Sitochangia tena damu kwenye Mpango wa Taifa wa Damu Salama

bornagain

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2012
Posts
3,383
Reaction score
1,357
Leo tarehe 28/06/2013 ndiyo nimeamua kutokuchangia tena damu kwa hao watu wanaojiita sijui Mpango wa Taifa wa Damu Salama (NBTS).Nimechukua pia jukumu la kuwashawishi hata ndugu zangu wasichangie tena damu na kama ni kosa basi nisamehewe tu.
Kisa chenyewe ni kwamba nina mgonjwa kalazwa Amana Hospital katika Manispaa ya Ilala, tokea wiki iliyopita amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa ambao unahitaji upasuajia mdogo, sasa daktari ni kila siku anamuambia kuwa inatakiwa apate watu wa kumchangia damu la sivo upasuaji hautawezekana maana Amana nzima hawana damu hata lita moja kwa hiyo mgonjwa inatakiwa atafute ndugu wa kumuongezea damu, tumeenda kwa ajili ya kuchukuliwa damu pale kwa ajili ya mgonjwa wetu tulipofika hospital bahati nzuri kuna daktari namfahamu yeye yupo Temeke nikampigia kumuuliza inakuweje hospitali ya Amana hawana damu,akaniambia nimpatie jina la daktari anaedai kuwa damu hamna.
Nilivompatia jina la daktari ni kwamba fasta mgonjwa wangu hakudaiwa tena damu na mambo yote yamekamilika sasa, baada ya kupeleleza nikaambiwa kuwa damu ni dili pale ilitakiwa mgonjwa atoe kama 20,000 mpaka 50,000.

Sasa kama kweli wananchi wanajitolea damu bure kwa nini hospitali wazifanye kama ni deal? Kuanzia leo sitochangia damu kwenye hao watu wanaojiita damu salama nitachangia specific kwa mgonjwa na sio kupitia hizo kampeni zao za kiwiziwizi tu
 
Duh......siku ukihitaji damu na hauna ndugu wa kukupa itakuaje? And finally upate damu ya stranger? Ni kama unasema hutafanya NECTA Kwasababu wasahishaji huwa wanachoka kwahiyo paper za mwisho wanasahisha vibaya....

We toa tu. Hujui kama itatolewa ruswa au la na hujui itamsaidia nani:wink2::wink2::wink2::wink2:
 
pole kwa maswahibu jamaa! lakini kuna taarifa imetolewa ili wananchi na wagonjwa watoe taarifa kwa wote wanaouza damu!
 
pole kwa maswahibu jamaa! lakini kuna taarifa imetolewa ili wananchi na wagonjwa watoe taarifa kwa wote wanaouza damu!

Ndugu yangu hizo namba wanazotoa wakubwa ni geresha tu, mfano ni kweli umepewa namba kwamba ukifika Ubungo report kama utatozwa nauli zaidi ya 35,000/= Arusha - Dar then umefika Ubungo basi ni za shida sana sasa ukabahatika ukapata ya 35,000/= tena kwa mbinde sana.Kwa hiyo utakuwa na courage ya kupiga na kutoa taarifa eti umepanda kwa bei mbaya?Ndiyo hivo bwana kuna sehemu unaona umedhulumika lakini hata huwezi kutoa taarifa maana unaona kama vile ndiyo system ilivo
 

Mimi kampeni za kutajirisha wengine niliachana nazo zamani sana, ntakuwa natoa damu kwa mgonjwa specific and not otherwise.Hiyo damu wanapiga kampeni mpaka kwenye maredio eti ni bure kumbe wapi bwana ukiwa na mgonjwa utasikia oooo hatuna group z sijui mara ooooh tuna group O+ peke yake kumbe wanataka utowe hela.Yaani ukishatoa hela hata group Z unapata
 

Ni kweli lakini inauma sana pale wananchi wanapojipanga kukamuliwa damu wengine kwa mapenzi mema kabisa huku wakati hata lishe zao ni duni sasa linapofika suala la kuuza damu hiyo inakuwa issue sana,si bora wawaambie mapema kuwa unatolewa lita moja then unapata 20 thousands kama wao wanavotuuzia mahospitalini
 
Tanzania yetu hii sasa tutafanyaje.......kila sehemu matatizo

Sidhani kama kususa kutoa damu Ni solution nzuri...
 
Mkuu.@bornagain Itabidi nikija bongo niombe kibali toka Serikalini cha kuniruhusu kufunguwa Benki ya Damu nchini Tanzania.Ili tuweze kuwanusuru Wagonjwa ambao hawana Damu kwa bei nafuu ya ununuzi wa Damu unasemaje?
 
naomba kama raia mwema na mzalendo wa nchi hii, tuchangie damuna tusikatishwe tamaa na MANYANG'AU machache yaliyogeuza uzalendo wetu kuwa biashara yao....... waratibu wa damu salama wakaze buti zaidi na hatua dhidi ya wauza damu zisiwe tu uhamisho toka kituo kimoja kwenda kingine bali kali zaidi ili kurudisha imani yetu kwao
 
Hii nchi imelaaniwa... Yaani watu wanapiga dili mpaka kwenye damu??
 

Ni kweli lakioni ni ngumu maana hata namba si walishatoa 0712602100 lakini ni geresha tu
 
Pigeni namba hii mkiona mnazinguliwa na hao wanaotaka hela au wanasema hakuna damu: 0655282292 (ya watu wa damu salama)
 
Hii nchi ni balaa, nilimsikiliza yule jamaa anaeratibu utoaji damu salama nadhani last week tu kwamba mahitaji ya damu ni mengi kuliko damu inayokusanywa hivyo kinachofanyika kama hospitali haina damu kabisa inawaomba ndugu wachangie damu lakini kama atakosekana wa kuchangia damu basi hospitali itaomba damu kutoka mpango wa damu salama, sasa tatizo wao badala ya kuwaelekeza kwanini wanafanya hivyo wao wanafanya kibabe. Nadhani kuna haja kwa wanaojitolea damu kupewa upendeleo pindi anapopungukiwa yeye au familia yake ahudumiwe kwa haraka vinginevyo watu watakuwa wanabaki na damu zao
 
Benki ya Damu ni ya Kuweka na Kukopa damu mkuu. Ilibidi kwanza mchangine na baadae wawape ile iliyochangiwa na wengine kabla...ni ka SACCOS fulani ka damu.
 
pole kwa maswahibu jamaa! lakini kuna taarifa imetolewa ili wananchi na wagonjwa watoe taarifa kwa wote wanaouza damu!

Ving'amuzi hatuna si unajua tangazo ukiliona ndo linakaa kuliko kusikia
 
Mkuu wewe endelea kuchangia damu utapata malipo mbele ya Mungu.
 
Ndugu yangu usichukulie hasira na kuamua kususa kuchangia damu!hayo uliyokutana nayo ni tatizo la ufisadi kila mahali , na si kwamba inapaswa iwe hivyo!mimi baba yangu alikuwa na saratani ya damu hivyo alikuwa anaongezewa damu kila baada ya wiki moja au mbili.mara ya kwanza tulitakiwa tumtolee damu kwanza.tukaenda mimi ,mume wangu na mdogo wangu.baada ya kutolewa damu pale damu salama tulipeleka vyeti vyetu pale hospitali na kuanzia hapo baba alikuwa anaongezewa damu kila inapopungua kwa muda wote wa miezi Saba bila kuambiwa swala la kuchangia damu au kutoa pesa.naweza sema wewe uliangukia mikono mibaya ya mafisadi.pole ndugu yangu.
 
Mkuu wewe endelea kuchangia damu utapata malipo mbele ya Mungu.

Nina mpango wa kuchangia mara ya tisa muda si mrefu.
Nataka kujua kama Tanzania kuna chama cha Wachangiaji damu au la! Ili nijiunge. Kuna gharama za uzalendo. Itatupasa tuzigharamie na kutetea thamani ya uzalendo. Usikate tamaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…