Sitosahau, Special thread

Shy land

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2013
Posts
6,208
Reaction score
2,767
Je? Una tukio ambalo umewahi kukutana nalo katika maisha yako tangu uzaliwe hadi ulipo, na ambalo kwa namna lilivyotokea hutokaa ukalisisahau kabisa? Kama jibu ni NDIYO, Tuhabarishane hapa!

Iwe simulizi fupi mfano kukomba Mboga nakupewa kipigo cha ajabu, au pingine ni simulizi ndefu inayohusu mambo ambayo hutoyasahau katika maisha yako na unaona una sababu yakutujuza WanaJF ili tujifunze kupitia wewe.

Siyo vibaya kama tukahabarishana na watu wakapata fundisho kutoka kwako au pengine namna ya kutatua matatizo yanayotusibu katika jamii zetu.! mkasa wowote unaohusu maisha na ambayo umewahi kukutana nayo tuhabirishane wadau
 
sitosahau


mwaka huu filamu ambayo imetegenezwa na serikali kule kwenye mapango ya amboni tanga.
 
Sitosahau nilivyokamatwa kwa sababu ya kodi ya baiskeli kule Nachingwea
 
Mwaka 2008, April 17, Ijumaa, nilibanwa na mkojo nikiwa kwenye costa, katika Stendi ya Kabwe, Mbeya Mjini, kuelekea Mwakaleli. Kabla gari haijaondoka, nikaenda kukojoa uwanjani karibu na Barclays Bank. Kabla sijamaliza mkojo, nilikamatwa na jamaa fulani hivi, na akataka kunipa kichapo. Hapakuwepo na choo. Ilibidi nipige magoti na kumuomba msamaha, ndipo akaniachia. Nikarudi garini. Wasafiri wenzangu walinipa pole maana waliishudia sinema ile. Sitosahau! Na sijawahi kuisimulia hii kadhia popote zaidi ya hapa JF.
 

pole sana mkuu, hiyo inatokea sana ktk mazingira ya safari hasa ya mabasi.
 
Sitasahau 00's siku Ilboru secondary walikuja skuli kwetu Ekenywa Sec kuleta noma kisa ugomvi uliosababishwa na mademu. At that time ndo nimeanza form one chalii sana yani. Boarding students tulikuwa kama 60 hivi kwa ujumla (only boys then), na ilikuwa friday mida ya jioni kabisa so wanafunzi kibao wameondoka for the weekend, tukabaki roughly km watu 40 hivi. I don't know how we did it, ila we defeated them tukawakimbiza mpaka skuli kwao tukarudi na 'mateka' mmoja. Nakumbuka wale wababe walitaka kutufungia jikoni mi na dogo mmoja cos tulikuwa wadogo kinoma ingekuwa hatari kwetu, but i was not gonna miss all that fun for anything + nimezaliwa na kukulia Arusha (Thinking about it now, kweli ilikuwa hatari). Ile noma ilikuja kusuluhishwa na mkuu wa wilaya/mkoa (sina uhakika sana) mida ya night cos walirudi kumtaka 'mateka' wao and we weren't negotiating. Baada ya pale tulikuwa hatukatizi karibu na skuli kwao tukiwa na jezi za shule kwa muda mrefu sana.
 
Sitasahau siku moja nikiwa shule moja ya boarding machame tulizamia msosi (beche) msikitini. Actually tulialikwa na mchizi wetu ambaye alikuwa anaswali pale, tulikuwa wanne halafu wote wakristo ila tukajiandikisha kama waislam. Babaa muda wa swala ili tukimaliza ndo tule nikajiunga bana, nikafanya kama nilivyokuwa naona mpk nilipoona baadhi ya watu wamemaliza wanachomoka mmoja mmoja kwenye lines. Mzee nikajitoa na mimi nikawa nataka kupita mbele ya jamaa wa pembeni aliyekuwa bado anaendelea kuswali (nilikuja kuambiwa baadae ni makosa kufanya hivyo), nilishtuka jamaa kanirudisha nilipokuwa huku akiendelea na swala yake. Nikajua mchizi akimaliza kuswali lazima ani-mind na watastukia mi mamluki wanipe kipigo cha hatari, nili-sweat miguu na mikono ilikuwa km inamwagika maji, noma. Sema baada ya km dkk 1 hivi nilipata ujasiri nikapita kwa nyuma nikamkimbilia mwenyewe akanitoa wasi wasi.
 
kumbe kuna watu JF Wamekula chumvi! mkuu mwaka gan! ulilipa kodi ya kichwa.

Miaka ya 80 huko mkuu, watu tunawafungia ndani

wazazi wetu

Kisa kodi ya kichwa.

USIPOLIPA UNAPELEKWA KWENYE OFISI YA CCM

NDIO ILIKUWA MAHAKAMA UNAFUNGIA HUMO
 

Pole sana kamanda!!
 
Hii ilikuwaje Mkuu, fafanua kidogo.

Hii ilinyanyasa sana watu.

Watu walikuwa hawazalishi mali kutwa nzima ni kujificha

Tu milimani.

Au ni kuwafungia wazazi ndani ili mgambo wakija tunasema hawapo, mbaya zaidi walikuwa wanavunja

Na milango ili kuangalia kama kuna watu.

BIG GUP SANA MR CLEAN JAPO WATU WANAKUPONDA

ILA ULIFANYA VIZURI KUFUTA HII KODI.
 

Dah Mkuu kwa kusimuliwa mtu unaweza ukacheka sana.
Ila ndani yake na uhalisia wa kipindi hiko ni simanzi kubwa mno.
Poleni sana mliopitia kipindi hiko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…