Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 33,679
- 49,841
Nilikuwa kwenye mahusiano na mke wa mtu, ambapo bidada baada ya kunogewa alishauri tuzae mtoto, ambapo atabeba mimba yangu, na kumuhadaa mumewe kuwa ni mimba yake, pia na mtoto atakayezaliwa atatumia jina la mumewe. Kutokana na ushawishi, ilibidi nimkubalie na kwa sasa yuko karibuni kujifungua.
Kinachonitesa katika nafsi yangu kwa sasa, ni hapo mbeleni nitakapokua namuona mtoto, nikijua kabisa ni mtoto wangu lakini sina maamuzi naye, kwa sababu hatokuwa anatumia jina langu, naye pia hatojulishwa kuwa mimi ni baba yake; Inakuwa kama vile, mbegu nilimwaga kwenye mwamba.
Kwa hali hiyo, sioni faida yoyote kuzaa mtoto ambaye hatokuwa chini ya himaya yako.
Kinachonitesa katika nafsi yangu kwa sasa, ni hapo mbeleni nitakapokua namuona mtoto, nikijua kabisa ni mtoto wangu lakini sina maamuzi naye, kwa sababu hatokuwa anatumia jina langu, naye pia hatojulishwa kuwa mimi ni baba yake; Inakuwa kama vile, mbegu nilimwaga kwenye mwamba.
Kwa hali hiyo, sioni faida yoyote kuzaa mtoto ambaye hatokuwa chini ya himaya yako.