Siri gani ambayo huwezi kumwambia mtu yeyote kwenye maisha ya kweli lakini utaisema humu kwa kutumia anonymity? ?

Nimesha lala na mwanaume ambaye nampenda ila yeye hakujua kama nampenda na sikuwahi kumwambia yeye wala mwingine yeyote.

Niliiba kalmati ndani ya kabati na San vita kwa baba taibali bila kulipa. Sikuwahi mwambia yeyote.

Najua kuendesha gari manual ila nilipokuwa na baby hajui kuendesha manual nikamwambia sijui hata kuendesha gari na hadi kesho sijawahi mwambia. Kila nikienda mahali tuonane nachukua uber au bajaji. Nikiwa kwenye misele yangu nabadili gear kama Michael Schumacher.

Kasie Matata.
 
Thanks mkuu kwa kuelewa kilichoandikwa
 
Sina akili ila machoni mwa wengi na mwonekano wa msomi na mwenye hekima tele, yote haya kwasababu ya ulimi wangu na maneno yanayoendana na vitendo vyangu hivyo kuweza kuficha ujinga wangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…