Sipendi kukosea kuandika haya maneno kwa ufasaha

Evelyn Salt

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2012
Posts
70,916
Reaction score
141,437
Sipendi kuchanganya l na R katika uandishi, muda mwingine inabidi niepuke kutumia baadhi ya maneno ili nisiyakosee, naomba kueleweshwa haya maneno yanaandikwaje kwa ufasaha.

Je ni lipi sahihi
kachumbali au kachumbari?
Kulogwa au kurogwa
Mkwala au mkwara?

Nitaongezea nitakayokumbuka.
 

Sahihi
Kachumbari
Kurogwa
Mkwara
 
Shule hufundisha kuandika inavyotakiwa, lakini kuna mifala pakuweka L wao huweka R. Na penye R wao huweka L lakini wakiwa kwenye exam huandika sahihi kabisa.
 
tafsiri?
tafasiri?
tafasili?

fasili?
fasiri?
nipe usahihi hapo
 
Kusali / kusari??
au
Kuswali / kuswari??

(Nikiwa na maana kitendo cha kufanya ibada)
 
ongeza pia

mkristo?
mkristu?

tafakuri
tafakari?
 
ongeza pia

mkristo?
mkristu?

tafakuri
tafakari?
Mkristo/ mkristu, yote ni sahihi. Nimeona kristu hutumiwa zaidi na wakatoliki, na wengine husema kristo.

Tafakuri ni sahihi
Tafakari ni sahihi
Ni maneno tofauti kwa uelewa wangu, tafakuri ikiwa ni funzo/somo unalolipata katika au baada ya tafakari (kufikiri kwa kina).
 
ongeza pia

mkristo?
mkristu?

tafakuri
tafakari?
Tafakari na tafakuri nnavojua mie yote ni maneno sahihi ila maana zake ni tofauti.
Tafakari ni kitendo cha kuwaza na kuwazua
Tafakuri ndio hayo uliyoyawaza sasa, yani tafakuri imetokea baada ya kutafakari (sijui nipo sawa!!)

Mkristu na mkristo hapo nadhani ni utofauti wa namna ya kutamka kati ya sehemu na sehemu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…