Nimemaliza kufanya utafiti wangu siku mbili zilizopita, nafikiri ni vizuri baadhi ya mambo machache nikayaweka hadharani ili wale vijana wetu wenye nia yadhati ya kujikwamua kimaisha waweze kuitumia. Ukiwa una kianzio cha tshs. 80,000/= na ukaamua kurudi kijijini kulima, na kwa kuanzia ukaanza na heka moja ambayo ukajitahidi kuihudumia vizuri pamoja na mifugo michache kama sungura kuku, bata, njiwa n.k. Mwaka unaofuata ukaongeza heka tano zaidi na mifugo kama mbuzi, ng'ombe, kitimoto(kwa wale ambao imani yao haiwazuii) na mwaka unaofuata ukaongeza heka kumi zaidi ukawa na jumla ya heka kumi na sita, utafiti umeonyesha ndani ya miaka mitano huyu kijana atakuwa na fuso moja, gari ndogo ya kutembelea na nyumba nzuri ya kuishi yeye na familia yake. Zao ambalo linashauriwa kuanza nalo ni ufuta, lakini ni muhimu kulima chakula kidogo na mboga. Nakaribisha mjadala kwa ajili kuboresha zaidi.