Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 76,107
- 160,001
1. Hadithi inayokuja
ni ya sungura sikia
hadithi uliyongoja
leo ninakuletea
2. Alitoka siku moja
njaa aliposikia
njaa aliposikia
sungura nakuambia
3. Siku ile akaenda
porini kutembelea
akayaona matunda
mtini yameenea
4. Sungura akayapenda
mtini akasogea
mtini akasogea
sungura nakuambia
5. Sungura karukaruka
lakini hakufikia
matunda hakuyashika
mkononi hakutia
6. Karuka tena karuka
lakini hakufikia
mwisho wake akachoka
kachoka hata mkia
7. Machozi yakamtoka
pembeni akasogea
pembeni akasogea
sungura nakuambia
8. Sizitaki mbichi hizi
sungura akagumia
naona nafanya kazi
bila faida kujua
9. Sio kama hakutaka
sasa nakupasulia
matunda aliyataka
ndiyo kisa akalia
10. Tunajua hakufika
alichoka kurukia ...
Tupieni mistari tumalizie kisa hiki cha rafiki
yetu sungura.
ni ya sungura sikia
hadithi uliyongoja
leo ninakuletea
2. Alitoka siku moja
njaa aliposikia
njaa aliposikia
sungura nakuambia
3. Siku ile akaenda
porini kutembelea
akayaona matunda
mtini yameenea
4. Sungura akayapenda
mtini akasogea
mtini akasogea
sungura nakuambia
5. Sungura karukaruka
lakini hakufikia
matunda hakuyashika
mkononi hakutia
6. Karuka tena karuka
lakini hakufikia
mwisho wake akachoka
kachoka hata mkia
7. Machozi yakamtoka
pembeni akasogea
pembeni akasogea
sungura nakuambia
8. Sizitaki mbichi hizi
sungura akagumia
naona nafanya kazi
bila faida kujua
9. Sio kama hakutaka
sasa nakupasulia
matunda aliyataka
ndiyo kisa akalia
10. Tunajua hakufika
alichoka kurukia ...
Tupieni mistari tumalizie kisa hiki cha rafiki
yetu sungura.