Bando la wiki
JF-Expert Member
- May 23, 2023
- 911
- 3,017
Kuna watanzania wamepanic kuhusu M23 kuchukua eneo la Goma DRC na kauli ya Paul Kagame wa Rwanda.
Ndugu zangu vita sio jambo la mchezo wala la kuliomba. Lakini pia tukumbuke hakuna nchi ndogo kwenye uwanja wa vita.
Wote tumeshuhudia namna Israel taifa dogo kijeografia lakini ilivyo wapelekea moto mataifa makubwa kama Yemen, Lebanon, iran na Syria.
Kuendesha vita ni gharama kubwa ndugu zangu, embu fikiria nchi kama Russia yenye uchumi mkubwa wa karibia trilioni 3 USD na Ukraine yenye uchumi mkubwa karibia dola Billion 200 Leo mwaka wa nne wanapigana lakini kila siku Ukraine anapita huko kwenye mataifa makubwa kuomba msaada.
Sasa nchi yetu maskini yenye uchumi dhoofu chini ya dola bilioni 78 tunataka kuingia kwenye vita visivyo husu mipaka yetu moja kwa moja. Nchi maskini ambayo bado inaangaika kujenga vyoo na madawati mashuleni ikaingia tena kwenye vita. Nchi yetu bado inaugulia vita vya Kagera vya mwaka 1978 ambavyo viliondoka na hazina na vijana wetu wengi waliouwawa kwenye vita hiyo. Bara hata vita ya Kagera tulikuwa tunapigania mpaka wetu kule kagera.
Vita ya DRC na Rwanda (M23) haituhusu moja kwa moja kwa sababu hakuna eneo letu linagombewa kwenye vita hiyo.
Kuhusu biashara yetu kupita hapo Goma kuelekea DRC, ni suala la kufanya mazungumzo ili mizigo ya wateja wetu ipite salama eneo hilo.
Nasisitiza tu serikali iongeze ngome za kisasa za jeshi mipakani hasa mipaka ya Rwanda na Burundi ili hao waasi wasiingie kirahisi ndani ya mipaka ya JMT.
Ndugu zangu vita sio jambo la mchezo wala la kuliomba. Lakini pia tukumbuke hakuna nchi ndogo kwenye uwanja wa vita.
Wote tumeshuhudia namna Israel taifa dogo kijeografia lakini ilivyo wapelekea moto mataifa makubwa kama Yemen, Lebanon, iran na Syria.
Kuendesha vita ni gharama kubwa ndugu zangu, embu fikiria nchi kama Russia yenye uchumi mkubwa wa karibia trilioni 3 USD na Ukraine yenye uchumi mkubwa karibia dola Billion 200 Leo mwaka wa nne wanapigana lakini kila siku Ukraine anapita huko kwenye mataifa makubwa kuomba msaada.
Sasa nchi yetu maskini yenye uchumi dhoofu chini ya dola bilioni 78 tunataka kuingia kwenye vita visivyo husu mipaka yetu moja kwa moja. Nchi maskini ambayo bado inaangaika kujenga vyoo na madawati mashuleni ikaingia tena kwenye vita. Nchi yetu bado inaugulia vita vya Kagera vya mwaka 1978 ambavyo viliondoka na hazina na vijana wetu wengi waliouwawa kwenye vita hiyo. Bara hata vita ya Kagera tulikuwa tunapigania mpaka wetu kule kagera.
Vita ya DRC na Rwanda (M23) haituhusu moja kwa moja kwa sababu hakuna eneo letu linagombewa kwenye vita hiyo.
Kuhusu biashara yetu kupita hapo Goma kuelekea DRC, ni suala la kufanya mazungumzo ili mizigo ya wateja wetu ipite salama eneo hilo.
Nasisitiza tu serikali iongeze ngome za kisasa za jeshi mipakani hasa mipaka ya Rwanda na Burundi ili hao waasi wasiingie kirahisi ndani ya mipaka ya JMT.