Siri ya mkopo wa Korea kwa Tanzania mpaka 2070

Siri ya mkopo wa Korea kwa Tanzania mpaka 2070

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
15,835
Reaction score
23,776

xxxxxxxxxxxxxx.jpeg

Mkopo Tanzania uliopata huu wa masharti nafuu una riba ya asilimia 0.01, unalipwa kwa miaka 40, na una fungate (grace period) ya miaka 25. Yaani unaanza kulipa baada ya mwaka wa 26.

Tanzania haijagawa chochote kubadilishana na mkopo nafuu kutoka Korea kama wasio-wazalendo wanavyopotosha.
Tanzania inapata mkopo wa masharti nafuu kupitia Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo (EDCF) kwa mara ya tatu.
  1. Mara ya kwanza dola za kimarekani milioni 733 (2014-2020);
  2. mara ya pili dola bilioni 1 (2021-2025).
  3. mkopo wa tatu ni dola bilioni 2.5 (2024-2028)
Maana yake ni kwamba , 2024 tumechukua Mkopo, 2060 ndio tutaanza kulipa na 2064 tuwe tumemaliza.

Rais atakayekuja kulipa huu mkopo Yupe Darasa la Sita shule ya Msingi, na waziri Fedha wa wakati huo huenda hajazaliwa.

Wazungu wanaona mbali kuliko Tai, wanakupa mkopo wa muda mrefu, wanakopesha nchi tofauti tofauti na marejesho miaka tofauti tofauti maana yake wanawahakikishia watoto wao, wajukuu zao na vitukuu vyao hata visipofanya kazi, hata wakiinhgia vita na Korea kaskazini kwa miaka 20 mfulilizo bado wana maokoto toka nchi zilizokopeshwa.

WANYONGE WANAWAZA ILA HAWASEMI HAYA :-
Viongozi/Marais 48 Korea-Africa Summit. Kwanini wanakubali kuitwa na mtu mmoja tu wakati sisi tuna umoja wa Afrika, huyo aliyewaita si angeweza kuja kwenye makao makuu ya African Union?
 
Hivi hii mikataba why huwa haiwekwi wazi kila mtu akajisomea na kuona?

Yaani kungekuwa na namna ya ku access na kujisomea au website hivi au mfumo ambao mtu yoyote anaweza kusoma hizi contracts?

Hizi kelele zisingekuwepo kila mtu angekuwa na majibu sahihi, kila mnavotoka mafichoni mnakuja na boko na kupishana na wengine waliotoa maelezo pia.
 
Life is not easy like that way sisi ni akina nani mpaka tuwe tunapendelewa ivo acheni kupotosha
 
Hivi hii mikataba why huwa haiwekwi wazi kila mtu akajisomea na kuona?

Yaani kungekuwa na namna ya ku access na kujisomea au website hivi au mfumo ambao mtu yoyote anaweza kusoma hizi contracts?

Hizi kelele zisingekuwepo kila mtu angekuwa na majibu sahihi, kila mnavotoka mafichoni mnakuja na boko na kupishana na wengine waliotoa maelezo pia.
Serikali haiweki mikataba wazi kwakuwa inasemekana Vibao vya spidi barabarani mpaka leo hatujaweza kusoma kuwekewa mikataba ni kutuchosha.
Naona ibaki wawe wanasaini na kusoma kwa niaba yetu.
 
Rais atakayekuja kulipa huu mkopo Yupe Darasa la Sita shule ya Msingi, na waziri Fedha wa wakati huo huenda hajazaliwa.

Wazungu wanaona mbali kuliko Tai, wanakupa mkopo wa muda mrefu, wanakopesha nchi tofauti tofauti na marejesho miaka tofauti tofauti maana yake wanawahakikishia watoto wao, wajukuu zao na vitukuu vyao hata visipofanya kazi, hata wakiinhgia vita na Korea kaskazini kwa miaka 20 mfulilizo bado wana maokoto toka nchi zilizokopeshwa.
Umenipa tafakuri, bado natafakari.
 
Dah hii ni hatari sana kwa taifa letu cc km wazalendo tunaumia sana au mnataka hii nchi kwenye machafuko hyo mikopo

Mbona sioni faida zake sasa kulikuwa na maana gani kuingia mkataba na dp world kama matatizo hayajaisha na bado tunakopa.???
 
Back
Top Bottom