Siri ya Mungu mwenye wivu; kwanini Mungu kuwachukua mapema wale tunaowasifu na kuwategemea kupitiliza?

Siri ya Mungu mwenye wivu; kwanini Mungu kuwachukua mapema wale tunaowasifu na kuwategemea kupitiliza?

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Kama kuna hatari unaweza kumsababishia ndugu, rafiki, kiongozi au yeyote unayemuhusudu ni kumsifia na kumtegemea kupitiliza.

Mungu mwenye wivu huwa anawasaidia wanadamu wanaowategemea kupitiliza wenzao tena kuwapa sifa kinafiki au kihalali kwa kuwapumzisha makaburini mapema wategemewa hao.

Hii ndio sababu kuna malalamiko mengi mbona huyu mpendwa, mchungaji, kiongozi, ndugu amendoka mapema jamani. Tena wengine wanalaumu kwa nini asingeondoka flani ambaya anaonekana hana faida?

Mungu huwa anataka kuwafundisha wanadamu wajue upumbavu wao wa kumtegemea na kumpa sifa za kiungu binadamu ambaye ni kiumbe wa mpito, maisha yake ni kama majani hunyauka ma kusinyaa muda wowote. Huwa anatumia hilo tukio kama funguo ya kiakili na kiroho kuwa Yupo wa kutegemewa halisi ambaye hapatikani na mauti.

Lakini usugu na ukichwangumu wa watu umepelekea kuendelea kuabudu sanamu na mawazo ya maiti hao kama mbadala wa kitokuwepo kwao. Dini nyingi za jadi,kiislam,Kibudha/Hindu kikristo zinaabudu sanamu za mawazo na mbao/chuma za waliwahusudu.

Hili lilimpata Isaya, Alimuelewa Mungu vizuri baada ya Mjomba wake Mfalme uzia kuwa amefariki. ISAYA 6.

Hili lilimpata Mwanasiasa Herode kwa kufia jukwaani na kukumbiwa na wasifiaji wake.

Hili lilimpata Bibi yangu mmoja aliyepata strock kwa Mungu kumchukua mtoto wake tegemezi na aliyesifiwa kama Mungu mpaji. Baadae bibi huyo hiyo Strock ikamuondoa. Hakukubaliana ma maamuzi ya Mungu.

UFANYE NINI SASA.
Usipende kuwapa sifa watu na utukufu wa kiungu uliopitiliza. Hata kama ni kinafiki utawasababishia matatizo kama wao hawatakuwa na hekima ya kuzikwepa sifa hizo.

Usipende kutaka kubugia kila sifa na utukufu unaopewa na watoto, wafuasi, wafanyakazi wenza, au ukoo. Zikizidi zitakuondoa.

Kuwa mnyenyekevu.

No hilo tu
 
Kwamba Mungu hawezi chuja kua hizi ni sifa za kinafiki au za kihalali?

Kikubwa asikie tu wamesema "Ukifa huozi" "Nani kama wewe? Hakuna"

Analala na wewe mbele
Jambo ukilifanya kwa muda mrefu na kwa kupitiliza linageuka kuwa tabia hata ukifanya kinafiki.

Uwezo wa mpokeaji kutofautisha kati ya sifa za kinafiki na za halali ni mdogo hasa akiwa katika mode ya kuleweshwa na sifa hizo. Tukio hilo likifanywa kwa kupitiliza na kwa wingi linamadhara makubwa kwa mpokeaji kuliko mtoaji.

Huinua harakati za kujiiona muungu. Na hicho ni kiburi. Na sifa ya kiburi huwa kinafuatiliwa kwa karibu na anguko.
 
Hili pana mtumishi aliionya kuhusu Magufuli kumpa sifa ya kiMungu hawakusikia majibu yakawa hayo.
Mungu utukufu wake ashei na mwanadamu.
Check kinachomkuta mama Kanumba,nk.
Ukiweka sana tumaini lako kwa mtu mwenza,mtoto nk yaani akili na mawazo Yako huko unamchulia huyo mtu achukui round ana rip maana unafanya ibada ya sanamu.
Mshukuru Mungu kupitia mtu hii umlinda mtu.
 
Kwani hamjasoma maandiko " Mungu ufutilia mbali kiburi Cha wanadamu,ukiwa na kiburi maanguko ni lazima.
 
Mkuu huwa unategemea wanadamu?! Anyways, tafsiri ya Mungu kuhusu maisha bado ni fumbo kwa wanadamu wengi! Mungu anachokimaanisha kuhusu kuishi ni tofauti na wanadamu wanachokimaanisha!
Wanadamu ni viumbe wa mahusiano. Tunategemea. Ndio maana Muumbaji alisema sio vyema mtu akae peke yake. Ndio maana Kaini alipewa adhabu ya kukaa katika nchi isiyo na watu ( Upweke). Huu tunauita utegemezi mlalo ( horinzontal)

Kinachoendesha utegemezi kati ya mtu na mtu ni utegemezi wima ( vertical). Ukiuchukuq huu utegemezi wa kiuungu na kumpachikia mtu kama ndio suluhisho 100% la maisha yako hii inaitwa laana.

BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA. YEREMIA 17:5
 
Duuh

Mama yangu amehangaika na mama ntilie kunisomesha akimuomba Mungu kila siku nifanikiwe katika maisha ili nije niwe msaada kwake. Baada ya kijana wake kuula, na mama yangu kuanza kuishi maisha "angalau" na kuanza kumshukuru Mungu kwa uweza wake na kunitegemea mimi kumprovaidia mahitaji yake, hapa tatizo ni nini? Nikifa huoni mama yangu au mtu mwingine anaenitegemea atateseka??


Mungu atusaidie tuelewe hekima zake kwa undani. Tafsiri za kibinadamu wakati mwingine zinachanganya.​
 
Hili pana mtumishi aliionya kuhusu Magufuli kumpa sifa ya kiMungu hawakusikia majibu yakawa hayo.
Mungu utukufu wake ashei na mwanadamu.
Check kinachomkuta mama Kanumba,nk.
Ukiweka sana tumaini lako kwa mtu mwenza,mtoto nk yaani akili na mawazo Yako huko unamchulia huyo mtu achukui round ana rip maana unafanya ibada ya sanamu.
Mshukuru Mungu kupitia mtu hii umlinda mtu.
Ni sahihi.
Na ikifikika suala la Mungu na mtu, huwa hakuna dini. Hata kama ni atheist humuamini katika nadharia zako atakushukia.
Amefanya hivyo kwa wakina Nebukandeza, mungu mtu. Kilochomuokoa ni kukubali kunyenyekezwa baada ya kuguzwa akili alizozitegemea na kuwa chizi wa kukaa porini miaka 7.

Mungu anaponyenyekeza waabudiwa huwa hakuna anayeweza kuingilia kati. Hakuna Daktari, hakuna mganga, hakuna elimu, hakuna nadharia inaweza kuuzuia mkono wa Mungu katika harakati zake za kuzimq extremes za huma worshiping
 
Duuh

Mama yangu amehangaika na mama ntilie kunisomesha akimuomba Mungu kila siku nifanikiwe katika maisha ili nije niwe msaada kwake. Baada ya kijana wake kuula, na mama yangu kuanza kuishi maisha "angalau" na kuanza kumshukuru Mungu kwa uweza wake na kunitegemea mimi kumprovaidia mahitaji yake, hapa tatizo ni nini? Nikifa huoni mama yangu au mtu mwingine anaenitegemea atateseka??


Mungu atusaidie tuelewe hekima zake kwa undani. Tafsiri za kibinadamu wakati mwingine zinachanganya.​
Kabla hujatoboa alikuwa anamtegemea Mungu. Kosa linakuja atakapoacha kumtegemea Mungu aliyekuwezesha nakukutegemea wewe 100% na uwezeshaji wako.

Unajukumi la kumsaidia na kumwambia pamoja na Yote ni Mungu ndio wa kutegemewa. Asikupe hadhi ya uungu. Mungu ndio mpaji.

Mungu hawezi kutoa adhabu au fundisho kubwa kama hili kabla hajatoa onyo na hatari ya kuendelea. Mafunzo kama haya huja baada ya upuuziaji mkubwa wa maonyo yaliyotolewa kabla.
 
Usipende kutaka kubugia kila sifa na utukufu unaopewa na watoto, wafuasi, wafanyakazi wenza, au ukoo. Zikizidi zitakuondoa.
Nimesoma uzi wote, neno kwa neno kila mstari na kila aya nikawa sijui maudhui, ila huu mstari umemaliza kila kitu, mwenye masikio na asikie, mwenye macho na aone, asiyekuwa navyo vyote atafutiwe namna ya kupata ujumbe
 
Back
Top Bottom