Siwezi kununua mbwa wa kizungu Sh. Milioni 3 kwa sababu hawana utofauti na mbwa koko

Duh! Mkuu mbona umekasirika hivyo? Hao Mbwa mbona hawafundishwi kila mara? kuna mahala ukipakosea Mbwa wote wanakuwa hawako sawa. Mimi nafuga hao wa kisasa lakini hawafundishwi kila mara mara moja niliyo wafundisha wako sawa mpaka leo.
3M kununua mbwa halafu utegemee asikasirike..!! Sema nini, wakati unakandya kununua mbwa kwa 3M, anakuja kukulinda ukiwa na vitu vya shilingi ngapi? Huo uwiano ndo unatia hasira. Nina TV ya 2M, nije ninunulie mbwa wa 3M kuja kuilinda TV ya 2M? Hapo ndo hasira huanzia
 
Tuliwahi kuwa na mbwa mkali na hakupewa mafunzo yoyote lakini alikuwa zaidi ya mbwa wa kisasa Hawa gharama.

Huyu mbwa Kila asubuhi alikuwa anatupeleka shule kipindi hicho tuna amka saa10 alfajiri kwenda shule anatupeleka Hadi tunafika. Ikumbukwe kipindi hicho kulikuwa na mapori wanyama hasa nyegele alikuwa anapambana nao na kuwaua niajabu lakini walikuwa Wana surrender!

Kwenye uwindaji Wala hakuwa anafukufuza wanyama kama digidigi swala nk alikuwa anafata harufu Yao. Na akimkamata kama ni myanyama mdogo anamleta Hadi ulipo. Kama ni mkubwa anakufuata na kukuelekeza alipo wanyama kama pongo Kwa kisukuma alikuwa anawaua mno.
 
Yuko wapi kwasasa huyo rafiki?
 
Price na Value ni vitu viwili tofauti.Watu wenye pesa hawalipi sababu umetaja bei, bali sababu ya thamani ya kitu. Ndo maana kuna mtu yuko tayari kutoa 3M akanunua full grown GSD....wakati wewe unaona thamani ni mbuzi na ng'ombe.
Kuna mtu ananyumba vyumba viwili na anaona hana huhitaji wa nyumba kubwa na hapo ana watoto watano na kuna mwamba ana mtoto mmoja but ghorofa, sqm 2000, swimming pool etc na wanaishi watu wanne tu..
Kuna watu wanalipia utelezi 3000/= anamshangaa anayetoa 50,000/= na hapo kuna mtu anatoa 500,000/=.
Kuna mtu ana C.C 3600 na kuna mwamba ana C.C 1200 anamashangaa wa 3600 sababu wote wanatembea wamekaa.
Kuna mtu anatoa 300M anachukua plot/nyumba mbezi beach, kuna mwingine anashangaa why huyu asiende Kibaha akachukua plot safi kwa 30M tu nyingine akanunua ng'ombe.
Kuna mtu anakipia ada 7M mwingine 150,000/= huyu anamshangaa huyo wa juu kupoteza pesa..
ISSUE NI VALUE. - THAMANI - THAMANI
 
Hapa Sinza kuna mmiliki mmoja alimbana mguu
Mbwa wake (ajali ya gari ndani kwake)

Sasa kapona lakini hatembei sawa,
na kidonda kimeshapona.
Kumrekebisha ili atembee sawa,
Upasuaji na Gharama ya matibabu jumla inatakiwa Tsh.1.5 Mil.
Wewe kuweza?
 
Chuma Hicho Na SasA Kinatema Che Che
Your browser is not able to display this video.
 
Mil 3 ununue mbwa? Wakati unaweza kukuta mahali vilikozaliwa vimbwa vingi ukachukua kimoja bure tu ukakifunza. Nenda sehemu waliko wale wawindaji uone walivyo na mbwa wakali
Nimetoka kununua mil 5 mmoja kaka...
 
Sio mtaalamu sana kwenye hii field ila uwezo alionao German Shepherd kiakili kabla hata hajafundishwa usipime kabisa... kuna puppy moja hapa kijiweni kashiajua kufungua mlango wa ofisi.. msipolock milango dakika sifuri mnamkuta anawasubiri jikoni kwenye fridge hasa akiwa na njaa au akikosa mtu wa kucheza naye nje.. akikua kidogo sijui itakuaje..
ila upo right mbwa ni mbwa tu ila wanawafanyia selective breeding
 
Ninachojua wewe huna hela, halafu ni Mnyalu unawachukulia mbwa kama kitoweo cha kawaida
 
Sema sisi sio watu wakufuatilia sana ila mtandaoni vipo hadi vitabu ambavyo vinakulekeza lugha za mbwa. na ni namna gani unaweza ukamtengeneza mbwa wako akawa kama ww unavyotaka awe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…