Sizitaki Mbichi Hizi!!

Sizitaki Mbichi Hizi!!

Asprin

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2008
Posts
68,223
Reaction score
96,083
Najua wengi mlikuwa bado hamjazaliwa lakini hebu angalieni wazee tulivyokuwa tunapiga mashairi.
Shairi hili nalidediketi kwa vidume vya JF vinaoongoza kwa kupigwa vibuti na mabinti wa JF wakiongozwa na monitor wao The Finest.

Hadithi inayokuja, ni ya Sungura sikia,
Hadithi uliyongoja, leo ninakuletea,
Alitoka siku moja, njaa aliposikia,
Njaa aliposikia, Sungura nakuambia

Sikuile akaenda, Porini kutembelea,
Akayaona matunda, mtini yameenea,
Sungura akayapenda, mtini akasogea,
Mtini akasogea, Sungura nakuambia.

Sungurakarukaruka, lakini hakufikia,
Matunda hakuyashika, mikononi hakutia,
Hakika alisumbuka, nguvuze zikapungua,
Nguvuze zikapungua Sungura nakuambia.

Mtazame hapo juu Sungura amelegea,
Mtazame na miguu, matunda anarukia,
Atafanya sikukuu, matunda akifikia,
Matunda akifikia, Sungura nakuambia.

Karukatena karuka, matunda akarukia,
Mwisho Wave akachoka, kachoka hata mkia,
Penye mti akatoka, pembeni akasogea,
Pembeni akasogea, Sungura nakuambia.

“Sizitakimbichi hizi” Sungura akagumia,
“Naona nafanya kazi, bila faida kujua”,
Yakamtoka machozi matunda akalilia,
Matunda akalilia, Sungura nakuambia.

Siokama hakutaka, sasa nakupasulia,

Matunda aliyataka, ndiyo kisa akalia
Tunajua hakufika, alichoka kurukia,
Alichoka kurukia, Sungura nakuambia.

Hadithi nimemaliza, nimekwisha simulia,
Jambo moja sikiliza, rafiki yangu sikta,
Usikose kujikaza, mazuri kukazania,
Utamshinda Sungura, utapata mbivu hizi.

TGIF!

Nyie vijana wa sasa, mkitongoza mkakataliwa msibwatuke eti "hamtaki tena kwanza eti mbichi" wakati mnaumia moyoni. Mbona wazee tunajilia vyetu kiulaini?

Kutongoza ni Fani na Kipaji:
Source ODM.

Weekend njema!!





 


Karukatena karuka, matunda akarukia,
Mwisho Wave akachoka, kachoka hata mkia,
Penye mti akatoka, pembeni akasogea,
Pembeni akasogea, Sungura nakuambia.


"Sizitakimbichi hizi" Sungura akagumia,
"Naona nafanya kazi, bila faida kujua",
Yakamtoka machozi matunda akalilia,
Matunda akalilia, Sungura nakuambia.


Siokama hakutaka, sasa nakupasulia,
Matunda aliyataka, ndiyo kisa akalia
Tunajua hakufika, alichoka kurukia,
Alichoka kurukia, Sungura nakuambia.


Hizi beti tatu, zimenifanya nicheke, hivi kweli vijana wa siku hizi wanaweza kweli kuwa kama Sungura!? ukimzungusha siku mbili tu, kesho humuoni tena!
 
Wale wanao tongozea wenzao wanaitwaje hivi!!!!!!!!!:A S embarassed:

WanITWA "Makuwadi", Babu yangu alinisimulia eti zamani alikuwa hodari wa kuwaandikia wavulana wenzie barua za kutongozea kisha wanampa ujira wa pesa mbili au tatu
 
Hadithi hii inatufundisha nini babu?
Haikufundishi wewe bali tule tuvijana tunavyokutongoza afu unavipiga chini? Ushatongozwa na wangapi hapa JF? Kama vipi nijibu kwa PM!
 
WanITWA "Makuwadi", Babu yangu alinisimulia eti zamani alikuwa hodari wa kuwaandikia wavulana wenzie barua za kutongozea kisha wanampa ujira wa pesa mbili au tatu

Mi ndo naifanya hapa mujini lakini nakula kwanza mimi ndo namkabidhi jamaa aendelee
 
Hizi beti tatu, zimenifanya nicheke, hivi kweli vijana wa siku hizi wanaweza kweli kuwa kama Sungura!? ukimzungusha siku mbili tu, kesho humuoni tena!

Unajua siku hizi idadi ya wanaume ni wachache kuliko wanawake, ukijifanya kulinga mwenzio anajiuliza nitampataje
 
Mi ndo naifanya hapa mujini lakini nakula kwanza mimi ndo namkabidhi jamaa aendelee
Hahahaha..... kulaaaleki, ndo ile ya kizuri kula na nduguyo siyo?

Unajua siku hizi idadi ya wanaume ni wachache kuliko wanawake, ukijifanya kulinga mwenzio anajiuliza nitampataje
Ngoja hii post nimforwardie MwanajamiiOne. Nikisemaga mie ananiita mzushi!!
 
Haaaa haaa haaa,my babu habari yako binafsi kwanza!
Naona leo unadili na vijana wako,ungeongeza ubeti mmoja wa kuwatia moyo kuwa wasijali wakajipange upya na kuweka vina na mizani lol!
Siku hizi watu wanamalizana kwa sms tu na km ni kibuti ni humo humo wala hakuna kurusha ngumi!
Babu hii kitu mie niliimba sana enzi hizo darasa la tatu km sikosei na mwalimu wangu mpendwa Foibe!
Nakutakia wikend njema Babu!
 
Du weka pia hadithi ya adili na sikiri au Ziwa jipe,watoto wageuka mawe,gulio la katerero,Tola anakula Gizani,Adunje na Jogoo
 
Kulikuwa na picha ya sungura ameruka juu lakini akasjhindwa kuyafikia matunda,...., mwaka 1980 darasa la 4! Lingine lilikuwa

KARUDI BABA MMOJA, TOKA SAFARI YA MBALI;
KAVIMBA YOTE MAPAJA, NA KUTETEMEKA MWILI;
WATOTO WAKE WAKAJA, ILI KUMTAKA HALI;
WAKATAKA NA KAULI, IWAFAE MAISHANI.

AKATAMKA MGONJWA, NINAUMWA KWELI KWELI;
HATA KAMA NIKICHANJWA, HAITOKI HOMA KALI;
ROHO NAONA YACHINJWA, KIFO KINANIKABILI;
KAMA MNATAKA MALI, MTAYAPATA SHAMBANI
.
 
Kama huna kalenda nyumbani kwako, angalia atakacho post ODM utajua leo ni ijumaa.


Source: klorokwini a.k.a lawyer a.k.a fellow tablet a.k.a majununi!
 
Kama huna kalenda nyumbani kwako, angalia atakacho post ODM utajua leo ni ijumaa.


Source: klorokwini a.k.a lawyer a.k.a fellow tablet a.k.a majununi!
Hivi nani alikuwekea dhamana? We si ulikuwa lupango?
 
Haaaa haaa haaa,my babu habari yako binafsi kwanza!
Naona leo unadili na vijana wako,ungeongeza ubeti mmoja wa kuwatia moyo kuwa wasijali wakajipange upya na kuweka vina na mizani lol!
Siku hizi watu wanamalizana kwa sms tu na km ni kibuti ni humo humo wala hakuna kurusha ngumi!
Babu hii kitu mie niliimba sana enzi hizo darasa la tatu km sikosei na mwalimu wangu mpendwa Foibe!
Nakutakia wikend njema Babu!


Cantalisia huyu mwalimu Foibe alikuwa mkoa gani?



 
Asprini mimi hiyo avatar yako inaniacha hoi,
hata usiposema mimi ninacheka.
 
Haaaa haaa haaa,my babu habari yako binafsi kwanza!
Naona leo unadili na vijana wako,ungeongeza ubeti mmoja wa kuwatia moyo kuwa wasijali wakajipange upya na kuweka vina na mizani lol!
Siku hizi watu wanamalizana kwa sms tu na km ni kibuti ni humo humo wala hakuna kurusha ngumi!
Babu hii kitu mie niliimba sana enzi hizo darasa la tatu km sikosei na mwalimu wangu mpendwa Foibe!
Nakutakia wikend njema Babu!
Kumbe na wewe kakongwe?
 
Back
Top Bottom