Swahiba wangu,kinachofanya niseme unataka kuoa kwa kuongozwa na tamaa zako za kimwili na sio kwa kufuata lengo halisi lililoelekezwa na mwenyezi Mungu ni maneno yako mwenyewe hayo ya rangi ya blue.Wewe unatumia vibaya hii ruhusa kugeuza ufuska na kuuita ndoa.Au maneno yako hapo ndivyo Quran takatifu inavyoagiza hivyo kuwa muoe wake wengi sbb dunia ni kubwa na wazuri ni wengi?
Ofa yako ya kutaka kunifanya mke wa pili iwapo bado sijaolewa naikataa kwa jina la Yesu.Kamwe siwezi kuwa mke wa pili,sbb naamini mim ni malkia mwenye hadhi ya kuwa na himaya yangu peke yangu.Bora niwe bachelor maisha yangu yote kuliko kushiriki mume na mwanamke mwenzangu.
mkuu wangu hata hivyo naona kama nimekutupia shutma nyingi nikasahau kuwa wewe sio mwenye makosa,wenye makosa ni hao wanawake wanaokubali kuolewa uke wenza.Wangekua wanakataa sidhani kama mngepata nafasi ya kuona kuwa wanawake ni kama mashati,ukiona ya kwanza yamepauka hayana mvuto tena unakwenda dukani kutafuta zuri linalovutia.
Nakutakia kila la kheri mkuu wangu ktk ndoa yako ya pili,usinisahau ktk pilau.