Sitaki kutukanwa, nataka nishauriwe

Mkuu sawa lakini kumbuka ni ruhusa na si wajibu....na itakuwa vema ukaoa mjane nadhani hii ruhusa ilitolewa kutakuwa na resson behind na sio kimatamanio zaidi tafuta mjane mstiri ana mkeo atafurahi.... wenye dini watanisahihisha hapa...!

good luck

Tumepewa sifa kama nne za kuamua kumuowa mwanamke na ile ya uzuri imetangulizwa! Uzuri unaleta hamu au siyo?
 
Awali ya yote Mabrouk! Ila nakusia nafsi yako na yangu pia katika kuwa muadilifu kaka! Allah akutangulie katika hilo, akupe mke mwenye imaan, awaja'alie wote afya njema, rizk ya halal na watoto wema InshaALLAH!
Inshalla nitajijuwa zaidi kuwa ninao uadilifu hapo nitakapoowa wa pili. Unajuwa uhakika unakuja uwanjani wakati wa mechi sio mazoezi.
 
Hiyo hela kwa nini usiwasaidie watoto yatima.Manake ndo nyie mkifa mnaacha watoto wengi mtaani wakipata shida.

Mimi ndio nataka kuowa sio pesa yenye kutaka kuowa! Kama fedha ndio kuowa basi Kina Reginald Mengi wangeowa wengi tu. Suala la kuowa ni uamuzio sio pesa!
 

Nafsi mchumba wangu ndio inayoleta yote hayo! Nafsi yako inapokuwa haijazidiwa ni rahisi kuona waziwazi lakini nafsi hiyo hiyo ikipenda inaweza ikawa haioni sawsawa na watu wanaweza wakashangaa yale unayoyavumilia.
Sasa mwenzangu iwapo nafsi yangu imeshataka niongeze mke, mke wangu wa kwanza amekubali kuiridhisha nafsi yangu na kuna muhusika wa tatu ambaye kama mke wangu wa kwanza ameshakubali hiyo unayoiita kugawa mapenzi kuna ubaya gani?
 

Sawa mdogo wangu kwani kila kitu ni mipango dunia ya sasa, lakini pia tukumbuke yuko mpangaji zaidi mwenye mipango ya jumla!
 
Tafadhali baba, mimi sio waya hata unitafutie pacha wangu na kutuconnect kwenye receiver moja kwa manufaa yako binafsi!!! Na kama wasiwasi unatolewa kwa namna hiyo, basi ni heri nijikung'unte mwenyewe udondoke!
Mwenye kujaribu hajuti kukataliwa.
 
sababu za kutaka mke wa pili ni kwa sababu za tamaa za mwili au mengineyo,,kama mmoja hajaweza kukutosheleza wa pili unadhani anaweza?

Kwani kama nina tamaa za mwili kwanini niowe si nitafute usiku mmoja na mchana mwengine? Hilo linawezekana vizuri!
 

La Hapana! Mbona sijasema kuwa ninaowa kwasababu ya hamu ya mwili. Ninachoona mimi ni kuwa wewe unafikiri ndowa inaishia kitendo cha ndowa. Si hivyo kama unavyofikiria wewe.
Kwanini usiniulize kwanini nataka kuowa mke wa pili nawe unaruka tu kuwa nina roho mbaya! Je iwapo mke wangu ana matatizo yanayomfanya asiweze kulea watoto, kwa mfano? Je iwapo mke wangu ananidharau? Bado utaniona mimi nina makosa? Hata hivyo hili la kuopwa ni uhuru wangu ambao hakuna anaeweza kuniingilia kama vile mke wangu anaposema kuwa hanitaki kwasababu zake, unafikiri nitamlazimisha? Tatizo la jamii yetu ni ngono na uhusiani wa jamii mbili unahusanishwa na ngono tu. Hili ndio tatizo kuwa kila mmoja hapa anaruka na kufikiri kuwa naowa kwa kutafuta ngono.
 
umepima afya? huna kisukari usije ukatusumbua kwa kutafuta dawa za kuongeza nguvu kwa kawaida mke wapili huwa ananguvu kwa mwanzo.
ila maisha magumu ebu vumilia
 
umepima afya? huna kisukari usije ukatusumbua kwa kutafuta dawa za kuongeza nguvu kwa kawaida mke wapili huwa ananguvu kwa mwanzo.
ila maisha magumu ebu vumilia

Nauthamini ushauri wako! Lakini usiwe na waswasi gari bovu halibururwi na bovu bali hubururwa na gari nzima! Kuhusu maisha ndio hayo hayo wala sina tamaa kuwa 2015 italeta mabadiliko!
 

Unaweza ukanipa sababu za msingi katika hayo maamuzi yako?? Nafsi yako inakutumaje kwa huyo mke wa pili utakaemuoa?
 
Unaweza ukanipa sababu za msingi katika hayo maamuzi yako?? Nafsi yako inakutumaje kwa huyo mke wa pili utakaemuoa?

Kwa kuanzia nimempenda nae naamini ananipenda! Najaribu kutekeleza haki ya watu wawili mimi na yeye wala sitaki kupata dhambi kwani nimeshaona kuwa hatujiwezi.
 
Mapambano ni sehemu ya raha! Mimi ni mpambanaji na nahisi nimpe afuweni mwenzangu!
umechemka mkuu kuongeza mke nisehemu ya tatiyo unalojijiongezea ushauri wangu kuliko uogenye nibora umuache kwanza huyo japo pia sikushauri umuache tafuta chanzo isije kua wewe nichanzo huyo
 
huyo wa pili umeshampata?ushamuonja?kama ushampata umeshaikurubia zinaa na kama ushamuonja basi umeshazini!na wazinifu unapajua mahali pao bila shaka!achana na mawazo hayo ndugu!si vibaya mkajifunza kwetu tunaooa mke mmoja!
 
Mimi ndio nataka kuowa sio pesa yenye kutaka kuowa! Kama fedha ndio kuowa basi Kina Reginald Mengi wangeowa wengi tu. Suala la kuowa ni uamuzio sio pesa!

usipotoshe watu mkuu!huwa mnaambiwa unaweza kuoa zaidi kama unauwezo wa kuwatunza!na je kuwatunza ni nini ktk dunia ya leo kama si pesa au uwezo zaidi kipesa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…