Sio lazima kuwa na mtazamo hasi kwa kila kilichofanywa/anzishwa na Hayati Dkt. Magufuli

Sio lazima kuwa na mtazamo hasi kwa kila kilichofanywa/anzishwa na Hayati Dkt. Magufuli

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Ni kama kumejitokeza bidii ya kujaribu kuipa mitazamo hasi karibu kwa kila jambo au mradi ulioasisiwa na Mwendazake.

Kwa mfano mradi kama wa Bwawa la Julius Nyerere, mimi ni kati ya Watu waliokuwa wanapinga kuwekeza matrilioni ya pesa za Walipakodi kwa mradi unaotegemea maji, ambayo tayari uzoefu unaonesha kutetereka kwa miradi kama hiyo iliyotangulia.

Kwa mradi wa kununua Ndege, SGR n.k. huko nilikuwa hamsini hamsini na sikuwa msimamo wowote rasmi. Lakini kwa kuwa miradi hii ilishaanza sioni tena kama kuna haja ya kuitazama kwa upande mmoja tu wa hasi.

Zaidi ni kama kupoteza muda maana tayari ipo inaendelea, kwa nini sasa tusijaribu kuiangalia sasa kwa mitazamo chanya, kwamba kwa kuwa tayari ipo sasa nini kifanyike kuanzia hapa kwenda mbele.

Nini kifanyike Ndege tulizokwishanunua ziwe na manufaa badala ya hasara. Kwanini tusijifunze kwa Wenzetu wa Ethiopia? Kama wao wanaweza kwani sisi ni Viazi sana kwamba hatuwezi kufanya chochote?
 
Mnajitekenyaaaaaaaaaa

Alafu mnacheka wenyewe😂😂😂😂

Mataga mpo wa kila rangi. Alafu msitupangie kazi maaamaae nyinyi😀
Tujifunze kuwaza na upande chanya maana hata Wahenga walisema hakuna kisichowezekana chini ya jua.
 
Kwa ujumla Magufuli alishindwa kuongoza nchi.
CV aliyoacha haimruhusu kuwasogelea Malaika achilia mbali kuwaongoza.
 
Ni kama kumejitokeza bidii ya kujaribu kuipa mitazamo hasi karibu kwa kila jambo au mradi ulioasisiwa na Mwendazake.

Kwa mfano mradi kama wa Bwawa la Julius Nyerere, mimi ni kati ya Watu waliokuwa wanapinga kuwekeza matrilioni ya pesa za Walipakodi kwa mradi unaotegemea maji, ambayo tayari uzoefu unaonesha kutetereka kwa miradi kama hiyo iliyotangulia.

Kwa mradi wa kununua Ndege, SGR n.k. huko nilikuwa hamsini hamsini na sikuwa msimamo wowote rasmi. Lakini kwa kuwa miradi hii ilishaanza sioni tena kama kuna haja ya kuitazama kwa upande mmoja tu wa hasi.

Zaidi ni kama kupoteza muda maana tayari ipo inaendelea, kwa nini sasa tusijaribu kuiangalia sasa kwa mitazamo chanya, kwamba kwa kuwa tayari ipo sasa nini kifanyike kuanzia hapa kwenda mbele.

Nini kifanyike Ndege tulizokwishanunua ziwe na manufaa badala ya hasara. Kwanini tusijifunze kwa Wenzetu wa Ethiopia? Kama wao wanaweza kwani sisi ni Viazi sana kwamba hatuwezi kufanya chochote?
Hili taifa linapungukiwa hicho kitu. Viongozi hawapendi kuendeleza mazuri ya watangulizi wao. Na hii imetupelekea tunakuwa na miradi mingi ambayo haikamiliki kwa asilimia [emoji817].

Kuna changamoto kubwa Sana aisee kwenye utawala wa huyu mama binafsi naiona. Maana anafika mahala anajitenga na Hayati utadhani she had no hand on the projects. Watu wanasema hovyo mwenda zake amekaa kimya tu.
 
Back
Top Bottom