Sipendi kuona mume wangu anakosa hela, huwa nampa hela, je inatokea kwa wanandoa wote?

Sipendi kuona mume wangu anakosa hela, huwa nampa hela, je inatokea kwa wanandoa wote?

Unajua kutetea nakuifanya upya ndoa yako.wewe niwatofauti lakini usijali kwani ninyi ni mwili mmoja ndoto zako nizake na zake ni nizako pia. Hakika wewe niwapekee kama nimapenzi ya mungu utatimiza tu ndoto zako

Sent using Jamii Forums mobile app
Wow wow Nimependa hapo "Kama ni mapenzi ya Mungu utatimiza tu ndoto zako" asante mpendwa.Hii amani niko nayo hata naonaga bado wakati wa Mungu haujafika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una watoto wadogo, ni bora ungewafungulia acc yao maana unasema huhitaji kwa ajili ya shule maana bado wadogo that's wrong
Hata wewe kuna wakati ulikuwa mdogo kwa hiyo fanya hima usisubiri wakue ndio uanze kuhangaikia mikopo.
Weka sasa wafaidi baadae.

Kama unaona yako hayaendi bora uweke kwa ajili ya watoto.

Yeye ni hustler mwache ahangaike wewe weka zako
 
Mpendwa nimekuelewa vizuri ila naomba tu utambue kwamba hizi hela nampa mume wangu sizijutii na sijawahi kujutia kumpa na Mungu shahidi ninampa kwa moyo mmoja na ndani yangu nina amani.unaposema kumchoka mume wangu sijawahi kuwaza na sintakuja kumchoka inshort naonaga Mungu kanipendelea sana kunipa yeye.he is such a blessing to my life .kwenye maisha naamini katika amani na sio kitu kingine chochote hata kama hatuna kitu but as long as kuna amani mimi ndo kitu kikubwa kwangu.Hakuwahi nikosesha amani.pakiwa na shida mahali tunaweka sawa kwa upendo .yeye Ndio chanzo cha amani yangu ndo maana sitaki kabisa akose amani niko tayari kufanya kila ninaweza arelax.

Sent using Jamii Forums mobile app
Too good to be true
 
Hapo emoj uko unafanya yale Mwenyezi Mungu aliyowapa wanandoa waishi kwa upendo na kusaidiana. Lakn naliona tatizo lako ukilikuza litaleta chanzo cha matatizo. Kama una ndoto yako mshirikishe mmeo then mtashauriana na sio kuanza kufikiria vitu vya umimi labda kama unaona anaweza kungeuka. Nakuombeni muishi kwa kushirikishana mwambie nina wazo hili na hill nataka nifanye hivi he will support you. Lakini ukianza mimi nifanye kimya kimya sio dhana ya ndoa yenye maelewano.

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante mpendwa.ndoto zangu nilishamuambia hata kabla hatujaingia kwenye ndoa.sina nia mbaya kushare hapa kwamba nahitaji kubadilika hapana maana ndani yangu kweli nina amani na ninachofanya.nimelileta kama wanandoa tulione kwa pamoja na walio kama mimi.kama ni kubadilika ningeshabadilika maana ukimwambia mtu ni wachache sana wanaona its ok wengi wanakimbilia Negative tu.kuleta hapa tuko wengi wanandoa na wasomi .nimeleta nikutane na waoniona positive na walio kama mimi.otherwise nasema tena Asante sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
yaani nilivyoona unashukuru kwa kupata mume ambaye sio mlevi nimeacha kusoma kabisa.....
 
Una watoto wadogo, ni bora ungewafungulia acc yao maana unasema huhitaji kwa ajili ya shule maana bado wadogo that's wrong
Hata wewe kuna wakati ulikuwa mdogo kwa hiyo fanya hima usisubiri wakue ndio uanze kuhangaikia mikopo.
Weka sasa wafaidi baadae.

Kama unaona yako hayaendi bora uweke kwa ajili ya watoto.

Yeye ni hustler mwache ahangaike wewe weka
Mpendwa asante. Ila tuna joint acc.yaani kiufupi mpendwa hakuna hela inayotumika vibaya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Najua hutumii vibaya ila angalia future ya watoto I mean waandalie usisubiri kumekucha
All the best
 
Ndoa ni yenu wawili lakini kila mmoja anatimiza malengo yake kivyake cha kushangaza zaidi wewe upo busy kumsuport mwenzio mbona yeye hakusupport?hakuna hata sehemu moja umesema yeye naye alitoa pesa akakupa ili ufanye kitu Fulani..ni wewe tu ndio mtoaji..kweli huu ndio upendo wa mshumaa

Sent using Jamii Forums mobile app
Mpendwa ananisaport but mimi akinipa pesa namwambia no.yaani nikichukua hela kutoka kwake ujue kweeeli nahitaji hizo hela.but mara nyingi anipata naongea nae mpaka anaielewa kwamba aendelee kupanua biashara zaidi na hata idea zingine za biashara hii yangu itafanyika tu online hivyohivyo but kwa sasa afanye yeye.na nakuwa na amani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
You are the real defination ya Mke mwema.Unaongozwa na upendo wa dhati na siyo upendo wa vitu.Mungu aendelee kukubariki.
 
Habari wapendwa.Naomba kwa wale wanandoa mnisaidie hapa kama ni kawaida kwa wanandoa ama ni nini?.

Namshukuru Mungu tulipata kuoana na mume wangu ,kweli Maisha ni mazuri tunafurahia ndoa yetu na watoto wetu pia. Namshukuru Mungu pia amenipa mume ambaye sio mlevi wala mpenda starehe yaani inshort hela hachezei anafanyia vitu vya maana sana.

Kuna wakati tulifungua joint account ilivyofika kiwango tulikuwa tunataka tukakubaliana akazitoa na akafanyia kazi nzuri sana kwa uaminifu. Na pia mara nyingi nikiwa na hela ambazo najua sizitumii kwa muda huo nampa anafanyia biashara zake baadaye nikihitaji anazirudisha.

Kabla na baada pia ya kuolewa nina ndoto nyingi za mimi kufikia level fulani na nilimshirikisha pia na akalifurahia.

Sasa tatizo linakuja kwamba kweli mpaka leo karibia miaka minne sasa hakuna kitu nimefanya katika kuachieve ndoto zangu, nimepiga kihatua kidogo sana, Hela naweka akiba inafikia kabisa kiasi nataka kutimiza malengo yangu but najikuta tu nimempea mume wangu bila yeye kuniambia nimsaidie.

Yaani niko hivi sipendi kuona mume wangu hana amani au akiwaza wapi apate hela au akiniambia hasara aliyopata katika business muda mwingine nachukua card yangu ya bank naenda kutoa hela zote nampa kwa kumwambia hii hela siko na kazi nayo na naona niweke huko kwa business yako so zitumie tu kule usirudishe. (But lengo langu ni kutaka tu ajisikie vizuri pamoja na hasara aliyoipata hela nyingine imekuja) Na ukimpa anapeleka pale kwa uaminifu kabisa.

Hela ya matumizi akinipa kweli namrudishia sijui kwanini but naona tu kwanini nichukue hela wakati mahitaji madogomadogo ya nyumbani naweza toa hela na vile bado hatujaanza kusomesha so mahitaji sio mengi si bora hiyo hela aendelee kuizungusha kwa biashara.

Basi naona tu hivyo na nakuwa na amani. Weekend hii ilikuwa nikachukue frame ya kufanyia kabiashara kangu (hili hata sikumwambia kwamba nimeshapata frame) but juzi akaniambia habari ya kiwanja alichokiona mjini sehemu nzuri sana na kina title na alipokuwa anaongea anaonesha kabisa kwamba we real need that land.

Hakuniambia toa hela wala nini but mimi "emoj mwenyewe nikamwambia niko na pesa nikaenda bank nimetoa hela zote hadi za mtaji wa biashara yangu ninayofanya online nimempa. Nimebakiwa tu na 100k za kuniweka hadi mwisho wa mwezi nianze upya kusave .

Wapendwa jamani hii ni kwangu tu ama ni kwa wanandoa wote???.
Sifanyi chochote kuachieve my dreams but niko na Amani sana ndani ya moyo wangu kwasababu my husband is so happy napenda tu kumwona ana furaha sitaki kabisa apate stress kisa hela au kisa mambo yake hayaendi vizuri.

Namuombea sana na pale naweza kutoa pesa natoa sana na pale pa kumencourage namuencourage sana na kwa mimi hakuna kitu mimi nimejifanyia and am happy.hii itakuwa ni nini??? [emoji23][emoji23][emoji23].

Sent using Jamii Forums mobile app
M/Mungu naomba nipatie mke kama uyu!!

[emoji125] [emoji125]

Sent from my iphone 6s using Jamii Forum Mobile app
 
Uko na maximum care juu ya familia. Na ndio kitu kinatakikana japo kuna haja ya kujifunza baadhi ya shughuli za kibiashara ili uwe na experience na kipato zaidi.
 
Ndoto zilikuwa zako ulipokuwa single sa hivi umeolewa ni zenu coz ninyi sasa ni mwili mmoja so kama kuna vitu viko achieved those are your dreams satop saying hujaachieve dreams zako

Umesema kila ukimpa mumeo anafanyia kitu mlichopanga kwa uaminifu na wewe uko happy hujihisi kupungukiwa chochote and your family is happy what is it that you need to worry???
Dah kwa madini haya mm naomba hata unifanye mchepuko wako.....najua sitoki patupu wahenga walinena mgagaa na upwa hali wali mkavu!
 
Wala si ujinga! nadhani hiyo unayofanya ndo dhana ya mwili mmoja.Yaani chake, chako! endelea tu na lifestyle yako kama unafeel amani moyoni mwako.Kila lakheri.
 
leo nimeamka na kucheka tu! sijui why nimecheka! ila umesema mwenyew mumeo anaifanyia biashara kwa uaminifu bas we endelea kumpa tu mamy !... ila kwa mie mhenga.... kuna shida sehem...why kila mara alie lie shida kwako!hajawah kukuambia mke wangu mwezi huu tumeingiza faida kias hiki! au ni mm tu sijakuelewa!

anywys umepata mume mtaftaj pambana muongeze kipato huna haja ya kujitenga nae! pls waweza kuja share nasi hapa mwaka 2020 biashara za mumeo km hutojali! am very positive to you my dear emoji!! ili na sisi tulioshindwa kushare biashara na waume zetu tujue tunakosea wapi!

kuhusu wewe kutoarchive ur dreams wala usihofu unaachieve kupitia mgongo wa mumeo kitu ambacho ni afya sana kwa ndoa zetu !hilolisikutie hofu mamy

............nimecheka sana sana .....
demi
Neybright
Heaven Sent
espy
Nalendwa

mkuje mfundwe huku
[emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] dahhhh Mimi ilinitokea aiseeee nilimpenda mwanaume alikuwa nakazi akaja akasimamishwa kazi mpaka akiumwa ni juu yangu kuanzia chai ya asubuhi ,mchana,jioni nimimi maji anayooga Mimi akienda kutafuta Kazi ela ya nauli ni kwangu Jamani kiukweli nilimpenda sana ikaja tokea kanipa mimba nililia kwababu Mimi mpaka babu akatupangia pakukaa kitanda,kijiko,uma,madumu ya maji ,godolo majiko ,vyakula ikawa Na mimba yangu mwanaume anaondoka anaenda kutafuta riziki akirudi hana kitu Mimi niliweka moyoni mpaka kesho hakuna ndugu yangu hata mzazi wangu aliejua nilikuwa nalala njaa siku hamna chakula natoka naenda nyumbani najifanya naenda kusalimia maana najua nikiondoka nabebeshwa vitu kiukweli babu yangu ananipenda sana nakumbuka Na mimba mwanaume aliondoka siku 3 yupo kwao mlandiz ameniachia 2000 tu Jamani nilikuwa kimya nikitoka nacheka namajirani nikiingia kwangu nalia nikichoka nalala nilinunua unga nilikuwa nikisikia njaa nakologa uji nakunywa mpaka anarudi siku naenda kujifungua hana ela alikimbia aibu alinitelekeza Na mtoto toka siku nazaaa nikaludi akaja akaomba msamaha akidai aibu alikimbia familia isingemuelewa hana ela namimi nimefanyiwa operation kubwa ,Jamani baada ya kupata Kazi mwanaume alinitelekeza Na mtoto Wa miez 3 nililudi nyumbani kwababu sitasahau mpaka unaingia kaburini Watoto Wa babu mashangazi walinitesa nawananitesa Mwanangu namimi tulikuwa tunanyimwa chakula baba mtoto ukimtafuta anakutukana,mtoto akiumwa anamwambia naakifa utamla nyama Jamani kiukweli alisahau yote niliomfanyia mpaka Leo Mwanangu anamiaka 8 ata ada ya mtoto au hata pencil hajui ya baba yake bola uwekeze

Kwa mwanao sio mwanaume jamani[emoji24] [emoji24] [emoji24] [emoji24] [emoji24] [emoji24] [emoji24] huyu Dada namhurumia Jamani akumbuke kunakifo hivi mungu akimchukua Watoto hujawawekea misingi kuna ndugu pia wakija kufilisi Mali utalia Na nani pia kumbuka uyo mwanaume ni binadamu akija kubadilika utaishije imeandikwa alaaniwae amtegemeaye mwanadamu katika bible Dada jisimamie Mimi sio baba mtoto tu nishakuwa Na uhusiano mwingine mwanaume anashida unajitoa Jamani mwisho Wa siku akipata kwake huna thamani ila wakiwa Na shida niwapole sana katika hao wawili sitopenda mwanaume eti mpaka nimsaidie ni ngumu akomae nahali yake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom