Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kama nauli ya chinongwe Dar ilikua 22,000/= kwa basi laa machinga la kupitia Mwena ndanda to Dsm,huu mkasa utakua wa miaka hii ya karibuni 2019-2021 Feb....Pole ndugu------SEHEMU YA KUMI NA TATU - - - - -
Nilipoona pamepambazuka nikashuka kwenye mti nikawa naelekea barabarani kuona kama kweli usafiri upo maana kwa mazingira ya kawaida Ile barabara unaweza Dhani hakunaga bus linalopita pale. Kama dakika sita hivi nikawa nipo maeneo ya barabara huku nikiwa naona wamama na wazee wakiwa wanaenda kwenye kazi zao za kila siku ikiwemo kilimo na ufugaji,ile nikiwa nimetulia nikawaza kama pesa yangu ipo mfukoni kuangalia mfuko wa nyuma siioni kucheki mfuko wa mbele nikaikuta nikasema hapo sawa Sasa nina Amani ya moyo japo kiasi lakini kwa kuwa nauli ninayo ninatumai kila kitu kitaenda Sawa. Baada ya mda mchache Kuna Dada alipita karibu yangu nadhani alikuwa anakatiza kwenda shambani maana mbele kidogo kulikuwa Kuna mashamba ya ufuta alipopita mm nikawahi kumsalimia Kisha nakamuuliza bus huwa linapita saa ngapi, huyu Dada akasema saa tatu ndohuwa linapita japo Kuna mda linaweza kuwahi pia.
Nikamwambia Asante kumbe inabidi nikae chonjo mda ndio huu yule Dada akauliza kwani unasafiri au unapokea mgeni? Nikamwambia nasafiri ndio maana nipo na begi la safari yule binti akaguna akaendelea na safari. Baada ya dakika kadhaa nikaja kugundua kumbe nimechafuka taabani Shati ipo hovyo, suruali chafu mwili wote haupo sawa nikasema hivi hapana itabidi nitafute sehemu yenye maji ninawe tu uso then kwakua kwenye begi Kuna Shati bado sijavaa Ile itanisave. Kuja kuangalia nikamwona yule Dada bado hajafika mbali kwa kuwa mimi ni kamanda ikabidi nikimbie kumuwahi mpaka nikamfikia, nikamwambia samahani Dada sijasahau chochote ila nilikuwa naomba kama una maji ninawe tu uso nitashukuru sana. Bahati nzuri alikuwa na maji kwenye kidumu cha Lita tano akafungua vimizigo vyake kulikuwa kuna kikombe ameweka akamimina maji nikanawa japo sikuwa na mafuta nikasema haina shida maana hakuna anaenijua huku. Yule Dada akaendelea na safari zake mm nikabaki pale nikafungua begi ili nibadilishe Shati japokuwa suruali ilikuwa chafu ila uzuri ilikuwa na rangi ya kaniki kwahiyo nilipangusa vumbi kwa maji nilikuwa nanawia ikakaa poa ila ukisogea uchafu unaonekana tena mwingi tu.
Nilipofungua begi nikakuta Ile Shati ndohaitamaniki kabisa kumbe yule jamaa aliefungua begi langu kule polini aliipakaza midamu pia alikuwa nguo zote anazibwaga chini na pale chini ndosehemu pia walichuna yule mnyama, nikiangalia hii niliovaa nayo kituko bora yenye midamu ila shida ni nyeupe zile damu zinaonekana kila sehemu. Ikabidi niende kwenye mti flani nikakaa kutuliza kichwa changu maana kupanda kwenye bus na Ile hali sio rahisi. Nilikaa kwenye ule mti baada ya hapo sikuelewa kilichoendelea kumbe nikajiinamia nikapiga usingizi mzito sana. Nikiwa kwenye ndoto nikawa nasikia sauti "wahi upande kaka bus linaenda mbali hili". Nikakurupuka kutoka usingizini kuangalia mbele nikasikia muungurumo wa bus na nipo mbali kidogo na barabara maana nilipoenda kumfata huyu binti anisaidie maji sikurudi barabarani kwahiyo nikaanza kukimbia kwenda barabarani mpaka bus nikiwa naliona kwa macho yangu linapitiliza huku nikimbwata kwa nguvu sauti yenye mlipuko "SIMAMAAAAAAA“....." SIMAMAAAAAAAA", lakini holaa juhudi hazikuzaa matunda Sasa pamoja na bus kupitiliza ilinibidi begi nilishike kwenye mkono nikavuta pumzi baada ya hapo niliondoka kwa kasi ya kulipuka kama Mbape anaechezea Monaco kwa mkopo, dakika sifuri nipo barabarani huku nikiwa napukuta mkono kwenye site mirror ya dreva maana bus halikuwa mbali sana nikaona mwendo wa bus umepungua na kusimama kabisa. Nilipofika kwenye gari nikapanda safari ikaanza Ile naingia ndani kutafuta siti kila mtu ananishangaa ninavyovuja mijasho niponipo tu wenge la kutosha nikawa sipo sawa kimsingi.
Tukapita mpaka maeneo ya Ile shule ya chinongwe huku nikiwa na huzuni sana. Nilipoenda kukaa kulikuwa Kuna Dada mmoja tukakaa nae ila ajabu nikuwa kila mda alikuwa ananiangalia nilivyo kwa jicho la kuibia mm nikawaza nikasema ndoishakuwa hivi Sasa nitafanyaje. Safari iliendelea ikafika mda nikarelax tu na gari ilipokaribia main road konda akapita kuchukua nauli nikamwambia mm nina 22000 Sina 25000 akasema toa, nikampa akarudisha 3000 yangu huku safari ikiendelea na uelekeo ni Dar Es Salaam japo baada ya hapo itabidi niende mkoa wa pwani mlandizi huko ndokuna rafiki wa baba angu nilielekezwa nikakae. Tukapita baadhi ya vijiji ila tulipokaribia lindi mjini eneo moja linaitwa DARAJANI ni mbele kidogo kutokea mnazi mmoja ukiwa unaelekea lindi mjini, Bus la machinga likaharibika ikawa ni saa tano kasoro hivi. Nikajua ni hitlafu tu baada ya dakika kumi hivi tutasepa. Kumbe tatizo lilikuwa serious sana walihangaika kulitengeneza zaidi ya masaa matatu lakini hakuna kilichofanyika kufika saa nane hivi abiria wakaanza kuwaka wakidai waagiziwe bus jingine ili tuweze kuondoka. Kumbe tulikuwa tunabwata tu maana wafanyakazi wa lile bus wote waliondoka akabaki dereva peke ake. Abiria wakasema kama hamtaki kutuletea bus jingine mtupe nauli zetu.
Mpaka inafika saa tisa hakuna jipya, ilibidi abiria mmoja apige simu kwa traffic polisi waje eneo husika na baada ya mda wakafika huku wakimkoromea dreva kwanini hataki kupiga simu kwa boss alete bus jingine ili abiria tuondoke na kila abiria alisema hata saa sita usiku wao wataondoka hawataki kulala lindi. Wale polisi wakapiga simu kwa boss akaja meneja wa kampuni ni mwarabu kembamba hivi kilikuja na harrier nyeusi huku kanagonga konyagi. Kalipofika kakauliza KIDAGAA yupo wapi? Yule dreva akasema kidagaa kaenda mjini anakuja mda si mwingi, nadhani kidagaa ni yule konda. Abiria wakawa wanawaka kweli huku njaa zimetuponda nikaona yule meneja mwarabu anajibu kwa dharau akisema "Mnawahi wapi nyinyi acheni kututisha" halafu anaongea mbele ya polisi huku anavuta sigara. Kitendo kile kilinifanya nikakwazika sana nikajisemea moyoni "your richness can't buy our dignity", ikabidi ninyanyuke nikamsogelea nikaona kashtuka huenda kutokana na mwonekano niliokuwa nao nikamwambia usiogope NAOMBA NIRUDISHIE NAULI YANGU kakajibu kwa jaziba kakasema mpumbav wee leta hiyo tiketi, nikatoa tiketi mfukoni kakaangalia halafu kakaingia mfukoni kakanipa 23000 yangu kakasema haya katafute gari Lako nikamwambia poa. Ni kaingia kwenye bus nikachukua begi langu nikakaa pembeni kuangalia ustaraabu mwingine. Baada ya mda kidogo huyo kidagaa akafika na spea ili watengeneze chapu bus liondoke, walikukuruka lakini wakaufyata.
Ngoma ilipoonekana ni ngumu ikabidi yule mwarabu aagize Kosta yake sijui inapiga root gani akasema iende haraka GEREJI ifanyiwe service ya kutosha maana inabidi ipeleke abiria Dar Es Salaam halafu pia wachukue Costa yoyote hapo lindi mjini ije uchukue abiria wake wakakae pale stend maana kuendelea kukaa pale darajani ni kupoteza mda. Kweli baada ya Lisaa Costa ikafika kuwapakia wale abiria wote wakiwa na mizigo yao tena zilikuja mbili ili waweke kambi lindi mjini kusubiri Kosta yake ifanyiwe service waondoke kwenda Dar Es Salaam maana gari kubwa lilikuwa halitengenezeki tena kwa mda huo. Costa zilipofika tu yule mwarabu akasema pakia wote ila huyu jamaa alierudishiwa nauli simtaki tena nadhani kwanza hata muonekano wake akili zake haziko Sawa. Kidagaa ambae ndomfanyakazi wake anaemwamini akasema 'imeisha iyoo'. Abiria wote wakaondoka nikabaki mimi tu maeneo yale na baadhi ya mafundi waliokuwa wanalinda lile bus.
Sina hili wala lile nikaona bus limewaka ila boss wao akasema walipeleke sehemu moja inaitwa mnazi mmoja wakalilaze, huenda bado lilikuwa na shida somewhere. Kwahiyo wakaondoka wote mimi nikabaki pale huku nikishuhudia jua linazama kwa macho yangu bila kugusa chochote mdomoni lakini safari yangu haina matumaini tena kama mwanzo. Nilikaa sana pembeni kidogo mwa Ile barabara mpaka mida ya saa moja hivi Kuna Majamaa yakapita nikayauliza kama nitapata msaada wa usafiri wakasema wao sio wa husika wa mambo hayo ila sehemu nilipo si salama Kwangu inabidi niondoke maana pale darajani Kuna matukio makubwa ya kiharifu huwa yanatendeka. Nikaona hapa nimelikoroga ikabidi nitulize akili yangu vizuri nikasema ngoja kwanza niangalie zile namba za simu kwenye karatasi za yule mzee wa mlandizi nikipata simu nimpigie kuwa sitafika Leo ila labda kesho mda wowote maana kama saizi ni saa mbili kasoro mlandizi nitafikaje Leo Leo. Nikachukua begi nikafungua zipu ya mwisho maana ndonahifadhi namba kwenye karatasi na line yangu ya simu. Kuja kucheki sioni line wala karatasi yenye namba za simu. Nikasema hapana hili ni wenge tu ngoja niangalie vizuri, nilipekua begi Zima sikuona line yangu yenye pesa 20000 niliyotumiwa na baba wala karatasi yenye mamba zangu muhimu [emoji22], nilikuja kugundua yule mpumbav wakule polini aliekuwa anakagua beg langu hovyo bila ustaraabu ndoaliangusha hivi vitu kwahiyo nikawa nimekosa vyote. Sasa ngoma iliyobaki nikutafuta usafiri mida hiyo ikawa ni saa tatu kasoro usiku kwa kuhisi na eneo nililopo niliambiwa si salama sana kwahiyo hapanifai inabidi niondoke.
......... Inaendelea usichoke.........
Kama wewe ndio unaanzia kujifunza hapa haujioni kama wewe ndio bado kula kulala.Hii story Ina inspire Sana na Ina mafunzo mengi hata Kama haina uhalisia kwa asilimia Mia
Nawashangaa Sana hao wanaobeza na kukejeli Nahisi hao wanaokejeli na kubeza Ni watoto wa mama hawaelew Nini maana ya msoto
Nyie watoto wa mama kaeni kwa kutulia wanaume tunajifunza vitu hapa
[emoji1][emoji1][emoji1]acha zako wwKama wewe ndio unaanzia kujifunza hapa haujioni kama wewe ndio bado kula kulala.
Itabidi umchangie.....jamaa bando limemuishiashusha mzigo
Aisee!------SEHEMU YA KUMI NA TATU - - - - -
Nilipoona pamepambazuka nikashuka kwenye mti nikawa naelekea barabarani kuona kama kweli usafiri upo maana kwa mazingira ya kawaida Ile barabara unaweza Dhani hakunaga bus linalopita pale. Kama dakika sita hivi nikawa nipo maeneo ya barabara huku nikiwa naona wamama na wazee wakiwa wanaenda kwenye kazi zao za kila siku ikiwemo kilimo na ufugaji,ile nikiwa nimetulia nikawaza kama pesa yangu ipo mfukoni kuangalia mfuko wa nyuma siioni kucheki mfuko wa mbele nikaikuta nikasema hapo sawa Sasa nina Amani ya moyo japo kiasi lakini kwa kuwa nauli ninayo ninatumai kila kitu kitaenda Sawa. Baada ya mda mchache Kuna Dada alipita karibu yangu nadhani alikuwa anakatiza kwenda shambani maana mbele kidogo kulikuwa Kuna mashamba ya ufuta alipopita mm nikawahi kumsalimia Kisha nakamuuliza bus huwa linapita saa ngapi, huyu Dada akasema saa tatu ndohuwa linapita japo Kuna mda linaweza kuwahi pia.
Nikamwambia Asante kumbe inabidi nikae chonjo mda ndio huu yule Dada akauliza kwani unasafiri au unapokea mgeni? Nikamwambia nasafiri ndio maana nipo na begi la safari yule binti akaguna akaendelea na safari. Baada ya dakika kadhaa nikaja kugundua kumbe nimechafuka taabani Shati ipo hovyo, suruali chafu mwili wote haupo sawa nikasema hivi hapana itabidi nitafute sehemu yenye maji ninawe tu uso then kwakua kwenye begi Kuna Shati bado sijavaa Ile itanisave. Kuja kuangalia nikamwona yule Dada bado hajafika mbali kwa kuwa mimi ni kamanda ikabidi nikimbie kumuwahi mpaka nikamfikia, nikamwambia samahani Dada sijasahau chochote ila nilikuwa naomba kama una maji ninawe tu uso nitashukuru sana. Bahati nzuri alikuwa na maji kwenye kidumu cha Lita tano akafungua vimizigo vyake kulikuwa kuna kikombe ameweka akamimina maji nikanawa japo sikuwa na mafuta nikasema haina shida maana hakuna anaenijua huku. Yule Dada akaendelea na safari zake mm nikabaki pale nikafungua begi ili nibadilishe Shati japokuwa suruali ilikuwa chafu ila uzuri ilikuwa na rangi ya kaniki kwahiyo nilipangusa vumbi kwa maji nilikuwa nanawia ikakaa poa ila ukisogea uchafu unaonekana tena mwingi tu.
Nilipofungua begi nikakuta Ile Shati ndohaitamaniki kabisa kumbe yule jamaa aliefungua begi langu kule polini aliipakaza midamu pia alikuwa nguo zote anazibwaga chini na pale chini ndosehemu pia walichuna yule mnyama, nikiangalia hii niliovaa nayo kituko bora yenye midamu ila shida ni nyeupe zile damu zinaonekana kila sehemu. Ikabidi niende kwenye mti flani nikakaa kutuliza kichwa changu maana kupanda kwenye bus na Ile hali sio rahisi. Nilikaa kwenye ule mti baada ya hapo sikuelewa kilichoendelea kumbe nikajiinamia nikapiga usingizi mzito sana. Nikiwa kwenye ndoto nikawa nasikia sauti "wahi upande kaka bus linaenda mbali hili". Nikakurupuka kutoka usingizini kuangalia mbele nikasikia muungurumo wa bus na nipo mbali kidogo na barabara maana nilipoenda kumfata huyu binti anisaidie maji sikurudi barabarani kwahiyo nikaanza kukimbia kwenda barabarani mpaka bus nikiwa naliona kwa macho yangu linapitiliza huku nikimbwata kwa nguvu sauti yenye mlipuko "SIMAMAAAAAAA“....." SIMAMAAAAAAAA", lakini holaa juhudi hazikuzaa matunda Sasa pamoja na bus kupitiliza ilinibidi begi nilishike kwenye mkono nikavuta pumzi baada ya hapo niliondoka kwa kasi ya kulipuka kama Mbape anaechezea Monaco kwa mkopo, dakika sifuri nipo barabarani huku nikiwa napukuta mkono kwenye site mirror ya dreva maana bus halikuwa mbali sana nikaona mwendo wa bus umepungua na kusimama kabisa. Nilipofika kwenye gari nikapanda safari ikaanza Ile naingia ndani kutafuta siti kila mtu ananishangaa ninavyovuja mijasho niponipo tu wenge la kutosha nikawa sipo sawa kimsingi.
Tukapita mpaka maeneo ya Ile shule ya chinongwe huku nikiwa na huzuni sana. Nilipoenda kukaa kulikuwa Kuna Dada mmoja tukakaa nae ila ajabu nikuwa kila mda alikuwa ananiangalia nilivyo kwa jicho la kuibia mm nikawaza nikasema ndoishakuwa hivi Sasa nitafanyaje. Safari iliendelea ikafika mda nikarelax tu na gari ilipokaribia main road konda akapita kuchukua nauli nikamwambia mm nina 22000 Sina 25000 akasema toa, nikampa akarudisha 3000 yangu huku safari ikiendelea na uelekeo ni Dar Es Salaam japo baada ya hapo itabidi niende mkoa wa pwani mlandizi huko ndokuna rafiki wa baba angu nilielekezwa nikakae. Tukapita baadhi ya vijiji ila tulipokaribia lindi mjini eneo moja linaitwa DARAJANI ni mbele kidogo kutokea mnazi mmoja ukiwa unaelekea lindi mjini, Bus la machinga likaharibika ikawa ni saa tano kasoro hivi. Nikajua ni hitlafu tu baada ya dakika kumi hivi tutasepa. Kumbe tatizo lilikuwa serious sana walihangaika kulitengeneza zaidi ya masaa matatu lakini hakuna kilichofanyika kufika saa nane hivi abiria wakaanza kuwaka wakidai waagiziwe bus jingine ili tuweze kuondoka. Kumbe tulikuwa tunabwata tu maana wafanyakazi wa lile bus wote waliondoka akabaki dereva peke ake. Abiria wakasema kama hamtaki kutuletea bus jingine mtupe nauli zetu.
Mpaka inafika saa tisa hakuna jipya, ilibidi abiria mmoja apige simu kwa traffic polisi waje eneo husika na baada ya mda wakafika huku wakimkoromea dreva kwanini hataki kupiga simu kwa boss alete bus jingine ili abiria tuondoke na kila abiria alisema hata saa sita usiku wao wataondoka hawataki kulala lindi. Wale polisi wakapiga simu kwa boss akaja meneja wa kampuni ni mwarabu kembamba hivi kilikuja na harrier nyeusi huku kanagonga konyagi. Kalipofika kakauliza KIDAGAA yupo wapi? Yule dreva akasema kidagaa kaenda mjini anakuja mda si mwingi, nadhani kidagaa ni yule konda. Abiria wakawa wanawaka kweli huku njaa zimetuponda nikaona yule meneja mwarabu anajibu kwa dharau akisema "Mnawahi wapi nyinyi acheni kututisha" halafu anaongea mbele ya polisi huku anavuta sigara. Kitendo kile kilinifanya nikakwazika sana nikajisemea moyoni "your richness can't buy our dignity", ikabidi ninyanyuke nikamsogelea nikaona kashtuka huenda kutokana na mwonekano niliokuwa nao nikamwambia usiogope NAOMBA NIRUDISHIE NAULI YANGU kakajibu kwa jaziba kakasema mpumbav wee leta hiyo tiketi, nikatoa tiketi mfukoni kakaangalia halafu kakaingia mfukoni kakanipa 23000 yangu kakasema haya katafute gari Lako nikamwambia poa. Ni kaingia kwenye bus nikachukua begi langu nikakaa pembeni kuangalia ustaraabu mwingine. Baada ya mda kidogo huyo kidagaa akafika na spea ili watengeneze chapu bus liondoke, walikukuruka lakini wakaufyata.
Ngoma ilipoonekana ni ngumu ikabidi yule mwarabu aagize Kosta yake sijui inapiga root gani akasema iende haraka GEREJI ifanyiwe service ya kutosha maana inabidi ipeleke abiria Dar Es Salaam halafu pia wachukue Costa yoyote hapo lindi mjini ije uchukue abiria wake wakakae pale stend maana kuendelea kukaa pale darajani ni kupoteza mda. Kweli baada ya Lisaa Costa ikafika kuwapakia wale abiria wote wakiwa na mizigo yao tena zilikuja mbili ili waweke kambi lindi mjini kusubiri Kosta yake ifanyiwe service waondoke kwenda Dar Es Salaam maana gari kubwa lilikuwa halitengenezeki tena kwa mda huo. Costa zilipofika tu yule mwarabu akasema pakia wote ila huyu jamaa alierudishiwa nauli simtaki tena nadhani kwanza hata muonekano wake akili zake haziko Sawa. Kidagaa ambae ndomfanyakazi wake anaemwamini akasema 'imeisha iyoo'. Abiria wote wakaondoka nikabaki mimi tu maeneo yale na baadhi ya mafundi waliokuwa wanalinda lile bus.
Sina hili wala lile nikaona bus limewaka ila boss wao akasema walipeleke sehemu moja inaitwa mnazi mmoja wakalilaze, huenda bado lilikuwa na shida somewhere. Kwahiyo wakaondoka wote mimi nikabaki pale huku nikishuhudia jua linazama kwa macho yangu bila kugusa chochote mdomoni lakini safari yangu haina matumaini tena kama mwanzo. Nilikaa sana pembeni kidogo mwa Ile barabara mpaka mida ya saa moja hivi Kuna Majamaa yakapita nikayauliza kama nitapata msaada wa usafiri wakasema wao sio wa husika wa mambo hayo ila sehemu nilipo si salama Kwangu inabidi niondoke maana pale darajani Kuna matukio makubwa ya kiharifu huwa yanatendeka. Nikaona hapa nimelikoroga ikabidi nitulize akili yangu vizuri nikasema ngoja kwanza niangalie zile namba za simu kwenye karatasi za yule mzee wa mlandizi nikipata simu nimpigie kuwa sitafika Leo ila labda kesho mda wowote maana kama saizi ni saa mbili kasoro mlandizi nitafikaje Leo Leo. Nikachukua begi nikafungua zipu ya mwisho maana ndonahifadhi namba kwenye karatasi na line yangu ya simu. Kuja kucheki sioni line wala karatasi yenye namba za simu. Nikasema hapana hili ni wenge tu ngoja niangalie vizuri, nilipekua begi Zima sikuona line yangu yenye pesa 20000 niliyotumiwa na baba wala karatasi yenye mamba zangu muhimu [emoji22], nilikuja kugundua yule mpumbav wakule polini aliekuwa anakagua beg langu hovyo bila ustaraabu ndoaliangusha hivi vitu kwahiyo nikawa nimekosa vyote. Sasa ngoma iliyobaki nikutafuta usafiri mida hiyo ikawa ni saa tatu kasoro usiku kwa kuhisi na eneo nililopo niliambiwa si salama sana kwahiyo hapanifai inabidi niondoke.
......... Inaendelea usichoke.........
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Ofsa tupia episodes 6 za haraka haraka hii stori inanisahaulisha madeni.
Mm ntakaeandika tanzania na aliendandika prutable unaona tuko sawa,anyway .....
SawaSiyo wanaume wote, hao ilikuwa ni kwa mpango maalum!
Huwezi kupita mapito ya wanaume ww,kinachowabeba nyie ni kipochi manyoya [emoji1787]Dah!mi najionaga Nina matukio Mpwa yako kibokoooo.
Elezea kidogo mkuuMwanaumee km mwanaumee ktkt utafutaji tunapitiaa mengi sanaaa ,hapaa ninaposomaa uzii huu napitiaa magumu mpk naonaa ninachokisomaa kwa jamaa bado naonaa alipitiaa madogo maana yy bora hata alikuwa anakutanaa na binadamu Wanamsaidiaa mia mia mbiliii ,kuliko mm nilikutana na wanyamaa badala ya binadamu walitakaa kuniuaa nakunila kbs ,ila MUNGU acha aitwe MUNGU [emoji120][emoji120][emoji120]
-------SEHEMU YA KUMI NA MOJA - - - - - -
Nilipokula chipsi yai makamu akaja kuniletea maji ya kunywa nakunionyesha sehemu za muhimu kama Choo na bafu. Nikalala fofofo japo ni chini kwenye sakafu lakini usingizi ulikuwa mtamu sana kutokana na uchovu mzito niliokuwa nao tangu nimeondoka Dar Es Salaam sikuweza kulala kwenye chumba zaidi ya hapo shule ya sekondari chinongwe. Asubuhi palipopambazuka makamu akaendelea na majukumu yake maana ndomtu pekee alikuwa yupo karibu na mimi kwa wakati huo. Mida ya saa sita hivi mchana akaniita nahitajika ofisini mkuu wa shule kafika. Nilipoenda yule mkuu akasema aone vyeti baada ya hapo akaniambia je nipo kwa malipo au Bure?. Nikaona huu ni mtego hapa nisilete tamaa ikabidi nijibu shortly kama swali linavyouliza nikasema 'bure', wakatabasamu Kisha mkuu wa shule akasema kuwa ngoja aitishe kikao cha dharura na walimu wenzake halafu saa saba hivi nitaitwa kwahiyo nikatoka nikaenda chumbani nilipopewa hifadhi ya mda. Baada ya nusu saa tu nitaitwa yule mkuu kwa kigugumizi akasema walimu wenzake wamependa sana swala hili ila niwape mda wajipange maana siwezi kufundisha tu bure bila hata ya vocha hiyo ni Violance. Mimi nikawaka nikasema violence kiaje Kati mm ndonimeamua nisilipwe nyinyi msijali mm nitafundisha bure kwahiyo rekebisheni mazingira ya msosi tu maana pakulala tayari japo kuwa ni chini ya sakafu ili msijali.
Walipoona nimekuwa mkali wakajua kweli kijana kapondeka, kwahiyo mkuu akampigia simu Afisa elimu kata kwamba aje Kuna dharura, yule Afisa elimu kata alipofika wakaamuru nitoke ndani niwaache wajadili. Baada ya mda mfupi nikaitwa wakasema niwe mvumilivu watajitahidi kufanya kikao cha wazazi mwezi ujao kwahiyo niende nyumbani wataniita. Yule Afisa Elimu kata akasisitiza kuwa yeye ndie atashughulikia swala Hili la michango ya pesa kwa wazazi ili angalau niwe napata ya Sabuni maana vinginevyo sitaishi. Maisha bila pesa ni uongo aliongeza. Kuna mda inabidi kushuka chini tu kuepusha taflani maana nilikuwa ugenini hivyo ikabidi nikae tu kimya ila nilijua fika haya mambo yote huyu makamu JAFE ndokapenyeza. Baada ya mjadara mrefu nikakubali yule Afisa elimu kata akaondoka nae mkuu wa shule akasema twende kijijini cente nikapate chakula japo nilijua ni mbinu zakunipoza machungu. Awamu hii hata sikuwa na hamu ya chakula maana nilikereka sana nikajisemea hii ni laana au nini? Mbona mambo hovyo kiasi hiki shida nini. Anyway tukapanda kwenye pikipiki na mkuu wa shule mpaka center ya kijiji kufika pale mama ntilie hauzi kingine zaidi ya WALI NJUGU. nikaagiziwa sahani moja ya Wali njugu nikala nikashiba japo msosi ulikuwa local sana kama Wali maharage wa shule ya sekondari songea boys [emoji23][emoji23][emoji23].
Baada ya hapo akanirudisha shuleni niende nikapumzike ila tulipofika tu nikamwita yeye mkuu na makamu nikawaambia hali yangu ya kiuchumi sio nzuri na mfukoni nina buku tano tu hivyo kusafiri kesho ni uongo maana nauli Sina. Wakaniuliza kwani naenda wapi nikasema Dar Es Salaam ila nivumilieni nijaribu kuwaomba ndugu zangu pesa wakituma ndonitaondoka. Mkuu akasema Sawa wewe kaa tu hata siku 3 maana ugali utakuwa unakula huu wa wanafunzi, kumbe pale shuleni Kuna wanafunzi mchana wanakula palepale kwahiyo nitakuwa nachukua ugali wa kutosha mpaka nachajioni. Baada ya hapo mkuu akasepa tukabaki mm na makamu maana makamu anakaa hapo hapo shuleni kwenye Kota za walimu,yule makamu akawa anasema umeamini maneno yangu? Nilikwambia mapema hapa hakuna kitu huyu mkuu kakusumbua tuuu.
Mtihani uliokuwa mbele yangu ni sehemu ya kwenda baada ya hapo nilipo maana Sina jipya tena. Ilibidi niombe simu ya makamu nijaribu kuwapigia simu ndugu jamaa na marafiki kuomba msaada wa nauli. Makamu akanipa kisimu chake kidogo akasema nitumie kwa mda huo baadae atachukua nikasema poa. Jaribu huku na kule kuomba nauli lakini wapi. Sehemu ya kwenda sijajua ila nauli kwanza mengine yatafata. Mwisho wa siku ilibidi nipige simu kwa baba angu kijijini nimwambie ukweli wote, Ile kupiga tu akasema ni bora nimepiga maana kanitafuta sana hata hivyo anahitaji nimsaidie 5000 ya dawa jino lake bado linamsumbua sana. Machozi yalinitoka [emoji22].
Nikamwambia baba ebu kwanza avute pumzi Kisha nikasema ukweli wote wa yale yaliyonitokea sikumficha hata moja baada ya hapo nikamwambia nimekwama huku ruangwa kwenye miji ya watu akasema kwann sikumpa taarifa? Nikamwomba msamaha akaniambia nivumilie kidogo atanipa taarifa kama atafanikiwa, kumbe mle ndani kulikuwa Kuna debe nne za mahindi akaenda kuuza zote akanitumia 20000 halafu ndani wakabaki na Unga tu waliosaga siku mbili zilizopita. Nilisikitika sana ila sikuwa na option baada ya mda akapiga tena simu akasema nauli aliyotuma haitoshi kunifikisha kijijini kwetu kwahiyo amemuomba rafiki yake wa zamani sana yupo mlandizi sehemu moja inaitwa DOSA AZIZI niende huko kashaongea nae, nikamwambia anitumie namba zake akanitumia mda huohuo.
Nikiwa nipo kwenye mawazo mazito pamoja na kwamba nimetumiwa hiyo pesa ila najua niendako nitakuwa mzigo tu sitakuwa na msaada wowote lakini no way itabidi asubuhi niondoke tu. Ghafla makamu akaja kuchukua simu yake akauliza kama nimepata nauli nikamwambia hapana, nilikataa kwa kuwa nilikuwa kwenye msongo mkubwa wa mawazo maana nimekumbuka sana. Alipochukuwa simu yake akaondoka, midaa ya saa mbili hivi usiku Kuna mtoto flani wa kike kanakaa kwenye hizo Kota za walimu kaliingia kwenye mjengo nilimo mimi kakaenda uwani haraka Kuna kitu kalienda kuchukua Ile kanataka kutoka namm nikakaita mlangoni Kwangu Ile kukiita tu kumbe mama ake alikuwa anaona mwanzo mwisho kale kabinti kakawa kanaona aibu kunitazama namm nikakashika mkono nikaona kamelegea, ghafla nikasikia sauti nzito inaita WE MARIAM lahaulaaa alikuwa ni yule madam muiraki kumbe huyu ni mtoto wake wakumzaa.
Niliposkia tu hiyo sauti moyo ulienda mbio kutazama ni yule madam nae makamu akawa ametoka nje kuongea na simu ikabidi nikaachie mkono kale kabinti yule madam akaongea kwa sauti "we mkaka kumbe umekuja huku kubaka watoto zetu?. Nikajisemea moyoni" Nilidhani yamekwisha kumbe ndoyanaanza", Kiukweli tamaa iliniponza tu haka kabinti tangu asubuhi nilikuwa nakamezea sana mate ni kirefu kiasi cheupe kama unawajua wamburu walivyo lakini pia kana kishepu kiasi hakana tumbo kabisa yani kamekatika, kwahiyo kalipopita kuchukua ule mpira nadhani wanachezaga netball mimi nikasema haka Katoto bado kamoto nikikafunua hata dakika mbili hazifiki nishamaliza kazi maana papuchi yake ni tofauti na Ile miji mama inayosimama pale buguruni sokoni usiku. Mambo ya kabadilika yule binti akaitwa akaanza kupokea kichapo cha kufa mtu mpaka makamu akaenda kumpokonya fimbo yule madamu, makamu akauliza nini shida? Akaambiwa kila kitu kilichofanyika baina yangu na mtoto wake. Yule mtoto approximately Ana miaka 16 au 17 hivi.
Makamu baada ya kuambiwa hivyo akaja moja kwa moja Kwangu anafoka, kumbe ndonia yako we mbwa, fataki firauni weeee sijakaa Sawa akaniwasha kerebu moja nzito sana kwenye shavu na mitama, pamoja na hayo yote sikutaka kabisa kupaniki maana wangepiga kayowi nikajaziwa kijiji. Nikaona yule madam kachukua simu akawa anampigia simu mkuu wa shule nae pia makamu anapiga kwa huyo huyo mkuu wa shule, nikasema Leo ngoma hii sio nyepesi nimelikoroga. Pressure ilinipanda sana japo nilijua hii kesi haifiki mbali maana siku fanya nae simple harmonic motion. Kwahiyo makerere yote yale nilijua ni vita ya mieleka tu sio urusi na Ukraine.
Dakika kadhaa nikaona mkuu wa shule kafika na pikipiki anahema kama kakimbizwa nikaona ghafla Kwangu kanishika Shati huku anauliza kwa jaziba kwanini nimebaka, nilicheka kidogo japo kwa fedheha, ni kapigwa kofi kwenye lile lile shavu nililopigwa kerebu na makamu mpaka nikahisi kama pamevimba. Nikajibu kwa upole kuwa sijabaka huyu madam katukuta tumeshikana tu mikono tena sio chumbani ni hapa kwenye mlango wa chumba changu. Wote wakiwa kwenye taharuki nikaona makamu kistarabu akamwita mkuu wa shule pembeni wakateta kwa dk kumi hivi Kisha wakaniita wakaniuliza nina bei gani mfukoni?. Nikawa jibu nina 5000 nikaona yule makamu anatoa 20000 mfukoni kwake akanipa akasema kwenye ISHU za wanafunzi wako very serious na mwanafunzi yoyote atakae Pata ujauzito huwa wanawekwa kwenye wakati mugumu sana na wakubwa zao ikiwemo maafisa elimu na wakurugenzi kwahiyo hilo jambo nililotaka kulifanya ilikuwa ni hatari Sana. Wakaniambia huyu madam hanaga dogo kesho asubuhi anaweza kufikisha hili swala kwenye kamati ya nidhamu kuhusu uwepo wa kibaka kwenye shule hii kwahiyo beba begi Lako usiku huu yani mida hii tunayozungumza uwe umeondoka tunaamini wewe ni mwanaume utajua mbele ya safari, asubuhi Kuna Bus la linaitwa MACHINGA huwa linapita hii barabara linatokea NACHINGWEA linaenda Dar Es Salaam asubuhi utapanda uende kwenu kwahiyo nenda ndani beba vitu vyako uondoke. Wote watatu walionekana kujaa upepo na jazba kupita kiasi, nikaingia ndani nikabeba begi usiku wa saa nne nikaondoka kwenye eneo lile mbaya zaidi ni kijijini pamepoa sana mida hiyo ni kerere za chura tu ndozinasikika basi.
......... Inaendelea usichoke.......
Pole sana,Tarehe 4 mwezi wa pili 2020 nikiwa katika msongo wa mzito wa mawazo yaliyotokana na ugumu wa maisha nilijikuta nafanya maamuzi magumu bila kutarajia. Nilikuwa nakaa gheto maeneo ya buguruni sheli japo gheto lilikuwa na mshikaji wangu ambae tulisoma nae primary mawenzi shule ya msingi iliyopo moshi mjini mwaka 2006 ndotulimaliza darasa la saba hapo.
Nikiwa nimelala saa sita usiku naona napigwa mgongoni kwa nguvu kuamka namuona rafiki angu tunaelala chumba kimoja pia ndommiliki wa gheto mm kaniweka tu kishkaji, nikasema kulikoni jamaa akajibu kiunyenyekevu akisema "oya demu wangu kafukuzwa na Dada ake alipokuwa anakaa kwahiyo hana pakwenda nasaizi ni saa saba usiku amekuja yupo hapo kibarazani anataka tulale humu kwahiyo please wewe ni mwanaume ebu tafuta ustaraabu wa kuondoka saizi ukija asubuhi tutaweka mambo Sawa ".
Nikamwambia sasa mda huu mm niende wapi ndugu na Sina hata sehemu yakujiegesha!? Akajibu nitajua mwenyewe, ikabidi nivae niende kimboka night club kupoteza mda nikawa naangalia movie kwenye mabanda ya pale kimboka maana majamaa huwa hawalali. Ilipofika asubuhi nikatia timu bahati nzuri nikakuta wote wameamka ila wapo kitandani nikamsalimia shemeji pamoja na jamaa angu japo hawakuonesha uso wa tabasamu walikuwa serious kiasi ambacho nilishindwa kuwaongelesha.
Nilipotazama juu kwenye enga zakuwekea nguo zangu ghafla sikuona nguo yoyote, nilipouliza jamaa akasema nimekuwekea kwenye begi ili ukija usisumbuke kuzipanga maana shemeji ako kasema yeye hatoki atakaa hapahapa sasa hatuwezi kulala watatu. Ilikuwa ni kipindi kigumu sana Kwangu zaidi ya Alpha konde alipotolewa madarakani. Nikatazama juu chini nikawaza nikasema haina shida.
Nikabeba begi langu nikawaaga wakasema kila raheli. Nilikuwa na simu Aina ya tecno F1 na mfukoni nikawa na 20000 nikasema Poteleapote nitaenda popote pale kutafuta rudhiki.
Kwa pesa niliyokuwa nayo kukaa Dar Es Salaam hapakunifaa tena, hiki ndokipindi ambacho mikoani unapaona nafuu kuliko jiji la Dar Es Salaam. Nikiwa na begi langu Zito la nguo mpaka mida ya saa kumi jioni nilikuwa sijajua niende wapi na nitalala wapi. Nilipoona mda unakwenda ilibidi nimfate jamaa mmoja ivi yeye anauza nguo za jinsi buguruni sokoni kama unaenda shell nilipofika alinichangamkia akijua ni mteja kumbe ni mtu mwenye dhiki aliehitaji msaada. Sikupoteza mda ilibidi nimwambie ukweli yote yaliyotokea ila msaada wangu mkubwa ilikuwa anitafutie mteja wa kununua simu yangu.
Akasema nauzaje nikamwambia simu nauza 90000 tu jamaa akasema ngumu kupata mteja leoleo Sema ngoja nimpigie simu Dada mmoja anauza chakula Ana shida sana na simu kubwa. Yule dada akaja alivyoiona na alivyokuwa na pupa ya kumiliki smart phone nikajua tu huyu ni mteja. Jamaa akasema niongee nae ilibidi nimwambie nauza laki moja maana ngozi nyeusi ukitaja bei harisi ushahalibu. Yule Dada akasema ana 80000 nikajifanya nakataa akaongeza 5000 nikamwambia toa pesa akanipa nikampa simu akaagana na jamaa akaondoka. Sasa kimbembe kikaanza Kati ya mm na huyu Dalali.
Jamaa nikampa 5000 akasema niache utani inabidi nimpe 20000 nikacheka kidogo huku mdomo ukiwa umekauka maana mpaka jua lilizama sijapata chochote cha kuchezesha kinywa changu.
Nikamwambia 20000 hapana kutokana na shida niliyonayo jamaa akasema vinginevyo anamwambia yule dada hii simu ya uwizi arudishe. Nikaona isiwe tabu nikampa 10000 nikasema hutaki naondoka na pesa sirudishi maana ilibidi nikunje sura vinginevyo nitakwama. Jamaa akapokea.
Alipopokea Ile pesa nikapotea mda huohuo. Sasa kimbembe nipakulala maana ikawa ni usiku huku nikiwa nimechoka sana. Nikaingia bar moja ivi inaitwa sewa. Nikaongea na muhudumu akasema Vyumba kwanzia saa saba usiku mdaa huu ni short time. Kwa kuwa nilikuwa na shida nikavumilia Ilipofika saa saba nikawa hoi kweli kweli nikiwa nimekaa kwenye kiti huku bar ikiwa imefungwa yule muhudumu akaja akasema kaka pole nenda kalale chumba hicho apo. Akasema nimpe 4000 tu maana naonekana sipo sawa. Nikampa pesa yake Nikaingia kulala japo madadapoa walikuwa wanagonga sana mlango niwafungulie lakini sikujali.
Asubuhi kukapambazuka nikasema leo inyeshe mvua liwake jua sikai Dar. Mm nimemaliza kidato cha sita ila sikubahatika kuingia chuo kikuu lakini najua sana kufundisha. Nikasema hapa ngoja nikatafute kibarua cha kufundisha mikoani ila tu isiwe dodoma. Nikawaza sana nikasema hapa safari ni kwenda lindi. Nikachukua daladala mpaka mbagala, ilikuwa saa sita mchana, kufika pale wakasema mda huu Gari za lindi mpaka temeke hapa mbagala ipo gari ya kwenda kilwa mda huu inaitwa MASHALAH.
Kwasababu kichwa changu mda huo hakikuwa sawa nikasema nikate tiketi tu hata ya kwenda kilwa nitajua mbele ya safari. Wakasema nauli Dar mpaka kivinje ni 11000 halafu Dar mpaka kilwa ni 13000.
Saa sita na nusu tukawa tumeondoka Dar Es Salaam kuelekea kilwa nikiwa Sina ndugu wala yoyote anaenijua lakini nikiwa na Amani ya moyo kwakuwa kilwa sio sudani wala Uganda ni Tanzania pia.
Inaendelea...
Safari ya kuelekea Kilwa ikaanza. Nililipa nauli ya Dar Es Salaam to Kilwa shilling 13000 mfukoni mpaka na panda bus nikawa nimebakiwa na 70000 tu kutokana na pesa nyingine Jana usiku Nililipa gest 4000 asubuhi kabla ya kwenda kukata ticket nilienda saloon kunyoa kwa 2000 baadhi ya pesa nilikula mihogo na maji ya kunywa njiani. Ubovu nikuwa kwenye siti nilikuwa nimekaa na mtoto mdogo wa kike ambae alipakiwa na mzazi wake ila yeye huyo mzazi hakuwa anasafiri sasa akaniambia kuwa nimsaidie kumwangalia lakini pia konda alikuwa amepewa taarifa kimsingi ni mtoto ambae huenda ni miaka 11 au 12 huyu dogo yeye alikuwa anashukia somanga. Kwahiyo nikakosa hata msaada wa kuanzia nikifika kilwa itakuwaje maana nilikuwa nategemea labda mtu nitakae kaa nae atanipa mawazo namna ya mji ulivyo na jinsi ya kuhendo swala langu. Tukiwa safarini ilibidi nimuulize huyu dogo endapo anaijua kilwa ili tu nipate pakuanzia dogo akasema yeye hajawahi fika anaishiaga tu somanga maana ndo kwao. Nikapiga moyo konde nikajisemea moyoni kuwa liwalo na liwe itajulikana.
Tukiwa safarini niliona kibao kimeandikwa IKWIRIRI gari likasimama kwa dakika chache nikajiuliza kulikoni tena kumbe Kuna wa mama walisimamisha wakapanda lakini cha ajabu walikuwa wananuka shombo ya samaki na mabeseni yao. Kuna mmoja alikuja kusimama karibu yangu nikamuuliza kama Ana samaki akasema Sina mwanangu samaki zimeisha. Nikakausha huku mawazo ya kwenda nisipopajua yanakuja nakunikosesha raha kabisa. Mungu yumwema baada ya dakika chache nilipata usingizi mzito sana hii nikutokana na siku ya jana kutokupata usingizi wa kutosha namm kulala Kwangu nikupumzisha mawazo. Nilikuja kushtuka kutokana na makerere mengi yawafanyabiashara wadogo wadogo hususani wanaouza biskuti, korosho, mahindi ya kuchoma na kadharika, kuangalia pembeni dogo simuoni niliyeambiwa nimwangalie nikasema kulikoni tena nikaamka chapu kwenye siti nikaenda kumuuliza konda dogo niliekaa nae yuko wapi??. Konda akasema nina mambo mengi kaka huyo dogo ni yupi? Nikamwambia nilikuwa nimekaa nae siti moja mm nikalala lakini cha ajabu simuoni konda akasema keshashuka. Nikamuuliza kwani somanga tumepita maana mm ni mgeni konda akasema nipande kwenye bus hapo tulipo ndosomanga yenyewe na dogo kashapokelewa na wazazi wake tayari.
Nikapanda kwenye gari. Bus likaiacha somanga na safari ya kwenda kilwa ikawa imewaka moto, niliona bus limejaza wa mama ambao walikuwa wanauza samaki kwenye bus. Kwa kuwa nilikuwa na njaa sana nikasema hapa samaki ni bei sana nilifanya mistake kutokununua muhindi wa jero somanga anyway nitauliza kama ana samaki hata wa buku mbili hata kambale nitatafuna usabato nauweka pembeni.
Nikiwa nasubiri afike Kwangu yule mama muuza samaki nikawaza wale wa mama wa mwanzo waliopandia IKWIRIRI kwani ni tofauti na hawa? Mbona siwaoni? Pembeni Kuna mzee mmoja alipandia somanga kwahiyo tukawa siti moja nikamuuliza akasema wale kwao ni somanga IKWIRIRI huwa wanaenda kuuza samaki wakiisha wanarudi somanga, nikasema hapo Sawa
Mama muuza samaki akawa amefika Kwangu nikamwambia sogeza beseni nichague mwenyewe mama akasogeza beseni la samaki nijichagulie.
Kucheki kwenye beseni niliona samaki wakubwa tupu Aina ya kibua na Changu. Nikajisemea moyoni hapa nimetoka patupu hawa samaki bei yake siiwezi lakini acha tu nimuulize ni bei gani akitaja nimrushe aendelee kuwauzia wengine. Yule Dada akasema samaki ni buku buku. Nikasema ebu rudia tena? Akasema kaka bei haipungui samaki mmoja ni elfu moja. Jamani sikuweza kuamini samaki mkubwa ambae Dar Es Salaam ni 7000 somanga anauzwa buku. Nikasema hapa ndo penyewe nikamwambia anifungie samaki wa buku mbili.
Nikachagua samaki wangu huku nikiwa na tabasamu la kusahau shida kwa dakika chache nitakazotumia kumnyanvua samaki na minofu yake. Mama akachukua samaki akawafunga kwenye gazeti na kumimina chumvi kiasi. Kwa kuwa biashara ni cash to cash basi ikabidi nitoe wallet nimpe pesa yake. Ningaingiza mkono mfuko wa nyuma sikuona wallet nikasema hivi kumbe nimeweka mfuko wa mbele kuangalia mfuko wa mbele wallet hakuna, nikasema nini tena nikaangalia mifuko yote Hola jasho jembamba likianzaga tu kunitoka ujue kweli. Yule mama akasema napitia nikamwambia Sawa aendelee tu kuwauzia abiria wa nyuma akianza kurudi atapitia...
Ikabidi niangalie chini ya seat huenda imedondoka yani Sasa mpaka mwili ukawa unatetema kichwa hakipo sawa na wale samaki nikawadondosha chini kwenye abiria huwa wanapita tukiwa tumekaa.
Nikasema hapana sio kweli wallet imeenda wapi?? Ilibidi nipaniki nikamnyanyua yule mzee tukiokuwa tumepanda nae mzee alivyoniona tu kuwa sipo Sawa nikaona akasimama nikawa naangalia kila Engle ya seat lakini sikupata wallet yangu yenye pesa zangu.
Abiria wa pembeni yangu wakaniuliza kulikoni nikawaambia kilichotokea wakaishia tu kunipa pole. Nikajisemea labda nikiweka kwenye begi? Lakini sio kweli maana mpaka begi linawekwa kwenye boot la bus nilichomoa pesa yangu nikiwa ndani ya bus nikanunua maji tukiwa Mbagala rangi tatu. Nikiwa nimechanganyikiwa nikasikia konda anatangaza kijiji flani jina nimesahau Kuna jamaa yupo nyuma akasema kwa sauti "shusha" konda akamwambia asogee mbele maana washafika ikumbukwe kuwa Ile misamaki kipindi nasechi wallet yangu nilidondosha chini ya tule tunjia twakupita abiria, jamaa aliekuwa anashuka akapiga akazikandamiza na American buti zake samaki zote zikawa chapati tena zikagandamana na kapeti la bus.
Ile nasema we jamaa umekanyaga samaki zangu akajibu kwa hasira hapo ndo bakuli ilipo samaki unazibwaga njiani, ikabidi ninyamaze Sasa nikawa sipo Sawa kabisa maana wallet siioni samaki sijalipia na mama ndo huyo anakuja kutoka nyuma kudai pesa ya samaki shilling 2000 na samaki zimekanyagwa hazitamaniki kiasi ambacho hata paka hawezi kula.
SEHEMU YA TATU
SEHEMU YA NNE
SEHEMU YA TANO
SEHEMU YA SITA