trudie
JF-Expert Member
- Jan 15, 2014
- 3,668
- 8,745
Habari wanaJF, natumai tunajiandaa kuumaliza mwaka 2022, na kuupokea mwaka 2023 salama na kwa amani tele. Leo nashea kakisa kadogo kalikonipata wakati mtoto miaka kadhaa nyuma.
Miaka 21 imetimia sasa toka nilipopata kisa hiki nikiwa mtoto mdogo. Miaka ya 2001 nikiwa binti wa pekee nina miaka 8 nilikuwa naishi na mama yangu. Kipindi hicho mzee alikuwa anakaa sana site ( shughuli za magari) na mara nyingine anakuwa nyumbani.
Basi kutokana na mama kuwa na biashara zake siku nyingine anachelewa kurudi nikawa naogopa kukaa mwenyewe ananikuta namsubiri nje usiku. Hivyo akamuomba baba mkubwa mtoto wake mmoja wa kiume aliyenizidi miaka kama 3 au 4 tuishi nae kuondoa upweke.
Basi siku zikaenda ikafika siku mwisho wa mwaka 31.12.2001 siku ya mkesha wa kuupokea mwaka mpya 2002. Usiku ulipofika mama akatuaga anaenda kanisani kwa ajili ya mkesha na akatusihi tutulie ndani tufunge mlango mpaka atakaporudi tukatii. Basi mida imeenda kufika saa 4 usiku shamra shamra zikaanza ngoma na nyimbo zinapigwa nje.
Mikesha ya zamani ilikuwa na vibe sana sio kama miaka hii kila mtu anatulia ndani. Watu wa rika mbalimbali walikuwa wanajichanganya kuimba na kupiga ngoma na madumu huku wakicheza mtaa kwa mtaa.
Tumekaa ndani tunasikiliza tuu shangwe nje zinaendelea, kaka yangu akaniambia kwanini tusiende na sisi tukacheze nikamwambila ila mama katukataza tusifungue mlango kuna wezi na watekaji wa watoto tusije tukauawa. Kaka yangu akaniambia acha woga vaa koti na viatu halafu kila mtu atabeba kisu ndani ya koti atakayejaribu kututeka tunamuua.
Basi nikavaa koti langu na viatu vya boot ( siku hizi wanaziita American boot) wanavaa sana wanaume ila enzi zile tulikuwa tunavaa hadi watoto wa kike na soksi na gauni fresh. Tukaweka visu ndani ya makoti, tukamwaga maji kwenye madumu, beba madumu hao funga mlango funguo nikaweka mfukoni tukatoka kufwata ngoma za mkesha huku ma sisi tunapiga madumu na kuimba.
Sent using Jamii Forums mobile app
View attachment 2464313
Miaka 21 imetimia sasa toka nilipopata kisa hiki nikiwa mtoto mdogo. Miaka ya 2001 nikiwa binti wa pekee nina miaka 8 nilikuwa naishi na mama yangu. Kipindi hicho mzee alikuwa anakaa sana site ( shughuli za magari) na mara nyingine anakuwa nyumbani.
Basi kutokana na mama kuwa na biashara zake siku nyingine anachelewa kurudi nikawa naogopa kukaa mwenyewe ananikuta namsubiri nje usiku. Hivyo akamuomba baba mkubwa mtoto wake mmoja wa kiume aliyenizidi miaka kama 3 au 4 tuishi nae kuondoa upweke.
Basi siku zikaenda ikafika siku mwisho wa mwaka 31.12.2001 siku ya mkesha wa kuupokea mwaka mpya 2002. Usiku ulipofika mama akatuaga anaenda kanisani kwa ajili ya mkesha na akatusihi tutulie ndani tufunge mlango mpaka atakaporudi tukatii. Basi mida imeenda kufika saa 4 usiku shamra shamra zikaanza ngoma na nyimbo zinapigwa nje.
Mikesha ya zamani ilikuwa na vibe sana sio kama miaka hii kila mtu anatulia ndani. Watu wa rika mbalimbali walikuwa wanajichanganya kuimba na kupiga ngoma na madumu huku wakicheza mtaa kwa mtaa.
Tumekaa ndani tunasikiliza tuu shangwe nje zinaendelea, kaka yangu akaniambia kwanini tusiende na sisi tukacheze nikamwambila ila mama katukataza tusifungue mlango kuna wezi na watekaji wa watoto tusije tukauawa. Kaka yangu akaniambia acha woga vaa koti na viatu halafu kila mtu atabeba kisu ndani ya koti atakayejaribu kututeka tunamuua.
Basi nikavaa koti langu na viatu vya boot ( siku hizi wanaziita American boot) wanavaa sana wanaume ila enzi zile tulikuwa tunavaa hadi watoto wa kike na soksi na gauni fresh. Tukaweka visu ndani ya makoti, tukamwaga maji kwenye madumu, beba madumu hao funga mlango funguo nikaweka mfukoni tukatoka kufwata ngoma za mkesha huku ma sisi tunapiga madumu na kuimba.
Sent using Jamii Forums mobile app
View attachment 2464313