Siri ya 4th July na vifo vya waasisi wa taifa la Marekani

Siri ya 4th July na vifo vya waasisi wa taifa la Marekani

Habari za jioni wanajukwaa bila kupoteza muda niende kwenye mada kama kichwa cha uzi kinavyosema
View attachment 787245

Kwa ufupi taifa la marekani lilipata uhuru wake kutoka kwa wakoloni wa kiingereza Julai 4,1776, ila tarehe hii ilinishangaza sana kutokana na mtiririko wa matukio ya waasisi wa taifa hili ambao walifanikiwa kushika urais tukiachana na George washington ambaye ndio alikuwa Rais wa kwanza wa taifa hilo, na marais hao ni kama ifuatavyo

1.JOHN ADAMS
View attachment 787218

Huyu alikuwa rais wa 2 wa Marekani na alitawala kati ya mwaka March 4, 1797 hadi March 4, 1801 na kufariki July 4, 1826 ambayo ndio ilikuwa maazimisho ya miaka 50 ya kutangazwa uhuru wa nchi ya marekani na alifariki kwa tatizo la moyo.

2.THOMAS JEFFERSON
View attachment 787221

Huyu alikuwa Rais wa 3 wa marekani na alitawala kuanzia March 4, 1801
March 4, 1809 na kufariki July 4, 1826 siku ambayo pia ilikuwa yakuadhimisha miaka 50 ya uhuru ikimaanisha hawa wawili yaani adams na jefferson walifariki siku moja tena kwa homa za muda mrefu tu!!

3.JAMES MONROE
View attachment 787224

Huyu alikuwa Rais wa 5 wa marekani na alitawala kuanzia March 4, 1817-March 4, 1825 na kufariki July 4, 1831 nyumbani kwa binti yake huko New york tena kwa maradhi ya kawaida tu!!

4.JAMES MADISON
View attachment 787225

Huyu alikuwa Rais wa 4 wa marekani na alitawala kati ya March 4, 1809 hadi
March 4, 1817, tofauti na hao wa hapo juu Madison akiwa amebakiza siku 6 tu ili afikie 4th july ili akamilishe seti kama wenzake waliomtangulia alikuwa na changamoto ya kiafya iliyopelekea awe na matatizo ya kiakili na akiwa amezidiwa sana alipewa dawa ya kumsaidia kumsogeza masiku ila alikataa kunywa ndipo alifariki june 28 1836 ila inaonekana nia yao ilikuwa afike pia tarehe 4 kama wenzake.

Baada ya kusoma ulinganifu huu nimeona nilete mada hii kwa Great thinkers mnisaidie je vifo vya waasisi wa taifa hili yaani 3 kati ya 5 kufa tarehe 4 july na 1 siku chache kabla, je ni kwa bahati mbaya tu au kuna siri nyuma ya pazia?? Na je ni kwanni huyu madison aligoma kunywa dawa za kumsogeza hadi tarehe 4?? Je kuna conspirancy nyuma ya vifo hivi kuangukia tarehe ya kuadhimisha uhuru wa marekani??

Naomba kuwasilisha

NB Moderator JamiiForums Mod Two Reserved Invisible nawashukuru sana kwa kumoderate uzi mapema

Karibuni wanajukwaa wote
mkuu wewe ni mzawa Wa wapi?
 
mkuu wewe ni mzawa Wa wapi?
Kma mzaliwa nimezaliwa Nairobi ila baba mkurya mama muha.... So utaamua kwetu wapi either buyungu ama kiabakari ama ruaraka/kenya ila tunahoji tu masuala haya hta kma hayatuhusu ila kuongeza maarifa tu hakuna jingine
 
Back
Top Bottom