Sioni tatizo RCs na DCs kujiita cheo cha wanayemwakilisha eneo husika, kama wanatekeleza majukumu ipasavyo

Sioni tatizo RCs na DCs kujiita cheo cha wanayemwakilisha eneo husika, kama wanatekeleza majukumu ipasavyo

Joined
Oct 1, 2019
Posts
8
Reaction score
2
Katika hafla ya kuwaapisha wakuu wa mikoa, Mhe. Spika amewaasa wakuu wa mikoa kuacha kujiita marais wa maeneo wanayoyaongoza akidai kufanya hivyo kunawafanya kujiona kama Rais.

Binafsi sioni tatizo kujiita jina la unayemwakilisha eneo husika. Lililo la msingi kwao ni kumwakilisha Rais kwa kutoa maamuzi sahihi kwa kuzingatia sheria, taratibu, kanuni na miongozo iliyopo.

Hawatakiwi kubana haki za msingi za wananchi na viongozi walio chini yao kwa sababu nyepesi binafsi. Wanatakiwa kuwa viongozi wanaoshaurika, wasikivu na wanaokubali kukosolewa na watu wenye mtazamo tofauti.

Wakitekeleza majukumu yao ipasavyo wananchi watawaamini na kuona kweli wanamwakilishi ipasavyo mheshimiwa Rais, na ziara za Rais haziwezi kupokelewa kwa mabango mengi ya kero zinazowakabili wananchi wa eneo husika.
 
Huyu Kwa Sasa Hivi Ukimsikiliza kwa Umakini utagundua Hata anachokuwa anakizungumza Hana Uhakika Nacho. Maana style yake ya Kiuongozi aliyokuwa anahitumia Enzi za Mwendazake na Kwa sasa ni Aibu.

Anaongea hata kile ambacho Hakiamini" Ndugai na Kutenda Haki" Wapi na Wapi...Refer issue ya LISSU na Kesi za Hakina MDEE na LEMA Bungeni
 
Umenikumbusha Mtu kusimama na kusema Mkoa wangu! Wananchi wangu! Hivi nani ana mkoa wake? Wananchi wangu wewe ni nani?
'Wapiga kura wangu wanashida kubwa sana ya maji na barabara'
 
SEHEMU YA KWANZA: KUHUSU MKUU WA MKOA

- Ni sehemu ya Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)

- Ofisi za Mkuu wa Mkoa zitakuwa kwenye Makao Makuu ya Mkoa husika

- Mkuu wa Mkoa atawajibika chini ya Waziri wa TAMISEMI

2. DHIMA YA KAZI HII

Kuhakikisha kuwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii yanapatikana kutokana na huduma bora za ushauri na uratibu ambazo zinajenga mazingira bora kwa Serikali za Mitaa na wadau kutoa huduma inayotarajiwa.

3. MAJUKUMU NA KAZI ZA MKUU WA MKOA

- Kuhakikisha uwepo wa Haki na Sheria kk mkoa

- Kuongoza na kusimamia operesheni za Maafa na Kufariji

- Kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa(RCC), Mkuu wa Mkoa atawajibika kufanya jitihada za kuhakikisha kutimizwa kwa sera za serikali juu ya Mkoa husika.

- Kufanya yale yote yatakayosaidia kuimarisha ulinzi na usalama wa mkoa kwa ushirikiano na serikali za mitaa.

4. ELIMU

Mkuu wa Mkoa itampasa awe na Elimu Ngazi ya Shahada(Degree) au inayoshabihiana na hiyo kutoka kwenye Taasisi ya Elimu inayotambulika.

5. UELEWA

Mkuu wa Mkoa atapaswa awe ni mwenye ufahamu kuhusu Utawala wa Sheria, Utawala bora, Kanuni za Haki Asilia (Natural Justice), Sera na taratibu zake, Uongozi na Utawala pamoja na masuala yote ya msingi ktk utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo.

6. UJUZI

Kimsingi Mkuu wa Mkoa anapaswa kuwa na stadi zote za uongozi;

Ujuzi wa kujenga umoja, ujuzi wa kutatua changamoto, ujuzi wa kutoa ushauri nasaha, ujuzi wa maridhiano, ujuzi wa kuhimili msongo/mihemuko, sambamba na ujuzi kuhusu mahusiano ya umma na uwezo wa kuzungumza vizuri mbele za watu.

7. SIFA BINAFSI

Aonyeshe uwezo wa kutunza siri, kufanya maamuzi yenye tija, kufanya kazi pasipo mashinikizo, uelewa kuhusu mwenendo wa siasa na tamaduni za jamii, awe na heshima, mbunifu, mtenda haki, bila kusahau kuheshimu miiko ya kazi.

8. UZOEFU

Ni lazima Mkuu wa Mkoa awe ni mtu mwenye uzoefu kuhusu masuala ya utawala/siasa usiopungua Miaka 10.

9. MSHAHARA

Mkuu wa Mkoa atalipwa kiwango cha mshahara kwa taratibu zilizoainishwa na Ofisi ya Utumishi (kwa sasa salary scale yake ni LSS(P) 4).

Katika hayo umeona wapi kuwa hawa ni wawakilishi wa Rais,wawakilishi wa rais kwa maana ya kuteuliwa hao wapo wengi tu,lakini kwa maana ya kuutumikia umma kila mfanyakazi katika ofisi ya umma ni mwakilishi wa Rais.
Ni majigambo tu yasiyokuwa na maana.
 
Ah, sawa. Sasa na wewe tukuite Mbowe sisi nakamanda wa Iringa kwa sababu weye ni mwenyekuti wetu ingawa umebwagwa Ubunge puu?
 
Huwezi ku
Ah, sawa. Sasa na wewe tukuite Mbowe sisi nakamanda wa Iringa kwa sababu weye ni mwenyekuti wetu ingawa umebwagwa Ubunge puu?
Kujiita cheo ambacho si chako nafikiri si sawa,unless unataka kutumia tittle hio kutishia watu,au kwa maslahi yako au kikundi.....
 
Kigamboni tuliambiwa kuanzia diwani,katibu tarata mpaka mkuu wa wilaya ni maraisi wa Kigamboni na wanafanya wanachotaka
 
SEHEMU YA KWANZA: KUHUSU MKUU WA MKOA

- Ni sehemu ya Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)

- Ofisi za Mkuu wa Mkoa zitakuwa kwenye Makao Makuu ya Mkoa husika

- Mkuu wa Mkoa atawajibika chini ya Waziri wa TAMISEMI

2. DHIMA YA KAZI HII

Kuhakikisha kuwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii yanapatikana kutokana na huduma bora za ushauri na uratibu ambazo zinajenga mazingira bora kwa Serikali za Mitaa na wadau kutoa huduma inayotarajiwa.

3. MAJUKUMU NA KAZI ZA MKUU WA MKOA

- Kuhakikisha uwepo wa Haki na Sheria kk mkoa

- Kuongoza na kusimamia operesheni za Maafa na Kufariji

- Kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa(RCC), Mkuu wa Mkoa atawajibika kufanya jitihada za kuhakikisha kutimizwa kwa sera za serikali juu ya Mkoa husika.

- Kufanya yale yote yatakayosaidia kuimarisha ulinzi na usalama wa mkoa kwa ushirikiano na serikali za mitaa.

4. ELIMU

Mkuu wa Mkoa itampasa awe na Elimu Ngazi ya Shahada(Degree) au inayoshabihiana na hiyo kutoka kwenye Taasisi ya Elimu inayotambulika.

5. UELEWA

Mkuu wa Mkoa atapaswa awe ni mwenye ufahamu kuhusu Utawala wa Sheria, Utawala bora, Kanuni za Haki Asilia (Natural Justice), Sera na taratibu zake, Uongozi na Utawala pamoja na masuala yote ya msingi ktk utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo.

6. UJUZI

Kimsingi Mkuu wa Mkoa anapaswa kuwa na stadi zote za uongozi;

Ujuzi wa kujenga umoja, ujuzi wa kutatua changamoto, ujuzi wa kutoa ushauri nasaha, ujuzi wa maridhiano, ujuzi wa kuhimili msongo/mihemuko, sambamba na ujuzi kuhusu mahusiano ya umma na uwezo wa kuzungumza vizuri mbele za watu.

7. SIFA BINAFSI

Aonyeshe uwezo wa kutunza siri, kufanya maamuzi yenye tija, kufanya kazi pasipo mashinikizo, uelewa kuhusu mwenendo wa siasa na tamaduni za jamii, awe na heshima, mbunifu, mtenda haki, bila kusahau kuheshimu miiko ya kazi.

8. UZOEFU

Ni lazima Mkuu wa Mkoa awe ni mtu mwenye uzoefu kuhusu masuala ya utawala/siasa usiopungua Miaka 10.

9. MSHAHARA

Mkuu wa Mkoa atalipwa kiwango cha mshahara kwa taratibu zilizoainishwa na Ofisi ya Utumishi (kwa sasa salary scale yake ni LSS(P) 4).

Katika hayo umeona wapi kuwa hawa ni wawakilishi wa Rais,wawakilishi wa rais kwa maana ya kuteuliwa hao wapo wengi tu,lakini kwa maana ya kuutumikia umma kila mfanyakazi katika ofisi ya umma ni mwakilishi wa Rais.
Ni majigambo tu yasiyokuwa na maana.
Msalimie TumbiliwaGombe
 
Katika hafla ya kuwaapisha wakuu wa mikoa, Mhe. Spika amewaasa wakuu wa mikoa kuacha kujiita marais wa maeneo wanayoyaongoza akidai kufanya hivyo kunawafanya kujiona kama Rais.

Binafsi sioni tatizo kujiita jina la unayemwakilisha eneo husika. Lililo la msingi kwao ni kumwakilisha Rais kwa kutoa maamuzi sahihi kwa kuzingatia sheria, taratibu, kanuni na miongozo iliyopo.

Hawatakiwi kubana haki za msingi za wananchi na viongozi walio chini yao kwa sababu nyepesi binafsi. Wanatakiwa kuwa viongozi wanaoshaurika, wasikivu na wanaokubali kukosolewa na watu wenye mtazamo tofauti.

Wakitekeleza majukumu yao ipasavyo wananchi watawaamini na kuona kweli wanamwakilishi ipasavyo mheshimiwa Rais, na ziara za Rais haziwezi kupokelewa kwa mabango mengi ya kero zinazowakabili wananchi wa eneo husika.
Huyo speaker amelewa ukuu. Yaani ameshindwa kuelewa wanajiita marais kwenye maeneo yao kwa msingi gani? Huyu anatakiwa kurejeshwa kwenye akili.
 
Back
Top Bottom