Skendo ya irene uwoya inataka kuniaribia ndoa!!!!!

Wanawake wengine akili zao ni 1-1.

hujambo Husn?
Mbona kinamama mnajikandia tena wenyewe?mimi natupiwa mawe na kina Aspirin kwa kuwakingia kifua ati!
Stand together bana iwe in rain or sunshine!
 
Bora 1-1... yani ni 0-0.

Lakini wife wangu yupo poa na nampenda sana... Lakini ndio nimeshindwa kabisa kumuelewa kwenye hili.
Kama ni hivyo straight wife wako siyo muaminifu ana makando kando yake.
Kifupi upo ridht uliimagine situation kama hiyo ingekuwa kwako. Ni kama kusema mimi ningekuwa JK ningemfukuza Lowassa chamani halafu mkeo aanze kukasirika inatilisha mashaka kidogo.
Cha kufanya acha kulilia lia nampenda mke wangu wakati hakutendei haki. Kuwa wa kiumeni, mwite muulize kwa upole amekasirika nini katika kauli yako na sababu zake. Akeleta nyodo badilika kuwa hali itakuwa tete endapo hutapata majibu yanayoeleweka.
 
hujambo Husn?
Mbona kinamama mnajikandia tena wenyewe?mimi natupiwa mawe na kina Aspirin kwa kuwakingia kifua ati!
Stand together bana iwe in rain or sunshine!

bishanga hapo hatujikandii ila huwezi kutetea kila kitu hata kama unaona hakipo sahihi kisa tu unabelong kwenye hilo kundi.
Habari yako binafsi?
 
Well, reaction lazima ingekuwepo hasa kwa vile unamzungumzia mwanamke mwenzake.
Lakini kimsingi haikutakiwa kudumu, hadi kufikia hatua ya kubembelezwa na bado anaweka msimamo wa kununa. Naamini hayo yalikuwa ni mazungumzo tu na comments katika story hata yeye angaliweza ku comment namna hiyo.
Ndoa haijaribiwi, inaweza kuvunjika/kung'oka ghafala kama shina la mpapai.
 
Katika hali kama hii kosa langu lipo wapi. Mimi ndio ungekuwa msimamo wangu huo, nisingeweza kumwambia uongo na hata hivyo ilikuwa tunapiga story tu.

Au ningemdanganya tu kumridhisha!!. Lipi sahihi!!.

Utakuwa umefanya kosa kubwa sana kama utabadili msimamo na kuwa "Artificial" ili kumbembeleza fulani..kwani siku nyingine utashindwa kusema ukweli ili kulinda ndoa..

Ndoa hailindwi kwa nidhamu ya woga.. Ndoa inalindwa kwa ukweli..
 

NK nafikiri kucompare na ndoa zingine ni vizuri ili kujifunza namna wenzenu wanafanikiwa katika maisha yao ya ndoa na kama wanafail na nyie msije mkafanya yanayowafanya wafail.
Jamaa alichokifanya nafikiri ni namna nyingine ya kufikisha ujumbe kwa mkewe kwamba usifanye hiki. Hata huo mfano uliotoa ni namna nyingine ya kusema "usirudi sa nane za usiku". Sasa kama mwanaume anarudi sa kumi na mbili hapo ingebidi afurahi maana anajua katika hilo hana kosa.
Mfano big x angesema "mke wangu ungetoa kauli kama za irene uwoya nisingefurahia hata kidogo". Hapo hajasema kama angetoa talaka au la, je huyo mke angekasirika?
 
Wanawake wengine akili zao zinaku zipo deactivated, jaribu kuzi activate kwa makofi. Hawezi kununa kijinga halafu na wewe unamchekea. Tandika makofi.

Hahahah... we hapo ndio unataka kuongeza balaa.
 
Ukiona hivyo mke wako alikuwa na plan ya kufanya kama Irene, sasa ume pre-empty her plans> Usimbembeleze, wewe mwache, mwambie huo ndio msimamo kwako na kama kuna siku atafanya hivyo ajue ndio basi

Duh!!! mzee unaniongezea hasira... hawezi fanya hivyo bana. ni vile hajategemea mi kumwambia hivyo.
 
Umeoa au umeolewa?
Chunguza nyenendo za mkeo, kisha kuchoka hivyo.
Kama unabisha mwambie akiendelea kuuchuna unamwacha, uone atakavyo furahi kuachana nawe.

Nimeoa bana.......... Ninaweza nikazua balaa lingine kumwambia hivyo. Bora nikae kimya.
 
mhhh hako kajineno nako ka kumfanya mtu anune jamani atakosa makubwa halafu atakuwa anaishi na kivuli cha mtu.....jifanye mjinga uyajue yaliyomo na yasiyomo
 
Mkuu no doubt kwamba mkeo anakupenda sana na hafikirii kuachana na wewe. Mwombe msamaha kiukweli ulikosea. Unapoongea na my wife kuwa makini sana katika kuchangia. Mfano ungeweza kumjibu 'wewe mke wangu ulivyo na hekima huwezi kufanya hivyo'.

Shukurani mjomba. Tatizo vitu vingine tunaomba msamaha basi tu kuwalidhisha..... Huoni ukiwa mtu wa kuomba msamaha hata kama kosa ni la ukweli si atakudharau sana mwanamke. mi nadhani bora kukaa kimya kujifanya kama umesahau hiyo ishu. hasira zake zikipungua atasahau na ataelewa kwanini nilisema vile. Ni bora kuwa na msimamo.
 

Sasa hapo si ningekuwa nabembeleza sana.......... Je kama akiuliza tena ungefanyaje... majibu si yangekuwa ni kumtimua tu. Mi nadhani kuna makosa mengine mtu hutakiwi kujifanya neutral ..... Ni bora kutoa msimamo wako wa uhakika... hata kama atamind kama mimi hivi......... baadae ataelewa tu nilikuwa namaanisha nini. Mi nadhani amenimind ni kwa vile hajategemea kusikia maneno kama hayo kutoka kwenye kinywa changu.
 
mtoe auti tu ama mpelekee zawadi,anahitaji kubembelezwa tu!kesi ndogo hiyo
 
Me nadhani ame miss kubembelezwa na kudeka kidogo,usibadili msemo badli mpe kizawadi kidogo soo liishe
 
Mkuu inaonekana unadekeza sana, mbona hivyo ni vijineno vidogo tu
 
huyo mkeo nahisi naye ana mambo ya uyowa,sasa nini cha kumkera hapo ni nini?usilegeze msimamo kama alikuwa na wazo la kutesti we mbanie,vinginevyo atakupandia kichwani.
 

Yaani mkuu wala hujakosea kwa ulicho mjibu wife wako, umemweleza ukweli. Jaribu kumbeleza na kumuomba msamaha wakizushi c unajua hao wenzetu wanavopenda kudeka ili aone kama unamjali sana,
 
mume ***** wewe,mwenzio ndikumana nae alianzishiwa hivi hivi akawa anakataa kama ww,
hapo huna mke na usishangae akatimka kwasababu hiyo.
jipange
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…