Uchaguzi 2020 Sioni dalili za Dkt. Magufuli kushindwa kutetetea kiti chake cha Urais uchaguzi wa Oktoba, nimevunjika moyo kama mtumishi wa umma

Uchaguzi 2020 Sioni dalili za Dkt. Magufuli kushindwa kutetetea kiti chake cha Urais uchaguzi wa Oktoba, nimevunjika moyo kama mtumishi wa umma

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Mimi huwa mara zote napenda kusema ukweli. Niwe kazini, barabarani au nyumbani ukweli ndio ngao yangu.

Kwa hakika Mimi sitamchagua Magufuli wala mwana CCM yeyote kwa ngazi yoyote ile katika uchaguzi huu.

Ila kwa hali inavyoonekana Magufuli atashinda tena kwa kura za ndio. Hii imesababishwa na mambo mawili

1. Jinsi alivyominya upinzani (demokrasia).

2. Upinzani kushindwa kumsimamisha mgombea mmoja.

Membe apate kura, Lissu apate kura, Mzee wa ubwabwa naye apate kura. Labda ile sheria ya 50% ingetumika hapa nchini kidogo kampenyo kangeonekana.

Magufuli atashinda , ila nikiwaza kama mtumishi wa umma ninayelipwa mshahara mdogo na ninategemewa naumia sana.

Ndani ya utumishi wangu wa miaka 5 na mwezi mmoja nimeshindwa kujiendeleza kielimu, pesa sina. Nimejenga kajumba pembezoni mwa jini na kununua kigari cha kutolea mkosi ambacho nakitumia weekend tu mara nyingi kwa visafari vya church. Kazini siendi nayo mara kwa mara kwasababu ya kubana matumizi.

Maana naona hali ya watumishi sisi itakuwa mbaya, kuacha kazi tunashindwa kwasababu ya mafao yetu mmeyashikia. Vinginevyo mwezi wa saba mwaka huu ningemwaga manyanga nikalime kwetu Njombe.
 
Huo ndo ukweli, watu hasa wahitimu wa vyuo na Watumishi, wavuvi na wafanyabiashara wanatamani muujiza Lisu ashinde, jipeni moyo maana hata Daudi alimshinda Goliath kimzahamzaha tu, lakini ndiyo sifa ya M/Mungu, huviinua vinyonge nakuwaabisha wenye nguvu😰😰
 
Kila mtu ana wajibu wa kujituma na kuguswa na maendeleo ya kudumu ya taifa lake, tulichelewa Sana!

Nilimsikia Lissu akisema kuwa wale waliotumbuliwa kwa kuwa na vyeti feki atawalipa fidia pia, sijui Sheria alizosomea Ni kwaajili ya kutetea mabeberu pekee!

The bitter truth is that " Magufuli is gonna win again for presidency"
 
1. Magufuli is here to stay.

2. Hata ukiongezewa mshahara your life wont get better but it will become much worse.

3. CCM wana mapungufu mengi but among the choices hakuna mwenye nafuu zaidi ya CCM.
 
Labda kwa hivi
1.jpg
 
Mimi huwa mara zote napenda kusema ukweli. Niwe kazini, barabarani au nyumbani ukweli ndio ngao yangu.

Kwa hakika Mimi sitamchagua Magufuli wala mwana CCM yeyote kwa ngazi yoyote ile katika uchaguzi huu...
Sasa Kama wewe una kazi, una kajumba, una kausafiri sisi wengine ambao hatuna hayo yote mbona hatulii??

unamlaumu bure MAGUFULI wakati wewe ndo unashindwa kujiongeza.

watu hawana hayo yote uliyonayo Ila wanaishi kwa amani bila malalamiko Wala majungu.

pambana na hali yako.
 
Magufuli kiongozi mzuri sana. Nakushauri kura mpe Magufuli ya Urais alafu kura ya ubunge na udiwani wape wapinzani ili tumiliki halimashauri na bunge hapo utakua uwewini. Zaidi kuliko kumkataa kiongozi ambaye anasimamia analoamini Magufuli.
 
Mkimchagua Magufuli ni lazima kodi upande ili apate pesa za kumalizia zile white elephant projects alizoanzisha. Mishahara na kikokotoo mtazidi kula spana.
 
Hii nchi ina wafu wengi, hata mtu anashinda kwa hila na mbinu chafu bado majitu yanakuja kusifu na kuona fahari kabisa!
 
1. Magufuli is here to stay

2. Hata ukiongezewa mshahara your life wont get better but it will become much worse

3. CCM wana mapungufu mengi but among the choices hakuna mwenye nafuu zaidi ya CCM
Kwa ulichosema namba 2, huna akili kabisa, ulaaniwe wewe na kizazi chako.
 
Mkimchagua Magufuli ni lazima kodi upande ili apate pesa za kumalizia zile white elephant projects alizoanzisha. Mishahara na kikokotoo mtazidi kula spana.
Hiyo treni yenyewe dar to Moro mpaka 2025 itakuwa bado haijaanza kazi ila nyumbu zimeahidiwa nyingine mpaka Mwanza
 
Mimi huwa mara zote napenda kusema ukweli. Niwe kazini, barabarani au nyumbani ukweli ndio ngao yangu.

Kwa hakika Mimi sitamchagua Magufuli wala mwana CCM yeyote kwa ngazi yoyote ile katika uchaguzi huu..
Mkuu, miaka mitano umejenga na kununua gari bado unalalamika? Watu wanataka wapate kazi leo kesho wajenge ghorofa. Vumilia tu mkuu hii mitano tena.
 
Watanzania wengi wamemchoka.
Bila polic.
TBC.
NEC.
Jiwe ni jepesi mnooooo
 
Kwa ulichosema namba 2, huna akili kabisa, ulaaniwe wewe na kizazi chako.

unahitaji akili kubwa kuelewa uchumi, unateseka kwa sababu uelewi uchumi ukoje, nia ya kuwepo ni nn, we ukishaona ela nyingi unadhan ndo maisha umepatia
 
Back
Top Bottom