Sisi watanzania ni wachafu sana ndio maana wageni wakija tunafukuzwa mjini ,wageni 36 tu shule ,masoko zimefungwa!

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
1,604
Reaction score
3,715
Nilijua wageni wanapokuja ni fursa kwa wenyeji, nilidhani watanzania watafundishwa namna nzuri ya kufanya biashara zao na kunufaika na wageni wanapokuja badala yake sisi hatujui kujiweka smart na kuuweka mji wetu smart sasa tunatimuliwa mabarabarani huko sisi ni Wachafu tutaharibu sifa ya nchi yetu nzuri ,Iko siku watakuja viongozi wa Dunia akina Putin, Kim jong UN ,watakuja kutuambia twende kwa muda Rufiji Mwanalomango huko ili kupisha wageni la mkuu limesikika
 
Katika mkoa mchafu Tanzania ya kwanza ni Dar.
Huo mkutano bora wangepeleka Moshi au Arusha au hata Dodoma.

Dar posta tu ile ukishuka chini hapa kwenye fukwe unaweza jiuliza marambili sisi waTz tuna shida gani kila kitu chetu ni hovyo.
 
Katika mkoa mchafu Tanzania ya kwanza ni Dar.
Huo mkutano bora wangepeleka Moshi au Arusha au hata Dodoma.

Dar posta tu ile ukishuka chini hapa kwenye fukwe unaweza jiuliza marambili sisi waTz tuna shida gani kila kitu chetu ni hovyo.
Nyie watu! Hata kama Dar ina mapungufu yake, lakini hapa Tz hakuna mkoa unaweza kuuingia Dar hata kwa robo! Dar ipewe heshima yake! Mikoa yote sijui Arusha, mwanza, Dodoma hata ikiungana haiwezi ifikia Dar
 
Dar jiji lina kila harufu mbaya unayoijua huku Duniani.

Mamlaka zilitazame sana hili jambo.
Halafu Serikali mbona kuna mikoa wanaitelekeza na inaweza kuwa na potential sawa na Dar , mfano Tanga, Lindi na Mtwara.
 
Walikuja marais wawili wa US-Bush na Obama fuatilia heka heka zilizokuweko.
Lakini safari hii ya hawa wageni imefanya serikali yetu kwenda mbali.
ile naikumbuka mana siku obama anaenda pale hyat enz ile kempiski nilikuwepo pale pale on the spot. nilishudiq wale mbwa ambao naskia wamefuzu kutumia computer wale k9.
hivi mbona sioni helicopter zikizunguka? jana nimeona gar flan hiv kama kifaru posta ljmeziba njia pale nbc posta
 
Mtu upo Magulyati huko ndani ndani, unaandika habari za Dar es Salaam ambayo unaiona tu Azam 2 mechi za NBC ligi kuu...

Kwa sasa barabara za CBD na pembezoni zote zipo kwenye uundwaji upya kwa sababu ya uwekaji wa BRT na kuna vichochoro vingi vimefungwa...

Sasa ongezea na kufungwa kwa barabara kwa muda kwenye ujio wa hao maraisi wa nchi za Afrika, ina maana CBD isingeweza kufikika kabisa...

Serikali yetu miaka nenda rudi imekuwa ikihubiriwa kuwa kuna haja ya kuwa na CBD's kadhaa ile ya Ilala imeshajaa na hakuna namna ya kuiboresha lakini serikali ni kama imetia pamba masikioni...

 
wengi hao ni viongozi wa nchi kwahiyo usalama wao ni muhimu kuliko chochote, wana maadui zao hatutaki nchi yetu ndio iwe kituo cha hao maadui kulipiza kisasi kwa hao wageni wetu, tulieni fata maelekezo suala sio uchafu ni usalama kwanza
Kwamba MTU akipanga tukio anaweza kushindwa? Tena kwa Tanzania?? Subutuuuu
 
Masoko gani yaliyofungwa?
 
Kwamba MTU akipanga tukio anaweza kushindwa? Tena kwa Tanzania?? Subutuuuu
Panga wewe halafu nenda, ndugu zako watakuzika bila usumbufu, shida mnaleta dharau kwa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, nakuhakikishia tuna vijana wana uwezo mkubwa sana hapa Tanzania wewe jichanganye
 
Nata tukioga tumeambiwa tusiende mjini😭
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…