Siridhiki na Maelezo ya Baraka Kizuguto Kuhusu Kanuni ya Kadi Tatu za Njano

Amavubi

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2010
Posts
30,156
Reaction score
13,258
Baraka Kizuguto yupo live STAR TV

Pamoja na kwamba siujui huu mchakato ulivyokwenda lakini kwa maelezo ya Baraka Kizuguto naona hajaweka suala hili vizuri na kuna kitu kipya ameongeza hapa kwamba

  1. Iliyopitisha Kanuni Hii ni Kamati ya Utendaji sababu ina mandate na kumbe si Bodi ya Ligi
  2. Kwamba wadau walioridhia wapo wengi na akasema dhana ya wadau wa mpira ni pana sana


Kwamba Kanuni za Ligi zinaweza kupitishwa na mdau yoyote mradi awe wa mpira au chombo maalum?

Nachokoza tena mada
 
anajiuliza ni kwa nini ni Yanga tu wanaokomalia suala hili, mchezo dhidi ya Standi hawakukata rufaa kadhalika mchezo dhidi ya Prison Yanga hawakukata rufaa hivyo wanachodai ni malalamiko tu
 
kwamba mabadiliko ya kanuni hiyo yalienda sambamba na uundwaji wa chombo cha kuendesha ligi ambacho kimeshatoa adhabu kwa wachezaji kama akina Aggrey Mrris na Juma Said Nyoso na kwa nini timu zisilalamikie adhabu hizo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…