ANTHONY KWEKA
JF-Expert Member
- Mar 26, 2013
- 958
- 379
Mkuu, hapo haingaliwi nani atafaulu na kwa kiwango gani.Nia sio kupunguza ziro na kufurahisha wananchi.Lengo la kupanga viwango vya ufaulu kwa kuzingatia maandalizi ni muhimu sana.Kama mtu alistahili ziro basi aipate baada ya kuhukumiwa kwa haki na sio kwa kuviziwa bila kujua.
ni kweli kabisa mzee ila hawarudii kusahosha ila wanataka kucheza na madaraja na mambo mengine watoto wafaulu. hili jambo wanalifanya kisiasa eti wanasema necta ilifanya makosa kuanzisha utaratibu mpya bila kuhusisha wadau. lakini ukizingatia necta ni baraza kubwa na linaongozwa na kanuni na sheria husika za nchi sio rahisi kufanya mistake ndogo kiasi hicho ila hiyo ni njia ya kudanganya watanzania kujipatia umaarufu wa kisiasaWatanzania wenzangu Serikali imetanganza kufuta matokeo yote ya kidato cha nne na kusahhisha upya
Binafsi sioni kama ndio dawa ya tatizo hilo!! Serikali ingeweza kuwafanya watahiniwa warudie tena mtihani wao!!Sababu hata ambao walichora Zombie wajipe muda wa kujisomea upya!! Baadhi ya wanafunzi waliomba kusahihishiwa upya lakini matokeo yalionyesha wengi walifeli zaidi!!Nikionacho mimi ni wizara kujaribu kufuta hizo zero ili kuweka takwimu sawa ila hatutakua tumeisaidia Elimu yenyewe kitaaluma!!
Kama ni hivyo mbona mahesabu rahisi kwa kuwa wengi walipata ziro yaani 60% assume wote hawa walikuwa na wastani wa marks 35 ambayo NECTA waliichukua kama F kwa sasa ni D huoni wataangukia kwenye div 4 ya points 28 sasa ndio malengo ya watahiniwa wengiMtihani hausahihishwi upya bali NECTA wameagizwa kugrade marks za wanafunzi upya kwa kufuata viwango vilivyotumiwa 2011 na miaka ya nyuma. Imeonekana kuwa mwaka 2012 walitumia viwango vipya ambavyo wamebadili wenyewe bila kushirikisha wadau wengine wa elimu. Mfano F katika somo hutolewa kwa alama 0 hadi 20. Wao walibadilisha na kufanya iwe 0 hadi 34 bila kuwashirikisha wadau wengine wa elimu.
Watanzania wenzangu Serikali imetanganza kufuta matokeo yote ya kidato cha nne na kusahhisha upya
Binafsi sioni kama ndio dawa ya tatizo hilo!! Serikali ingeweza kuwafanya watahiniwa warudie tena mtihani wao!!Sababu hata ambao walichora Zombie wajipe muda wa kujisomea upya!! Baadhi ya wanafunzi waliomba kusahihishiwa upya lakini matokeo yalionyesha wengi walifeli zaidi!!Nikionacho mimi ni wizara kujaribu kufuta hizo zero ili kuweka takwimu sawa ila hatutakua tumeisaidia Elimu yenyewe kitaaluma!!
Je unadhani ukitumika huo utaratibu matokeo yatakuwa mazuri? Maana ziro zilkuwa nyingi ambapo walitumia 35 kama F sasa hiyo itskuwa kama D huoni bado watapunguza ziro kdg na kwenda four?