Sitasahau tulivyonunua TV na deki mwaka 1989, hakuna kuigusa na inalala chumbani

Sitasahau tulivyonunua TV na deki mwaka 1989, hakuna kuigusa na inalala chumbani

wewe ni miongoni mwa wachache wenye bahati sana,1989 nyumbani kuna tv?????

Sent using Jamii Forums mobile app
Lazima ulikuwa familia mambo safi, hiyo miaka kumiliki tv ni sawa na leo kuwa na gari rav4,kruger,vanguard,brevis,
miaka hiyo mtaani kwetu sinza kwa remmy karibu na makazi ya kocha wa simba abdala kibaden, kulikuwa na jamaa wawili tu Wenye TV, tulikuwa tunasmbiwa ni mabaharia, muvi za Arnold, komando joni, za kihindi tulizicheki huko ama kwa kukaribishwa sebuleni au kuchungulia dirishani.
Ushamba WA luninga uliendelea Sana mpaka 94,wakati itv na radio one zinaanza!!
Tumetoka mbali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio national yale ya zamani lipo kama kabati la maandazi hivi, tuning yake ni kuzungusha kama redio mkulima, picha ni black n white, baadaye yakaanza ingia makaratasi fulani unabandika mbele ya kioo kuona rangi...

Inakuwa kama ya mbao hivi!
 
Kilichonivutia kwenye hii thd ni jinsi Baba yako alivyokua na roho nzuri na utu, hakua na majivuno,aliruhusu mpaka majirani kujumuika nanyi kuangalia movie,alijitolea tv yake ili watu wafuatilie msiba wa Baba wa taifa,

Kama mshua yupo hai mpe big up sana toka kwangu,
hivyo ndivyo tunatakiwa kuishi na walimwengu,majivuno hayafai,Dunia ni mapito tu.
 
Shikamooo
Kwa kumbukumbu zangu. Tv au screen za mwaka 1989 zilikuwa na remote ya waya. Kwa maana remote ina waya. iliyounganishwa na tv au screen kama jamaa anavyosema.
Zilikuwa zinaitwa svreen kwa kuwa zilionyesha mikanda tu. Hakukuwa na tv.
Hizo screen au tv na deki zake zilikuwa zinasajiliwa na kulipiwa kodi kila mwaka. Zilikuwa na kadi kama yalivyo magari.
Ziliposambaa kukawa na mfumuko maduka ya kukodisha kanda. Unajiandikisha kila ukiazima kanda vhs unalipa. Hakukuwa na cd wala flsh wakati huo.
Majumba ya sinema yakafa.
Tv ya kwanza ilianza kuonekana dsm mwaka 1993. DTV. Baadaye ndio ITV ikaanzishwa 1995.
Miaka hiyo 1985 mpka 1990 ubalozi wa marekani ulikuwa unapeleka udsm kuinyesha taarifa za habari za ABC tv ya kwao iliyorekodiwa. CNN ilianzishwa mwaka 1985


Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikuwa darasa la 6 siku hiyo nikarudi nyumbani baba alikuwa Dar, jioni tukasikia honi ya gari nje ya nyumba tukatoka kumpokea, siku hiyo akasema tusiguse chochote tukae mbali akashusha box kubwa 1, box la saizi yakati 1 na box kubwa zaidi 1, badae akanipa mfuko wa Rambo ambao ulikuwa na waya mrefu nikataka kuingia nao ndani akasema nikae nao pale nje, basi bwana lile box kubwa kabisa likafunguliwa lilikuwa na jenereta akaliweka nje, (hapo hata hatujasalimiana vizuri na kujuliana hali) akaweka petrol lita 10 iliyokuwa kwenye dumu jeupe, akaweka na oil ilikuwa kwenye kichupa fulani hivi, akachukua ule waya mrefu akaufungua mpaka ndani.

Kule ndani alitwambia tukae mbali tusiguse chochote, akaniambia niangalie kwenye buti kuna box nililete haraka sana, nikatoa box halikuwa zito nikalipeleka akatoa ka kitabu na vimbao na ma tairi akasoma kidogo kijitabu kisha akaunganisha vijimbao na matairi si ikatokea stand, daah tuliona mzee ni mtaalamu sana akaijaribisha pale kuiendesha nikataka namimi niisukume kidogo nikala kofi la shingo, siku mind maana nilikuwa interested kujua kitakacho fuata.

Basi bwana juu kabisa ya ile stand aliweka dubwasha kubwa lililokuwa kwenye box na lilikuwa na kioo na lina chogo, kwakuwa sikuwahi kuliona kabisa maishani sikujua ni nini, nilihisi ni kama redio hivi, pale katikati akaweka kudude flani kama redio ila chenyewe ni kidogo, akaunganisha kila kitu akatoka nje akawasha jenereta (jenereta sikulishangaa maana tulikuwa na jingine dogo kwaajili ya taa na redio siku moja moja akifurahi.

Alivyowasha akachomeka ule waya akawasha swichi kule ndani taa ikawaka kwenye extension flani hivi ya duara, akaingia huku anapiga mruzi, akatoa kasha juu lina picha ya wanyama halafu ndani ya kasha akatoa dude kama kanda ya tape ila lenyewe kubwa akasema huu ni mkanda sawa? tukasema sawa akatwambia hii ni deki na hii ni SCREEN hakusema TV alisema SCREEN sasa nikamuuliza screen kazi yake nini? akasema ngoja uone.

Akawasha akachukua remote akaset tukaanza kuona wanyama, palepale nikatoka mbio hadi nyumba yapili nikawaambia wanaitwa home wakaja familia nzima, haikutosha nikavuka nyumba kadhaa nikaenda kwa mwalimu Stive nikamwambia anaitwa nyumbani, nilienda kwa mwalimu Stive maana alikuwa anachapa sana ukichelewa namba sasa kufuta hilo nilimwalika na chaajabu walivyokuja walivutiwa sana, sikuhiyo tulikaa nao mpaka sa 7 baba akawaambia tutaendelea kesho.

Kesho yake mwalimu alinipitia na baiskeli tukaenda nae shule kiroho safi na baada ya kurudi alikuja home tukala baba alivyorudi akaenda chumbani akaileta tukaangalia, baada ya siku chache watu walikuwa wanajaa sana akawa anaitoa nje na kila siku tulikuwa tunaangalia mkanda uleule wa wanyama.

Miezi michache badaye akanunua UNGO (Dish kubwa sana la nyavu, nikubwa kweli kweli) akaja na fundi toka dar kuufunga na akazungushia fensi ya senyenge pale kwenye ungo.
Alinunua pia antena ya samaki

Ratiba ya matumizi:
Baba akisafiri hakuna kuangalia
Hakuna mtu anayeruhusiwa kugusa chochote isipokuwa kwa ruhusa yake
Ukipiga kelele au kujifanya unajua zaidi ni tiketi ya kwenda kwenu

Kwenye msiba wa Mwalimu TV yetu ilipelekwa uwanjani watu wa vijiji kadhaa wakajumuika nasi kufuatilia msiba ule na kulikuwa na bonge la nguzo lilisimikwa kwaajili ya kufunga antena.

NASIKITIKA KWAKUWA SASA ILE TV HATA KUIMILIKI NI AIBU ILA BADO NI NZIMA HADI LEO, DEKI ILIKUFA, JENERETA IPO LAKINI UMEME UPO PIA.

Enzi zile TV ilinisaidia kuwa na watoto wazuri japo tulifanya kitoto ila walikuwa madem zangu.
Mkuu shikamoo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikuwa darasa la 6 siku hiyo nikarudi nyumbani baba alikuwa Dar, jioni tukasikia honi ya gari nje ya nyumba tukatoka kumpokea, siku hiyo akasema tusiguse chochote tukae mbali akashusha box kubwa 1, box la saizi yakati 1 na box kubwa zaidi 1, badae akanipa mfuko wa Rambo ambao ulikuwa na waya mrefu nikataka kuingia nao ndani akasema nikae nao pale nje, basi bwana lile box kubwa kabisa likafunguliwa lilikuwa na jenereta akaliweka nje, (hapo hata hatujasalimiana vizuri na kujuliana hali) akaweka petrol lita 10 iliyokuwa kwenye dumu jeupe, akaweka na oil ilikuwa kwenye kichupa fulani hivi, akachukua ule waya mrefu akaufungua mpaka ndani.

Kule ndani alitwambia tukae mbali tusiguse chochote, akaniambia niangalie kwenye buti kuna box nililete haraka sana, nikatoa box halikuwa zito nikalipeleka akatoa ka kitabu na vimbao na ma tairi akasoma kidogo kijitabu kisha akaunganisha vijimbao na matairi si ikatokea stand, daah tuliona mzee ni mtaalamu sana akaijaribisha pale kuiendesha nikataka namimi niisukume kidogo nikala kofi la shingo, siku mind maana nilikuwa interested kujua kitakacho fuata.

Basi bwana juu kabisa ya ile stand aliweka dubwasha kubwa lililokuwa kwenye box na lilikuwa na kioo na lina chogo, kwakuwa sikuwahi kuliona kabisa maishani sikujua ni nini, nilihisi ni kama redio hivi, pale katikati akaweka kudude flani kama redio ila chenyewe ni kidogo, akaunganisha kila kitu akatoka nje akawasha jenereta (jenereta sikulishangaa maana tulikuwa na jingine dogo kwaajili ya taa na redio siku moja moja akifurahi.

Alivyowasha akachomeka ule waya akawasha swichi kule ndani taa ikawaka kwenye extension flani hivi ya duara, akaingia huku anapiga mruzi, akatoa kasha juu lina picha ya wanyama halafu ndani ya kasha akatoa dude kama kanda ya tape ila lenyewe kubwa akasema huu ni mkanda sawa? tukasema sawa akatwambia hii ni deki na hii ni SCREEN hakusema TV alisema SCREEN sasa nikamuuliza screen kazi yake nini? akasema ngoja uone.

Akawasha akachukua remote akaset tukaanza kuona wanyama, palepale nikatoka mbio hadi nyumba yapili nikawaambia wanaitwa home wakaja familia nzima, haikutosha nikavuka nyumba kadhaa nikaenda kwa mwalimu Stive nikamwambia anaitwa nyumbani, nilienda kwa mwalimu Stive maana alikuwa anachapa sana ukichelewa namba sasa kufuta hilo nilimwalika na chaajabu walivyokuja walivutiwa sana, sikuhiyo tulikaa nao mpaka sa 7 baba akawaambia tutaendelea kesho.

Kesho yake mwalimu alinipitia na baiskeli tukaenda nae shule kiroho safi na baada ya kurudi alikuja home tukala baba alivyorudi akaenda chumbani akaileta tukaangalia, baada ya siku chache watu walikuwa wanajaa sana akawa anaitoa nje na kila siku tulikuwa tunaangalia mkanda uleule wa wanyama.

Miezi michache badaye akanunua UNGO (Dish kubwa sana la nyavu, nikubwa kweli kweli) akaja na fundi toka dar kuufunga na akazungushia fensi ya senyenge pale kwenye ungo.
Alinunua pia antena ya samaki

Ratiba ya matumizi:
Baba akisafiri hakuna kuangalia
Hakuna mtu anayeruhusiwa kugusa chochote isipokuwa kwa ruhusa yake
Ukipiga kelele au kujifanya unajua zaidi ni tiketi ya kwenda kwenu

Kwenye msiba wa Mwalimu TV yetu ilipelekwa uwanjani watu wa vijiji kadhaa wakajumuika nasi kufuatilia msiba ule na kulikuwa na bonge la nguzo lilisimikwa kwaajili ya kufunga antena.

NASIKITIKA KWAKUWA SASA ILE TV HATA KUIMILIKI NI AIBU ILA BADO NI NZIMA HADI LEO, DEKI ILIKUFA, JENERETA IPO LAKINI UMEME UPO PIA.

Enzi zile TV ilinisaidia kuwa na watoto wazuri japo tulifanya kitoto ila walikuwa madem zangu.
Kweli age ni namba tu mtu wa 89 uko shule mm sijazaliwa vizuri ila leo wooote ni familia moja humu na watu wanapendana na kutukanana pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kilichonivutia kwenye hii thd ni jinsi Baba yako alivyokua na roho nzuri na utu, hakua na majivuno,aliruhusu mpaka majirani kujumuika nanyi kuangalia movie,alijitolea tv yake ili watu wafuatilie msiba wa Baba wa taifa,

Kama mshua yupo hai mpe big up sana toka kwangu,
hivyo ndivyo tunatakiwa kuishi na walimwengu,majivuno hayafai,Dunia ni mapito tu.
Lakini hata majirani wazamani walikuwa wazuri, ila wengi wasasa hawachelewi kukubebea vitu ndani
karibisha ndani kila siku uone mpaka masufuria ya jikoni yataondoka, vijiko ndiyo usiseme

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Duh umenikumbusha mbali sana....nyie mlikuwa wa kishua sana....miaka hiyo mi nakumbuka mzee wangu (RIP) alikuwa anarudi na ile mashine ya picha za mgando kama projector flani alikuwa anaiazima ofisini kwao....lakini alikuwa mkali sana...yaani mtu haruhusiwi kuisogelea ....kwa hiyo akipress inatokea picha ukutani mara picha ya mnyama amesimama , mara mgambo anaruka,mara mtu kapanda farasi..hapo tunakuwa tumetulia kimya sana na madirisha yamefungwa..kila picha ikitokea anasubiri kama dk 3 halafu anauliza tayari nitoe?..nakumbuka watu wallikuwa wanajaa kichizi home wakishajua mshua amerudi na alikuwa anaifungia chumbani kwake...baada ya muda wa siku kadhaa alikuwa anairudisha ofisini kwake aliko i azima....hapo tulikuwa tuna mind kichizi.....kipindi hicho nakumbuka ukitaka kuona video chogo lazima uende ukumbi wa CCM na ilikuwa lazima ulipie...hapo ndipo palikuwa pagumu....zamani raha sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lazima ulikuwa familia mambo safi, hiyo miaka kumiliki tv ni sawa na leo kuwa na gari rav4,kruger,vanguard,brevis,
miaka hiyo mtaani kwetu sinza kwa remmy karibu na makazi ya kocha wa simba abdala kibaden, kulikuwa na jamaa wawili tu Wenye TV, tulikuwa tunasmbiwa ni mabaharia, muvi za Arnold, komando joni, za kihindi tulizicheki huko ama kwa kukaribishwa sebuleni au kuchungulia dirishani.
Ushamba WA luninga uliendelea Sana mpaka 94,wakati itv na radio one zinaanza!!
Tumetoka mbali

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahahaaaa
 
Back
Top Bottom