Sitta: Katiba mpya izuie rais kubeba familia yake

Sitta: Katiba mpya izuie rais kubeba familia yake

Sitta hana credibiity ya kutoa maoni haya, yeye mwenyewe si msafi.
 
Mke wa Rais je? tujue wajibu wake na mipaka!!
 
Niliandika uzi kuhusu cheo cha mke wa rais kama ni haki kikatiba, je rais kama taasisi ina mke? au sio sahihi huyu mama kuitwa mke wa kikwete, na wala sio mke wa rais maana sisi hatujampigia kura Kikwete pamoja na mke wake. Kwa VILE MODS WANAELEWA SANA KULIKO MCHANGIAJI YOYOTE ILIFUTWE THREAD. Heri sita kasema.
 
kiongozi ni mme au mke, au mme na mke wake au mke na mme wake (Azimio la Arusha kwenye miiko ya Viongozi) ila nina wasiwasi kama Rais pia ni mtu na mke wake au mke na mme wake, si vibaya kwa mke wa Rais kufanya shughuli za kijamii zinazowezesha kuleta maendeleo lakini sio kama mkuu wa nchi. Aidha mke wa Rais kuendelea kujiwekea madaraka kama Mjumbe wa viti vya juu katika Chama siyo sahihi. Ni vema viongozi wajifunze kwa Mwalimu, ku-restrain familia zao kuingilia mambo ya nchi maana sio kuwa wanapendwa na wanaokutana nao kama wanavyoambiwa ni ama wanajipendekeza kwao au wanawaogopa.

Kwa Rais wetu jambo hili hakuliangalia mapema ndiyo maana mama na mwana wameingia, ila kuna wakati mwenyewe aliwakemea kwa mambo yasiyowahusu. Ila inapokuwa kwa mke bwana ukemeaji unakuwa finyu. Ni kweli Mke wa Rais ni public figure ila kwa nia ya kutunza nidhamu, hatutaki baada ya muda mke wa Rais au jamaa yake akashika kazi ya mama wa kwanza wa Kenya aliyepita aliyekuwa ana wakosovo watu publicly. Hiyo siyo sawa ila pia mke wa Rais kuwa kiongozi hiyo pia siyo sawa. Nadhani Katiba inaweza kubainisha kuwa Mke wa Rais, au Mtoto wa Rais asiwe kiongozi wa ngazi za utawala wowote au a-restrain kwenye mambo ya kisisasa ili amjengee Rais credibility maana uwezo wao siyo sawa. Nakubaliana na usemi kuwa Hatumchagui mke wa Rais bali Rais, ila kwa wenzetu mkeo na familia ni kigezo cha kuchaguliwa maana kama ni viruka njia huwezi kuchaguliwa. Tupendekeze kweli kuwa na mipaka ya uongozi na hasa inapokuja familia.

Alamsiki
 
WAZIRI wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amewasihi Watanzania wazuie katiba mpya isitoe rais dikteta na mwenye kutumia madaraka vibaya kwa kuinufaisha familia yake au jamaa walio karibu naye.

Sitta amesema analiona taifa linaelekea kwenye hatari kubwa, kwamba baadhi ya viongozi wanahangaika kuingiza mambo binafsi yenye maslahi ndani ya rasimu ya katiba mpya badala ya kuangalia utaifa.

"Hawa wanaoingiza mambo yao binafsi si watu wazuri kwa taifa letu, tukiwaacha waendelee na mchezo wao katiba mpya itakuwa chungu sana kwetu," alisema.

Sitta alisema Watanzania wanatakiwa kutengeneza katiba nzuri itakayomzuia rais atakayechaguliwa kuwa mroho na kutumia madaraka yake kuinufaisha familia yake au jamaa walio karibu naye.

Kiongozi huyo alitoa onyo hilo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua mkutano wa Baraza la Taifa la Vijana la Rasimu ya Katiba mpya unaotarajia kumalizika kesho.

Sitta alisema misingi ya utawala bora ndiyo silaha kubwa ya kuhakikisha viongozi wanaochaguliwa hawafanyi kazi kwa udikteta au masilahi binafsi.

"Nawasihi ndugu zangu tusikubali katiba mpya ijayo ikachezewa na wajanja wachache maana tukifanya hivyo kuna hatari tukatengeneza rais na serikali ya kidikteta" alisema.

Alisema kwa muda mrefu Tanzania imekuwa na historia ya kufuata misingi ya utawala bora hivyo ni vizuri jambo hilo likaendelezwa.

Sitta alibainisha kuwa katiba ni muhimu kwa mustakabali wa Tanzania na lazima wananchi wajenge utamaduni kuiheshimu na kuilinda huku wakiwaepuka watu wanaotaka kuwania madaraka kwa masilahi binafsi.

"Tunahitaji kiongozi mwenye kujali masilahi ya Watanzania, hatuhitaji yule mwenye kujali tumbo lake au la familia yake, haya yote yatafanikiwa kama tutaweka vipengele kwenye katiba yetu itakayowabana watu wa aina hiyo," alisema.

Muundo wa Muungano
Waziri Sitta alisema rasimu ya katiba mpya ilenge kupunguza gharama za uendeshaji wake kwa sababu Watanzania ni masikini na wanahitaji maendeleo.

Alibainisha kuwa hakubaliani na mapendekezo ya rasimu ya katiba mpya iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya uwepo wa mawaziri 15 kwenye Serikali ya Muungano ilhali mambo ya Muungano yapo saba.

Aliongeza kuwa wabunge 150 na mawaziri 15 wa Serikali ya Muungano ni kutapanya fedha za walipakodi wanadidimia kwenye lindi la umasikini.

"Wananchi wanahitaji maendeleo, tujikite kupunguza matumizi na mbwembwe mbwembwe zisizo na tija kwa taifa," alisema.

Alisema nchi nyingi za Afrika zimekuwa zikisuasua kupiga hatua kwenye maendeleo kwa kuwa fedha nyingi zinatumika kwenye uendeshaji wa serikali badala ya kupelekwa katika sekta zenye kuwainua kiuchumi wananchi.

Apinga marais watatu
Sitta alipendekeza kuwa kama muundo wa serikali tatu unaopigiwa debe na baadhi ya watu utafanikiwa ni vema vyeo vya marais wawili wa Zanzibar na Tanganyika vikafutwa ili kuiepusha nchi kuwa na marais watatu.

Alisema nchi mbalimbali zitaicheka Tanzania kama itakuwa na marais watatu ambao wote inaweza ikatokea wakakutana nje ya nchi.

"Tutakuwa watu wa ajabu sana huko kwa wenzetu, yaani sisi masikini halafu tuna marais watatu? Hizi gharama tunazotaka kumtwishwa mwananchi za nini?" alihoji.

Alisema kama kutakuwa na serikali tatu ni vema kukawepo na rais mmoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wengine wakapewa majina mengine kama Makamu wa Rais au Waziri Mkuu.

Sitta aliongeza kuwa hapingi muundo wa serikali tatu, bali hakubaliani na hoja ya uwepo wa marais watatu.

Aliongeza kuwa hoja ya kutaka marais hao watatu inashabikiwa na wenye uroho wa madaraka, wanaodhani inaweza kuwa njia rahisi kwao kufikia malengo yao ya kisiasa.

"Kuna watu wana kiu kubwa ya kuitwa mheshimiwa rais, ndiyo maana wanapigia debe uwepo wa marais watatu, nawaona ni wabinafsi tu hawana jambo jingine," alisema.

Ila kuhusiana na marais watatu kweli ni issue, mie ningependekeza tukawa na Serikali tatu na ili tusiwe na mgongano Selikali hizi ziongozwe na Waziri Mkuu au Waziri Kiongozi na tuwe na Rais mmoja, ila sasa wenzangu wa Zenj hilo wanaona soo. Ila kama wangeitwa hivi na mapendekez ya mamlaka na madaraka yakawa kama inavyopendekezwa naona tungekuwa na uhuru mzuri. Maana watakuwa Waziri Mkuu Mtendaji au Waziri Kiongozi Mtendaji, mambo machache ya Muungano yatashughulikiwa na Rais wa Muungano na isiwe vichekesho kama sasa ambapo hata Wizara zisizo za muungano zina Mawaziri toka Zanzibar, maana kama mawaziri wa wizara hizo wanakutana say EA Community, representation ni ya Zanzibar tu. Hii siyo fair. Na wizara za muungano zikiwa na mawaziri unaweza kupata Wazri Zanzibar au Bara na Naibu upande mwingine. Basi
 
Sitta ametumia mgongo wa rasimu kuelezea anachokichukia. Isingekua rasimu angeweza kuelezea haya yanayomhusu m/kiti wa chama chake?
Ni kweli serikali tatu ni gharama kama anavyosema au ccm wana agenda ya siri?

WAZIRI wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amewasihi Watanzania wazuie katiba mpya isitoe rais dikteta na mwenye kutumia madaraka vibaya kwa kuinufaisha familia yake au jamaa walio karibu naye.

Sitta amesema analiona taifa linaelekea kwenye hatari kubwa, kwamba baadhi ya viongozi wanahangaika kuingiza mambo binafsi yenye maslahi ndani ya rasimu ya katiba mpya badala ya kuangalia utaifa.

“Hawa wanaoingiza mambo yao binafsi si watu wazuri kwa taifa letu, tukiwaacha waendelee na mchezo wao katiba mpya itakuwa chungu sana kwetu,” alisema.

Sitta alisema Watanzania wanatakiwa kutengeneza katiba nzuri itakayomzuia rais atakayechaguliwa kuwa mroho na kutumia madaraka yake kuinufaisha familia yake au jamaa walio karibu naye.

Kiongozi huyo alitoa onyo hilo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua mkutano wa Baraza la Taifa la Vijana la Rasimu ya Katiba mpya unaotarajia kumalizika kesho.

Sitta alisema misingi ya utawala bora ndiyo silaha kubwa ya kuhakikisha viongozi wanaochaguliwa hawafanyi kazi kwa udikteta au masilahi binafsi.

“Nawasihi ndugu zangu tusikubali katiba mpya ijayo ikachezewa na wajanja wachache maana tukifanya hivyo kuna hatari tukatengeneza rais na serikali ya kidikteta” alisema.

Alisema kwa muda mrefu Tanzania imekuwa na historia ya kufuata misingi ya utawala bora hivyo ni vizuri jambo hilo likaendelezwa.

Sitta alibainisha kuwa katiba ni muhimu kwa mustakabali wa Tanzania na lazima wananchi wajenge utamaduni kuiheshimu na kuilinda huku wakiwaepuka watu wanaotaka kuwania madaraka kwa masilahi binafsi.

“Tunahitaji kiongozi mwenye kujali masilahi ya Watanzania, hatuhitaji yule mwenye kujali tumbo lake au la familia yake, haya yote yatafanikiwa kama tutaweka vipengele kwenye katiba yetu itakayowabana watu wa aina hiyo,” alisema.

Muundo wa Muungano
Waziri Sitta alisema rasimu ya katiba mpya ilenge kupunguza gharama za uendeshaji wake kwa sababu Watanzania ni masikini na wanahitaji maendeleo.

Alibainisha kuwa hakubaliani na mapendekezo ya rasimu ya katiba mpya iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya uwepo wa mawaziri 15 kwenye Serikali ya Muungano ilhali mambo ya Muungano yapo saba.

Aliongeza kuwa wabunge 150 na mawaziri 15 wa Serikali ya Muungano ni kutapanya fedha za walipakodi wanadidimia kwenye lindi la umasikini.

“Wananchi wanahitaji maendeleo, tujikite kupunguza matumizi na mbwembwe mbwembwe zisizo na tija kwa taifa,” alisema.

Alisema nchi nyingi za Afrika zimekuwa zikisuasua kupiga hatua kwenye maendeleo kwa kuwa fedha nyingi zinatumika kwenye uendeshaji wa serikali badala ya kupelekwa katika sekta zenye kuwainua kiuchumi wananchi.

Apinga marais watatu
Sitta alipendekeza kuwa kama muundo wa serikali tatu unaopigiwa debe na baadhi ya watu utafanikiwa ni vema vyeo vya marais wawili wa Zanzibar na Tanganyika vikafutwa ili kuiepusha nchi kuwa na marais watatu.

Alisema nchi mbalimbali zitaicheka Tanzania kama itakuwa na marais watatu ambao wote inaweza ikatokea wakakutana nje ya nchi.

“Tutakuwa watu wa ajabu sana huko kwa wenzetu, yaani sisi masikini halafu tuna marais watatu? Hizi gharama tunazotaka kumtwishwa mwananchi za nini?” alihoji.

Alisema kama kutakuwa na serikali tatu ni vema kukawepo na rais mmoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wengine wakapewa majina mengine kama Makamu wa Rais au Waziri Mkuu.

Sitta aliongeza kuwa hapingi muundo wa serikali tatu, bali hakubaliani na hoja ya uwepo wa marais watatu.

Aliongeza kuwa hoja ya kutaka marais hao watatu inashabikiwa na wenye uroho wa madaraka, wanaodhani inaweza kuwa njia rahisi kwao kufikia malengo yao ya kisiasa.

“Kuna watu wana kiu kubwa ya kuitwa mheshimiwa rais, ndiyo maana wanapigia debe uwepo wa marais watatu, nawaona ni wabinafsi tu hawana jambo jingine,” alisema.



Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mke wa Rais je? tujue wajibu wake na mipaka!!

Wajibu wa mke wa rais ni kukaa home na kuhakikisha mume wake anakula vizuri na kupata nafasi ya kupumzika.. Na vile vile kuiangalia familia yake kwa kuwa mumewe hatakuwa na muda wa kutosha kutokana na majukumu makubwa ya kuliongoza ya taifa.. Hicho ndicho alichokifanya mama Maria.. Hawa wa kisasa unawaona muda hata hawana.. mashindano yako kwenye dubious taasisi..
 
6 anamhofia lowasa tu, hana kipya.. kwasasa anahaha ile mbaya. anajutia kuwa spika dhaifu wa bunge, kwakuwa hakuweza kuifanya kazi ya bunge kwa umakini kufanikisha maslahi ya chamadola kama ambavyo mama makinda alivyojitahidi kutenda mpaka sasa, ikapelekea muda wake ukapunguzwa na sasa ana haha, kuhakikisha ule msemo wa tukose wote unatimia.
 
Wajibu wa mke wa rais ni kukaa home na kuhakikisha mume wake anakula vizuri na kupata nafasi ya kupumzika.. Na vile vile kuiangalia familia yake kwa kuwa mumewe hatakuwa na muda wa kutosha kutokana na majukumu makubwa ya kuliongoza ya taifa.. Hicho ndicho alichokifanya mama Maria.. Hawa wa kisasa unawaona muda hata hawana.. mashindano yako kwenye dubious taasisi..
unataka uniambie ndivyo michelle obama anavyofanya kwa mumewe kama festileideee wa waamerika? ha ha ha
 
Binafsi huwa namuona Mh Sitta kama muimba taarabu tu. Ni mtu wa vijembe na wa kulia na malalamiko mengi. Sio mtu wa action yeye ni kuropoka tu kila kukicha. Ajifunze kuchukua hatua kama kiongozi na sio kupiga vijembe kama anaimba taarabu. Hafai kuwa kiongozi mkuu wa nchi.
 
Wajibu wa mke wa rais ni kukaa home na kuhakikisha mume wake anakula vizuri na kupata nafasi ya kupumzika.. Na vile vile kuiangalia familia yake kwa kuwa mumewe hatakuwa na muda wa kutosha kutokana na majukumu makubwa ya kuliongoza ya taifa.. Hicho ndicho alichokifanya mama Maria.. Hawa wa kisasa unawaona muda hata hawana.. mashindano yako kwenye dubious taasisi..
mume kiguru na njia, mke naye kiguru na njia velevile sasa hata mila za ndoa sijui zinatekelezwa vipi?
 
mume kiguru na njia, mke naye kiguru na njia velevile sasa hata mila za ndoa sijui zinatekelezwa vipi?

Ha ha ha.. Ndo maana watoto wanafeli pamoja na kusomeshwa kwenye best schools..! Muda wa wazazi kukaa na mtoto na kuangalia alichosoma hawana.. Ni vizuri kwenye katiba mpya kiwepo kifungu kinachoelezea kazi za mke wa raisi.. Kumpikia mumewe na kuangalia watoto nyumbani period..
 
unataka uniambie ndivyo michelle obama anavyofanya kwa mumewe kama festileideee wa waamerika? ha ha ha

Ninachoweza kukuambia kuhusu American first ladies ni kwamba hawana hizi dubious taasisi.. Na wala huwasikii wamepitishwa ujumbe kwenye vyama vyao..
 
Binafsi huwa namuona Mh Sitta kama muimba taarabu tu. Ni mtu wa vijembe na wa kulia na malalamiko mengi. Sio mtu wa action yeye ni kuropoka tu kila kukicha. Ajifunze kuchukua hatua kama kiongozi na sio kupiga vijembe kama anaimba taarabu. Hafai kuwa kiongozi mkuu wa nchi.
umenena mkuu, binafsi nilikuwa sijajua namna ya kumwelezea huyu mtu. :A S thumbs_up:
 
Kuhusu Raisi kuibeba familia yake, hii imekaa vip jamani? Any Reference?

Kweli hili la familia lina mantic kuangaliwa, nadhani alimaanisha ukoo, ebana kwa vyovyote lazima ukoo wa Rais utakuwa mkubwa sana, Ile hulka ya mwanadamu kupenda kuishi kwa ndugu mwenye uhakika wa chakula, na wengine wa kujichomeka tu humo, sasa tabu inakuja wote hawa wanahudumiwa na Ikulu, noma!
 
Tena huyu jamaa sijui kwa nini siku hizi anavunga kuwageuka wenzie, huu sio aina fulani mpya ya unafiki kweli?! Hawa ndio wanaofanya amendment hata kwenye amri kumi za Mungu, bila aibu!
 
Back
Top Bottom