genocide iliua watutsi pekee na wahutu waliopinga mauaji!! Ila RPF haikuua mtu kabisa??

Uganda huko ndio inafundishwa Darasani bila unafki. History 1 kuna topic ya Rwanda civil war inaongelea jinsi Watutsi walivyokua na jeuri na kutesa wahutu. Na hawaiiti genocide ila Civil war na kwamba watutsi walivamia na wahutu walijilinda.

Cha kushangaza pia kuna topic ya Nyerere kwamba ni dikteta. Na aliua waganda wengi kuliko hata Idd Amin, lakini wakati huo huo Museveni hatajwi kwenye list ya madikteta!!

Kazi kwelikweli

Cc The Transporter
 
Katika huu uzi kwa maelezo mengi ya mwandishi sijaona sababu ya kuficha jina la balozi kwa kuwa hakukuwa na jambo lolote illegal humu.why hiding the name?ikiwa huyo balozi alifanya jambo la kishujaa kama hilo why afichwe? But pia inawezekana mwandishi ameathiriwa sana na kucheck movies au kusoma novels hivyo akajikuta anaingiza ingiza mambo hayo ambayo ni fiction kuleta utamu.
 
Alijichanganya na pengine haelewi. Aende Yemen akaangalie wanaouana ni dini gani. Somalia na Sudano majority ni dini gani

Mkuu unazungumzia uislam wa Rwanda, Tanzania au duniani kote?
Kule Zanzibar waislam wanabaguana sababu ya siasa, ethnic (upemba uarabu na uunguja ubantu).
Mashariki ya kati wanauwana kati ya waislam wa Shia na wa Sunni.

Mkuu pitia upya taarifa zako.
 
Inaendeleaaa...........

Nilipoishia nikiwa IMhala hoteli najiandaa sasa namna ya kuwahi kuamka mapema kuwahi kituoni kwangu kuripoti asubuhi. Mapema tu nikaamua nikajianda safi kabisa nikaanza safari ya kuelekea kituoni kwangu, nikashudia kitu cha ajabu ambacho sikukizoea .Dar ukiamka saa kumi na moja alfajiri kwa miaka hiyo hata kwa sasa ukifika stand utakaa tu kidogo hadi saa kumi na mbili au nani nusu hivi unaweza kuwa umepata usafiri na kuondoka iwe kwa texi au daladala wanyarwanda swala la kuamka mapema hilo kwao hapana labda sijui kama wamebadilika kipindi hiki, basii mtu mzima nikawa stand barabarani nasubiri daladala huwezi amini hadi saa moja moja kamili asubuhi hakuna cha daladala wala nini nikamuuliza jirani yangu pale stand hii ukoje akaniambia mabasi yanaanza kufika saa mbili kamili au na nusu nikamuomba anionyeshe texi nipande akaniambia hakuna stand ya texi Unachotakiwa kufanya unasimama barabarani unapungua gari lolote dogo mkono itakayosimama basi hiyo ndo taxi mnaelewana bei anakupeleka, mimi nikafanya hivyo kweli nikawa nimepata usafiri tukaelewana (sikukumbuki tulikabiliana bei gani ila alipeleka hadi ubalozini getini) nilishuka nikajitambulisha kwa mlinzi akiniruhusu kuingia ndani nikaingia hadi mapokezi nikatoa barua yangu ya ajira nikapokelewa safii kabisa na watumishi wenzangu sasa hapo nikawa majihisi nipo nyumba tunaongea lugha moja tunaelewana safii mzee nikapumzishwa sebule ndogo kumsubiri balozi afike nijitambulishe ili sasa taratibu zingine zifuatwe.

Muda si mrefu balozi akafika alikuwa mwanamama mweupe kama mpemba mama mtu mzima( naomba nisilitaje jina lake) akanikaribisha tukaongea maeneo ya hapa na pale ikawa baadae akaaga nikabaki na wasaidizi wake sasa ndo nikawa nimeingia mzigoni rasmi nikiwa na mabegi yangu yote( ikumbukwe kule hotelini niliaga kuwa sirudi hivyo niliondoka na kila siku changu hadi ubalozi).

Iko hivi ubalozi wowote lazima uwe na baadhi ya vyumba vya siri na wazi hivyo vya siri( naomba nisivizungumzie na kazi yake ni nini kwa kuwa sio lengo) basi katika vile vyumba viwili nikakabidhiwa chumba kimoja kwa ajili ya kupumzika mimi na mizigo yangu nikawa naishi pale ubalozini kwa muda kama week mbili hivi nalala naamka nafanya shughuli ndogondogo za ofisi mda wa kazi ukiisha watumishi wenzangu wananitembezA mjini ,taratibu nikaanza kuzoea mjii mawazo ya kupanga uswahili yakaanza kuingia akilini mwangu ,baada ya muda nikaomba kuhamia mtaani nikakubaliwa bila shaka ( hili niliweka sawa kwanza madhumuni ya vyumba vy pale ubalozini sio kufanya kuwa makazi ya kudumu unakaa kwa muda unajipanga kidogo then unaanza kuishi mtaani) .

Basi mzee mzima nikapa nyumba yangu pale Gikondo karibu na bandari kavu huwa wanakuita MAGERWAA kama sijakosea speeling basi nikawa nimepata nyumba nakuanza maisha nikiwa single kabisa sina hata mtoto wa kusingiziwa nje maisha ya kaanza hapo ( RWANDA hadi sasa hakunaga mambo ya kupanga chumba kimoja kule ukipanga unatakiwa upange nyumba nzima ) maisha yakawa yanaendelea ni kazini nyumbani taratibu vijana wakaanza kunizoea majirani wote wakaanza kunizoea pia sasa sikujua walikuwa wanavutiwa na nini kwangu ila baadae niligundua kuwa walikuwa wananipenda kwasababu naongea kiswahili hivyo nikiwa naongea wanafurahi japo sikuwa na uhakika kama wananielewa au vipi? Akafikia hata wakifanya sherehe zao majirani lazima wamletee barua ya mwaliko mimi nikihudhuria wanafurahi sanaa walikuwa wananiita mswahili. Neno la kwanza kujifunza la kinyarwanda ilikuwa salama AMAKURU yani habari yako.

Maisha yakaendelea pale kazini, ikawa ni mwendo wa kazi kwenda mbele hadi kufikia mwaka 1990 hapo yani nikawa na miezi sita na siku kadhaa kigali miezi yote hiyo nilikuwa sijatoka nje ya mji wa kibali.

Niseme mwaka huo ndo nilianza kupata ufahamu juu ya maisha halisi ya Wanyarwanda mtaani kwangu ikawa nikialikwa kwenye sherehe nakuta watu wale wale (naomba nieleweke hapo kwa mfano unaishi mtaa moja kuna kaya nyingi tu lakini ule mtaa ukawa kama kuna mgawanyiko flani hivi yani ukiitwaa kwa mzee john unamkuta mzee Amosi yupo hivyo kwa mzee Amosi unakuta mzee john yupo halafu mtaani kuna watu wengine hawashirikishwi kabisa japo wapo mtaani hapo.) hii ikawa unanitatiza ikabidi nianze kufanya utafiti wangu kwa siri ikiwemo kuwauliza watumishi wenzangu pale ubalozini.

Pale ubalozi kulikuwa na dereva ambao alikuwa anasaidia anahudumu pale ubalozini,siku moja nikamuuliza kuhusu hilo jambo alichonijibu ni kuwa hicho kinachotokea na ndo maisha halisi ya Wanyarwanda yani Watusi na Wahutu hawafungamani katika mambo mbalimbali akasema kuwa kuna hali ya ubaguzi wa hali ya juu hasa Wahutu kuwabagua Watusi ambao ni wachache sanaa na hilo ndo nilipokuwa nilishuhudia kwa takribani kipindi cha mwanzoni ila nikawa siajelewa mtusi yupo na mhutu yupo na unamtambuaje mtusi na mhutu unamtambua aje ukawa mtihani sasa kwangu.

Baada ya kulielewa hilo sawasawa ndo ikawa sababu ya mimi kukacha tena kwenda kwenye sherehe za majirani kwani nilihisi kinachotengezwa hapo si jambo jema ikafikia mahala jirani akiniiona nimesimama na jirani mwingine ana nuna au ananipita bila hata kutusalimia ikawa inanishangaza kwakweli CHUKI YA UKABILA NI MBAYAA SANAA.usiombe.

Maisha yakaendelea kama kawaida ila nikaona Nihamie mtaa mwingine kuwakomoa wale majirani, nikawa nimehama pale nikahamia mtaa mwingine nikajitahidi nisiwe na mazoea kama ya awali nikawa ni kazi ,nyumba ,matembezi mjini kurudi nyumbani na kulala.

Hatimae mwaka ukapita ukaingia mwaka wa pili ya ni 1992 hapo ndipo kuna kipindi rwanda kukawa na mambo ya ajabu sanaa yani mnaweza mkawa mmelala wanakuja watu wana silaha, mapanga na mashoka usiku wanawamsha wote mnawekwa kwenye foleni unasikia huyu ni ing'otanyi ukiambiwa hivyo ujue jamaa watakuchukua wanaondoka na wewe ndo kwa heri na ukujifanya kubisha pale pale unageuzwa asusa yani unakataa katwa mapanga watu wanakuona ,ila niligundua waliokuwa wanafanyiwa hivyo wengi wao waikuwaWatusi wakawa wanadai kuwa huwa wanatoroka kwenda kupata mafunzo ya kijeshi polini na wanarudi kimya kimya uraiani kuchora ramani ya uvamizi kuisaidia kikundi cha waasi wa RPF.kwa miaka hiyo uvamizi wa RPF maeneo ya mipakani ulikuwa wa mara kwa mara hadi kufikia jeshi la rwanda kuhamia mipakani kulinda ila mashambulizi hayakukomaa japo majeshi ya serikali yalikuwa tunajitahidi kuzima uasi

Sasa turudi kwa wale watu wanaokuja usiku na bunduki na magruneti na mapanga kusaka watu wanaowaita ing'otanyi ,badaae nikagundua kuwa wale jamaa wanaitwa interahamwe yani kwa kiswahili wavamizi wa pamoja hapa naomba niongelee jambo moja muhimu sanaa kwa faida ya wasomaji, dalili ya kwanza kabisa ya uvunjifu wa amani au vurugu za kikabila au vita ni pale utakapo ona vikundi vya kisiasa, au vya kidini vinakuwa na walinzi au vikundi vya ulinzi halafu wanamilishwa bunduki halafu mkuu wa jeshi la polisi au majeshi anakaa kimyaa hakemei wala kutoa katazo lolote ukiona hivyo Unachotakiwa kufanya uza mali zako zote hamia nchi unapoona wewe ni salama kwako mapema sanaa.

Kilichotokea interahamwe walikuwa kwa mfano kama green gard wa Ccm au red bregard wa chadema , mara ghafla wakawa wanaonekana mtaani wamevaa nguo za chama chao cha MRND wakiwa na silaha kabisa za kivita wanatembea mtaani wanaimba nyimbo za kujipamba chama chao na rais wao hii maanake nini ukiona hivi juu chama tawala hakina imani tena na jeshi hivyo wakaona bora silaha zinaoagizwa na serikali wapewe makada wa chama wajilinde wenyewe, makada wakawapa interahamwe, interahamwe wakawa wNaogopeka kuliko hata polisi au jeshi wakiingia dukani kwako wakichukua mkate au siagi haruhusiwi kuhoji, kuhoji tu umekula kwako utachakazwa kwa kipigo vibaya sanaa sasa ikawa ukiwa na kesi hata kama aliekuonea ni interahamwe ukipeleke kesi polisi hakuna kitakachoemdelea ,kama umemkariri nenda kwa bosi wake huwa anakuwa Kada wa chama mfano mabalozi unamuelezea pale kwa kutia huruma ndani ya dakika sufuri anaitisha gwaride kama huyo aliokuonea ni wa eneo hilo ukimtambua anamcharaza vibaya fimbo mbele za watu ata kama kakupora kitu lazima arudishe hapo hapo ikawa inankishangaza sanaa binafsi nikiwa eneo la nyehere-gikondo kuna moja alinipora saa nikaenda kwa kada akaitwa akanirudishia tena bila ubishi kama kauza au katupa analipa pesa atakayoitaja kada (balozi) haijalishi hicho alichokupola kina dhamana gani.


Leo nimejitahidi kuandika ndefu nitaendelea kesho nimechoka sanaa........itaendelea.

Sent using Jamii Forums mobile app
Duuuh..
 
Hapo kwa Nyerere mambo ni moto hahahahhaahha

Mtaala wa Rwanda tokea 2016 unaruhusu sio tu kuendelea kufundishwa kwenye somo la history ila hadi masomo mengine!!

Ila shida imehodhiwa kwa matakwa ya kuwatukuza watutsi na RPF. Kwamba genocide iliua watutsi pekee na wahutu waliopinga mauaji!! Ila RPF haikuua mtu kabisa??

Uganda huko ndio inafundishwa Darasani bila unafki. History 1 kuna topic ya Rwanda civil war inaongelea jinsi Watutsi walivyokua na jeuri na kutesa wahutu. Na hawaiiti genocide ila Civil war na kwamba watutsi walivamia na wahutu walijilinda.

Cha kushangaza pia kuna topic ya Nyerere kwamba ni dikteta. Na aliua waganda wengi kuliko hata Idd Amin, lakini wakati huo huo Museveni hatajwi kwenye list ya madikteta!!

Kazi kwelikweli

Cc The Transporter
 
Kuwa salama kwa Tanzania sio kwamba inshu za ukabila au udini hazikufanya au hazipo Ila n distance Kati ya hzo pande ndio ilkua inafanya Hilo Jambo lisiwezekane sie tuna eneo kubwa Sana alafu population yetu n ndogo katika eneo tulilonalo Mana Kuna distance Zaid ya 300km kuuacha utamadun mmoja Hadi mwingine.

Hvyo sehemu Kama Burundi, kenya, Rwanda na Uganda walifanikiwa Sana sababu yakuwa na eneo dogo na population kubwa kwenye eneo Moja pia DRC na Sudan.

Hata hapa Tanzania wanatamani Sana tuingie kwenye machafuko ya sisi kwa sisi ili waje kusema wanalinda Aman wajichukulie vyakao

Hawa wanasiasa Tena Hawa maarafu ndio agents wa kutupeleka huko kaa chin uwafuatilie utaona Kuna kitu huyu JPM anajitahidi kufikisha kijiti salama Sana japo JK ilkua imebaki kidogo tuu tuingie humo kumbuka ya green guard, red gurd, cuf sijui iliitwaje Mara panyaroad Mara vikund vya kijingajinga tuu.
Ww Sasa unapuyanga kwahiyo panya road walipandikizwa na wazungu,?
 
Back
Top Bottom