Sipendi - Special thread

Sipendi - Special thread

Sipendi tabia ya watu wanaoumwa kikohozi, wakiwa kwenye basi au umati wa watu kukohoa huku wanajifunika kwa kiganja cha mkono badala ya leso.
 
Kuna watu wana tabia za ajabu sana. Unakuta mtu anakuja kukulilia shida, anaomba umkope pesa huku akiahidi atarudisha tu mara pesa yake itakapotoka.

Unakubali na pesa unampatia kwa makubaliano kuwa atalipa mara tu pesa yake itakapokuwa tayari. Muda wa kukulipa unafika mara anaanza stori za... Oh unajua najenga.... Pesa nimepeleka kwenye ujenzi... Mara ooh.. Kuna dogo nimemlipia ada.... Mara tena... Oh unajua mama mgonjwa..... Mara nilipata msiba!! Vijisababu kibao ambavyo hata hukutegemea na havikuwa ktk makubaliano yenu.

Matokeo yake sasa, anaanza kulipa pesa kwa mafungu tena kwa mpesa au tigo pesa na makato juu.... Mwishkni unakuta pesa yako yote ni kama umeitoa kafara! Mishoni kiasi kidogo kinabakia kwake na hana uwezo wa kulipa huku akiendelea kuleta vijisababu kibao.

Tubadilikeni jamani. Hizi tabia zina boa sana.

We umekuja kukopa halafu iweje wakati wa kulipa unakija na stori kibao. Lipa pesa ya watu hakuna mtu yupo interested kujua stori zako au matatizo yako! Timiza ahadi kwanza..... Kila mtu ana shida zake. Na ieleweke kuwa mtu akikukopa pesa haina maana kuwa hakuwa na matumizi na pesa hiyo, ila tu ni jambo la huruma na kukuamini.
Dawa yao ndogo. Mwambie akulipe Mara atakapopata. Hatarudi. Baada ya miaka 3 utajikuta hakuna MTU atakaye kuja kukopa kwako.
 
Cpendi unamtongza mdada alaf anakupga piga chenga hatak kukupa kipoch manyoya,
 
Sipendi tabia ya watu kukojolea kuta za nyumba.
 
Sipendi mgomo wa madereva... Nilitembea km 50 kutoka home hadi job ( wasirudie tena)

umelionaje lakini zoezi? ulikuwa na muda gani hujafanya mazoezi ya kutembea? binafsi nawashukuru wagomaji na naomba wagome tena!
 
Sipendi tabia ya baadhi ya wana jf members kuwa na ID zaidi ya 1.

kama akina nani hao hebu wataje tuwaseme ili wajirekebishe upesi na wawe kama sisi wenye kutumia id moja tu twenty four seven au siyo!
 
Sipendi tabia ya mtu anashikashika pua kila saa halaf akikuona anakupa mkono aaghhhh
 
Siipendi tabia ya wapangaji wanaopenda kukaa karibu na chooni mpaka wengine tunahairisha kwenda choooni!
 
Sipendi ID za jf huwezi kujua men or jike ni yupi
Badilikeni jamani wengine mnakosa bahati ya kutongozwa ohooooo

kwa mfano naomba kujua wewe ni mwenzetu au mwenzao? hapa namaanisha kijinsia!
 
yaani inakera kwakweli! vimaswali maswali havina mbelewala nyuma kuchoshana tu

acha kuzuga, kuna mwanamke ambaye hapenda kutongozwa? wengi mnapenda ila hamjionesh kuwa mnapenda!
 
Sipendi wanaume wanaovaa suruali zenye rangi kama upinde wa mvua.
 
Back
Top Bottom